Kubenea wa MWANAHALISI amenunuliwa na mafisadi?

Hii ni saikologia nyepesi; huyu jamaa ametumwa ili amfanye Kubenea asiwandike hao aliowataja kwa kuhofu kuwa akiwaandika atakuwa anatekeleza au kuthibitisha tuhuma. Ukweli utabakia kuwa yeyote ambaye si- mwadilifu ajiandae kusomwa kwenye Mwanahalisi na mambo yake yatawekwa wazi tu. Hakuna wakuonewa haya, wala wa kupendelewa, wala atakaye weza kumnunua Kubenea. Kubenea angekuwa wa kununuliwa angeshanunuliwa zamani sana. Hilo hata R.A na wenzake wote wanalijua. Ushauri wangu kwa uliyetumwa kuandika haya, waambie wahusika waache usanii, na uabadhilifu wa mali za umma, na walitumikie taifa letu kwa uaminifu. Habari zao zitasomwa na wao watapongezwa, vinginevyo wajiandae kuanikwa uovu wao.
Appreciated
u hv spoken ma mind
 
Wamejivua gamba. Nijuavyo mimi mdudu ajivuae gamba ni nyoka pekee, hakuna asiyefahamu kuwa nyoka ni mdudu mwenye sumu kali iletayo madhara kwa binadamu na viumbe wengine hai. Ajivuapo gamba inamaanisha kuwa hujiondoa uzee na kuwa nyoka mpya ambaye hata sumu yake huwa kali zaidi. Tutegemee nini baada ya chama chetu kujivua gamba?
 
Kijembe ambacho mmoja wa mapacha watatu wa ufisadi, Rostam Aziz Abdulrasul, alikirusha kwa Saed Kubenea kuwa anaweza kumnunulia mtambo wa kuchapishia gazeti lake la MwanaHalisi mapema mwaka huu, kimegeuka kuwa "azma iliyotimia" baada ya mwandishi huyo machachari aliyejizolea sifa kemkem kwa ujasiri kutiwa mfukoni na sasa ni sehemu ya majeshi ya Rostam ya kumlinda na kuwasambaratisha wabaya wake!

Kubenea ambaye mwaka juzi alishambuliwa na watu "wasiojulikana" na kumwagiwa tindikali machoni karibu apofuke, kasahau yote hayo na sasa ni silaha ya kuaminika ya Rostam katika kujihami dhidi ya kampeni kali ya CCM inayoongozwa na Katibu Mwenezi Taifa Nape Nnauye ili mkuu wake mpya Rostam abakie na gamba lake.

Taarifa za ndani kwenye duru za mwanahabari huyo zinasema kijembe kile cha kumnunulia Kubenea mtambo wa kuchapishia magazeti kimefanyiwa kazi na Kubenea yuko mbioni kupata mtambo mpya wa kisasa lakini kwa sharti la kuachana na habari hasi za Rostam na Lowassa kwenye gazeti lake na kuendesha kampeni kali dhidi ya msururu wa watu aliopewa katika miaka mitatu ijayo. Baadhi ya watu hao ni JK na familia yake, "Mtoto wa Mkulima", Magufuli, Chilligati, Nape, Sitta, Anne Kilango, Ole Sendeka, Lembeli, Mwandosya, Membe, Kinana, Mwakyembe, Mkuchika, Chatanda na Kigoda. Kubenea kakubali dili hilo ambalo tayari limemwingizia zaidi ya sh. milioni 20.

Gazeti la MwanaHalisi ambalo limekuwa kwa muda mrefu msumari wa moto kwa mapacha watatu wa ufisadi kutokana na Kubenea kuamini kwamba wawili kati ya mapacha hao watatu walihusika na mpango wa kumtoa roho au kumpa kilema cha maisha, halitabeba taarifa tena za Lowassa wala Rostam ila za wabaya wao hao.

