Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Katika Bunge lililopita, CCM kwa makusudi na kimkakati kwa kushirikiana na Chama Tawala Kishiriki Zanzibar yaani CUF kwa kuwatia mfukoni NCCR na John Cheyo walikukihujumu Chama Kikuu cha Upinzania Tanzania CHADEMA kwa kuja na tafsiri mpya ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambayo ilibuniwa na CUF na kusimamiwa kikamilifu na Spika wa Bunge na Naibu wake John Ndugai kufanikisha hujuma dhidi ya Demokrasia kwa kuwalazimisha CHADEMA kufunga ndoa ya mkeka na Vyama vingine vya upinzani.
Tundu Lisu au Tundi Lisu kama inavyotamkwa na Spika Makinda alisema waziwazi kuwa sheria za Tanzania zinaruhusu ndoa ya wake wengi, lakini haitambui ndoa ya waume wengi akimaanisha kuwa CUF haiwezi kuolewa na CCM kule Zanzibar na papo hapo kuwa na ndoa nyingine na CHADEMA.
Tafsiri mpya ya Kambi rasmi iliyoasisiwa na CUF na kuthibitishwa na CCM kwa kungwa mkono na Cheyo, Mrema na NCCR ililenga kuvunja nguvu ya CHADEMA Bungeni na nchini kwa ujumla. Sote tunakumbuka hoja ya Hamad Rashid wakati akichangia tafsiri mpya ya Kambi Rasmi ya Upinzani jinsi ilivyochochea malumbano baina ya CHADEMA dhidi ya CCM na Vyama vingine vya Upinzani. Hata pale Mh. Lisu alipomuomba Spika amuamuru Hamad Rashid kufuta maneno ya kuudhi; kwa unafiki wa hali ya juu Spika Makinda alimtaka Hamad Rashid afute kauli yake lakini Spika pasi aibu wala woga na kwa kutumia madaraka yake vibaya akabandika neno lake lakini message sent, kauli ambayo iliongeza munkari kwa wachangiaji waliofuata na kugeuza Bunge kuwa sehemu ya kashfa na matusi na kuanika udhaifu mkubwa wa kiuongozi wa Spika Makinda kwa kubali kuwa sehemu ya malumbano yale. Wengi tunakubali kuwa ule ulikuwa mkakati wa kuimaliza CDM ambao waliamua kutoka nje kuonyesha kutokubaliana na tafsri mpya ya Kambi rasmi ya upinzania iliyokuwa njiani.
KURUHUSIWA KWA MAANDAMANO YA CHADEMA KANDA YA ZIWA NA KUFELI KWA MKAKATI WA CCM NA 'WAPINZANI' VIBARAKA
Bila shaka Wadau mtakubaliana nami kuwa wa uzoefu wa upinzani hapa nchini huwa si rahisi Vyama vya upinzani kuruhusiwa kirahisi kufanya maandamano. Rejea maandamano ya rasimu ya Katiba ya CUF Dar na Maandamano ya CHADEMA Arusha.
Kwa hiyo naamini kabisa kuwa kuruhusiwa kirahisi kwa CHADEMA kufanya Maandamano kule Mwanza na Musoma bila Polisi kuleta sababu za 'kiintelejensia' za kuzuia Maandamano hayo ni mbinu ya CCM na Serikali yake kupima kama Mkakati wao wa Kifisadi dhidi ya CHADEMA Bungeni ulifanikiwa au la.
Maandamano ya Kihistoria ya CHADEMA Mwanza na Musoma yamethibitisha kuwa kinyume kabisa na matarajio ya CCM na CUF. Watanzania ndio kwanza wamezidi kuonyesha kuiunga mkono CHADEMA na kuwaonyesha CCM kuwa WAtanzania sasa wamegundua michezo michafu ya CCM na wanasonga mbele kwa kuonyesha imani ya hali ya juu kwa CHADEMA.
Naamini hili laweza kuwatia kiwewe CCM na huenda wakaanza tena kuitumia Polisi kuleta sababu za 'kiintelejensia' ili kuwazuia CHADEMA kuandamana. Nawaambia wasijaribu kucheza na nguvu ya umma!
