Krismas hii Ngina amenitoa jasho kweli!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Kule kwetu kijijini enzi zetu tulikuwa tunajua sikukuu tatu tu kwa mwaka, kulikuwa na sikukuu ya idi, Krismas na kuzaliwa kwa chama cha TANU, kwa hiyo wazazi walikuwa hawaumizi kichwa sana kuhusu nguo za sikukuu, kwani ni sikukuu moja tu tulikuwa tunapata nguo mpya. Kwa wakiristo walikuwa wanapata nguo mpya wakati wa Krismas na waislamu walikuwa wanapata nguo mpya wakati wa Idi.

Hata hivyo nikisema nguo mpya sina maana ya baba kwenda dukani na kununua nguo mpya kwa ajili yako, hapana. Nguo mpya ilikuwa na maana baba kuchukua suruali yake ya zamani, kuikata kwa wembe vizuri bila hata kukupima. Halafu angeipinda chini kwa umahiri mkubwa. Shughuli ingekuja kwenye ukubwa wa kiuno. Kwa sababu hakuwa na ujuzi wa kupunguza kiuno, angetafuta mkwiji, yaani tambara kama mkanda. Angekuita na kuanza kukupa semina kwanza kabla hajakupa hiyo nguo mpya. Angekwambia, yeye kama baba wa familia anajitahidi sana kuona familia yake inafurahiya sikukuu. Angesema, kuwa amejitolea hata kutoa nguo yake ya pekee kwa ajili yako. Halafu angekupa hilo suruali ambalo alikuwa analivaa siku akienda kuwasalimia wakwe zake tu.

Angekwambia ujaribu sulupwete hilo na angekupa pamoja na ule mkwiji ili sulupwete hilo lisidondoke. Angekusaidia kufunga mkwiji na kukuambia, 'hebu tembea.' Halafu angesema, ‘umependeza kwelikweli.' Kwa sababu ya utoto na ushamba wa wakati ule usingejua kwamba, sulupwete hilo linakufanya ufanane kama kifurushi cha viazi vitamu. Lakini, kwa sababu kule kwetu wakati ule, kila mmoja alikuwa anakatiwa kipande cha suruali na baba yake na kuhesabiwa kuwa amepata nguo mpya, hakuna aliyejali. Nawasifu sana wale wazee wa enzi za utoto wetu. Ni kweli kabisa, nguo mpya maana yake ni nguo ambayo hujawahi kuivaa. Kama baba yako aliivaa na kukupatia wewe, kwako ni lazima iwe mpya.

Lakini huku mjini na kwa watoto wa sasa, mambo ni kinyume kabisa. Krismas hii wanangu hawa watatu wamenitoa jasho kwelikweli, hususan huyu binti yangu Ngina, Binti huyu ananipa ugonjwa wa moyo kila uchao. Wiki moja kabla ya ujio wa sikukuu hii ya Krismas wanangu walitaka kujua nitawanunulia nguo za aina gani. Niliwambia hali ya uchumi hairidhishi na nikaona ni wazo zuri kusingizia umeme. Niliwaambia, kiwanda cha kutengeneza fedha kimesimama kuzalisha kwa sababu ya umeme. Huyu mwanangu Ngina mwenye kiherehere kama bibi yake mzaa mama, alinikata kalma na kusema, ‘baba fedha zinatengenezwa Ulaya siyo hapa nchini. Tuna orodha ya nguo tunazotaka tunataka kwenda na fasheni safari hii, mie bila skin jinzi hapatatosha hapa.'

Nikajua walimu wa siku hizi ni wataalamu hasa, yaani mtoto wa darasa la nne ameshafundishwa kuwa fedha zinatengenezwa Ulaya! Ikabidi nijifanye sikusikia maelezo ya huyu binti yangu ambaye kwa kawaida ndiye anayeongoza migomo kwenye familia yangu. Nikawaambia kama wanataka, nitajitahidi kila mmoja apate gauni, shati na suruali ya mtumba. Kusikia hivyo, watoto wakasema, itakuwa ngumu wao kukubali kuvishwea mitumba. Ngina alikuja na wazo mbadala, alisema, kama sina hela ni afadhali tuuze TV yetu. Lakini wenzake walipinga lile wazo wakidai watakosa kuona Ze Comedy. Ngina hakukubali kushindwa akaja na wazo lingine akitaka niuze Music System yangu ili wapate nguo za sikukuu. Nilipinga wazo hilo na kumfokea kwa kuwa na mawazo mufilisi. Lakini wapi, Ngina hakubali kushindwa, alinijia juu akidai ni jukumu langu kuhakikisha wao wanapata nguo za sikukuu, kwa hiyo nipunguze jazba tuweze kujadili hadi kufikia muafaka. Nilimuonya achunge kauli zake za maudhi.

