Kufanikiwa Maandamano ya CDM ni kufeli kwa Mkakati wa CCM Bungeni

Ibrah

JF-Expert Member
Mar 22, 2007
2,729
528
Katika Bunge lililopita, CCM kwa makusudi na kimkakati kwa kushirikiana na Chama Tawala Kishiriki Zanzibar yaani CUF kwa kuwatia mfukoni NCCR na John Cheyo walikukihujumu Chama Kikuu cha Upinzania Tanzania CHADEMA kwa kuja na tafsiri mpya ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambayo ilibuniwa na CUF na kusimamiwa kikamilifu na Spika wa Bunge na Naibu wake John Ndugai kufanikisha hujuma dhidi ya Demokrasia kwa kuwalazimisha CHADEMA kufunga ndoa ya mkeka na Vyama vingine vya upinzani.

Tundu Lisu au Tundi Lisu kama inavyotamkwa na Spika Makinda alisema waziwazi kuwa sheria za Tanzania zinaruhusu ndoa ya wake wengi, lakini haitambui ndoa ya waume wengi akimaanisha kuwa CUF haiwezi kuolewa na CCM kule Zanzibar na papo hapo kuwa na ndoa nyingine na CHADEMA.

Tafsiri mpya ya Kambi rasmi iliyoasisiwa na CUF na kuthibitishwa na CCM kwa kungwa mkono na Cheyo, Mrema na NCCR ililenga kuvunja nguvu ya CHADEMA Bungeni na nchini kwa ujumla. Sote tunakumbuka hoja ya Hamad Rashid wakati akichangia tafsiri mpya ya Kambi Rasmi ya Upinzani jinsi ilivyochochea malumbano baina ya CHADEMA dhidi ya CCM na Vyama vingine vya Upinzani. Hata pale Mh. Lisu alipomuomba Spika amuamuru Hamad Rashid kufuta maneno ya kuudhi; kwa unafiki wa hali ya juu Spika Makinda alimtaka Hamad Rashid afute kauli yake lakini Spika pasi aibu wala woga na kwa kutumia madaraka yake vibaya akabandika neno lake lakini message sent, kauli ambayo iliongeza munkari kwa wachangiaji waliofuata na kugeuza Bunge kuwa sehemu ya kashfa na matusi na kuanika udhaifu mkubwa wa kiuongozi wa Spika Makinda kwa kubali kuwa sehemu ya malumbano yale. Wengi tunakubali kuwa ule ulikuwa mkakati wa kuimaliza CDM ambao waliamua kutoka nje kuonyesha kutokubaliana na tafsri mpya ya Kambi rasmi ya upinzania iliyokuwa njiani.

KURUHUSIWA KWA MAANDAMANO YA CHADEMA KANDA YA ZIWA NA KUFELI KWA MKAKATI WA CCM NA 'WAPINZANI' VIBARAKA


Bila shaka Wadau mtakubaliana nami kuwa wa uzoefu wa upinzani hapa nchini huwa si rahisi Vyama vya upinzani kuruhusiwa kirahisi kufanya maandamano. Rejea maandamano ya rasimu ya Katiba ya CUF Dar na Maandamano ya CHADEMA Arusha.

Kwa hiyo naamini kabisa kuwa kuruhusiwa kirahisi kwa CHADEMA kufanya Maandamano kule Mwanza na Musoma bila Polisi kuleta sababu za 'kiintelejensia' za kuzuia Maandamano hayo ni mbinu ya CCM na Serikali yake kupima kama Mkakati wao wa Kifisadi dhidi ya CHADEMA Bungeni ulifanikiwa au la.

Maandamano ya Kihistoria ya CHADEMA Mwanza na Musoma yamethibitisha kuwa kinyume kabisa na matarajio ya CCM na CUF. Watanzania ndio kwanza wamezidi kuonyesha kuiunga mkono CHADEMA na kuwaonyesha CCM kuwa WAtanzania sasa wamegundua michezo michafu ya CCM na wanasonga mbele kwa kuonyesha imani ya hali ya juu kwa CHADEMA.

Naamini hili laweza kuwatia kiwewe CCM na huenda wakaanza tena kuitumia Polisi kuleta sababu za 'kiintelejensia' ili kuwazuia CHADEMA kuandamana. Nawaambia wasijaribu kucheza na nguvu ya umma!

