Semilong
JF-Expert Member
- Mar 5, 2009
- 1,712
- 219
sasa haya ndiyo yaliyosemwa kwenye mkutanoKama mwana JF nadhani nina jukumu la kuwaletea habari za yaliyojiri kwenye huu mkutano mkuu wa ccm uliomalizika takriban dk 90 zilizopita.
Mgeni rasmi alikuwa Mweka Hazina wa CCM, Amas Makalla.
Wanachama na wapenzi wa CCM waliohudhuria walikuwa kati ya 200 - 300
Mengi yalizungumzwa ikiwa ni pamoja na maendeleo ya Tawi la CCM Uingereza hadi hali ya kisiasa Tanzania.
Maswali yaliulizwa ya mchanganyiko, kuhusu Muungano, Ufisadi, Matatizo ya Arthi, Lengo la CCM Uingereza n.k
My Take: CCM wako Serious katika kujenga hili Tawi na Matawi mengine nje ya Tanzania, kwa wale ambao bado wanaona watafanikiwa kwa kubeza juhudi hizi za CCM nawapa pole. CCM wamejizatiti na kadri wana JF wanavyoendelea kubeza ndivyo Chama kinavyojichimbia mizizi vijijini na sasa nje ya Tanzania. Chama cha Mapinduzi kinajenga viongozi wa kesho kuanzia huku walipo.
Kila la kheri.
kazi kweli kweli