hakuna hasara, ni faida sana tena hakuna raha kama ya kuandamana na mpenzi/mke/mume wako!
tena uswahilini mvuta bangi mmoja anaweza akaamua kuanza kukutukana matusi ya nguoni mbele ya wife.hapo itabidi ufe(upigane) kulinda heshima inapobidini jambo zuri lakini inategemea na maeneo mnayoambatana.maeneo ya uswahilini ni karaha tupu na umbea kila kona kiasi kwamba mnakuwa hamuoni hata hiyo raha ya kuwa pamoja.
kuandamana kila sehemu ni ishara kwamba you are both comfortable and proud of each other, in many cases hii kitu huboresha penzi na kuongeza maelewa na kuaminianaKuna watu huandamana na wake zao au wapenzi wao popote waendapo,hao huitwa kumbikumbi,na wapo wanaosema,kuandamana na mpenzi wako kila uendako si tabia nzuri,
ina hasara nyingi sana kuliko faida Mwana JF unasemaje?
Kuna watu huandamana na wake zao au wapenzi wao popote waendapo,hao huitwa kumbikumbi,na wapo wanaosema,kuandamana na mpenzi wako kila uendako si tabia nzuri,
ina hasara nyingi sana kuliko faida Mwana JF unasemaje?
Ni vyema sana kuandamana pamoja
au mie cjawaelewa maandamano mnayoyazungumzia hapa? yaani leo tunatoka job tnaandamana bar huko wanakodaigi wanaenda kupoteza mawazo ya kikazi tunatoka huko cjui saa 4-5? au ni maandamo ya kivipi? mana hayo mie ctayaweza kabisa, hivi mtaandamanaje kila mahali?
kuandamana, bar,hotelini,vikao vya arusi.sherehe,mpirani,kuona ndugu,kanisani,msikitini,kwenye muziki/burudani,shambani,safarini............
Ni vema kuandamana lakini siyo ndo kila siku kila mahali. Nahisi kama inaweza fika wakati mtabore hivi! Mmelala wote usiku kucha mnazunguka wote mchana kutwa....siku mbili tu mmeshachokana. Stori zitaisha maaana matukio yote mpo pamoja! Au kuna kitu sijaelewa hapa! to me kuandamana occassionally kuna 'ladha' zaidi kuliko kila siku! Hata kisaikolojia kuna nyakati mtu anahitaji muda wa kuwa peke yake.