Mathalan, toleo la kesho kutwa la MwanaHalisi tayari lina taarifa ndefu ya Daniel Porokwa akiwamwagia sumu "maadui" wa RA na EL bila kujali kuwa gazeti lake lilimwandika Porokwa mwaka jana kuwa kibaraka wa Lowassa baada ya kujitoa kugombea Ubunge jimbo la Monduli. Porokwa "alizawadiwa" kazi ya Katibu Msaidizi wa CCM wa Wilaya, gari mpya aina ya NOAH, shilingi milioni 2, na ng'ombe kadhaa baada ya kujisalimisha na kukubali Lowassa amkanyage kichwani kwa mila eti ya Kimasai kama siyo ya kishirikina.


Huyu ni mtu wa magamba ameandika hii.Ni aina nyingine ya Crap!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Homeboy

Jamaa anauza story hakuna kitu kama hicho! Ni vita wanapigana Magamba hao wanajaribu kumtumia Kubenea kama AK47. Kubenea is not that much cheap. Wanajua Magazeti yao ya Uhuru, Mzalendo, Habari leo hayauziki.

afadhali Rev umenishusha pumzi maana kuuza heshima uliyoijenga tangu unazaliwa kwa 20M ingekua kichekesho cha mwaka

Kubenea anatakiwa atambue kwamba utu haununuliki wala kuuzika, bali hudhalilishwa na kudhalilishwakutegemea na maanuzi ya mtendewa na si mtenda!!
 
Uongo mtupu huu! Kubenea bado na mwaminia..ni mmoja wa wanahabari makini walioko tanzania..mafisadi hawana nafasi.
 
Kubenea ni mtu aliyejijengea heshima sana katika tasnia ya uandishi wa habari na bila shaka gazeti lake linasomwa sana kwa sababu linaaminika na kuheshimiwa. Sitaki kupuuza yanayozungumzwa kwa sababu yeye ni binadamu na kila binadamu ana udhaifu wake. Lakini sitaki pia kuamini moja kwa moja kauli hii kwa sababu Kubenea anajua, pengine kuliko mtu yeyote, gharama alizolipa kwa kusimamia misimamo yake imara na kwa sasa hana la kupoteza kwa kuendelea kushikilia misimamo hiyo.

Lakini ni vizuri tukaelewa kwamba mapacha hawa watatu kwa sasa wamechanganyikiwa na wako tayari kuingia gharama yoyote ile katika kuhakikisha kwamba wanabaki salama na kujaribu kupigana kuifanikisha ndoto yao, ambayo hata hivyo HAITATIMIA. Jambo la kutilia maanani ni kwamba katika hali isiyo ya kawaida, msimamo mkali wa Mwanahalisi kuhusu mapacha hawa watatu toka baada ya maamuzi ya NEC mwezi uliopita umekuwa ni wa kutiliwa mashaka kwa sababu kwa kiasi kikubwa gazeti hili limejikita katika kukosoa na kuchambua maudhui ya maamuzi hayo, kiasi hata cha kuwaponda viongozi wakuu wa chama cha CCM, kuliko kuangalia the positive aspects of NEC deliberations. Hili lina hatari ya kutafsiriwa kama kupooza nguvu ya maamuzi yale na KWA KIASI FULANI INAWAPA NAFUU MAPACHA WATATU.

Kama hilo lina tafsiri ya kununuliwa au la sina hakika, labda matukio ya huko mbele yatatupa mwanga halisi. Hata hivyo milioni 20 kwa Kubenea ni dhihaka!
 
Taarifa za ndani kwenye duru za mwanahabari huyo zinasema kijembe kile cha kumnunulia Kubenea mtambo wa kuchapishia magazeti kimefanyiwa kazi na Kubenea yuko mbioni kupata mtambo mpya wa kisasa lakini kwa sharti la kuachana na habari hasi za Rostam na Lowassa kwenye gazeti lake na kuendesha kampeni kali dhidi ya msururu wa watu aliopewa katika miaka mitatu ijayo. Baadhi ya watu hao ni JK na familia yake, "Mtoto wa Mkulima", Magufuli, Chilligati, Nape, Sitta, Anne Kilango, Ole Sendeka, Lembeli, Mwandosya, Membe, Kinana, Mwakyembe, Mkuchika, Chatanda na Kigoda. Kubenea kakubali dili hilo ambalo tayari limemwingizia zaidi ya sh. milioni 20.

