Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Ukweli ni kwamba hatujui yatamsaidia vipi mwananchi, lakini yanaweza kabisa kuleta mabadiliko makubwa ya uongozi katika Tanzania. Chama kipya kinaweza kuingia madarakani na kikaja na sera tofauti ambazo zitapunguza au kuondoa kero na manun'guniko mbali mbali ya wananchi kama vile mikataba ambayo haina maslahi kwa Tanzania na Watanzania.

CCM (TANU) imekaa madarakani miaka 46 sasa lakini bado maendeleo yetu ni madogo mno. Tunaweza tukasema wakati wa mwalimu tulikuwa hatuna vianzo vingi vya mapato kama ilivyo sasa. Tunakusanya kodo ya bilioni 260 kwa mwezi, tuna mikataba ya madini ambayo haina maslahi yoyote kwa Tanzania, gesi kuna afadhali kidogo. Ufujaji wa mali ya umma umekithiri, kwa mfani ununuzi wa magari ya kifahari.

Sasa kama CCM itameguka lolote linaweza kutokea, ama kwa manufaa ya Tanzania na Watanzania ama kwa manufaa ya wajanja wachache. Kama nchi inaweza kuongeza ukusanyaji wa mapato hadi kufikia bilioni 260 kwa mwezi na bado wananchi wengi hawaoni mabadiliko yoyote basi kuna kasoro kubwa sana.

Baada ya miaka 46 ya uhuru kuna haja ya CCM kumeguka, hili linaweza kabisa kuwa mwanzo wa mapinduzi ya kweli ndani ya Tanzania, hakuna haja ya kusubiri miaka mingine 46.

Sioni kama kuna usanii wowote, usanii ni kuombea dua CCM iendelee kubaki madarakani na nguvu ilizonazo ili kufuja pesa za walala hoi na kudai eti kumeguka kwa CCM hakutakuwa na manufaa kwa mwananchi. Wote hatulijui hili kunaweza kukawa na manufaa au la.
 
Mzee Bubu,

Heshima mbele, tunakuwa waangalifu sana kwenye kuliangalia hili suala la makundi, maana hata hili la mtandao kule BCS tuliambiwa kuwa litafanya maajabu makubwa kwa wananchi litakapopata power, na here we are!

One thing I know, ni kwamba watu waliokaa madarakani for the last 44 years, wanaweza kumeguka tu pale itakapoonekana kuwa kuna dalili za kushindwa na upinzani, kumbuka kuwa haya makundi sasa hivi na siku zote yanaunganishwa na one goal, ambayo ni power, I saw it kwenye uchaguzi uliopita,

Alll the heavyweights wa nchi, walikuwa hawaamini kuwa Muuungwana anaweza kuwa rais, the minute wamegundua kuwa ndiye atakayekuwa, wote wakabadilika na kuanza kumuuunga mkono, isipokuwa mtu mmoja tu mzee KK, ambaye sasa hivi ni mshikaji wake anyway, na anao mpak mahawara wawili ambao ni mawaziri,

sasa wananchi ni lazima tuwe careful kwa sababu hata hizi maneno ya makundi kumeguka zinaweza kuwa ni planted stories by hao hao, kwa sababu after hiii ya ac ni kitu gani hawawezi fanya ku-cling to power? Warioba alijaribu kupiga kelele lakini wapi sasa na yeye ni one of them!
 
CCM imekuwa madarakani kwa muda mrefu kiasi kuwa wamechukulia for granted kuwa uongozi wa nchi ni haki ya CCM. Mimi nafurahi kwepo kwa makundi haya huko CCM ili kidhoofike na hivyo kuacha kuchukulia uongozi for granted. Kikishagawanyika, makundi yote mawili hayatakuwa na nguvu tena ya kujihakikishia madaraka. Kwa hiyo wataanza kushindana katika kuwatumikia wananchi kwa dhati ili wapate uongozi.
 
Ukweli ni kwamba hatujui yatamsaidia vipi mwananchi, lakini yanaweza kabisa kuleta mabadiliko makubwa ya uongozi katika Tanzania. Chama kipya kinaweza kuingia madarakani na kikaja na sera tofauti ambazo zitapunguza au kuondoa kero na manun'guniko mbali mbali ya wananchi kama vile mikataba ambayo haina maslahi kwa Tanzania na Watanzania.

CCM (TANU) imekaa madarakani miaka 46 sasa lakini bado maendeleo yetu ni madogo mno. Tunaweza tukasema wakati wa mwalimu tulikuwa hatuna vianzo vingi vya mapato kama ilivyo sasa. Tunakusanya kodo ya bilioni 260 kwa mwezi, tuna mikataba ya madini ambayo haina maslahi yoyote kwa Tanzania, gesi kuna afadhali kidogo. Ufujaji wa mali ya umma umekithiri, kwa mfani ununuzi wa magari ya kifahari.

Sasa kama CCM itameguka lolote linaweza kutokea, ama kwa manufaa ya Tanzania na Watanzania ama kwa manufaa ya wajanja wachache. Kama nchi inaweza kuongeza ukusanyaji wa mapato hadi kufikia bilioni 260 kwa mwezi na bado wananchi wengi hawaoni mabadiliko yoyote basi kuna kasoro kubwa sana.

