Kufungua tawi la chadema udom

Tumekupata vilivyo Miradibubu,umetutia ahueni kidogo.
Tutatoa hata michango ya mali kufanikisha hilo.Ikumbukwe kwamba Dodoma ni ngome kuu ya CCM,hivyo inahitajika nguvu za ziada.Nawapongeza CHDEMA UDOM,kwa jitihada zinazoendelea hapo.Ni wazo zuri ofisi ziwe mjini kati pale,coz naamini mtapata wageni wengi sana toka sehemu mbalimbali za nchi hapo tawini.Ningependa tu kuwaomba muwe chachu kwa matawi mengine hapo dom,ni dhahiri matawi mengine,pamoja na CDM Mkoa,bado ni dhaifu sana hapo dom,Tumeshuhudia hayo wakati wa kampeni.Msifanye kazi kama tawi tu la UDOM,Tunaomba mfanye kazi kama ya operation pia,Enendeni mpaka jimbo la Bahi,kule upinzani haupo kabisa na Badwel mbunge wa ccm alipita kiulaini kabisa,ni mbunge mzuri na zahitajika nguvu za ziada kuvunja ngome yake,ni wasomi kama nyinyi mnaweza kulikomboa.Nasema mwende kila jimbo la dom coz nyie mchanganyiko wa watu mbalimbali toka kona mbalimbali za nchi,so haitatosha mkifanya kazi kama tawi tu,mkaikomboe Mvumi pia.Lakini nina wasiwasi mahala fulani,wingi wenu wanachadema hapo UDOM,Ungetosha kabisa kuchukua jimbo la mjini 2015,endapo wakati wa kupiga kura mngekuwa DOM,kama kawaida CCM watakifunga chuo wakati wa kupiga kura ili msipige kura,hapo ndipo tutalikosa jimba tena,sijui mmejipangaje.Pale SAUT Mwanza temefanikiwa kuifukuza CCM kabisa mkoa wa Mwanza na ni kwa jitihada za wanaCDM tawi la SAUT.Sasa tunafanya jitihada kuifukuza CCM kanda nzima ya ziwa na hilo tutalithibitisha uchaguzi ujao.Tuko nyuma yenu kwa hali na mali.
 
Haya ni mapambazuko yenye kutia matumaini, moyo huo wa kimapinduzi mkiuelekeza kwa vijana wanaosoma kwenye shule za yeboyebo pindi mpatapo nafasi, CCM haita himili NGUVU YA UMMA 2015. Ni aibu kwa kijana wa kisasa kukumbatia CCM inayofilisi nchi hii..


Mapambano yote yataendelea kama kawaida na moto tunaoenda kuuwasha hauwezi kuzimwa na mwanadamu yeyote
 

Tehe tehe teheeeeeee, ama kweli mfa maji haachi kutapatapa, watu wanazungumzia strategies wewe unasema wanajigamba na UDOM, CCM wameshakata tamaa.

Wewe ni miongoni mwa watu ambao ni fake great thinkers, huwezi sema unashangaa wana CHADEMA kucomment kwenye ishu kama hii, J.F inawawakilisha watanzania maana wakati wa kuji register hakuna sehemu unayoulizwa kuwa wewe ni CCM au CHADEMA, ukiona members wengi wa jamiiforums ni chadema basi ujue ndio hali halisi kwamba watanzania wengi wenye akili timamu ni wafuasi wa CHADEMA.

Big up wana UDOM, idadi yenu ni kubwa sana, Taifa linategemea ukombozi kutoka kwenu.

Nimeipenda sana mistari hiyo iliyo kwenye red. Umesahau kusema ukiona baadhi ya members wachache hapa ni CCM ujue ni vichwa wazi. Teh teh teh teh teh.Ninakupa big up!
 
Nilichukia sana chuo hiki kwa sababu wachakachuaji walituaminisha ni chao na waliomo chuoni ni wao.
Miradibubu umenifariji sana. Naweza kusema tu tupo pamoja. Chadema oyeeeeeeeeeeeeeeeeeee hakuna kulala mpaka kieleweke.
 
74403_1708548314231_1253767086_1995815_752604_n.jpg
photo.php
 
mawenzi,

chelea chelea utakuta mwana si wako.

mimi ni mwalimu mipango dodoma na nina kadi ya chadema, na wala sijifichi kwani naamini katika demokrasia na maendeleo baada ya kugundua kuwa hakuna dalili yoyote ya mapinduzi.

pia tuko wengi, ni uhuru wa raia. bora tu usivunje sheria ya utumishi.

sijifichi, na naringia hilo. karibu tujiunge. ukiona vipi nenda pale majengo sokoni, karibu na cana lodge annex ndio ofisi ya mkoa. chukua kadi yako na anza kuringa mara moja!
 
Miradibubu mimi binafsi nimekuamini 100% kutokana na ukweli uliouweka hapa. Kwanza umesema Gilead Terry kada wa ccm alieshindwa urais Udom,huyu kijana namjua vizuri tangu anasoma Loyola high school pale mabibo dsm ni mccm damudamu. Pia yule Thobias Mwesiga uliemsema bila kumtamka wazi namjua pia,yeye kasoma Rubya seminari kwa miezi 7 kisha akatimuliwa kwa uhuni. Umesema kweli,sisi wanachadema tutawapa nguvu kadri ya uwezo wetu. Hata kama hatuna fedha kama mafisadi ccm,tutatumia elimu zetu kuikomboa Tanzania. Viva Miradibubu,aluta continua!
 
Höngera sana wana udom kuingia upinzani.
Ila wajameni huyu mtoa mada ananitia shaka na jina lake la miradi bubu! Je, huu mradi wake wa tawi ni wa kweli au bubu?
Bw/Bi. Miradi bubu nakuomba uanzishe mradi wa ukweli ambao utakuwa chachu ya kuamsha vijana wa kitanzania hasa wasomi. Ninaomba agenda kubwa iwe umoja na uzalendo wa kweli ambao utalenga kuboresha maisha ya kila mtanzania.
Ningependa pia ktk tawi hilo paibuke watu kama Dr. Slaa ambao wataanza kuibua uozo ktk utawala wa Udom maana nasikia kuna miungu watu huko ambao wanafanya mambo yasiwe shwari.
Pia ningependa suala la udini lilohuburiwa sana na baadhi ya viongozi kpnd cha kampeni kama mtaji wao wa kukusanya kura lishughulikiwe ktk ngazi ya tawi ili kuvunja uzandiki na unafk wa mafisadi.

Hongereni sana. Cha msingi tuweke uzalendo na utu mbele, na chachu ya maendeleo iwe kwa maslahi ya umma na sio mtu binafsi. La sivyo kuna hatari ya kugeuka toka wepesi hadi wazito!!

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Udom!
 
Höngera sana wana udom kuingia upinzani.
Ila wajameni huyu mtoa mada ananitia shaka na jina lake la miradi bubu! Je, huu mradi wake wa tawi ni wa kweli au bubu?
Bw/Bi. Miradi bubu nakuomba uanzishe mradi wa ukweli ambao utakuwa chachu ya kuamsha vijana wa kitanzania hasa wasomi. Ninaomba agenda kubwa iwe umoja na uzalendo wa kweli ambao utalenga kuboresha maisha ya kila mtanzania.
Ningependa pia ktk tawi hilo paibuke watu kama Dr. Slaa ambao wataanza kuibua uozo ktk utawala wa Udom maana nasikia kuna miungu watu huko ambao wanafanya mambo yasiwe shwari.
Pia ningependa suala la udini lilohuburiwa sana na baadhi ya viongozi kpnd cha kampeni kama mtaji wao wa kukusanya kura lishughulikiwe ktk ngazi ya tawi ili kuvunja uzandiki na unafk wa mafisadi.

Hongereni sana. Cha msingi tuweke uzalendo na utu mbele, na chachu ya maendeleo iwe kwa maslahi ya umma na sio mtu binafsi. La sivyo kuna hatari ya kugeuka toka wepesi hadi wazito!!

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Udom!
Ondoa shaka juu ya hili jina kwani limetokana na riwaya moja tamu sana inayoibua ufisadi wa CCM tangu Azimio la Arusha mpaka kusambaratika kwake, Riwaya hiyo inaitwa Miradi Bubu ya Wazalendo ambayo imeandikwa na Prof. Gabriel Ruhumbika, Ukiweza jaribu kuisoma inatueleza wapi tulipo iacha njia
 
Kweli sasa wana udom mnaonekana kukomaa nafahamu kwamba siasa haziruhusiwi mazingira ya chuoni lakini nje ya chuo ni ruksa so i hope there will be no any stambling block in your endeavour kwa sababu ccm wana matawi karibu vyuo vyote na nakumbuka jk miaka ya hivi karibuni alizindua tawi la ccm chuo cha mzumbe. Mimi niko mitaa ya kati dodoma ntaomba mnipe kazi ya ukatibu mwenezi wa tawi na ntaifanya kazi hiyo kwa moyo wa kujitolea zaidi ili kukikuza chama... Ushauri mwingine naomba baada ya tawi hilo kufunguliwa juhudi zifanyike kuunda umoja wa wanachama wa cha chadema wa vyuo vya elimu ya juu mkoa wa dodoma ukijumuisha vyuo vya udom, st. John, mipango, cbe, madini na vingine kikiwemo chuo kipya cha loyola kinachojengwa eneo la nzuguni nje kidogo na manispaa ya dodoma. Lengo ni kuhakikisha mwaka 2015 tunaizika CCM rasmi.

