Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Jeshi la Wananchi lipo nyuma ya harakati za Kikwete, ila hatima ya harakati zao ni kuipasua nchi vipande vipande, maana wako makamanda wanaoiunga mkono CHADEMA, waache wacheza na moto, waache wanasiasa wacheze siasa zao.
najua watu wanalinda vitumbua vyao, Tanzania haina viashiria vya uvunjifu amani ambavyo POLICE wameshindwa kutatua kiasi cha JWTZ KUONA HAJA YA KUTOA tAMKO. hatari iko mbele.
Ni huu ni mkakati maalumu wa kutaka wapinzani waonekane kama wachokozi, wachochezi.
Kama ulimwangalia yule kamanda wa JWTZ wakati anatoa lile onyo, alikuwa na ile gulity concious, alikuwa hawatazami wasikilizaji wake machoni. Ni pale tu alipokuwa anaongelea vyombo vya habari ndipo aliwatazama wasikilizaji. Vitu vya kizushi utavitambua tu, naamini yeye mwenyewe alijua na kuamini kuwa aliyokuwa anayasema hayakuwa ya kweli bali alikuwa anatumika na kikundi cha wanasiasa kuvuruga uchaguzi... WATASHINDWA!