Wakubwa wana wa JF,Nilikua nafuatilia issue moja hapo TAKUKURU wiki chache zilizopita na kuna wakati nilizuiliwa kwenda hapokwa kisingizio kuna mkutano ullikua unaendelea hivyo hawaruhusu wageni. Mimi nilikua nafuatilia "mambo yangu".Ila baadae nilikuja kupata habari kwamba hakukuwa na mkutano wowote ila kulikua na uchinguzi unaendelea kwa sababukuna watu walivunja/waliingia ndani/ walitaka kuchoma moto au walichoma moto na kuiba baadhi ya nyaraka MUHIMU sanahivyo wengi wa wafanyaazi walipewa likizo ya dharura kupisha uchunguzi kufanyika.Nimefuatilia sana suala hilo nimegonga mwamba kupata ukweli nini kimetokea. Ukweli niliopata ni mmoja tu kwamba ni kwelikuna tukio lililotokea na baadhi au asilimia kubwa ya wafanyakazi walizuiliwa kuingia ofisini.Je usallama wa watoa taarifa uko wapi????? je mbona umma haukujulishwa kuhusiana na hujuma hiyo????Je ni nyaraka zipi MUHIMU zilizopotea au kuharibiwa?????? Je kuna suspect waliokamatwa??Nawasilisha hija