Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Ya'rabi miye nalia
Haya n'nashuhudia
Ya shari twajitakia
Ya mambo ya kuchukia
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Twaona yanatukia
Kama giza latujia
Wenyewe twashingilia
Totoro twaliingia
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Kwa mbwembwe wametujia
Ahadi watumwagia
Tabasamu za udhia
Nazo wanatupatia
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Ati kura watakia
Zamu tena walilia
"Zaidi" waaahidia
Wabongo twashingilia!
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Kasi zaidi zajia
Nguvu zaidi walia
Ari zaidi mamia
Na uzembe zidia!
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Nikisema wachukia
Eti ninapandizia
Chuki isiyoishia
Kwa wale wenye nia
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Sasa nawaulizia
Ni vipi tutafikia
Yale tunayotakia
Kwa mwendo wa kurudia
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Ubovu ukirudia
Kwa kasi ya kuzidia
Fisadi ukimpatia
Nguvu ya kumzidia
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Vipi mtaifikia
Njozi mnayotakia
Mazuri mnayolilia
Si kwamba mmefulia
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Zaidi mwaitakia
Hiyo mtajipatia
Na zaidi mtalia
Huku mnashangilia
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Mwenye akili sikia
Ubongo wako tumia
Usifuatie hisia
"zaidi" kukumbatia
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Lazima kuulizia
Ni vipi walishindwia
Zaidi kutupatia
Miaka iloishia?
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Mbona waliwaachia
Mafisadi kutambia
Kamati kuwaundia
Na kesi kuwatungia?
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Mbona hawakutupatia
Ubora wa kuzidia
Elimu ikazidia
Maisha kushangazia?
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Majambazi wazidia
"zaidi" wamejazia
Ni vipi watazidia
Ya zaidi kuzidia?
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Barabara twapitia
Mahandaki yazidia
Na magonjwa pindukia
"zaidi" twajitakia?
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Zaidi mwajizidia
Mmezidi twachukia
Mmbwembwe mmetuzidia
Twazidi kuwakimbia!
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Natamati natamia
Beti ninazifungia
Wazo nimewapatia
Ya nini cha kuchukia
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

ZAIDI NTAZIDIA
WAKIZIDIA NAZIDIA
NIKIZIDI NAZIDIA
ZAIDI YA KUZIDIA!
Kubeba asobebeka, akibebwa habebeki!

Na. M. M. Mwanakijiji (Ngurumo ya Ushindi a.k.a Sauti ya Kijiji)
 
Ya'rabi miye nalia
Haya n'nashuhudia
Ya shari twajitakia
Ya mambo ya kuchukia
Kabebwa asobebeka!

Twaona yanatukia
Kama giza latujia
Wenyewe twashingilia
Totoro twaliingia
Kabebwa asobebeka!

Kwa mbwembwe wametujia
Ahadi watumwagia
Tabasamu za udhia
Nazo wanatupatia
Kabebwa asobebeka!

Ati kura watakia
Zamu tena walilia
"Zaidi" waaahidia
Wabongo twashingilia!
Kabebwa asobebeka!

Kasi zaidi zajia
Nguvu zaidi walia
Ari zaidi mamia
Na uzembe zidia!
Kabebwa asobebeka!

Nikisema wachukia
Eti ninapandizia
Chuki isiyoishia
Kwa wale wenye nia
Kabebwa asobebeka!

Sasa nawaulizia
Ni vipi tutafikia
Yale tunayotakia
Kwa mwendo wa kurudia
Kabebwa asobebeka!

Ubovu ukirudia
Kwa kasi ya kuzidia
Fisadi ukimpatia
Nguvu ya kumzidia
Kabebwa asobebeka!

Vipi mtaifikia
Njozi mnayotakia
Mazuri mnayolilia
Si kwamba mmefulia
Kabebwa asobebeka!

Zaidi mwaitakia
Hiyo mtajipatia
Na zaidi mtalia
Huku mnashangilia
Kabebwa asobebeka

Mwenye akili sikia
Ubongo wako tumia
Usifuatie hisia
"zaidi" kukumbatia
Kabebwa asobebeka!

Lazima kuulizia
Ni vipi walishindwia
Zaidi kutupatia
Miaka iloishia?
Kabebwa asobebeka!

Mbona waliwaachia
Mafisadi kutambia
Kamati kuwaundia
Na kesi kuwatungia?
Kabebwa asobebeka!

Mbona hawakutupatia
Ubora wa kuzidia
Elimu ikazidia
Maisha kushangazia?
Kabebwa asobebeka?

Majambazi wazidia
"zaidi" wamejazia
Ni vipi watazidia
Ya zaidi kuzidia?
Kabebwa asobebeka?

Barabara twapitia
Mahandaki yazidia
Na magonjwa pindukia
"zaidi" twajitakia?
Kabebwa asobebeka

Zaidi mwajizidia
Mmezidi twachukia
Mmbwembwe mmetuzidia
Twazidi kuwakimbia!
Kabebwa asobebeka!

Natamati natamia
Beti ninazifungia
Wazo nimewapatia
Ya nini cha kuchukia
Kabebwa asobebeka!