OMBI LANGU KWA CHADEMA
Mimi nasuburi maandamno mengine ya CHADEMA Arusha na nawashauri waje tena na maandamano yale yale ya kupinga mchezo mchafu uliofanywa na CCM na Serikali kutusimamishia Meya bila kushrikisha Vyama vingine, kupinga DUWANZI na Kupanda gharama za umeme na maisha kwa ujumla. Arusha hapatatosha na Maandamano ya Mwanza yatakuwa chamtoto!
 
kamanda uyasemayo hapa yote yanatija, CCM waliweka mtego usiyo kuwa na malengo, ila kufanikiwa kwa CHADEMA ni salamu kwa ccm kuanza kujiuliza walipo toka walipo na wanapo kwenda sasa
 
Hayo uliyo sema ni kweli kabisa mkuu, nakumbuka Maria Hewa (MB) alisema bungeni kuwa watu wa Mwanza walikosea wakaati wa uchaguzi kuchagua, Maandamano hayo pia yatakuwa majibu kwa mbunge huyo wa viti maalumu kuwa Mwanza hawakukosea/hawajakosea bali walitimiza wajibu na wamemuonesha kuwa aliyosema bungeni ni pumba tu hawayajali. HONGERENI WANA WA MWANZA KEEP IT UP! Mpaka tuwazibe sehemu za kupumulia hao sisiem (Jiji njemu)
 
CCM wanajaribu kutumia kila intelijensia iliyopo kuyazodoa maandamano ya CDM na kuwarrubuni baadhi ya watu kuwa ni kupoteza muda.

Lakini kama wangalikuwa na UFAHAMU wasingelala juu ya kitu kinachofanyika sasa hivi ndani ya CDM...Hakuna siku inayopita bila cdm kutajwa kwenye Media, na picha kuonyeshwa, huku neno CCM likizidi kuyoyoma na kudharaulika machoni mwa watu.

Hadhara niliyoionA kwenye maandamano pale MUSOMA leo nimepigwa na butwaa!...Nimeambiwa na Mheshimiwa Mbunge mmoja wa CDM ambaye yupo kwenye kazi hii maalum, kuwa ameshuhudia wafanyakazi wakiacha ofisi zao wazi na kuungana msafara ili watembee japo kilomita moja, na kisha kurudi maofisini kwao...si jambo la mzaha hata kidogo.

Lau kama hawa ccm wangelikuwa na jicho la 3, wangeliona kuwa HUJUMA zote wanazofanya Bungeni dhidi ya cdm ni mfano wa petroli inayomwagwa juu ya moto...na bahati mbaya vyombo vingi vya habari viliweka wazi kuwa Mama Anna Makinda ni zao la kifisadi, hivyo hata kama ataongea ukweli gani, lazima upande wa pili wahoji mno.
 
Trust me,....
kwa sasa hivi hakuna sehemu wata zuia maandamano na wafanye kama Arusha kule.

Macho ya dunia nzima yako Africa,Jk na serikali yake hawataki kuonekana kuwa wananyima wananchi haki ya kukusanyika au kuandamana!
Wanajua/walijua kabisa kwamba wange zuia maandamano kule mwanza nk basi chadema wangefanya kwa kulazimisha, na kama wangetumia nguvu kama kule Arusha tena (kwa sasa hivi) naamini unge msikia Ban kin moon akikemea mauaji Tanzania!

Kwa sababu hiyo basi,viongozi wetu ambao ni watalii katika dunia hii,hawataki kujichafulia muonekano wao kwa wakubwa (UN)
 
CHANGAMOTO!

Lets think of post CCM Tanzania,

CCM ni tatizo japo si tatizo pekee, kuna mambo sharti tuanze kuyatazama ili tusije kuiondoa CCM lakini matatizo ya ufisadi na kutokuwajibika yakabaki pale pale.
 
good idea.japo hata kama chama tawala kitakachofuatia kitaendeleza kutokuwajibika nao tutawatoa!sisi watz wa kawaida tunataka kuona maendeleo na tija kwenye maisha ya kila siku!hata waje ccu ama ccp,wakileta longolongo tupa kulee!then wanasiasa watajifunza kuwajibika automatically.
<p>
CHANGAMOTO!</p>
<p>&nbsp;</p>
<p>Lets think of post CCM Tanzania, </p>
<p>&nbsp;</p>
<p>CCM ni tatizo japo si tatizo pekee, kuna mambo sharti tuanze kuyatazama ili tusije kuiondoa CCM lakini matatizo ya ufisadi na kutokuwajibika yakabaki pale pale.
</p>
<p>&nbsp;</p>
 
maandamano ya jana mbeya ilikuwa ishara tosha ya wananchi kuchoshwa na magamba!tukifanikiwa kupata tume huru ya uchaguzi tutatambua tatizo liko wapi.kama ni uelewa wa wananchi (ili waeleweshwe) ama kama kuna majini yanayokula kura (kama alivyowahi kulalamika mzee wa mapesa)
 