Baada ya miaka 46 ya uhuru kuna haja ya CCM kumeguka, hili linaweza kabisa kuwa mwanzo wa mapinduzi ya kweli ndani ya Tanzania, hakuna haja ya kusubiri miaka mingine 46.

Sioni kama kuna usanii wowote, usanii ni kuombea dua CCM iendelee kubaki madarakani na nguvu ilizonazo ili kufuja pesa za walala hoi na kudai eti kumeguka kwa CCM hakutakuwa na manufaa kwa mwananchi. Wote hatulijui hili kunaweza kukawa na manufaa au la.
Hivi tujiulize nini hasa kinawafanya wawe na Makundi?Na Chama Ni Wanachama ambao ni watu, je hao ambao wametoka kwenye CCM Hiyo uliyosema haijaleta maendeleo kwa kutoridhishwa na nafasi walizopo kiuongozi watabadilika vipi kimaadili? je kutoridhishwa kwao kwa nafasi za uongozi walizonazo kunatusaidiaje walalahoi wote ktk Nchi yetu Tanzania?
 
Mimi naamini kwamba kuvuja kwa pakacha ni nafuu ya Mchukuzi!...

CCM kama kweli wana matatizo ndani basi ndio mwanzo wa kuwepo na mfumo mpya wa Uongozi. Ni vizuri kuwa na positive hope kwa sababu ogonvi kati ya makundi haya ni kuhsu ULAJI tu! hakuna kingine! Kuna kundi linafaidika zaidi ya jingine na bora kwetu yaendelee hivi kwani mmoja wao akishindwa kuvumilia atauanika ukweli kwa wananchi!..
hadi leo hatufahamu kwa undani nini hasa kazi za Mtandao na akina nani wamejichimbia ktk lingo hili.
Na kumbuka ili kumshinda mwenza lazima mmoja wao atakuwa anasimamia haki!... suluhisho ndani ya chama ni ishara mbaya zaidi kwetu kwani watakuwa wamekubaliana jinsi ya kugawana. Na wakikubaliana wao basi tumeliwa na kundi kubwa zaidi...kundi ambalo litatumaliza vibaya zaidi.
 
Mzee ES heshima ikurudie na wewe Mkuu. Ukweli ni kwamba mimi naamini CCM kuna makundi yaliyosababishwa na uchaguzi wa kupata mgombea wa CCM katika uchaguzi mkuu wa 2005. JK ili kuhakikisha anarudisha umoja ndani ya CCM alitakiwa kuwapa nyadhifa hata wale ambao hawakumsupport katika kuwa mgombea wa CCM.

Bado ana nafasi ya kurekebisha kasoro hiyo ili kuleta umoja ndani ya CCM. Watanzania wengi tulikuwa na imani kubwa sana na JK, lakini baada ya zaidi ya mwaka mmoja imani zetu zimepungua sana, sijui ni watendaji wabovu aliokuwa nao au ufuatiliaji finyu.

Kwa hali hiyo basi kama makundi haya yatasababisha CCM kumeguka basi hili linaweza kuinusuru Tanzania na Watanzania kwa kupata chama kipya madarakani ambacho kitakuja na sera mpya ambazo zitakuwa ni sera za kweli za kuyakwamua matatizo mbali mbali ya Watanzania.

CCM sasa hivi imekuwa na nguvu mno na hata kuwa na jeuri ya kutowasikiliza wananchi katika maswala mbali mbali yakiwamo ya ufujaji wa mali za umma kwa kununua magari ya anasa ambayo hayaendani na hali halisi ya nchi yetu, mikataba ya ubabaishaji, rushwa iliyokithiri n.k. Kama alivyosema mjumbe mmoja, kuvuja kwa pakacha.....
 
http://www.mwananchi.co.tz/habari/habari0.asp
Nchimbi sasa anataka urais akiwa na Kamalla wote wana PHD fake. na masters fake

Hapo ndipo ujue Tanzania ilivyo na matatizo ya kupata viongozi kama watendeleza jadi kuwa viongozi wanatoka CCM. Kumbuka wote wamo kwenye serikali ya sasa hivi na wote walisoma pamoja pale Mzumbe kabla ya kununua Ph.D kama waalimu wao. Unaweza kufanya extrapolation kuona mambo yenyewe yakoje sasa hivi. Ndiyo maana somewhere nikasema ni afadhali Amina Chifupa kuliko Emmanuel Nchimbi na wafuasi wake. AC anajiamini wakati EN hajiamani bali anategemea kutumia mbinu chafu; tatizo la JK sasa hivi ni sawa kabisa na kama alilo nalo EN.

