Wadau mnakumbuka kupigana siku ya kufunga shule enzi za mwalimu, ukigombana na mwenzio unamsubiri siku ya kufunga shule. Tukumbusha ulishawah kubondana siku kama hiyo.
hakyananani usinikumbushe mablia wakati niko vidudu( chekechea) kuna kijamaa kilinivizia na kunipiga ngwala na kukimbia to make things even worse kwao walihama so tulipofungua sikukaona... hakyanani nakatafuta mpaka leo ukimuona mwambie NIKIMKAMATA lazima nimrudishie ngwala kama ule alionipiga kimagendo.... alooo sisahau mpaka leo
Dah umenikumbusha mbali sana. Mie ndo nilikuwaga mgomvi namba moja wakishindwa kupigana lazima wanitafute nikifika tu wote wanashangilia ila kilichonitokea wakati niko darasa la 2 sitasahau nilimpiga msichana mmoja mpaka leo kuna kiungo hana yaani leo ugomvi sitaki tena hata unichokoze nakuangalia tu
vishadida vinachukua mchanga upute.. ukiputa unaambiwa ulipe ng'ombe hapo hata kama jamaa umuwezi bac unabidi ujitutumue... kumbuka sheria (sio rasmi) ilikuwa ukitolewa nundu au damu umeshindwa... mashuhuda wataingilia ugomvi huku wakishangilia "katolewa nundu" hapo ukitaka kuendelea na ugomvi unaonekana mkorofi... duh!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.