hivi karibuni, serikali ililifungia gazeti la mwanahalisi kwa madai ya 'kuhatarisha' usalama wa taifa. Uamuzi huo wa serikali kuwafungia mwanahalisi wawezakuwa na maana kwa maana halisi ya kuhatarisha uslama wa taifa.
Lakini mwenye akili lazima ajiulize swali hili; je, ni mwanahalisi pekee ndilo 'linalohatarisha' usalama wa taifa?
Hii radio imaan ambayo hurusha matangazo ya uchochezi wa dhahiri kwa waislamu dhidi ya serikali na wakristo, hai-hatarishi usalama wa taifa?
Hivyo vyombo vinavyohusika na kufuatilia na kuthibiti vyombo vya habari ikiwamo wizara ya habari na tcra, ni kweli havijui kinachorushwa na kuhubiriwa na radio imaan?
Kama vyombo husika havijui kinachorushwa na kuhubiriwa na radio imaan na baadhi ya magazeti ya kidini basi ni wazi kuwa miaka michache ijayo tanzania itakuja kuwa na rais ambae ni mlemavu wa kusikia (kiziwi) na kuona (kipofu), rais wa aina hiyo, kwa kuwa haoni angetegemea kupata ushauri kutoka kwa washauri wake, lakini kwa kuwa hasikii basi hilo halitawezekana!
hapa naona unataja vyombo vya habari vya kiislam tu.lkn jua vikifungiwa na vyenu kamawapo fm vitajifunga wenyewe. Maana maandamano yakwanza yatafikia redio maria kuvifunga kwa nguvu