Tupo pamoja mkuu ninyi ndio wadau wenyewe na pasipo watu kama wewe hatutafika mbali, mapambano yanaendelea
 
jana nilikuwa katika afisi za CHADEMA za mkoa na nimepata taarifa zote.

ni kweli vijana wa udom wamenzisha tawi pale makulu - kata ya chadema. PIA NASIKIA WAMEMTIMUA yulE MWENYEKITI WAO aliyeenda kuchuana na nimrod halafu akapewa pesa akajitoa.

nimesikia hata kina salva rweyemamu na kina ridhiwani wanawapiga mkwala viongozi wa wanafunzi kuwa wako chadema.

tawi liko hai.
 
Salaam kwenu nyote wapenda maendeleo wa dhati hapa Tanzania. Ninayo furaha kubwa kuwataarifu kwamba sisi wanajumuiya ya Chuo Kikuu Cha Dodoma ambao ni wafuasi wa dhati wa CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO- CHADEMA, tumeamua kufungua tawi letu ambalo litaendelea kutuunganisha na kuweka pamoja nguvu zetu ili kuleta mabadiliko ya kweli.

Tawi hili linakusudiwa kuwa hapo maeneo ya mjini ambapo tutapangisha ofisi nzuri na tutawajibika kuilipia pango kwa muda wote. Litafunguliwa mwanzoni mwa mwezi januari 2011.

CHADEMA ina wafuasi wengi sana katika hiki chuo tofauti sana na wengine wanavyodhani.

Ninaomba kutoa uthibitisho wa hili kama ifuatavyo:

1. Wakati wa kampeni uongozi wa Chuo uliamua kutoa mabasi yanayotumiwa na wafanyakazi ili yawapeleke wafanyakazi kuhudhuria mkutano wa Kikwete uliofanyika hapa Dodoma.Tofauti na uongozi wa chuo ulivyotarajia mabasi yale hayakupata watu katika njia zote yalikotumwa.

Kwa mfano, katika eneo la Kisasa wanakoishi walimu mabasi mawili yale makubwa hayakuambulia hata mwalimu mmoja, njia ya Nkuhungu basi la watu 65, lilipata watu wawili tu na njia ya Mipango basi lilipata mtu mmoja tu.

2. Katika chaguzi zote za uongozi hapa chuoni ni kosa kubwa sana kwa mgombea kubainika kwamba yeye ni mwa CCM.

Kwani kitakachompata ni kukosa kura, mifano ni hii hapa kuna kijana anaitwa Tery yule alisoma risala ya kipuuzi siku Kikwete amaetangazwa kuwa mgombea wa CCM.

Risala hiyo ilipewa jina la risala ya wanafunzi wa elimu ya juu, huyu Tery aligombea nafasi ya uraisi wa serikali ya wanafunzi, kamuulizeni kilichompata ni nini, kwani kura hazikutosha.
Mfano wa piili unawahusu Wahadhiri walioenda kugombea kwa tiketi ya CCM, katika majimbo ya Manyoni mashariki na mwingine katika jimbo lililokuwa la Samwel Chitalilo, wote hawa waligombea uongozi wa UDOMASA - CHAMA CHA WANATAALUMA UDOM, walikosa kura si kwa kukosa uwezo bali tu kule kufungamana na CCM.

3. Serikali ya wanafunzi kushikiriwa na vijana machachari wa Chadema.

4. Mijadala mikali katika mabasi na maeneo ya ofisi inayowahusisha wafanyakazi wa chuo yote imekuwa ikiipinga CCM kwa kiwango kikubwa na kuifagilia CHADEMA.

5. Kipindi cha kampeni wafanyakazi wengi na kwa uwazi waliiunga mkono CHADEMA, kutokana na hali hii hakuna mwana CCM aliyekuwa tayari kuitetea ccm hata kwa wale walioenda kugombea kwa tiketi ya CCM hawakuweza kukabiliana na nguvu kubwa ya Chadema.

6.Kauli ya kikwete kuwaasa wana UDOM wasitumiwe na wanasiaasa baada ya kubaini kwamba CHADEMA ina nguvu kubwa sana hapa mpaka imefikia hali ya kuhitaji kufanya mkakati madhubuti wa kudhibiti halii hii kupitia uongozi wa juu wa chuo na kuleta makada wa CCM kuja kunusuru hali.

7. UDOM kuwa ndani ya kata iliyochukuliwa na CHADEMA- kata ya Dodoma Makulu, kuna mchango mkubwa sana wa wana UDOM katika kufanikisha hili.