Hata hivyo alikuja na wazo lingine, alinitaka nikakope. Alinishauri nikakope kwa jirani yetu mmoja ambaye aliwahi kunituhumu kwamba ninamilki mtandao wa wezi wa magari baada ya kuniona nikija na magari tofauti hapo nyumbani karibu kila siku. Magari ambayo yalikuwa ni ya kazini kwangu. Huyu jirani alinichongea Polisi nikaja kusachiwa na kupelekwa kituoni kutoa maelezo. Nilikuja kugundua kwamba ni nuyu jirani yangu ndiye aliyenichongea, kwani baada ya kukamatwa na kupelekwa Polisi huku nyuma alitamba kwamba mwaka huo lazima nifungwe.

Ilibidi nigeukie Dini na kuwaambia kwamba, hata bwana wetu Yesu Kristo katika kueneza Injili wakati huo alikuwa na nguo moja tu na hakuwahi kwenda na fasheni. Wote walinijia juu wakidai nimemkashifu Bwana Yesu Kristo na watamwambia mchungaji. Nikaona ule mjadala utakuwa hauishi kama nisipokuwa makini. Niliwaomba waandike mahitaji yao, kisha nitaangalia uwezekano wa kuomba mkopo kibaruani kwangu. Nikawa nimeufunga ule mjadala.Ama kweli watoto wa kizazi hiki, hawana maadili kabisa.
 
Watoto wa siku hizi wananifurahisha jinsi wanavyotambua haki zao mapema, hizi siyo enzi za ndiyo mzee tena, lol,.
 
Nadhani ni muhimu kuwafundisha watoto wetu negotiation skills. Na watambue kuwa sio kila wanachotaka maishani watapata 100%. Wanangu watajua one principle: tutakopa kwa ajili ya vital (sio hata basic needs tu! I mean food and shelter) na hatuko desperate for anything! Dingi, utatengeneza kizazi tunachoona maofisini, nina coaligue huwa wakija wale machinga wenye magari wanaotoka china na belgium kusanya, anakopa nguo zake na za wanae worth tshs 2M! Anakopa hadi miwani ya jua! Sijui anaishije huko mtaani kwake!
 
Duh! Nimeipenda na imenikumbusha zamani.hilo sulubwete.kwa watoto wengine ambao tulikuwa tukichimbwa biti na wazazi basi tulikuwa tunafanya maandalizi ya mda mrefu sana ili siku ikifika basi tayari tunakuwa na kianzio.
 
Sio hawana maadili bali baadhi yao wana akili zinazojitegemea, unatakiwa ufurahi badala ya kumsema hana maadili.
My dear Lizzy, kusema kweli ni kukosa maadili, yaani mwanangu mwenyewe wa kumzaa, ajibishane na mimi kama vile anajibishana na mtoto mwenzie! hiyo haikubaliki, wakati mwingine natamani kukatandika, sema tu kaliugua sana utotoni mwake!
 
Nadhani ni muhimu kuwafundisha watoto wetu negotiation skills. Na watambue kuwa sio kila wanachotaka maishani watapata 100%. Wanangu watajua one principle: tutakopa kwa ajili ya vital (sio hata basic needs tu! I mean food and shelter) na hatuko desperate for anything! Dingi, utatengeneza kizazi tunachoona maofisini, nina coaligue huwa wakija wale machinga wenye magari wanaotoka china na belgium kusanya, anakopa nguo zake na za wanae worth tshs 2M! Anakopa hadi miwani ya jua! Sijui anaishije huko mtaani kwake!


King umeongea jambo la maana sana. Watoto wa siku hizi, kwa vile baadhi yao huwa wanaona kila siku wanakula, wanavaa, wanaenda shulenzuri, basi huwa wanajisahau kuwa kuna kukosa na sio kila kitu wanachotaka wanakipata. Matokeo yake wanakuwa na matarajio makubwa sana hasa wanapokuwa wanahitaji kitu, hawaachi kukuganda. Nadhani kuwafundisha negotiations skill is the way.....
 
Nadhani ni muhimu kuwafundisha watoto wetu negotiation skills. Na watambue kuwa sio kila wanachotaka maishani watapata 100%. Wanangu watajua one principle: tutakopa kwa ajili ya vital (sio hata basic needs tu! I mean food and shelter) na hatuko desperate for anything! Dingi, utatengeneza kizazi tunachoona maofisini, nina coaligue huwa wakija wale machinga wenye magari wanaotoka china na belgium kusanya, anakopa nguo zake na za wanae worth tshs 2M! Anakopa hadi miwani ya jua! Sijui anaishije huko mtaani kwake!

