Ktk hili waziri wa Afya hastahili kuwajibika?

Kaitaba

JF-Expert Member
Jun 30, 2009
916
49
Ikiwa imepita miezi kadhaa tangu mamlaka ya chakula na dawa TFDA itangaze kuwa dawa za metakelfin zisitumike kwa sababu kuna za bandia,

Imegundulika kuwa dawa za kutibu malaria zinazoitwa Duo-cotexin zipo za bandia, na zinatumika mpaka sasa,

Sababu inayonifanya nione anatakiwa kuwajibika ni hii;

Hivi mimi na wewe tunaweza kutengeneza dawa? jibu ni hapana, ina maana wanaotengeneza za bandia ni wale waliopitia fani yake hivyo anawafahamu,

Kama zinatoka nje kama wao walivyojitetea, mipakani hakuna watendaji wake?,

Basi tuseme hausiki kwa njia moja au nyingine, basi ajiudhulu katika hali ya kuonesha kuwa amesikitishwa na madhala yatakayowapata watu waliokwisha tumia dawa hizi, na wanaoendelea kutumia hadi leo hii.

WATANZANIA TWAFWA!!!!!!!!!!!
 
Kaitaba

Kwanza kabisa, Metakelfin haijapigwa marufuku, ni ile metakelfin feki ndio tatizo

pili, suala la dawa feki [counterfeit] ni pana sana duniani!!! Lilianzia nchi zilioendelea hukohuko na hiyo biashara ilitokana na bei za juu za dawa. Tatizo ni zaidi ya tanzania, ni zaidi ya africa na linahitaji dunia nzima kupambana kwa pamoja, ni sawa na noti bandia---itakuwa sio fair kumwambia waziri wa fedha ajiuzulu simply kwasababu kuna noti feki

Cha maana hapa ni kuwezesha mfumo tulionao kusaidia na wenzetu kupambana na madawa feki. Vita bado ngumu kwasababu wanaoingiza hizi dawa wengi wanajulikana ila corruption ndio inatumaliza

Natamani mtu wa TFDA angekuwepo humu kutoa shule maana tupo wengi tunaohitaji kujua zaidi kuhusu dawa feki

Lastly, kulia pekee haisaidii, chapa mtu kiboko ya t*ko harafu asikizie maumivu
 
Wakunga wa jinsia yangu watanitibu mimi. Sijawatukana swahiba.

Sawa mkuu

Tatizo la nchi yetu ni kwamba clients huwa hatujui haki zetu kabisa.. na wahusika hawatupi nafasi ya kujua haki hizo
 
Lakini pamoja na hayo, hivi huyu waziri haoni kuwa wananchi wengi watakufa au kuugua kansa kwa sababu ya kutumia madawa feki ya malaria,

Mimi naona waruhusu chloroquin ziendelee kutumika, maana kabla hawajaizuia hakukuwa na dawa bandia,

Mzee mwinyi alipokuwa waziri wa mambo ya ndani, wananchi waliuawa kanda ya ziwa, ktk kuonesha kuskitishwa kwake, alijiuzuru, hata huyu afanye hivyo.
 
Lakini pamoja na hayo, hivi huyu waziri haoni kuwa wananchi wengi watakufa au kuugua kansa kwa sababu ya kutumia madawa feki ya malaria,

Mimi naona waruhusu chloroquin ziendelee kutumika, maana kabla hawajaizuia hakukuwa na dawa bandia,

Mzee mwinyi alipokuwa waziri wa mambo ya ndani, wananchi waliuawa kanda ya ziwa, ktk kuonesha kuskitishwa kwake, alijiuzuru, hata huyu afanye hivyo.

Ahh, ndugu yangu Kaitaba... watu wanatofautiana!!! Nadhani hajui kwamba kuna watu wanatamani ajiuzulu
 
Tatizo la Dawa Feki ni pana sana kama MTM alivyosema. Swali: Kuna waliokamatwa? Wametozwa faini au wapo Keko? Au wanatesa wakijiandaa kutuletea dawa feki nyingine?
 
Kwa vile dawa ni zile za bei kubwa, kuanzia 5,000/= na kuendelea, na zinatoka nje

umefika wakati serikali itengeneze dawa zote hapa hapa nchini na ziuzwe kwa bei nafuu badala ya kuagiza, hiki ndicho namaanisha ajitoe, wenye ubunifu waingie ofisini
 
Kwa Ufahamu wangu mdogo,metakelfin iliyopigwa marufuku ni ile ya pfizer (wenyewe tunaiita ya italy).Na tatizo la duo-cotexin fake si la leo na lilianzia kenya kitu kilichosababisha watengezaji kusikusanya duo-cotexin zote na kuziondoa sokoni.Walipofanya uchunguzi wakagundua nazo zimetengenezwa china.Walichofanya ni kutoa toleo jipya ambalo katika packet yake pana seal inayong'aa kutofautisha na zile fake.Sasa sina hakika kama wasanii wameweza pia kuitengeneza hiyo seal na kuiweka kwenye hizo dawa zao fake,lakini pia packet zao zinatofautiana.Lakini nakumbuka zote mbili zilikuwepo sokoni yaani zenye seal na zile zisizokuwa na seal,na mbaya zaidi nilipozifanyia uchunguzi zile zisizokuwa na seal,nilikuta zina namba ambayo uwekwa katika dawa inayoruhusiwa kuingia sokoni(ni kama tini namba) ambayo nafikiri utolewa na TFDA,kwa kweli nilishindwa kujenga hoja.Hivyo si vibaya ukitaka kununua duo-cotexin ukawa unatafuta ile yenye seal,atleast for the time being.Siasa za dawa nazo wakati mwingine ni ngumu sana kama mkataba wa richmond.
 
Not in TZ. mmeshindwa kutengeneza viatu na viberiti, dawa mtaweza?
Mafamasia tuanao wa kutosha, viwanda vipo kumbuka chloroquine kuwa ilikuwa inatengenezwa Keko pharmaceutical Industry (KPI), pia kwa sasa wameanza kutengeneza ARV`s.

Kama wameweza ARV`s watashindwa ant malarial
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom