Baada ya TANROADS Arusha kubomoa uzio wa wa hoteli ya Crest iliyofunguliwa siku kama tatu au nne zilizopita kumekuwepo na madai kadhaa kuwa Rais kakashifiwa. Wanasiasa wengine wamedai uongozi wa mkoa uwajibike. Yafuatayo ni maoni yangu:
1. Rais alienda kufungua hoteli na siyo kitu kingine na hoteli ilifunguliwa na inafanya kazi. Nasema Rais hajakashifiwa.
2. TANROADS walienda kubomoa uzio ambao ulijengwa kwenye Road reserve baada ya kuwa wametoa notice kisheria.Notice haikuwa ya kuvunja hoteli bali uzio. Walichofanya TANROADS ni sahihi. Hawakubomoa hoteli iliyofunguliwa na Rais. Rais hajakashifiwa. Kashfa ni yake mwenye hoteli kwa kukaidi maagizo ya TANROADS.
3. Hoteli bado iko intact. Anachotakiwa kufanya ni kujenga uzio eneo linalokubalika kisheria. Mimi ni mkazi wa Baraa na ninayo nyumba upande huo huo ambako hoteli hiyo ilipo. Nilipokamilisha kujenga nyumba yangu which is 50 metres from the centre of the road, uzio wa ukuta nilikuwa nimejenga ndani ya road reserve kiasi cha mita moja. Nilipewa notice na manispaa wakati huo ya kuuondoa ukuta. Ukuta-mind you- siyo nyumba. Sikubisha. Nilichukua mafundi nikawapa kazi ya kubomoa ukuta kwa kutoa tofali moja baada ya nyingine hadi ukuta ukawa haupo tena. Matofali hayo hayo nikajengea ukuta mwingine mita 10 ndani zaidi. Hakuna kilichoharibika. Nilitimiza wajibu wangu kwa kuwa raia mtiifu wa sheria.
4. Sasa swali nauliza. Kashfa kwa Rais hapo iko wapi? Baadhi ya wanasiasa wanataka uongozi wa mkoa uwajibike kwa kumpotosha Rais kweli wako sahihi?
5. Ninakumbuka mwaka 1971 Rais Nyerere alikwenda kufungua jengo la IPS likiwa linamilikiwa na AgaKhan, siku ya pili jengo hilo likataifishwa na serikali iliyokuwa chini ya Nyerere na akapewa Msajili wa Majumba. Nyerere hakukosea. Yeye alialikwa kufungua jengo. Lakini sheria ya Acquistion Buildings Act ya 1971 ikachukua mkondo wake. Mlio watu wazima huenda mnalijua hilo. Sasa JK kaenda kufungua hoteli na hoteli bado inafanya kazi kashfa hapo iko kwa JK au kwa mwen ye hoteli? Jamani let us be objective. Aliekashifiwa hapo ni Bwana Tarimo wala siyo Kikwete.
Mwenye hoteli ajilaumu mwenyewe asitake kumuingiza Rais kwenye upuuzi wake. Yeye sasa ndiye anaetaka kumkashifu Rais. Akajenge uzio kama sheria inavyotaka. Watu wengine jamani!!!
1. Rais alienda kufungua hoteli na siyo kitu kingine na hoteli ilifunguliwa na inafanya kazi. Nasema Rais hajakashifiwa.
2. TANROADS walienda kubomoa uzio ambao ulijengwa kwenye Road reserve baada ya kuwa wametoa notice kisheria.Notice haikuwa ya kuvunja hoteli bali uzio. Walichofanya TANROADS ni sahihi. Hawakubomoa hoteli iliyofunguliwa na Rais. Rais hajakashifiwa. Kashfa ni yake mwenye hoteli kwa kukaidi maagizo ya TANROADS.
3. Hoteli bado iko intact. Anachotakiwa kufanya ni kujenga uzio eneo linalokubalika kisheria. Mimi ni mkazi wa Baraa na ninayo nyumba upande huo huo ambako hoteli hiyo ilipo. Nilipokamilisha kujenga nyumba yangu which is 50 metres from the centre of the road, uzio wa ukuta nilikuwa nimejenga ndani ya road reserve kiasi cha mita moja. Nilipewa notice na manispaa wakati huo ya kuuondoa ukuta. Ukuta-mind you- siyo nyumba. Sikubisha. Nilichukua mafundi nikawapa kazi ya kubomoa ukuta kwa kutoa tofali moja baada ya nyingine hadi ukuta ukawa haupo tena. Matofali hayo hayo nikajengea ukuta mwingine mita 10 ndani zaidi. Hakuna kilichoharibika. Nilitimiza wajibu wangu kwa kuwa raia mtiifu wa sheria.
4. Sasa swali nauliza. Kashfa kwa Rais hapo iko wapi? Baadhi ya wanasiasa wanataka uongozi wa mkoa uwajibike kwa kumpotosha Rais kweli wako sahihi?
5. Ninakumbuka mwaka 1971 Rais Nyerere alikwenda kufungua jengo la IPS likiwa linamilikiwa na AgaKhan, siku ya pili jengo hilo likataifishwa na serikali iliyokuwa chini ya Nyerere na akapewa Msajili wa Majumba. Nyerere hakukosea. Yeye alialikwa kufungua jengo. Lakini sheria ya Acquistion Buildings Act ya 1971 ikachukua mkondo wake. Mlio watu wazima huenda mnalijua hilo. Sasa JK kaenda kufungua hoteli na hoteli bado inafanya kazi kashfa hapo iko kwa JK au kwa mwen ye hoteli? Jamani let us be objective. Aliekashifiwa hapo ni Bwana Tarimo wala siyo Kikwete.
Mwenye hoteli ajilaumu mwenyewe asitake kumuingiza Rais kwenye upuuzi wake. Yeye sasa ndiye anaetaka kumkashifu Rais. Akajenge uzio kama sheria inavyotaka. Watu wengine jamani!!!