Babylon
JF-Expert Member
- Feb 5, 2009
- 1,332
- 82
KUBENEA NAYE NI FISADI?
Suedi Kubenea ambaye anatokea kijiji cha BALENI kule kisiwani Mafia na ambaye ni mwenye gazeti lilkilo mstari wa mbele kupiga vita UFISADI amefanya kitendo ambacho kimetustua na kutunyongonyesha sisi wapiga vita ufisadi .
KUBENEA ambaye kwa sababu anazozijua yeye aliamua kufanya PRESS CONFERENCE YA KUMPA masaa 24 mheshimiwa ROSTAM AZIZ aombwe radhi baada ya kumhusisha Kubenea na UFISADI lakini katika hali isiyo ya kawaida Kubenea amechomoa bila sababu za msingi.
Taarifa zaidi toka Baleni Mafia zinasema kuwa ndugu jamaa na marafiki wamesikitishwa na kitendo cha kijana wao kutofanya hiyo press conference ambayo pamoja na mambo mengine ingemwanika ( whatever it means nowadays) mheshimiwa Rostam na kumweka wazi kwani Kubenea anazo DATAZ ambazo angemkoma "Nyani Giladi"
Na katika duru za waandishi kuna habari kuwa inawezekana kuwa naye kesha pewa chochote kama alivyokuwa akipewa na LOWASA ndio maana katulia...na hii inawezekana ni kweli kwani alikuwa anaitukana saaanaaaa serikali ya JK na JK mwenyewe akidai ni FISADI na mengineyo na hata ule mkutano na Lowasa aliahidiwa MATANGAZO KWENYE GAZETI LA MWANAHALISI lakini alipoona kimya (baada kuambiwa kuwa avute subira) akaamua kurudi na nguvu zote kuitukana bara bara serikali ya JK kuwa ni ya kifisadi
Mpaka alipomwagiwa tindikali baada ya gari lake kuvunjwa viooo
Lakini mafisadi hao hao aliowaita mafisadi ndio walimlipia gharama za matibabu kwenda INDIA India hivyo we should not rule out kuwa naye amekuwa compromised kwenye hili sakata ka ufisadi kwani price ya KUBENEA ni ndogo sana...matangazo kwenye gazeti lake na hivi sitoshangaa kusikia kuwa keshavuta kwa hao hao anaowaita MAFISADI kwa kwa sababu hivyo nadhani tunaweza kusema kuwa KUBENEA NAYE NI FISADI LAKINI inawezekana fisadi huyu anakula kote kote yaani kwa MENGI na kwa ROSTAM kwani ndio kawaida yake
Tuwe wakweli hapa hakuna asie ielewa hii serekali na matendo yake, jamaa wameshataka kumtowa Roho mara ya kwanza kwa kutumia tindi kali tukiwachilia hilo tukumbuke hata serekali imewahi kusema mafisadi wanapesa na uwezo kuiumbisha serekali yenyewe ,sasa nyinyi mnashadidia lazima iwe mnavyotaka nyinyi afanye hiyo PRESS CONFERENCE hata kama amesha pelekewa ujumbe rasmi kuwa zake zinahisabika.