Kuchangia au kutokuchangia? Hilo ndilo swali..

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
changiaCCM2010-2.PNG
Siyo swali gumu na wala siyo swali la mtego hata kidogo Jibu lake ni rahisi kweli kwani halihitaji uwe msomi wa elimu ya anga za mbali au uliyebobea katika sayansi ya Fizikia ya Nyota kuweza kutoa jibu lake. Ni swali ambalo kila mwana CCM anatakiwa awe na jibu lake na kila Mtanzania kuamua vile vile kulijibu.

Mwishoni mwa juma Rais Kikwete alizindua utaratibu wa kuchangia Chama cha Mapinduzi ili kiweze kushiriki vizuri uchaguzi mkuu na kushinda ili iweze kuongoza taifa letu kwa miaka mingine mitano. Katika uzinduzi huo lengo lao ni kuweza kukusanya kiasi cha shilingi Bilioni 40 ili kuweza kutimiza malengo mbalimbali ambayo yatafanikisha lengo hilo la kufanya vizuri kwenye Uchaguzi. Fedha hizi zikishakusanywa zitatumika:

- Kununua magari 60 kwa ajili ya kampeni
- Kununua pikipiki 170
- Baskeli 23,000
- Kukodi helikopta na ndege
- Matumizi mbalimbali ya makabrasha ya kampeni na uchaguzi

Ili kuweza kuchangia kwa njia ya simu mwana CCM au Mtanzania anayekiunga mkono Chama cha Mapinduzi anatakiwa atume neno “CCM” kwenda Namba 15377 ambapo atakuwa amechangia Shs 300, akituma neno “CCM” kwenda 15388 atakuwa amechangia Shs 500 na akituma neno “CCM” kwenda 15399 atakuwa amechangia Shs. 1000. Ni wazi kuwa CCM itatumia mbinu nyingine mbalimbali kuweza kufikia lengo hilo. Sasa tunajua ni kiasi gani kinahitajika, kitatumika vipi, na namna gani kuweza kuchangia. Baada ya kuyajua hayo hatuna budi kujiuliza kama tuchangie au tusichangie.

Kabla ya kuchangia jiulize!
Kwa vile najua watu wengi ambao ni mashabiki wa CCM watakuwa tayari kuchangia kwa sababu “Rais kasema” na kwa sababu wanataka chama chao kiendelee kutawala na wapo wengine ambao hawataki kusaidia upinzani ukomae na hivyo wako tayari kuunga mkono CCM basi nimeona ni vyema kujitolea kuwasaidia watu hawa ambao wana fedha na vitu mbalimbali ambavyo wako tayari kuviweka kwenye miguu ya CCM kujiuliza maswali kadhaa ambayo wakijibu ndiyo kwa yote mawili inawapasa watoe michango yao.
 

Attachments

  • kuchangiaaukutokuchangia.doc
    23 KB · Views: 131
Hivi kweli CCM inahitaji hayo magari na hizo pikipiki na hizo baiskeli? Kwani hawana hivyo vyombo vya kutosha?
 
"don't let them foool ya' or even try to school ya' "

SOURCE: marehem BOBU MALE.
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji

Kwanza nimeipenda hii na ningependa kutoa mchango wangu kama ifuatavyo

Hivi Mkulu alikuwa wapi kuongoza kampeni za kuchangia maafa ya watu wa Kilosa? Kama wana mpango wa kukusanya bilion 4.4 kutokana na SMS kulikuwa na haja gani ya kushirikisha Red alert, kutupotezea muda na matangazo yao ya Clouds? Hivi Mwanakijiji mlimpelekea ombi? Kutokana na hili naomba niongeze swali lingine hapo:

Kama Muungwana anaweza kukusanya pesa nyingi kiasi hiki kwanini alimwambia Gadafi wa Libya na kulialia kuwa bilion 15 ni nyingi kwa nchi masikini..si tungechanga tu!?

Mie naona kama wananchi wanaweza kuchangia mambo kama haya basi waaanze kujichangia mtaa kwa mtaaa na kuweka maendeleo kwa kila kata kuliko kuchangia kwa ajili ya kampeni ambazo hazitabadilisha maisha yao.

NB: Check PM mkuu
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji

Kwanza nimeipenda hii na ningependa kutoa mchango wangu kama ifuatavyo

Hivi Mkulu alikuwa wapi kuongoza kampeni za kuchangia maafa ya watu wa Kilosa? Kama wana mpango wa kukusanya bilion 4.4 kutokana na SMS kulikuwa na haja gani ya kushirikisha Red alert, kutupotezea muda na matangazo yao ya Clouds? Hivi Mwanakijiji mlimpelekea ombi? Kutokana na hili naomba niongeze swali lingine hapo:

Kama Muungwana anaweza kukusanya pesa nyingi kiasi hiki kwanini alimwambia Gadafi wa Libya na kulialia kuwa bilion 15 ni nyingi kwa nchi masikini..si tungechanga tu!?

Mie naona kama wananchi wanaweza kuchangia mambo kama haya basi waaanze kujichangia mtaa kwa mtaaa na kuweka maendeleo kwa kila kata kuliko kuchangia kwa ajili ya kampeni ambazo hazitabadilisha maisha yao.

NB: Check PM mkuu

Mkuu Gembe.. maswali yako haya ni mazito mno.. mtu akitaka kujaribu kuyajibu itakuwa ni kutafutana ugomvi

@Nyani, ukimuuliza mtu mwingine jibu litakuwa ni "hapana".. ukimuuliza mtu wa CCM jibu ni "ndiyo wanahitaji". Kumbuka kuwa jinsi walivyoweka ni kana kwamba chama hakina magari, usafiri n.k wanachofanya ni nyongeza tu.. halafu fikiria kila miaka mitano wananunua magari mapya.. hivi umewahi kusikia magari ya zamani ya CCM yakipigwa mnada.. au huwa yanaishia wapi?
 
Hivi kwani yale magari ya kihindi ya kijani ya kampeni 2005 yameishia wapi?
Kikwete needs a reality check, halafu eti yuko New york anapokea tuzo leo?
 
halafu fikiria kila miaka mitano wananunua magari mapya.. hivi umewahi kusikia magari ya zamani ya CCM yakipigwa mnada.. au huwa yanaishia wapi?

Si ndio hapo sasa! Maana mimi baada ya kusoma hilo tangazo nikajiuliza....hhmmm....hivi kweli hawa hawana hivyo vitu ama? Maana mwaka 2005 kulikuwa na uchaguzi....walitumia nini? Kama walikuwa na magari, pikipiki, na baiskeli....ina maana hawana tena hayo magari, hizo pikipiki na hizo baiskeli?

Halafu sielewi....wanahitaji hivyo vyomba vya usafiri kwa wagombea wapi? Raisi? wabunge? madiwani? au wote kwa ujumla? Hawa wabunge wetu si wana mashangingi hawa...kwa nini wasiyatumie magari waliyonayo tayari?

It's things like these that make me wanna pull hair.......grrrrrrrrrrr
 
Compaq

ukiichukia CCM itasadia?Ni sawa sawa na kumchukia kiziwi kuwa hakusikilizi..

I love politics coz inanifanya nijue tabia halisi za watu..
 
Bora wachangishane wenyewe wasiguse hela zetu za kodi au BoT.

Mi naona sawa tu maana hiki ni chama na wenye mapenzi nacho wachangie kama tunavyochangia harusi na misiba ya ndugu zetu. Cha msingi wasilete vifyatavyo;

1. Wasianzishe EPA mpya kwa ajili ya uchaguzi.
2. Wasilazimishe watu kwenye mashirika ya umma na vijijini kuchangia kwa lazima
3. Wasichote hela serikalini au hazina
4. Wasitumie magari au vyombo vingine vya Serikali kufanyia kampeni au kutumia muda wao kazini kufanya hivo badala ya ujenzi wa taifa
5. Waweke wazi at least kwa wanachama wao kiasi cha pesa walichopata na matumizi yake

Je vyama vingine navyo viseme wapi vinategemea kupata hela zao za kampeni ni vema vyote viwe wazi. Hii ni hatua nzuri kwa CCM tofauti na uchaguzi uliopita ambapo hawakusema walitoa wapi hela na baadae nyingine kupotea BoT (EPA???)
 
Hivi kwa nini huwa hatusikii miito ya kuchangia fedha za miradi ya maendeleo?

ukimuuliza atakujibu Miradi ya maendeleo inachangiwa na wahisani..

Mie hilo swali nimejiuliza sana..tena TV zote zioneshe hili la kuchangia maendeleo.Mie naona masuala ya maendeleo nayo yawe yanachangiwa kwa SMS na yapewe uzito ulelle kama huu alioutua Mkuu..

Sikujua kama Muungwana naye na blackberry na inakaa na yule jamaa mkubwa mkubwa..

ila nchi yetu bwana..mie huwa nashngaa..juzi niliwambia Mzee Mwanakijiji nimekata tamaa kabisa kuwarekebisha hawa watu ..sijui wana matatizo gani?
 
Bora wachangishane wenyewe wasiguse hela zetu za kodi au BoT.

Mi naona sawa tu maana hiki ni chama na wenye mapenzi nacho wachangie kama tunavyochangia harusi na misiba ya ndugu zetu. Cha msingi wasilete vifyatavyo;

1. Wasianzishe EPA mpya kwa ajili ya uchaguzi.
2. Wasilazimishe watu kwenye mashirika ya umma na vijijini kuchangia kwa lazima
3. Wasichote hela serikalini au hazina
4. Wasitumie magari au vyombo vingine vya Serikali kufanyia kampeni au kutumia muda wao kazini kufanya hivo badala ya ujenzi wa taifa
5. Waweke wazi at least kwa wanachama wao kiasi cha pesa walichopata na matumizi yake

Je vyama vingine navyo viseme wapi vinategemea kupata hela zao za kampeni ni vema vyote viwe wazi. Hii ni hatua nzuri kwa CCM tofauti na uchaguzi uliopita ambapo hawakusema walitoa wapi hela na baadae nyingine kupotea BoT (EPA???)

Wewe unaota..kuna mambo haujui ..EPA mbona ni ndogo..pesa za kampeni ?SMS hii si ni kwasababu ya sheria yetu mpya
 
attachment.php

Siyo swali gumu na wala siyo swali la mtego hata kidogo Jibu lake ni rahisi kweli kwani halihitaji uwe msomi wa elimu ya anga za mbali au uliyebobea katika sayansi ya Fizikia ya Nyota kuweza kutoa jibu lake. Ni swali ambalo kila mwana CCM anatakiwa awe na jibu lake na kila Mtanzania kuamua vile vile kulijibu.

Mwishoni mwa juma Rais Kikwete alizindua utaratibu wa kuchangia Chama cha Mapinduzi ili kiweze kushiriki vizuri uchaguzi mkuu na kushinda ili iweze kuongoza taifa letu kwa miaka mingine mitano. Katika uzinduzi huo lengo lao ni kuweza kukusanya kiasi cha shilingi Bilioni 40 ili kuweza kutimiza malengo mbalimbali ambayo yatafanikisha lengo hilo la kufanya vizuri kwenye Uchaguzi. Fedha hizi zikishakusanywa zitatumika:

- Kununua magari 60 kwa ajili ya kampeni
- Kununua pikipiki 170
- Baskeli 23,000
- Kukodi helikopta na ndege
- Matumizi mbalimbali ya makabrasha ya kampeni na uchaguzi

Ili kuweza kuchangia kwa njia ya simu mwana CCM au Mtanzania anayekiunga mkono Chama cha Mapinduzi anatakiwa atume neno “CCM” kwenda Namba 15377 ambapo atakuwa amechangia Shs 300, akituma neno “CCM” kwenda 15388 atakuwa amechangia Shs 500 na akituma neno “CCM” kwenda 15399 atakuwa amechangia Shs. 1000. Ni wazi kuwa CCM itatumia mbinu nyingine mbalimbali kuweza kufikia lengo hilo. Sasa tunajua ni kiasi gani kinahitajika, kitatumika vipi, na namna gani kuweza kuchangia. Baada ya kuyajua hayo hatuna budi kujiuliza kama tuchangie au tusichangie.

