Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Majira ya kiangazi ndiyo yanazidi kukolea kwa wabeba maboksi. Hata hivyo mbeba maboksi mwanagenzi amegundua balaa lingine ukiacha lile la vinguo vifupi ambavyo ufupi wake unazidi kupindukia kadri joto linavyoongezeka! Sasa amegundua ni kazi ngumu sana kujua kama mabinti ni watokao na wanaume au ni watokao na wanawake wenzao. Zaidi ya mara moja amejikuta akimzimikia binti na kuvunjika moyo pale anapogundua kuwa ana rafiki wa karibu wa kike. Hebu fikiria binti mrembo uliyemzimikia na kupeana kitarehe anapokujulisha baada ya kukupa kumbatio la kukuaga kuwa tayari ana mtu maishani mwake ila mtu huyo sio rafiki wa kiume kisha anakuambia hilo mliache maana ni mjadala mwingine! Mtu unajuaje ilhali hawana tofauti na wanawake wengine - kama ni hereni wanavaa, kama ni sketi wanavaa, na kama ni mvuto wa kike nao wanao! Kweli safiri uone! Sijui Rais wa Wabeba Maboksi anakabilianaje na adha hii kuu? Au ameshakubali yaishe! Pengine yule Rais mwingine naye alikuwa sahihi kabisa aliposema liwa ule!