[/QUOTE]

Mwanzisha mada ni mbunifu na mtunzi mzuri wa hadithi za kusadikika. Milioni 20 kamwe hauwezi kununua mtambo wa kuchapia magazeti na wala haufikii robo ya advance payment; wala haitoshi kununua uhuru wa mtu makini. Kama ilivyo ada ni lazima tuulize; source ya information hiyo iko wapi?

Anyway "money changes every thing" and can buy even people but never will money be able to buy People Power!!!!.
 
Kijembe ambacho mmoja wa mapacha watatu wa ufisadi, Rostam Aziz Abdulrasul, alikirusha kwa Saed Kubenea kuwa anaweza kumnunulia mtambo wa kuchapishia gazeti lake la MwanaHalisi mapema mwaka huu, kimegeuka kuwa "azma iliyotimia" baada ya mwandishi huyo machachari aliyejizolea sifa kemkem kwa ujasiri kutiwa mfukoni na sasa ni sehemu ya majeshi ya Rostam ya kumlinda na kuwasambaratisha wabaya wake!

Kubenea ambaye mwaka juzi alishambuliwa na watu "wasiojulikana" na kumwagiwa tindikali machoni karibu apofuke, kasahau yote hayo na sasa ni silaha ya kuaminika ya Rostam katika kujihami dhidi ya kampeni kali ya CCM inayoongozwa na Katibu Mwenezi Taifa Nape Nnauye ili mkuu wake mpya Rostam abakie na gamba lake.

Taarifa za ndani kwenye duru za mwanahabari huyo zinasema kijembe kile cha kumnunulia Kubenea mtambo wa kuchapishia magazeti kimefanyiwa kazi na Kubenea yuko mbioni kupata mtambo mpya wa kisasa lakini kwa sharti la kuachana na habari hasi za Rostam na Lowassa kwenye gazeti lake na kuendesha kampeni kali dhidi ya msururu wa watu aliopewa katika miaka mitatu ijayo. Baadhi ya watu hao ni JK na familia yake, "Mtoto wa Mkulima", Magufuli, Chilligati, Nape, Sitta, Anne Kilango, Ole Sendeka, Lembeli, Mwandosya, Membe, Kinana, Mwakyembe, Mkuchika, Chatanda na Kigoda. Kubenea kakubali dili hilo ambalo tayari limemwingizia zaidi ya sh. milioni 20.

Gazeti la MwanaHalisi ambalo limekuwa kwa muda mrefu msumari wa moto kwa mapacha watatu wa ufisadi kutokana na Kubenea kuamini kwamba wawili kati ya mapacha hao watatu walihusika na mpango wa kumtoa roho au kumpa kilema cha maisha, halitabeba taarifa tena za Lowassa wala Rostam ila za wabaya wao hao.

Mathalan, toleo la kesho kutwa la MwanaHalisi tayari lina taarifa ndefu ya Daniel Porokwa akiwamwagia sumu "maadui" wa RA na EL bila kujali kuwa gazeti lake lilimwandika Porokwa mwaka jana kuwa kibaraka wa Lowassa baada ya kujitoa kugombea Ubunge jimbo la Monduli. Porokwa "alizawadiwa" kazi ya Katibu Msaidizi wa CCM wa Wilaya, gari mpya aina ya NOAH, shilingi milioni 2, na ng'ombe kadhaa baada ya kujisalimisha na kukubali Lowassa amkanyage kichwani kwa mila eti ya Kimasai kama siyo ya kishirikina.

Mwanzisha mada ni mbunifu na mtunzi mzuri wa hadithi za kusadikika. Milioni 20 kamwe hauwezi kununua mtambo wa kuchapia magazeti na wala haufikii robo ya advance payment; wala haitoshi kununua uhuru wa mtu makini. Kama ilivyo ada ni lazima tuulize; source ya information hiyo iko wapi?