Nungwi aliwahi kusema kuwa EN atakuwa next president na nadhani Nungwi yuko karibu sana au ndiye EN mwenyewe kwa hiyo anajua ya moyoni kwake. Tusubiri another 20 years or more chini ya uongozi wa namna hii au tufanye mabadiliko mara moja, hiyo ni juu ya wananchi wa Tanzania wenyewe; wakitumia kura yao vibaya basi wameliwa tena. Ningeshauri kukata mzizi wa fitina mara moja mwaka 2010 kabla mambo hayajaenda vibaya zaidi.
 
Kaka Kichuguu.

EN ni mchawi mwenyewe au ana kamati yake ya ufundi? kwanini tusimtumie mechi ya Taifa stars na senegal june 2?
jee unayo Link ya Nungwi kudai Nchimbi ni next president? naiomba maana lisemwalo lipo.

huyo Msolla anafanya nini kukumbatia phd fake? DR.Mwakyembe kauwasha moto bungeni lakini hakuna action yeyote au Msolla nae fake?
nimepitia bunge la UK kuna wabunge 646 hakuna phd hata tano na professor ndio kabisa!
vipi Bunge letu limejaa madokta fake?
 
Kaka Kichuguu.

EN ni mchawi mwenyewe au ana kamati yake ya ufundi? kwanini tusimtumie mechi ya Taifa stars na senegal june 2?
jee unayo Link ya Nungwi kudai Nchimbi ni next president? naiomba maana lisemwalo lipo.

huyo Msolla anafanya nini kukumbatia phd fake? DR.Mwakyembe kauwasha moto bungeni lakini hakuna action yeyote au Msolla nae fake?
nimepitia bunge la UK kuna wabunge 646 hakuna phd hata tano na professor ndio kabisa!
vipi Bunge letu limejaa madokta fake?

Aisee link yenyewe ni hii hapa. Samahani kwa kuchukua muda mrefu kuipata kwa vile ilitolewa siku nyingi sana wakati tunajadili Ph.Ds za Mzumbe; ameandika hivyo kweye paragraph ya mwisho kabisa.
 
Ole waliojishika na utawal uliokwisha anguka.
Ukitaka kujua watu sasa ni vipofu, hawaoni CCM imeshaanguka...!

Wajishike wapi ni swali sasa, lakini hata hivyo wakati huu tukitafuta jibu, tujue mti wetu umeshaanguka.
 
Na hata hao wanaoitafuta Ikulu kwa udi na uvumba tabu tupu,mnakumbuka ile ishu ya wabunge wa CUF kupeleka vimada vyao ughaibuni? mnafikiri wakishika Dola nini ni kitafanyika zaidi ya kuhamishia ndugu na vimada vyao wote ughaibuni ! mara nyingi twashauriwa kuangalia tulipojikwaa sio tulip angukia
 
Na hata hao wanaoitafuta Ikulu kwa udi na uvumba tabu tupu,mnakumbuka ile ishu ya wabunge wa CUF kupeleka vimada vyao ughaibuni? mnafikiri wakishika Dola nini ni kitafanyika zaidi ya kuhamishia ndugu na vimada vyao wote ughaibuni ! mara nyingi twashauriwa kuangalia tulipojikwaa sio tulip angukia

Kwaiyo unashauri CCM waendelee kupewa madaraka na kuendelea kufisadika huku tunawaangalia, hii haiwezekani kwani hata waupinzani wakiingia wakachemsha tutawaondoa tu.
 
Ole waliojishika na utawal uliokwisha anguka.
Ukitaka kujua watu sasa ni vipofu, hawaoni CCM imeshaanguka...!

Wajishike wapi ni swali sasa, lakini hata hivyo wakati huu tukitafuta jibu, tujue mti wetu umeshaanguka.

imeagukaje chali au kifudifudi?Nini kimeiangusha ?fafanua ili nasi tuangue kilio au tufurahi
 
ccm haijaanguka bado lakini ipo njiani.....kila unapokwenda watu wanailaani.
 
Na hata hao wanaoitafuta Ikulu kwa udi na uvumba tabu tupu,mnakumbuka ile ishu ya wabunge wa CUF kupeleka vimada vyao ughaibuni? mnafikiri wakishika Dola nini ni kitafanyika zaidi ya kuhamishia ndugu na vimada vyao wote ughaibuni ! mara nyingi twashauriwa kuangalia tulipojikwaa sio tulip angukia

Hatusemi kuwa hakuna elements mbaya kwenye vyama mbadala wapo, ila kinaschozungumziwa hapa ni kutoa wapiga kura uoga.Ndiyo maana PNU imekataliwa kenya,pamoja na kuitoa kanu madarakani.Hii ndio siri ya madiliko kuwa kuna kipindi cha mpito kuelekea kwenye demokrasia iliyokomaa.Hpo hata poland ali9chaguliwa Lech Walesa na Solidarity yake,alipovurunda wanasiasa mahiri zaidi wakajitokeza nakufanikisha demokrasia endelevu.
Hiyo inamaanisha kuwa lazima bango la madiliko libebwe na watu wasioogopa vitisho vya watawala na hofu za akina Tomaso wa kisiasa .Lech Walesa na solidarity hawakuogopa vitisho vya wakomunisti wa Poland.
TYanzania bila CCM inawezekana play your part.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom