Huyu mpuuzi anafkiria al shabaab wanahitaji watu laki tano kupiga bomu, yapo matukio ambayo watu chini ya 10 wamepigwa bomu na al shabaab. So kama lengo lake ni kutuokoa atukodie na tax ili tuachane na dala dala mana ndani ya dala dala tunakuaga zaid ya 50.Kova ajiandae al shabaaab wakifanya kweli. Siombei, lakini ikitokea atafute pa kujificha.
Me Love Your comment. KAMA KWELI KUNA TISHIO LA AL SHABABU WAZUIE MIKUSANYIKO YOOTE HAPA DAR, KARIAKOO IFUNGWE KESHO, MECHI ZA SOKA ZIFUTWE, VYUONI NA MASHULENI PIA WASIENDE KWA KUWA TISHIO LA L SHABABU LIMEKUWA KUBWA. yaani hii nchi sijui usanii utaisha lini?? Ikibidi tutaandama hivyo hivyo mtupige mabomu na risasi muwasingizie alshababu.Unapokataza watu kuandamana kisa Al-Shaabab ni ishara tosha kwanza hao jamaa wapo hapa nchini.
Pili huo uwepo wao ni kwamba polisi imeshindwa kuwazuia wasiingie nchini,
Tatu wameshaingia, pia umeshindwa kuwazuia wasilete madhara.
Mikusanyiko iko mingi tu, si lazima iwe Maandamano ya Dowans.
Mbona wakati wa Kampeni za Siasa hawazungumzii Al Shaabab? Kwenye masoko makuu ya Nafaka kama Tandale, Urafiki, Tandika, Kariakoo kote huko mbona hawazngumzii hao Al Shaabab?
Ubungo Bus Terminal, Mwenge, Mbagala kote huko kuna mikusanyiko mikubwa ya watu, hao Alshaabab hawawezi kufika?
Jumamosi inayokuja kuna Mechi kati ya Simba na Yanga ambapo takriban watu Alfu 50 au zaidi wanategemewa kuingia, hakuna uwezekano wa hao Alshaabab kuwepo?
Yani hao Alshaabab wapo kwenye maandamano ya Dowans tu??!!!!
Kwanza kama kweli wapo, hao Alshaabab wakitaka hata hiyo mikusanyiko yao ya miaka 50 ya uhuru wa bendera watailipua tu.
Napata mashaka na uwezo wa huyu Mzee, kwani amekua mtu wa majigambo mengi kuliko uhalisia wa kitu.
Mkuu, atalionaje na yeye hatumii akili yake! Hiyo amri ya kukataza maandamano sio yake, niya Rostam Azizi kupitia makuadi wake walioko serikalini. Kova yeye ni kipaza sauti tu.Hili tishio la dowans hajawahi kuliona hata kidogo?
Tanzania tuna viongozi wa ajabu...!!! Kova kapiga marufuku maandamano ya kupinga Dowans kulipwa 111bns..... eti kwa ajili ya tishio la Al Shabab...
Source Radio Wapo FM..... Najisikia kuanza kulia.....
wehu ni wale wanaokiuka katiba ya nchiSuala la Dowans liko mahakamani na ni suala la kisheria sio mihemko.Wanaharakati wameishakula hela ya ma-donors wao kwa ajiri ya hayo maandamano ya kuwapotezea watu muda wao wa kujenga taifa.tusitumike kuwa daraja la mafanikio ya wengine.serikal imekata rufaa tena sasa unamuandamania nani kama sio wehu.
waache wako ktk nchi yaoHata akiwaruhusu hakuna la maana mtakalofanya.
Haya maandamano ni ya CDM kutaka kutuvurugia amani yetu ya Tz na si lingile lolote !
Tanzania tuna viongozi wa ajabu...!!! Kova kapiga marufuku maandamano ya kupinga Dowans kulipwa 111bns..... eti kwa ajili ya tishio la Al Shabab...
Source Radio Wapo FM..... Najisikia kuanza kulia.....