8. Wafanyakazi wa UDOM kusafiri kwenda mlimani yaani UDSM kumpigia kura mnyika hili ni kundi kubwa sana la vijana waliomaliza chuo hivi karibuni ambao wameajiliwa hapa UDOM, ilikuwa ni uzalendo wa hali ya juu sana kufanikisha hili na pasipo malipo yoyote zaidi ya kupigania haki ya WATANZANIA.

Hivyo basi kutokana na hoja hizo nane tumebaini kabisa ya kwamba Wana CHAADEMA tupo wengi sana na hivyo tunahitaji sehemu yetu itakayotuunganisha na kutupatia nafasi ya kujadiliana mambo yetu, tawi hili litakuwa kiungo muhimu kati ya Walimu, wanafunzi na wafanyakazi wengine waendeshaji.​

RAI YETU
Rai yetu kwenu ni juu ya kuhitaji kuungwa mkono katika mchakato huu, si uhitaji wa mali bali hasa mchango wa mawazo na ushauri kwani ni suala nyeti na ambalo halitawafurahisha wengi lakini tumeamua kufanya haya si kwa kushawishiwa na uongozi wa juu au wa mkoa wa CHADEMA.​

Pia kwa Wana CHADEMA wenzetu tunaomba tusaidiane klupambana na propaganda mbaya inayojaribu kuaminisha watanzania wote kwamba wafanyakazi na wanafunzi wote wa Udom ni CCM, ninajua wengine mnafanya hivyo kwa hasira baada ya kuzidiwa na nguvu ya propaganda na wengine ni kutokana na kukosa taarifa sahihi.​

Tunatambua kwamba CCM wanawagawia kadi wanafunzi hadi mabwenini tena kwa kuwaandika majina pasipo ridhaa yao na kuwaomba wawape picha passport size wawaletee kadi.
Pia wameweka viongozi wao wa matawi katika mabweni, licha ya jitihada hizi wanazozifanya bado upinzani una nguvu kubwa kwani wanafunzi wanaelewa nini ccm inafanya, na wale wachache wanaojiunga na ccm hapa chuoni ni kutokana na mtazamo potofu wa kudhani kwamba mtu hawezi kuajiriwa mpaka uwe na kadi ya CCM.​

Mtazamo huu tumepambana nao sana tena kwa kutoa mifano tukionesha watu walioamini hivyo huku mpaka wakati huu hali zao bado ni mbaya sana.​

Kimsingi huu ni mtazamo potofu amabao unawatafuna baadhi ya wasomi wetu katika vyuo vingi na hao ndio wanakuja kuwa watu kama Benson Bana kwani hata anavyoongea amejaa kujipendekeza zaidi ili akumbukwe, nadhani mlimuona jana kwenye kipima joto ITV,alivyokuwa anajikanyaga kuonesha namna ambavyo watanzania wana hali nzuri mpaka kufikia uwezo wa kuendesha magari.​

Ninaomba msitishwe na matamko yanayotolewa na baadhi ya watu yakihusisha sisi UDOM, mengine ni propaganda za ccm, mengine ni ya kutungwa na vijana wa CCM ambao wanasoma hapa na hata makao makuu CCM wanafahamu kwamba wapo hapa, hivyo basi ni lazima waoneshe kwamba wanafanya kazi kubwa.​

CHADEMA itaendelea kustawi hapa Udom hata kama viongozi wa ngazi ya juu wangefanya nini.​

Mungu ibariki CHADEMA , Mungu ibariki Tanzania na Viongozi wote wa CHADEMA​

umetumia vigezo ambavyo kisomi havikubaliki, wot im sayin is, wazo mlilo nalo ni zuri, but next tym unapotaka kupresent idea yako, iweke kisomi zaid, huwezi sema mabishano ya kwenye mabasi ni fact ya kukuonesha nyie ni wanaharakati, mlikua wapi kipindi kile moja ya kikundi cha wanafunzi wa Udom walivyokua wanaikashifu Chadema na dr. slaa, au hata kuponda kile kitendo cha kutoka bungeni,, anyway this no time for lawama, i gues my point umeinasa, wishin you luck in bringing devpt to dis rich poor country.........................
 
Safiiiiiii!! Hii nimeipenda sana, binafsi nilikuwa siamini propaganda za ccm kuwa udom wana wanchama wengi.Ni wazi, hakuna mwenye akili timamu akawa mwanachama wa ccm unless otherwise awe kibaraka wa mafisadi, na hao vibaraka ndio hatuwataki kabisa hao ni hatari zaid ya ukoma hao.uarabuni hao adhabu yao ni kitanzi tu!

HONGERENI SANA VIJANA, MKIPANGA TAREHE RAISMI MTUJURISHE TUJE KUWAPA SUPPORT!! BIH UP KUBWA!!
 
Back
Top Bottom