MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Nimekaa na kufikiria kitu. Nchi yetu tunasema ni secular na dini na serikali havi fungamani. Tunasema serikali haina dini lakini watu ndani ya serikali wana dini. Swali langu linakuja kama ni hivyo kwa nini viongozi wetu wengi huapa kwa kutumia vitabu vya kidini? Kwa nini wanaapa mbele ya Mungu wao lakini bado serikali yetu tunasema hakuna dini? Sijui kwa upande wa Uislamu ila kwa upande wa Wakristo najua kuapa ni dhambi kwa hiyo kwa nini viongozi wa Kikristo wana apa? Na wakati wa kiapo hapo wanaapa kwa Mungu, wananchi au kwa wote? Kama viongozi bado wanaapa kwa Mungu wao wamuaminio na bado huvunja hizo ahadi ni kwa vipi sisi wananchi tuna tegemea wata timiza ahadi zao kwetu? Labda ni mimi tu lakini hapa naona kuna walakini fulani.