ZAIDI NTAZIDIA
WAKIZIDIA NAZIDIA
NIKIZIDI NAZIDIA
ZAIDIA YA KUZIDIA!
Na. M. M. Mwanakijiji (Ngurumo ya Ushindi a.k.a Sauti ya Kijiji)



shairi lako zuri sana ndugu mwanakijiji lakini ukumbuke kasema mzee Sadan Abdul Kandoro ya kuwa
Mtu chake apendacho,hakina hila machoni
huridhika kuwa nacho, japo hakina thamani
mapenzi hayana kicho, yaamkapo moyoni
mwenye mapenzi, haoni ingawa macho anayo

kwa maana hiyo hata iweje atabebwa hivyo hivyo kwa kuwa tumempenda
 
Ahsante mkuu kwa utenzi murua,hakika tunajivuna kuwa na mtu kama wewe katika jamvi hili lisoisha ukoko. Tunaburudika,tunaelimika,tunakosoana inapobidi.
 
shairi lako zuri sana ndugu mwanakijiji lakini ukumbuke kasema mzee Sadan Abdul Kandoro ya kuwa
Mtu chake apendacho,hakina hila machoni
huridhika kuwa nacho, japo hakina thamani
mapenzi hayana kicho, yaamkapo moyoni
mwenye mapenzi, haoni ingawa macho anayo

kwa maana hiyo hata iweje atabebwa hivyo hivyo kwa kuwa tumempenda

umenikumbusha mbali sana!! thanks!
 
Tutapingana, tutatofautiana lakini wote tukiipenda nchi tunaweza kuikomboa!
 
Umekuja ki-vingine...

Atabebwa tu mwisho tutaingia naye shimoni.... kisa, mapenzi upofu
 
nami naunga mkono
tuendako mimi simo
tutaja pigana vigongo
tutapomrudisha humo
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

Akili zetu zi wapi
tumeshalewa makapi
sasa tukipewa pipi
hatujali letu lipi
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

Kura zetu tulikupa
imani nayo kakupa
mwenzetu ukatutupa
ukaiba hata EPA
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

Machozi najililia
mejiwa maharamia
nchi yangu Tanzania
amka taja jutia
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

Kasi gani waongeza
nguvu ipi watubeza
ya mwanzo we hukuweza
ya zaidi utaweza
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

na bado twashangilia
ajapo kutunadia
sera mpya watumia
ya kale umeitua
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

naomba mheshimiwa
tumechoka kuvamiwa
tweleze lifanikiwa
kuuondoa ukiwa
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

ama ndo yaleyale
watupigia kelele
na kutupeleka kule
likotutoa Nyelele
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

nabaki naililia
nchi yangu Tanzania
e Mola ninakujia
watoe watatuua
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

wametunyonya kutosha
nini wametubakisha
milango tu wanabisha
kututawala maisha
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

ila kwako ninakuja
najua wewe si Yahya
tuepushie hili ja
mpaka waone haya
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!

walitutukana sana
raisi bila hiyana
kura zetu siyo zana
kumnyima rudi tena
Kibeba visobebeka, silie vikilemea!
 
shairi lako zuri sana ndugu mwanakijiji lakini ukumbuke kasema mzee Sadan Abdul Kandoro ya kuwa
Mtu chake apendacho,hakina hila machoni
huridhika kuwa nacho, japo hakina thamani
mapenzi hayana kicho, yaamkapo moyoni
mwenye mapenzi, haoni ingawa macho anayo

kwa maana hiyo hata iweje atabebwa hivyo hivyo kwa kuwa tumempenda

Aliyasema Sadani, Abdul bin Kandoro,
Alilighani zamani, Wakati giza totoro
Zile Zama ujanani, elimu yetu totoro,
Kwa nini bado tubebe, kitu kiso na thamani?

Mapenzi hayana kificho, hiyo kweli nakubali,
Chochote nilichonacho, thamaniye ni halali,
watu kutolea macho, thamani yake dalili,
Katu tusiridhike, na kitu kiso thamani.

Mtu chake apendacho, budi kupendwa na wengi,
kuonwa na kila jicho, kusemwa na walio wengi
Umma ukisema hicho, pasipo kujali rangi
Kitu chenye thamani, ni kinachopendwa na wengi
 
Aliyasema Sadani, Abdul bin Kandoro,
Alilighani zamani, Wakati giza totoro
Zile Zama ujanani, elimu yetu totoro,
Kwa nini bado tubebe, kitu kiso na thamani?

Mapenzi hayana kificho, hiyo kweli nakubali,
Chochote nilichonacho, thamaniye ni halali,
watu kutolea macho, thamani yake dalili,
Katu tusiridhike, na kitu kiso thamani.

Mtu chake apendacho, budi kupendwa na wengi,
kuonwa na kila jicho, kusemwa na walio wengi
Umma ukisema hicho, pasipo kujali rangi
Kitu chenye thamani, ni kinachopendwa na wengi

Marehemu Joseph Mulenga alitungia wimbo akiwa na Sikinde
 
Back
Top Bottom