Anyway "money changes every thing" and can buy even people but never will money be able to buy People Power!!!!.
 
  • Thanks
Reactions: mja
MAFISADI HAWANA JIPYA WAMEDODA NA WAMEFULIA KISIASA..........................., bado naendelea kuamini kwamba mafisadi hawana jipya na watazidi kuchemsha na kundi lao lote na vijana wao wote wao ndio wanaopanga njama na kumuingiza madarakani kijana wao kutoka visiwani JAMAL KASSIM kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Mh Masauni(Mb) naamini hawatafanikiwa hata kidogo....nasema hata kidogo.

-wacha wamnunulia Kubenea hata JUMBO MASHINE PRINTER nini hicho kikoroboi cha milioni 20-30, ila njama wanazozipanga hazitafua dafu hata kidogo wanaplan nyingi kuliko uwezo wao wa kufikiri, wanahela nyingi hawajui wazifanyie nini, wanakundi kubwa lisilo kuwa na tija, hakuna watakalofanikiwa hao. plan wanazotumia kumuingiza JAMAL KASSIM kuwa mwenyekiti UVCCM hazitafua dafu ni bora litibuke tusubiri mwakani 2012 kuliko hizo njama zao, kikao kilichokaliwa na hao vijana wao wa mwmvulia chini ya HUSSEN BASHE BASHE wasidhani havijulikani vinajulikana na wanayoyafanya yanajulikana.

-WANAPINGO KAMA IFUATAVYO: kama LOWASA hawi rais 2015 basi kijana wao EMENUEL NCHIMBI awe rais na LOWASA kuwa WAZIRI MKUU TENA hiyo ndio hesabu yao hata hili wataula wa chuya kwa uvivu wa kuchagua, leo wamemgeuka mwanamama wao MARY CHATANDA kwa kuwa hakuweza kumsaidia demu wao BATILDA BURIAN kuwa mbunge ARUSHA MJINI sasa imekula kwao waendelee kuvurugana tu na kijana wao JAMES MILLYA mwalimu sijui shule ipi ya sekondari aendelee kutumika utadhani sio mmasai halisi.

-wanamthumu kijana wa watu bure MRISHO GAMBO bila sababu yeyote japo naye mwanzo alikuwa wao lakini hawakumpenda na baadae amejua ukweli sasa wanamuona mbaya, nchii kila aliyekataliwa na BABA W TAIFA MWALIM JULIUS KAMBARAGE NYERERE HAKUNA ATAKACHOFANYA KIKAKUBALIKA MILELE hata kama utamfanyia mtu madhali ni ww unafanya itakula kwako na hao unaowafanyia.

-LOWASA ALISHAKATALIWA NA BABA WA TAIFA watanzania wanajua hilo....................., Mzee kambarage alishawahi toa hundi ya DOLLA LAKI TANO AMBAYO LOWASA ALIHONGWA NA WAHINDI KUKIUZA KIPANDE CHA ARDHI LEO NDIO KUNA SHULE YA AGKHAN MZIZIMA PRIMARY SCHOOL, hii lilikuwa MKUTANO MKUU WA HALMASHAURI KUU 1995 watanzania hawajasahau na hawatasahau hilo. wakati huo alikuwa WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO.

-KUBENEA ATAKULA NAO SAHANI MOJA PAMOJA NA KUNUNULIWA HUO MTAMBO na hao aliotajiwa kuwashughulikiwa haita tokea mbona wanamiliki MAGAZETI YAO YA TAZAMA linatoka kila JUMANNE NA LIMESHINDWA KUFUA DAFU, WANAMILIKI MKAKATI linatoka kila IJUMAA nalo limeshindwa kufua DAFU? NINI WANATAPA TAPA HAWA WATU? WAMEFULA.

