Kubeba Laptop Chanzo cha Ugumba kwa Wanaume?!

Sophist

Platinum Member
Mar 26, 2009
4,484
3,400
Ndugu wote,
Habari kuu ya gazeti la Mwananchi la Jumatano Februari 8/2012 inasema kuwa mojawapo ya vyanzo vya ugumba kwa wanaume ni kubeba laptop. Habari husika inazingatia matokeo ya utafiti uliofanywa na watallamu wa tiba/afya ya uzazi, Muhimbili National Hospital. Tunaomba wanaofahamu watufafanulie uhusiano wa kiufundi/kisayansi kati ya kubeba laptop na ugumba kwa wanaume.
Tafadhali tujuze
 
Nashindwa kuelewa sababu ni nini hadi gazeti la mwananchi limeamua kuipa uzito hii habari eti zaidi ya nusu ya wanaume ni wagumba. nilitegemea kukuta habari hii kwenye magazeti ya udaku kama kiu na uwazi. cha kustaajabisha ni pale hao watafiti wanapo draw conclusion kwa kufikiri kwa kutumia masaburi.
HIYO ASILIMIA 50 WANAYOZUNGUMZIA NI KWAMBA IMEPATIKANA MIONGONI MWA WANAUME WALIOENDA KUPIMA. SASA HIVI KUNA MWANAUME ALIYE MZIMA MWENYE HAJA YA KWENDA KUPIMA KAMA SIO MGUMBA? ITS OBVIOUS KWAMBA HAO HAO WALIOENDA KUPIMA INGEWEZEKANA HATA WANGEKUWA HATA ASILIMIA 70.

SASA MNAFANYA UTAFITI KWA WATU WANAOJIHISI WANA TATIZO THEN RESULTS YAKE NDO MNAITUMIA KWA WHOLE POPULATION?
 
Theories zingine zinatungwa ( tena na watu ambao hata siyo wataalamu) na kutumika TZ tu ...
 
Ndugu wote,
Habari kuu ya gazeti la Mwananchi la Jumatano Februari 8/2012 inasema kuwa mojawapo ya vyanzo vya ugumba kwa wanaume ni kubeba laptop. Habari husika inazingatia matokeo ya utafiti uliofanywa na watallamu wa tiba/afya ya uzazi, Muhimbili National Hospital. Tunaomba wanaofahamu watufafanulie uhusiano wa kiufundi/kisayansi kati ya kubeba laptop na ugumba kwa wanaume.
Tafadhali tujuze
huu mwaka wa 8 sasa natumia laptop zaid kuliko desktop pia naambatana nayo kila ninapo enda.mungu kanijalia mtoto-binti mzuri,sura,akili,ujanja ni copyright na mimi mwenyewe kadoda11.na sasa hivi shemeji/wifi yenu kabeba tena ya miezi kadhaa sasa.nahitimisha tu kwamba huu utafiti ni wakichina.
 
Pia kuweka simu mfuko wa mbele unafanya jamaa awe mfupi.
Ukiweka mfuko wa nyuma inakufanya uwe mkamerun.
 
Hao waliowafanya utafiti watakua wametumia tumbo kufikiri,kuna uhusiano gani kubeba laptop na ugumba?? Vp kuhusu tv,redio,simu za mkononi? Hao watafiti ni makanjanja tu.
 
Mimi pia ni mmojawapo wa wenye mashaka na utafiti huo ukizingatia watoto wa mitaani wanazidi kuongezeka na utoaji mimba unazidi kushika kasi.
 
huu mwaka wa 8 sasa natumia laptop zaid kuliko desktop pia naambatana nayo kila ninapo enda.mungu kanijalia mtoto-binti mzuri,sura,akili,ujanja ni copyright na mimi mwenyewe kadoda11.na sasa hivi shemeji/wifi yenu kabeba tena ya miezi kadhaa sasa.nahitimisha tu kwamba huu utafiti ni wakichina.

Mkuu wala usitoke jasho kwa hizo taarifa.

Nilipoona tu huo utafiti umefanyika muhimbili sikujiuliza mara mbili, kama vipimo vyenyewe Madaktari wamegundua ni fake toka china unategema majibu gani sasa?

Mie nilifikiri Serikali itatangaza watu wote waliofanya vipimo pale hasa vya HIV warudie tena ili amani itawale.
 
Kwanza Gazeti la Mwananchi na Hos. ya Muhimbili watumbie wananchi nini chanzo cha Ugumba kabla ya Laptop

Otherwise hii habari niliiona thru Al jazeera News kuwa Waphilipino wamefan.ya research na kugundua Laptop inaweza sababisha ugumba hasa2 wale wanaopakata laptops.
Sikuizingatia sana hiyo habari in details
 
Inawezekana sijuhi ukuhusu sababu ....ila wireless facility emits a lot of rf wave na tunaweka karibu na viungo vya uzazi
 
Mikanda ya kiunoni kwa wanaume nayo inasababisha ugumba, hizi tafiti hizi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Nashindwa kuelewa sababu ni nini hadi gazeti la mwananchi limeamua kuipa uzito hii habari eti zaidi ya nusu ya wanaume ni wagumba. nilitegemea kukuta habari hii kwenye magazeti ya udaku kama kiu na uwazi. cha kustaajabisha ni pale hao watafiti wanapo draw conclusion kwa kufikiri kwa kutumia masaburi.
HIYO ASILIMIA 50 WANAYOZUNGUMZIA NI KWAMBA IMEPATIKANA MIONGONI MWA WANAUME WALIOENDA KUPIMA. SASA HIVI KUNA MWANAUME ALIYE MZIMA MWENYE HAJA YA KWENDA KUPIMA KAMA SIO MGUMBA? ITS OBVIOUS KWAMBA HAO HAO WALIOENDA KUPIMA INGEWEZEKANA HATA WANGEKUWA HATA ASILIMIA 70.

SASA MNAFANYA UTAFITI KWA WATU WANAOJIHISI WANA TATIZO THEN RESULTS YAKE NDO MNAITUMIA KWA WHOLE POPULATION?
Tafiti za kibongo Bwana! Uchakachuaji kwa kwenda mbele. Huu unaoitwa utafii ni aibu tupu. Hizo laptop zimeanza kuingia lini hadi ziwe "cause for male infertility"? Na wapi wamepata idadi ya wanaume hao wanaosemekana kutembea na hizo laptop? Halafu ni wanaume wangapi Tanzania wanamiliki hizo laptop hadi kuhalalisha idadi ua "Nusu ya wanaume" kuwa tasa? Sisi Tanzania tuna laptop nyingi zaidi ya huko zinakotoka ambako tatizo hili halipo? Hivi hawana hata chembe ya aibu ku-publish vitu vya kufinyanga na vya kipumbavu kama hivi na kutuaibisha wasomi wa Tanzania? Shame on them! Nakubaliana na Bwanga kwamba gazeti la Mwananchi nililokuwa naliheshimu sana na kulisoma "Online" huku niliko limejipunguzia hadhi kwa kuchapisha tafiti za kihuni na za mitaani toka kwa wahuni fulani kama ilivyo katika hili. Shame on them.
 
yaani cku izi kila kitu kinamadhara hata chakula tunachokula pia tunaambiwa ni kibaya kwa sababu ya mbolea ya kisasa.tutaepuka vingapi?
 
Can we get a thoroughly thought scientificevidence? I do not think the story is baseless. Medics please bail us out.There must be scientifically confirmed reasons indicating the correlation betweenelectronic waves emitted from Laptops and fecund. I think we should not dismiss the story as laugh stock.
 
Back
Top Bottom