KING COBRA
JF-Expert Member
- Nov 10, 2011
- 2,782
- 864
Tarehe 26/11/2011 ,Jeshi la polis Limeruhusu Maandamano ya Kuchangia Mradi wa Kutoa sumu na Chuo Cha Maadili Unao Ongozwa na askofu Gammanywa wa Wapo Radio uliopo Mtaa wa Loliondo Kurasini!!!Taarifa kutoka kituoa Cha Wapo Radio zinahamasisha Wananchi kuhudhuria Maandamano hayo ambayo yanalenga kuchangisha 500m. Mtangazaji amesisitiza watu wengi wahudhurie na kwamba mgeni rasimi atakuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye anafungua mradi huo baada ya Rais Jakaya Kikwete kutembelea Mda mfupi baada ya kusimikwa urais. Jambo la kushangaza Jeshi la polis limepinga marufuku maandamano ya Kupinga Mswaada jumamosi kwa sababu za Al shababu lakini wameruhusu maandamano kwa Askofu Gammanywa wa Loliondo