-WAMEKULA YA MBUZI WATAOTA MAPEMBE.............................!!!!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Mkuu nimekuvulia kofia. Hawa jamaa walivyogandwa na uchafu, brashi za Kubenea haziwezi kufua dafu hata wangemnunua. Na pengine huu ndiyo uthibitisho wa jinsi jamaa hawa ambavyo hawana strategy na wale wanaowazunguka nadhani wako busy kuwapotosha na kuwaibia. Hata hii counter offensive ya ku-dramatize CCJ watu wameshaishtukia na sasa watu wameshajua source ni nini. Mimi nadhani dhambi ya kupora haki ya wananchi haiwezi kupoozwa na mipango ya watu kutaka kuondoka CCM hasa katka mazingira yaliyochochewa na baadhi ya watu (hasa hao mapacha watatu) ambao ni wachafu na hawastahili kuwemo katika utumishi wa umma. Afterall, imedhihirika kwamba ukiondoka CCM na kurudi unaweza pewa nafasi kubwa tu na mfano ni rafiki yao Wassira.
 
Nyie CDM huyu RA mnaemtetea sasa hivi kwa ajili ya hivyo vijisent vyake muda si mrefu mmtajuta kumbukenei ya kwamba magazeti yanayomilikiwa na RA ndiyo yaliyokuwa yanaandika ya kuwa CDM wanawakilisha kanisa katoliki, mara CDM ni chagga deve.Manif, yote haya mmesasahau kwa ajili ya faida ya muda mfupi hii ndoa yenu na RACHEL lazima itakula kwenu

Mkuu nakugongea senksi. Wacha tuone, mengi yanakuja.
 
Mwanzisha mada ni mbunifu na mtunzi mzuri wa hadithi za kusadikika. Milioni 20 kamwe hauwezi kununua mtambo wa kuchapia magazeti na wala haufikii robo ya advance payment; wala haitoshi kununua uhuru wa mtu makini. Kama ilivyo ada ni lazima tuulize; source ya information hiyo iko wapi?

Anyway "money changes every thing" and can buy even people but never will money be able to buy People Power!!!!.
good point
 
Naomba Kubenea ajitokeze hapa atoe ufafanuzi nyie mnaomtolea mnakosea kuibuka tu nakutoa shutuma kwa huyu alieleta maada, mbona hamruhusu bongo zenu kujadili negative side?
Kubenea ni mtu makini sana na nina amini ni mmoja wa wana great thinkers jf pia naamini atachangia post hii.
Karibu KUBENEA......
 
Objective ni kumzuia Kubenea kuandika story ya Porokwa maana wanamjua Kubenea anavyojua kuweka utamu kwenye hoja. wanahofu hao! hakuna cha kununuliwa na RA au EL, wao wenyewe wakikusikia watakucheka, maana wanamjua Kubenea. Unafiki wa akina Nape, Sita na Mwakyembe lazima uanikwe kama ulivyoanikwa uovu wa akina RA na EL kiasi kwamba sasa tunawajua vilivyo. sasa endelea kuwaanika wote usimwache hata mmoja ili mwisho tupate cream ya watu waadilifu wenye uchungu wa kweli na si waganga njaa.

Mkuu hii stori yako mbona ina harufu ya kuwatetea mafisadi? Porokwa aliulizwa maswali kadhaa siku ile akashindwa kuyajibu na kudhihirisha kwamba he was not himself. Lakini issue ya kutaka kuhama chama mbona inakuzwa? Kwani ni kuua mtu?
 
Nyie CDM huyu RA mnaemtetea sasa hivi kwa ajili ya hivyo vijisent vyake muda si mrefu mmtajuta kumbukenei ya kwamba magazeti yanayomilikiwa na RA ndiyo yaliyokuwa yanaandika ya kuwa CDM wanawakilisha kanisa katoliki, mara CDM ni chagga deve.Manif, yote haya mmesasahau kwa ajili ya faida ya muda mfupi hii ndoa yenu na RACHEL lazima itakula kwenu

Mkuu sikuelewi, RA ni mwanachama wa CCM na rafiki mkubwa wa ******. Kifupi RACHEL ni CCM, sasa mbona unawaingiza CDM tena. Ndani ya CCM wote ni mafisadi tu, CDM kazi yao ni kupambana nao wote hata wakati wakiwa wananyosheana vidole.
 