Mwanangu,uliyoyasema ni ya kweli kabisa, kuna watu wanashindwa kutofautisha kati ya uhitaji na utashi na hao wako kila mahali duniani kote. mimi najitahidi sana kununua kulingana na uhitaji na siyo utashi................kama mulivyosema kitu muhimu ni uhakika wa kuwa na chakula, malazi na mavazi................Nikisema chakula sina maana ya Pilau, kuku, nyama, mayai, maini nk, na nikisema malazi sio kulala kitanda cha sita kwa sita, godoro la springi sijui la milioni ngapi na mito lukuki kitandani na midoli isiyo na idadi, na nikisema Mavasi sina maana ya Suti, skin jinzi, magauni ya Boutique, vipodozi vya gharama na kila aina ya ghasia................
 
kikazi kipya iko............... yan watoto wa siku iz wana mahitaj balaa. sijui kwa kwel 2nakwenda wap maana wamekuwa balaa.
umenichekesha bila skin jeans hapatoshi lol.
 
My dear Lizzy, kusema kweli ni kukosa maadili, yaani mwanangu mwenyewe wa kumzaa, ajibishane na mimi kama vile anajibishana na mtoto mwenzie! hiyo haikubaliki, wakati mwingine natamani kukatandika, sema tu kaliugua sana utotoni mwake!
Wala hawana makosa Mtambuzi kwa kuwa hivyo ndivyo walivyolelewa, mbona sisi tulikuwa na bado tuna maadili mazuri? kwanini wao wasiwe nayo? whats wrong with them? Kosa ni kwa walezi wala si mwingine au mtoto.
 
Umenikumbusha mengi hasa huo utaratibu wa nguo za sikukuu...baba yangu alipenda sana kunirushia makaptura yaliyokatwa kukoka katika suruali zake za zamani. Hakuwa maskini sana wakati ule,hebu fikiria meneja wa duka la kijiji,duka ambalo halikuwa na mshindani...kununua redio ya mbao lazima ujaze fomu maalum. RIP dad! Hata hivyo adhabu niliyompa ni kutotumia jina lake...majina ya ubin situmii jina lake...jamaa alikuwa mpuuzi sana,
 
mfundishe Ngina kuwa si kika atakacho atapata. Halafu usiwazoeshe watoto nguo mpya sikukuu. Mie wazazi wangu walikuwa wananipa nguo mpya miezi ya kawaida. Sikukuu hakuna nguo mpya
 
My dear Lizzy, kusema kweli ni kukosa maadili, yaani mwanangu mwenyewe wa kumzaa, ajibishane na mimi kama vile anajibishana na mtoto mwenzie! hiyo haikubaliki, wakati mwingine natamani kukatandika, sema tu kaliugua sana utotoni mwake!

Basi inabidi ujilaumu kwa kiasi kikubwa maana wewe ndie uliyetakiwa kumfunza maadili unayotamani/taka angekuwa nayo. Anza sasa ili mwakani aombe tu na ukisema haiwezekani atulie.
 
Mtambuzi pole sana. Namfagilia mwanao Ngina. Angeomba ndege au gari ningeshangaa lakini nguo!!! Hiyo kawaida fanya kazi inayolipa bana. Ongeza uwezo wako wa kupata pesa. Watoto wana imani na baba zao.
 
Kule kwetu kijijini enzi zetu tulikuwa tunajua sikukuu tatu tu kwa mwaka, kulikuwa na sikukuu ya idi, Krismas na kuzaliwa kwa chama cha TANU, kwa hiyo wazazi walikuwa hawaumizi kichwa sana kuhusu nguo za sikukuu, kwani ni sikukuu moja tu tulikuwa tunapata nguo mpya. Kwa wakiristo walikuwa wanapata nguo mpya wakati wa Krismas na waislamu walikuwa wanapata nguo mpya wakati wa Idi.

Hata hivyo nikisema nguo mpya sina maana ya baba kwenda dukani na kununua nguo mpya kwa ajili yako, hapana. Nguo mpya ilikuwa na maana baba kuchukua suruali yake ya zamani, kuikata kwa wembe vizuri bila hata kukupima. Halafu angeipinda chini kwa umahiri mkubwa. Shughuli ingekuja kwenye ukubwa wa kiuno. Kwa sababu hakuwa na ujuzi wa kupunguza kiuno, angetafuta mkwiji, yaani tambara kama mkanda. Angekuita na kuanza kukupa semina kwanza kabla hajakupa hiyo nguo mpya. Angekwambia, yeye kama baba wa familia anajitahidi sana kuona familia yake inafurahiya sikukuu. Angesema, kuwa amejitolea hata kutoa nguo yake ya pekee kwa ajili yako. Halafu angekupa hilo suruali ambalo alikuwa analivaa siku akienda kuwasalimia wakwe zake tu.

Angekwambia ujaribu sulupwete hilo na angekupa pamoja na ule mkwiji ili sulupwete hilo lisidondoke. Angekusaidia kufunga mkwiji na kukuambia, ‘hebu tembea.’ Halafu angesema, ‘umependeza kwelikweli.’ Kwa sababu ya utoto na ushamba wa wakati ule usingejua kwamba, sulupwete hilo linakufanya ufanane kama kifurushi cha viazi vitamu. Lakini, kwa sababu kule kwetu wakati ule, kila mmoja alikuwa anakatiwa kipande cha suruali na baba yake na kuhesabiwa kuwa amepata nguo mpya, hakuna aliyejali. Nawasifu sana wale wazee wa enzi za utoto wetu. Ni kweli kabisa, nguo mpya maana yake ni nguo ambayo hujawahi kuivaa. Kama baba yako aliivaa na kukupatia wewe, kwako ni lazima iwe mpya.

Lakini huku mjini na kwa watoto wa sasa, mambo ni kinyume kabisa. Krismas hii wanangu hawa watatu wamenitoa jasho kwelikweli, hususan huyu binti yangu Ngina, Binti huyu ananipa ugonjwa wa moyo kila uchao. Wiki moja kabla ya ujio wa sikukuu hii ya Krismas wanangu walitaka kujua nitawanunulia nguo za aina gani. Niliwambia hali ya uchumi hairidhishi na nikaona ni wazo zuri kusingizia umeme. Niliwaambia, kiwanda cha kutengeneza fedha kimesimama kuzalisha kwa sababu ya umeme. Huyu mwanangu Ngina mwenye kiherehere kama bibi yake mzaa mama, alinikata kalma na kusema, ‘baba fedha zinatengenezwa Ulaya siyo hapa nchini. Tuna orodha ya nguo tunazotaka tunataka kwenda na fasheni safari hii, mie bila skin jinzi hapatatosha hapa.’

Nikajua walimu wa siku hizi ni wataalamu hasa, yaani mtoto wa darasa la nne ameshafundishwa kuwa fedha zinatengenezwa Ulaya! Ikabidi nijifanye sikusikia maelezo ya huyu binti yangu ambaye kwa kawaida ndiye anayeongoza migomo kwenye familia yangu. Nikawaambia kama wanataka, nitajitahidi kila mmoja apate gauni, shati na suruali ya mtumba. Kusikia hivyo, watoto wakasema, itakuwa ngumu wao kukubali kuvishwea mitumba. Ngina alikuja na wazo mbadala, alisema, kama sina hela ni afadhali tuuze TV yetu. Lakini wenzake walipinga lile wazo wakidai watakosa kuona Ze Comedy. Ngina hakukubali kushindwa akaja na wazo lingine akitaka niuze Music System yangu ili wapate nguo za sikukuu. Nilipinga wazo hilo na kumfokea kwa kuwa na mawazo mufilisi. Lakini wapi, Ngina hakubali kushindwa, alinijia juu akidai ni jukumu langu kuhakikisha wao wanapata nguo za sikukuu, kwa hiyo nipunguze jazba tuweze kujadili hadi kufikia muafaka. Nilimuonya achunge kauli zake za maudhi.

Hata hivyo alikuja na wazo lingine, alinitaka nikakope. Alinishauri nikakope kwa jirani yetu mmoja ambaye aliwahi kunituhumu kwamba ninamilki mtandao wa wezi wa magari baada ya kuniona nikija na magari tofauti hapo nyumbani karibu kila siku. Magari ambayo yalikuwa ni ya kazini kwangu. Huyu jirani alinichongea Polisi nikaja kusachiwa na kupelekwa kituoni kutoa maelezo. Nilikuja kugundua kwamba ni nuyu jirani yangu ndiye aliyenichongea, kwani baada ya kukamatwa na kupelekwa Polisi huku nyuma alitamba kwamba mwaka huo lazima nifungwe.

Ilibidi nigeukie Dini na kuwaambia kwamba, hata bwana wetu Yesu Kristo katika kueneza Injili wakati huo alikuwa na nguo moja tu na hakuwahi kwenda na fasheni. Wote walinijia juu wakidai nimemkashifu Bwana Yesu Kristo na watamwambia mchungaji. Nikaona ule mjadala utakuwa hauishi kama nisipokuwa makini. Niliwaomba waandike mahitaji yao, kisha nitaangalia uwezekano wa kuomba mkopo kibaruani kwangu. Nikawa nimeufunga ule mjadala.Ama kweli watoto wa kizazi hiki, hawana maadili kabisa.

Kiongozi wa migomo kwenye familia!!!!!
teh!teh!teh!
nimeipenda hiyo
 
Back
Top Bottom