Kuelekea uchaguzi arumeru : Pengo la regia mtema laonekana kwa uhalisia hapa jf....

only83

JF-Expert Member
Oct 15, 2010
5,343
2,525
...Tangu harakati za kuwania kiti cha ubunge katika jimbo la Arumeru-Mashariki kuanza,kumekuwa na kila aina ya njia za kuhakikisha kuwa vyama vinavyoliwania jimbo hilo vinalipata.Njia hizo zimekuwa ni njema,na nyingine ni za kuchafuana hasa hapa JF..kumekuwa na watu wanaoanzisha hoja ambazo zinaonekana ni nia ya wazi ya kuhakikisha wanaanzisha mgogoro dhidi ya wana-CDM na uongozi au wanachama wenyewe kwa wenyewe...Nimekuwa nahuzunika kwasababu tunakosa mtu wa kutupa ukweli toka jikoni(Yaani ndani ya chama chetu)..Hali hii imenifanya nimkumbuke Dada Regia,kwa kweli alikuwa kama msemaji wa CDM hapa JF..hizi hoja nyepesi zingekuwa zimejibiwa zote.

...Lakini nadhani tutazimiss update wakati wa kampeni,sidhani kama tumepata mwana-CDM makini wakuweza kutupatia updates za ukweli kwenye chaguzi zetu kama ambavyo alikuwa anafanya Regia..Kwa hili nasema tumeanza kuliona pengo kwa uhalisia dada Regia...

NB:

Familia ya Dr Estelatus Mtema inapenda kuwakaribisha ndugu jamaa na marafiki zao wote kwenye kumalizia msiba(Arobaini) ya mpendwa wetu Regia Estelatus Mtema,itakayofanyika nyumbani kwao ifakara siku ya tarehe 3/3/2012.
Karibuni Sana

[h=6][/h]
 
Back
Top Bottom