Mbowe na slaa wote ni njaa tu, sasa wamepata mbulushi mwenye pesa, lazima watamsujudia.

Huyo mburushi kaamia lini CDM, taarifa nilizo nazo mpaka sasa ni kuwa yupo CCM, where he belongs.
 
Vuzuri sana bora yaishe,uhai ni bora kuliko sifa za kijinga we waache waseme tu we songa mbele,ulipomwagiwa tindikali waliishia kukupa pole je ungekufa si ungesahauliwa kama Katabalo nikukumbushe yule wa Loliondo Gate aliyefia DIA,wangapi wamekufa na wamesahauliwa wakati walijitoa muhanga watoto na ndugu zao wanateseka kwa manyanyaso ya moyo na shida za kila aina na waliofanya hayo wanapeta kwa sana,ufisadi ni kitu gani mbona hapa hakuna kiongozi wala mtumishi asiye fisadi wote mafisadi kwa kiwango chao mwenye kisu kikali ndiye anayefaidi zaidi,wewe ukiandika juu ya hayo wanapanga njama za kukuua na mateso mengine mengi kwani wewe uliumbiwa mateso? au kufurahisha watu fanya kazi yako uifaidi taaluma yako na uache umbea na wewe ufaidi uhuru wa kuishi siyo kila leo mara tindikali kakoswa kugongwa na gari n.k. ukishindwana nao ungana nao HONGERAAAAAAAA.:A S-rose:
 
Ni ukweli kabisa kuwa Kubenea amenunuliwa na mafisadi. Tatizo la Watanzania wengi ni wagumu kufikiri na kufanya uchambuzi wa mambo. Ukiangalia mwenendo wa habari zinatolewa na MWANAHALISI kwa zaidi ya mwezi sasa utaona gazeti hili limebadili mwelekeo kabisa.

Mei 18, 2011 niliweka post hii ifuatayo huku kwenye Jukwa la Siasa lakini moderators kwa "busara" yao waliona ni bora waitupilie mbali na kuificha kwenye folder ya Chit-Chat (porojo!):


Kubenea wa MWANAHALISI amenunuliwa na mafisadi?

Kuna tetesi kuwa Saed Kubenea, mhariri mkuu na mmiliki wa gazeti pendwa la MwanaHALISI naye ni miongoni mwa waandishi wa habari walionunuliwa na Rostam Aziz, Edward Lowassa na Andrew Chenge kwenye mkakati wa kuzuia mafisadi hawa wasifutwe uanachama wa CCM.

Tetesi ziliopo ni kuwa Kubenea kapewa pesa na mali kadhaa zenye thamani kubwa ili gazeti lake la MwanaHALISI liache kabisa kuwaandika habari yoyote mbaya (negative) kuhusu kina Rostam, Lowassa na Chenge tangu CCM ilipowataka wajitoe wenyewe kwenye uongozi.

Pamoja na kupigwa marufuku kuandika habari zozote mbaya kuhusu Rostam, Lowassa na Chenge, Kubenea pia amepewa kazi maalumu kuandika habari za kumchafua Rais Jakaya Kikwete, mtoto wake Ridhwani Kikwete, Samuel Sitta, Nape Nnauye, na viongozi wengine wa CCM.

Baada ya kuangalia mwenendo wa MwanaHALISI kwa wiki kadhaa na kuona ni kweli gazeti hili limekuwa na kigugumizi cha ghafla cha kuandika maovu ya Lowassa, Rostam na Chenge na badala yake linamshambulia Kikwete na Sitta kila kukicha, nimepata hofu kuwa huenda hizi tetesi si za kupuuza hata kidogo.

MUNGU IBARIKI TANZANIA!
 
Back
Top Bottom