Thats just the beginning,nia yetu ni mpaka kieleweke!wajua hakuna serikali dhalimu na yenye kuika haki za binadamu km ya ccm haiwezi kubali maandamano ambayo yanafanywa na umma,ndo maana nguvu nyingi zinatumika,eg hapa Arachuga,lakin msimamo wetu kama wana cdm uko palepale,kuwaelimisha jamii kwakutumia mikutano ya hadhara!mwanzo mwisho mpaka kieleweke!CDM TWANGA KOTEKOTE
 
Yote nimeyakubali. Ila mleta mada umenkumbusha kitu hapa,ivi chama kilichokuwa kinaitwa CUF kilienda wapi? Mara ya mwisho nlimsikia mtatiro kwenye kongamano la katiba udsm kisha kimya,au CUF walikuwa na hoja moja katiba? Jaman mitaani wamesahaulika wamebaki kwenye media!
 
Peoplesss Powerrrrr!!!!wakubali wakatae Chadema itasonga mbele tu.Ktk kikao cha Bunge kilichopita wakati Tindu Lisu anawasilisha mapendekezo ya baadhi ya vipengele ndani ya mahakama zetu alisema"msiniangalie mimi Kama Tindu Lisu au Kama Chadema bali changieni kwa faida ya Watanzania wote"lkn wabunge wa magamba kwa upeo wao mfupi wa akili pmj na kujali matumbo yao(njaa)hawakukubaliana na chochote.Binafsi nilitamani kuwa mchawi niwaue wabunge wote wa ccm kwa kushabikia ujinga(kuweka maslahi yao mbele)Viva Chadema na 2015 wale wote waliohujumu uchumi wa Watanzania wataenda kuanzisha timu ya mpira magereza
 
Ccm na anguko kuu............sasa wakati ni huu wa kuinyanyasa ccm na ccm-b
 
Kdogo jana kwenye taharifa ya habari ITV saa3:30 usiku waliirusha maandamano ya Mby ,duh! Kama ccm hawajuhi kufa basi mda wao umejiri, wakaangalie wenyewe wanachowafanya CDM ni kufuru kwa wenye ngozi za magamba

nilifurahi sana,wanambeya wako mguu kwa mguu na Cdm kila kona ya mji,twanga KoTeKoTe jamani 2015 haiko mbali,CCM walitubip sasa hv tunawapigia wanaingia uvunguni,na CDM daima hatuna gia ya rivasi katika hili mpaka2015 tutakapoingia magogoni,PIIPOOOOOOOOOOOOOOOOO
 
Katika Bunge lililopita, CCM kwa makusudi na kimkakati kwa kushirikiana na Chama Tawala Kishiriki Zanzibar yaani CUF kwa kuwatia mfukoni NCCR na John Cheyo walikukihujumu Chama Kikuu cha Upinzania Tanzania CHADEMA kwa kuja na tafsiri mpya ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambayo ilibuniwa na CUF na kusimamiwa kikamilifu na Spika wa Bunge na Naibu wake John Ndugai kufanikisha hujuma dhidi ya Demokrasia kwa kuwalazimisha CHADEMA kufunga ndoa ya mkeka na Vyama vingine vya upinzani.

Tundu Lisu au Tundi Lisu kama inavyotamkwa na Spika Makinda alisema waziwazi kuwa sheria za Tanzania zinaruhusu ndoa ya wake wengi, lakini haitambui ndoa ya waume wengi akimaanisha kuwa CUF haiwezi kuolewa na CCM kule Zanzibar na papo hapo kuwa na ndoa nyingine na CHADEMA.