OMBI LANGU KWA CHADEMA
Mimi nasuburi maandamno mengine ya CHADEMA Arusha na nawashauri waje tena na maandamano yale yale ya kupinga mchezo mchafu uliofanywa na CCM na Serikali kutusimamishia Meya bila kushrikisha Vyama vingine, kupinga DUWANZI na Kupanda gharama za umeme na maisha kwa ujumla. Arusha hapatatosha na Maandamano ya Mwanza yatakuwa chamtoto!
Tundu Lisu au Tundi Lisu kama inavyotamkwa na Spika Makinda alisema waziwazi kuwa sheria za Tanzania zinaruhusu ndoa ya wake wengi, lakini haitambui ndoa ya waume wengi akimaanisha kuwa CUF haiwezi kuolewa na CCM kule Zanzibar na papo hapo kuwa na ndoa nyingine na CHADEMA.
Tafsiri mpya ya Kambi rasmi iliyoasisiwa na CUF na kuthibitishwa na CCM kwa kungwa mkono na Cheyo, Mrema na NCCR ililenga kuvunja nguvu ya CHADEMA Bungeni na nchini kwa ujumla. Sote tunakumbuka hoja ya Hamad Rashid wakati akichangia tafsiri mpya ya Kambi Rasmi ya Upinzani jinsi ilivyochochea malumbano baina ya CHADEMA dhidi ya CCM na Vyama vingine vya Upinzani. Hata pale Mh. Lisu alipomuomba Spika amuamuru Hamad Rashid kufuta maneno ya kuudhi; kwa unafiki wa hali ya juu Spika Makinda alimtaka Hamad Rashid afute kauli yake lakini Spika pasi aibu wala woga na kwa kutumia madaraka yake vibaya akabandika neno lake lakini message sent, kauli ambayo iliongeza munkari kwa wachangiaji waliofuata na kugeuza Bunge kuwa sehemu ya kashfa na matusi na kuanika udhaifu mkubwa wa kiuongozi wa Spika Makinda kwa kubali kuwa sehemu ya malumbano yale. Wengi tunakubali kuwa ule ulikuwa mkakati wa kuimaliza CDM ambao waliamua kutoka nje kuonyesha kutokubaliana na tafsri mpya ya Kambi rasmi ya upinzania iliyokuwa njiani.
KURUHUSIWA KWA MAANDAMANO YA CHADEMA KANDA YA ZIWA NA KUFELI KWA MKAKATI WA CCM NA 'WAPINZANI' VIBARAKA
Bila shaka Wadau mtakubaliana nami kuwa wa uzoefu wa upinzani hapa nchini huwa si rahisi Vyama vya upinzani kuruhusiwa kirahisi kufanya maandamano. Rejea maandamano ya rasimu ya Katiba ya CUF Dar na Maandamano ya CHADEMA Arusha.
Kwa hiyo naamini kabisa kuwa kuruhusiwa kirahisi kwa CHADEMA kufanya Maandamano kule Mwanza na Musoma bila Polisi kuleta sababu za 'kiintelejensia' za kuzuia Maandamano hayo ni mbinu ya CCM na Serikali yake kupima kama Mkakati wao wa Kifisadi dhidi ya CHADEMA Bungeni ulifanikiwa au la.
Maandamano ya Kihistoria ya CHADEMA Mwanza na Musoma yamethibitisha kuwa kinyume kabisa na matarajio ya CCM na CUF. Watanzania ndio kwanza wamezidi kuonyesha kuiunga mkono CHADEMA na kuwaonyesha CCM kuwa WAtanzania sasa wamegundua michezo michafu ya CCM na wanasonga mbele kwa kuonyesha imani ya hali ya juu kwa CHADEMA.
Naamini hili laweza kuwatia kiwewe CCM na huenda wakaanza tena kuitumia Polisi kuleta sababu za 'kiintelejensia' ili kuwazuia CHADEMA kuandamana. Nawaambia wasijaribu kucheza na nguvu ya umma!
OMBI LANGU KWA CHADEMA
Mimi nasuburi maandamno mengine ya CHADEMA Arusha na nawashauri waje tena na maandamano yale yale ya kupinga mchezo mchafu uliofanywa na CCM na Serikali kutusimamishia Meya bila kushrikisha Vyama vingine, kupinga DUWANZI na Kupanda gharama za umeme na maisha kwa ujumla. Arusha hapatatosha na Maandamano ya Mwanza yatakuwa chamtoto!