Kabla ya kuchangia jiulize!
Kwa vile najua watu wengi ambao ni mashabiki wa CCM watakuwa tayari kuchangia kwa sababu “Rais kasema” na kwa sababu wanataka chama chao kiendelee kutawala na wapo wengine ambao hawataki kusaidia upinzani ukomae na hivyo wako tayari kuunga mkono CCM basi nimeona ni vyema kujitolea kuwasaidia watu hawa ambao wana fedha na vitu mbalimbali ambavyo wako tayari kuviweka kwenye miguu ya CCM kujiuliza maswali kadhaa ambayo wakijibu ndiyo kwa yote mawili inawapasa watoe michango yao.


CCM wanaweweseka hiyo michango ni danganya toto ya kuingiza fweza haramu kutoka kwa makuwadi wao wa nje. Mimi nina uhakika kabisa huu ndio mwanzo na mwisho wa Chama Cha Majambazi. Haiingii akilini kuona wanashadidia michango kutoka kwa walipa kodi i-hali wanafahamu uwezo wa walipa kodi wa Tanzania na walio wengi vijijini ni mdogo sana . This country has gone to the dogs. God Bless us and remove this imbeciles from power through your long arm.
 
Sijawahi kuguswa na hoja yeyote kuhusu hili zoezi la kuchangia chama tawala kama nilivyoguswa na "waraka" wako mzee mwanakijiji. Hudhuni yangu ni kuwa wengi hawatapata nafasi ya kuusoma. Kama tu ingewezekana ukaupeleka hata Mwanahalisi ili wenzetu wasiopitia mitandao wapate wasaa wa mawazo haya ya msingi.

Kitu kingine kinachonigusa ni wenzetu walio vijijini ambao ni wengi kuliko sisi tuliobahatika kuishi kweny umeme na maji ya kutoka kweny mabomba. Kwani wamekuwa ni rahisi kwao kurubuniwa kimwelekeo na hasa kutokana na hali ngumu ya kimaisha. Natamani wao wapate nafasi ya kuupiti waraka huu,lakini kwa sasa ningeomba wana JF wanaoweza wasiusome tu bali tuutoe nakala na kuwapatia webgine.Ikumbukwe lengo si kupinga Utawala uliopo ila ni kuwapa nafasi watu kufanya maamuzi sawia baada ya kujiuliza maswali sawia....
 
Kama waki wahukumu mafisadi mie nitachangia,sema kwa vile hakuna dalili za kuwahukumu na mda ndio umefika wauchaguzi jibu ni kutochangia. Ccm hawana sababu hata moja ya kuweza kunishawishi niwachangie hata shilling moja.
 
Mie naona kama wananchi wanaweza kuchangia mambo kama haya basi waaanze kujichangia mtaa kwa mtaaa na kuweka maendeleo kwa kila kata kuliko kuchangia kwa ajili ya kampeni ambazo hazitabadilisha maisha yao.

Tried that,still am.
Mitaani nako matatizo yapo.
Surbubia zetu (Dar es Salaam) hujumuisha watu wenye vipato mbalimbali (to a great extent).
Tatizo kubwa linalokumba community based initiatives sasa hivi ni ukosefu wa sauti moja. Wakati baadhi ya watu kwenye jamii wanaidentify tatizo fulani,wengine wanaliona kama upenyo wa kujiwezesha. As a result, watu wanabaki kuvutana kila kukicha.

Siasa zilizopo za baadhi ya mitaa ya Dar es Salaam ndio kabisaaa!Wazimu mtupu!
Mlolongo mreefu usio na kichwa wala miguu.Viongozi ni kurushiana majukumu kila kukicha.Wengi wao hata madaraka hujui wamepataje.

It's a headache!
 
Hawa wabunge wetu si wana mashangingi hawa...kwa nini wasiyatumie magari waliyonayo tayari?r

''Magari waliyonayo ni kwa ajili ya shughuli za kiserikali'' or so they say.
Hivyo basi,haitaleta picha nzuri (not that they care) iwapo magari haya yatatumika katika shughuli binafsi kama kampeni za kichama.
 
Back
Top Bottom