Kuanzisha ngo: Msaada tutani

MAKOLE

JF-Expert Member
Feb 5, 2012
618
280
Poleni na hongereni kwa kazi wana jf. Naomba kwa mtu anayefahamu hatua za kuanzisha NGO, Ushauri wa usajili na masuala mengine ya ki uzoefu wa namna ya kuendesha NGO anieleze kupitia jf. Tafadhalini naombeni msaada wenu waungwana. NGO yenyewe inahusika sana na mojawapo kati ya mambo yafuatayo; Msaada wa kisheria kwa wanawake, miradi ya utunzaji mazingira, misaada kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum na waishio katika mazingira maalum, elimu kwa waathirika wa HIV/AIDS.
 
Unachotakiwa kufanya ni kuandaa katiba, ambapo mtaonyesha na muundo wa NGO yenu, majina ya viongozi, waweka saini ambao lazima ionekane wamepitishwa na vikao halali vya wanachama wa hiyo NGO. Kwa sasa NGOs zote zinaratibiwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na watkupa muongozo wa jinsi ya kuandaa katiba ni vyem ukajitahidi kutembelea website yao utapata muongozo na muundo wa katiba unaotakiwa. Katiba yenu lazima ipitishwe na wakili, mtaenda kuilipia then mtawasilisha katiba na risiti kwa mratibu wa NGO pale wizara ya jinsia ambapo mtapewa cheti cha usajili.

Baada ya hapo kazi kwenu!
 
usisahau picha 2 kwa majina ya viongozi na c.v zao kwa kuongezea maelezo ya hapo juu.
 
Fuata maelekezo ya bwana ndyoko bt kwenye kupitsha katba mtaandaa mhtasari wa kikao na kuonesha members na kuwapitsha viongoz accordng 2 muundo wa NGO yenu. Then mtaambnsha cv ya m/kit, mhazn na katbu thn mtapeleka na copy 3 za katba kwa usajil! Members msiwe ndugu wa damu
 
Uwe na katiba nakala 8 iliyopitishwa na wanachama. Cv za viongozi zilizobandikwa picha upande wa kulia. Barua ya kuomba Usajili kwa katibu tawala wilaya, barua ya utambulisho toka mtaani ilipo NGO pamoja na ya mtendaji wa kata, muhtasari wa kikao ulipoitisha katiba pamoja na saini zao, saini za waanzlishi wa NGO. Lazima uwe na ofisi na physical address. Nenda kwa afisa tarafa wa eneo husika, atakukagua na kukupa maelezo mengine.
 
Uwe na katiba nakala 8 iliyopitishwa na wanachama. Cv za viongozi zilizobandikwa picha upande wa kulia. Barua ya kuomba Usajili kwa katibu tawala wilaya, barua ya utambulisho toka mtaani ilipo NGO pamoja na ya mtendaji wa kata, muhtasari wa kikao ulipoitisha katiba pamoja na saini zao, saini za waanzlishi wa NGO. Lazima uwe na ofisi na physical address. Nenda kwa afisa tarafa wa eneo husika, atakukagua na kukupa maelezo mengine.



Ni nakala 3 sio 8, ufafanuzi wako mzuri pia
 
nenda direct wizara husika, ukianzia huku ofc za tarafa na wilaya wana urasimu angali huko wizarani unapata huduma direct. Katiba ni nakala 2 tu.
 
Back
Top Bottom