Tafsiri mpya ya Kambi rasmi iliyoasisiwa na CUF na kuthibitishwa na CCM kwa kungwa mkono na Cheyo, Mrema na NCCR ililenga kuvunja nguvu ya CHADEMA Bungeni na nchini kwa ujumla. Sote tunakumbuka hoja ya Hamad Rashid wakati akichangia tafsiri mpya ya Kambi Rasmi ya Upinzani jinsi ilivyochochea malumbano baina ya CHADEMA dhidi ya CCM na Vyama vingine vya Upinzani. Hata pale Mh. Lisu alipomuomba Spika amuamuru Hamad Rashid kufuta maneno ya kuudhi; kwa unafiki wa hali ya juu Spika Makinda alimtaka Hamad Rashid afute kauli yake lakini Spika pasi aibu wala woga na kwa kutumia madaraka yake vibaya akabandika neno lake lakini message sent, kauli ambayo iliongeza munkari kwa wachangiaji waliofuata na kugeuza Bunge kuwa sehemu ya kashfa na matusi na kuanika udhaifu mkubwa wa kiuongozi wa Spika Makinda kwa kubali kuwa sehemu ya malumbano yale. Wengi tunakubali kuwa ule ulikuwa mkakati wa kuimaliza CDM ambao waliamua kutoka nje kuonyesha kutokubaliana na tafsri mpya ya Kambi rasmi ya upinzania iliyokuwa njiani.

KURUHUSIWA KWA MAANDAMANO YA CHADEMA KANDA YA ZIWA NA KUFELI KWA MKAKATI WA CCM NA 'WAPINZANI' VIBARAKA


Bila shaka Wadau mtakubaliana nami kuwa wa uzoefu wa upinzani hapa nchini huwa si rahisi Vyama vya upinzani kuruhusiwa kirahisi kufanya maandamano. Rejea maandamano ya rasimu ya Katiba ya CUF Dar na Maandamano ya CHADEMA Arusha.

Kwa hiyo naamini kabisa kuwa kuruhusiwa kirahisi kwa CHADEMA kufanya Maandamano kule Mwanza na Musoma bila Polisi kuleta sababu za 'kiintelejensia' za kuzuia Maandamano hayo ni mbinu ya CCM na Serikali yake kupima kama Mkakati wao wa Kifisadi dhidi ya CHADEMA Bungeni ulifanikiwa au la.

Maandamano ya Kihistoria ya CHADEMA Mwanza na Musoma yamethibitisha kuwa kinyume kabisa na matarajio ya CCM na CUF. Watanzania ndio kwanza wamezidi kuonyesha kuiunga mkono CHADEMA na kuwaonyesha CCM kuwa WAtanzania sasa wamegundua michezo michafu ya CCM na wanasonga mbele kwa kuonyesha imani ya hali ya juu kwa CHADEMA.

Naamini hili laweza kuwatia kiwewe CCM na huenda wakaanza tena kuitumia Polisi kuleta sababu za 'kiintelejensia' ili kuwazuia CHADEMA kuandamana. Nawaambia wasijaribu kucheza na nguvu ya umma!

OMBI LANGU KWA CHADEMA
Mimi nasuburi maandamno mengine ya CHADEMA Arusha na nawashauri waje tena na maandamano yale yale ya kupinga mchezo mchafu uliofanywa na CCM na Serikali kutusimamishia Meya bila kushrikisha Vyama vingine, kupinga DUWANZI na Kupanda gharama za umeme na maisha kwa ujumla. Arusha hapatatosha na Maandamano ya Mwanza yatakuwa chamtoto!

Hebu nikumbushe wenyeviti wa kamati za bunge za hesabu za serikali za mitaa, na serikali kuu ni wakina nani vile ?
 
Kdogo jana kwenye taharifa ya habari ITV saa3:30 usiku waliirusha maandamano ya Mby ,duh! Kama ccm hawajuhi kufa basi mda wao umejiri, wakaangalie wenyewe wanachowafanya CDM ni kufuru kwa wenye ngozi za magamba

nilifurahi sana,wanambeya wako mguu kwa mguu na Cdm kila kona ya mji,twanga KoTeKoTe jamani 2015 haiko mbali,CCM walitubip sasa hv tunawapigia wanaingia uvunguni,na CDM daima hatuna gia ya rivasi katika hili mpaka2015 tutakapoingia magogoni,PIIPOOOOOOOOOOOOOOOOO

Wingi wa watu sio upigaji kura , rejea ya Mrema nk ! wengi hawajajiandikisha sasa sijui watapigaje kura
 
Back
Top Bottom