Kuanzia leo wimbo HAKUNAGA naanza kuuchukia..

JF mwenyewe amesema leo,kwamba chuki za watu wengine zinasababishwa na wivu tu. Ndio wewe hapo. Hupendi kuona jinsi ambavyo CCM iko mahiri kaika ku=connect na vijana.
Hao waimbaji hawana mwenyewe. Hata CHADEMA wakiomba wanaweza kuwapata. In fact,Freeman Mbowe owns a discoteche,kwa hiyo umaarufu wake unategemea pop music.
Zamani nilipokuwa jeshini,nilikuwa napenda sna kwenda Mbowe Disco. Nilikuwa nafikiria ,sijafika Mbinguni,lakini kama nikifika,nitakuta kwamba it is very much like this Mbowe Disco.
 
sikuwahi kuupenda simple patronizing lyrics reflecting stupidity and simple minds of our people.
Ni sawa na ule wa kishtobe unamnunulia kuku jamani nazichukia.
 
Let's be real. Tanzania tunapita katika kipindi cha mpito na kigumu sana.

Watanzania wanaanza kuamka na kutaka mabadiliko. Mabadiliko yanayotakiwa ni lazima yahusiane na kubadilisha CCM maana CCM yenyewe milele haitajibadili kama hakutakuwa na nguvu kutoka nje kuilazimisha ibadilike.

Kila mwanamuziki (watu wenye nguvu sana duniani) anayejihusisha na CCM, anaonekana kama ni mtu anayetaka CCM iendelee kuwepo na hataki mabadiliko. Lazima mtu kama huyu kuna watu wengi sana wanaoichukia CCM, watamchukia na yeye. Ila kuna wale wa CCM basi watampenda zaidi. Ila hii ni hatari sana kwa mwana muziki.

Hata mtu kama Sugu kwa kujipambanua kuwa ni CHADEMA, kuna CCM kibao kwa sasa hawampendi hata kumsikiliza. Ndiyo ubaya wa mwana muziki kujiingiza kwenye mambo ya siasa.

Kwa mwanamuziki Tanzania kwa sasa, wee imba nyimbo zako na usijipeleke kwa Chadema, CCM, CUF nk. Ukijipeleka tu huko basi kumbuka kuwa utakuwa umepoteza washabiki kadhaa wa kundi la upinzani.

Marlow alionywa hapa mapema sana ila akaoba watu wanachemka. Hakuna mtu huwa hapendwi kama KIBARAKA. Kama mkitaka kwenda kwenye kampeni za CCM au CHADEMA, basi hakikisheni mnavuta hela ya kutosha na baada ya hapo, anzisha biashara nyingine kabisa na achana na muziki. UAMUZI NI WENU.
 
Nau-delete kwenye desktop na laptop ya nyumbani,
Desktop ya ofisini,
Mp4 ya gari napo nautoa,
Kisha namalizia na kwenye simu kabisa!!!!
Tena nkiusikia redioni au kuuona kwenye Tv nabadilisha channeli kabisa.
Nymbani kwako ukipigwa siji!!
Wala nkiukuta unapigwa njia fulani naibadili hiyo njia na kupita nyingine!!
 
Sijaona kosa la huyo dogo kiasi cha kumshangaa na kumsakama hivyo. Mbona mnakuwa wakali na kutema povu kama mmebwia foma. Hivi kama yeye ni mwanachama wa CCM aache kusifia chama chake amsifie nani sasa. Mbona Sugu ni mwana bongo fleva na ni mbunge wa CDM lakini wanachama wa CCM hawatoi povu na wanasikiliza nyimbo zake kama kawaida. Huo ni ubaguzi na chuki za kijinga.
Nyimbo za Sugu na VINEGA havina ITIKADI za vyama Bali ni reality ya maisha Sasa huyu kakurupuka kwani mmesahau ya Marlow na kibao chake CHA pipipi yaliyotokea? Au Bushoke ni nini kimempata??? Tena ask ur self why Roma hatari Nyimbo zake zitumiwe na CDM japo ni mwanachama wa CDM refer wimbo wake aw mathematics
 
JF mwenyewe amesema leo,kwamba chuki za watu wengine zinasababishwa na wivu tu. Ndio wewe hapo. Hupendi kuona jinsi ambavyo CCM iko mahiri kaika ku=connect na vijana.
Hao waimbaji hawana mwenyewe. Hata CHADEMA wakiomba wanaweza kuwapata. In fact,Freeman Mbowe owns a discoteche,kwa hiyo umaarufu wake unategemea pop music.
Zamani nilipokuwa jeshini,nilikuwa napenda sna kwenda Mbowe Disco. Nilikuwa nafikiria ,sijafika Mbinguni,lakini kama nikifika,nitakuta kwamba it is very much like this Mbowe Disco.
Ulimanisha JK?
 
kuanzia leo natangaza kuacha kufagilia wimbo wa HAKUNAGA kwa sababu mwanamziki aliyeimba wimbo huu SUma lee kaamua kuubadilisha maneno yake na kuwa HAKUNAGA kama CCM (nimeona kweny TV akiwa Mwanza).

umeniboa sana Suma Lee. laiti ungejua kuwa una mashabiki wa aina tofauti tofauti usingefanya kitendo cha kipuuzi kama hiki. umeboa sana

Ulitaka asiimbe akale wapi?Yeye yupo kazini bwana!
 
Suma Lee muacheni jamani, hivi kama hao wa chama kigumu wamezileta kirahisi rahisi aziachie kirahisi rahisi?
Wajinga ndio waliwao bana, Suma Lee ukipata tumia.
 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom