Kp cartoon: Ni 'Mwasia' gani anayeiongoza CCM na Tanzania kutoka mlango wa nyuma?

minda

JF-Expert Member
Oct 2, 2009
1,068
65
Kwenye 'Mwananchi' la jana, katuni ya kipanya inaonesha CCM (kombati la kijani) akishika remote control kuiendesha tv (Tanzania); huku nyuma ya huyo CCM akiwapo 'ponjoro' ambaye pia ana rimoti ya kuiendesha tv hiyo huku Kipanya akiuliza; " na huyo wa nyuma ni nani?"

Bila shaka msanii huyo atakuwa anamaanisha chama tawala; na huyo wa nyuma bila shaka atakuwa wa jamii ya kihindi, kiarabu au kiajemi (irani).

my take:

Ni 'ponjoro' gani anayeiongoza CCM na Tanzania kutoka mlango wa nyuma kwa mujibu wa KP?
 
kwenye 'mwananchi' la jana, katuni ya kipanya inaonesha ccccm (kombati la kijani) akishika remote control kuiendesha tv (tanzania); huku nyuma ya huyo ccccm akiwapo 'ponjoro' ambaye pia ana rimoti ya kuiendesha tv hiyo huku kipanya akiuliza; " na huyo wa nyuma ni nani?"



my take:

Ni 'ponjoro' gani anayeiongoza ccccm na tanzania kutoka mlango wa nyuma kwa mujibu wa kp?

Jibu umetoa mwenyewe

bila shaka msanii huyo atakuwa anamaanisha chama tawala; na huyo wa nyuma bila shaka atakuwa wa jamii ya kihindi, kiarabu au kiajemi (irani).

Aise mbona umeshajua kuwa ni M-Irani halafu unauliza
 
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-rada-tanil-somaiya-afanya-kufuru-ikulu.html
kwenye 'mwananchi' la jana, katuni ya kipanya inaonesha ccccm (kombati la kijani) akishika remote control kuiendesha tv (tanzania); huku nyuma ya huyo ccccm akiwapo 'ponjoro' ambaye pia ana rimoti ya kuiendesha tv hiyo huku kipanya akiuliza; " na huyo wa nyuma ni nani?"

bila shaka msanii huyo atakuwa anamaanisha chama tawala; na huyo wa nyuma bila shaka atakuwa wa jamii ya kihindi, kiarabu au kiajemi (irani).


my take:

Ni 'ponjoro' gani anayeiongoza ccccm na tanzania kutoka mlango wa nyuma kwa mujibu wa kp?
 
Aise mbona umeshajua kuwa ni M-Irani halafu unauliza


hapana mkuu! simjui?
nimeandika m-irani kwa sababu wakuu wengi wanajua kuwa irani ni nchi ya kiarabu na wakati ina waarabu 2% tu (wikipedia).
 


icon1.png
Fisadi wa rada Tanil Somaiya afanya kufuru IKULU

Ilikuwa ni siku ya Desemba 9, 2010. Tanzania ilikuwa inasherehekea miaka 49 ya Uhuru wa taifa. Baada ya kukagua gwaride Uwanja wa Taifa, Rais Jakaya Kikwete alifanya dhifa ya kitaifa Ikulu na kualika viongozi wa serikali, mabalozi, viongozi wa dini na wafanyabiashara wakuu.

Waalikwa wote, walikuwa wanaingia Ikulu kupitia mlango wa nyuma ulio karibu na bahari upande wa ferry. Lango kuu la kuingia Ikulu lilikuwa halitumiki kwa wageni siku hiyo na lilitumiwa na Rais na viongozi wengine wakuu. Magari yote, ikiwemo ya mawaziri na mabalozi yalipaki nje ya Ikulu kwenye uwanja mkubwa ulio karibu na ferry na wageni waalikwa waliingia kwa mguu kwenye viwanja vya Ikulu.

Mmoja wa wageni waalikwa mashuhuri wa Kikwete alikuwa ni Tanil Somaiya, mmiliki wa Shivacom Group of Companies.

Wakati mawaziri na mabalozi waliambiwa na maafisa usalama Ikulu watumie mlango wa nyuma wa kuingia Ikulu na kutembea mpaka kwenye gardens ambako sherehe ilifanyika, Tanil alipewa heshima ya kipekee na kuruhusiwa kutumia main entrance gate.

Tanil aliingia Ikulu na gari la kifahari jekundu (a red FERRARI) na kuipaki gari hiyo kwenye mlango mkuu wa kuingia IKULU ambako huwa gari la Rais ndipo linapaki.

Aliiacha FERRARI hiyo hapo kwenye lango la kuingia Ikulu kwa zaidi ya masaa mawili huku akijimwaga kwenye dhifa.

Mawaziri, mabalozi na vigogo wengine walibaki wamepigwa na butwaa iwaje wageni wote waambiwe waingie Ikulu kupitia mlango wa nyuma kwa mguu na kuacha magari yao nje halafu mfanyabiashara huyu apite main gate na kuweka gari lake kwenye main entrance ya lango kuu la kuingia Ikulu.

Tanil ni rafiki wa karibu na business partner wa Shailesh Vithlani, mfanyabiashara ambaye amekimbia nchi kutokana na kashfa ya rada.

Tanil, ambaye ametajwa kwenye WikiLeaks kuhusu rada, amehusishwa pamoja na Vithlani kwenye kashfa ya rada, military trucks, military choppers, Gulfstream presidential jet na scandal nyingine.

Inaeleweka kuwa Tanil alimchangia pesa nyingi sana Kikwete kwenye uchaguzi wa Rais uliopita na pia alitoa helikopta zake zitumike kwenye kampeni ya CCM, lakini hii ndivyo Ikulu ya Mwalimu Julius Nyerere inavyodharauliwa siku hizi?

Kwa kutumia main entrance na kupaki gari lake mbele ya lango kuu la Ikulu, Tanil alikuwa anataka kuwaonesha wageni wote kuwa yeye yuko karibu sana na Rais wa nchi na Ikulu ni kama nyumbani kwake.

Mbaya zaidi, kufuru hii ilifanywa siku ambayo Tanzania inaadhimisha uhuru wake. Kuna uhuru kamili kweli kama watuhumiwa wakubwa wa ufisadi wanafanya kufuru namna hii mpaka IKULU?

Unatarajia kweli Edward Hoseah wa PCCB anaweza kuondokana na uoga wa kumkamata Tanil kwa ufisadi wa rada wakati Rais wa nchi ni besti wake na Ikulu ni kama playground yake?


source: jamiiforums
 
MKUU MINDA, umesema maneno mazito sana, japo hujaweka source itakuwa umeshuhudia mwenyewe, right? Kama haya ni kweli, basi Hosea anahaki yakulalamika juu ya mkuu huyu.
 
hapana mkuu! simjui?
nimeandika m-irani kwa sababu wakuu wengi wanajua kuwa irani ni nchi ya kiarabu na wakati ina waarabu 2% tu (wikipedia).

Ethnic groups:​
Persian 51%, Azeri 24%, Gilaki and Mazandarani 8%, Kurd 7%, Arab 3%, Lur 2%, Baloch 2%, Turkmen 2%, other 1%
Religions:​
Muslim 98% (Shi'a 89%, Sunni 9%), other (includes Zoroastrian, Jewish, Christian, and Baha'i) 2%
Languages:​
Persian and Persian dialects 58%, Turkic and Turkic dialects 26%, Kurdish 9%, Luri 2%, Balochi 1%, Arabic 1%, Turkish 1%, other 2%
 
Yote tisa! Kumi katiba mpya tu, ambayo wananchi watapata nafasi ya kutoa maoni yao. Katiba ambayo itakuwa na vipengele vya kuwabana hawa wadudu mafisadi na viongozi wabadhirifu. Dawa ni kukaza uzi kwenye katiba tu!!!!!!!!!!
 
Ethnic groups:​
Persian 51%, Azeri 24%, Gilaki and Mazandarani 8%, Kurd 7%, Arab 3%, Lur 2%, Baloch 2%, Turkmen 2%, other 1%
Religions:​
Muslim 98% (Shi'a 89%, Sunni 9%), other (includes Zoroastrian, Jewish, Christian, and Baha'i) 2%
Languages:​
Persian and Persian dialects 58%, Turkic and Turkic dialects 26%, Kurdish 9%, Luri 2%, Balochi 1%, Arabic 1%, Turkish 1%, other 2%


asante mkuu! lakini kadiri ya wikipedia ni 2%. gonga hapa kisha nenda kwenye "7.Demography"

The exact ethnic breakdown of Iran is unknown as there are no official numbers, however some organizations have made estimates. The Library of Congress released the estimate: Persians (65%), Azerbaijani (16 %), Kurds (7%), Lurs (6%), Arabs (2%), Baluchi (2%), Turkmens (1%), Turkic tribal groups such as the Qashqai (1%), and non-Iranian, non-Turkic groups such as Armenians, Assyrians, and Georgians (less than 1%). According to them Persian is spoken as a mother tongue by at least 65% of the population and as a second language by a large proportion of the remaining 35%.[184]
 
kwenye 'mwananchi' la jana, katuni ya kipanya inaonesha ccccm (kombati la kijani) akishika remote control kuiendesha tv (tanzania); huku nyuma ya huyo ccccm akiwapo 'ponjoro' ambaye pia ana rimoti ya kuiendesha tv hiyo huku kipanya akiuliza; " na huyo wa nyuma ni nani?"

bila shaka msanii huyo atakuwa anamaanisha chama tawala; na huyo wa nyuma bila shaka atakuwa wa jamii ya kihindi, kiarabu au kiajemi (irani).


my take:

Ni 'ponjoro' gani anayeiongoza ccccm na tanzania kutoka mlango wa nyuma kwa mujibu wa kp?
Ibandike basi hiyo katuni...!!
 
Back
Top Bottom