kijana wetu NAPE naona amenza kudelete watu wote wanaomchallenge kwenye facebook..anataka abakiwe na watu wanaomsifia hata akichemsha....
Waheshimiwa wanaJF,
Salaams!
UPDATE:
Katibu Mukama ameamua kuwa wazi. CCM hawana orodha ya mafisadi wala hawajatoa siku 90 kwa mtu. "Kwa ujumla hakuna mwana-CCM msafi kama Mapacha watatu" aaaah!...ha..ha..haaaaah! Guys, I told you CCM ni nyoka kweli. Ndiyo maana hata Mwenyekiti wao hakuwa na mfano wowote mwingine katika kuelezea wanachokusudia kuwaaminisha wadanganyika isipokuwa mageuzi ya mara kwa mara ya nyoka kwa kuvua magamba tena alisahau kusema mwenye sumu kali.
Kama huzijui aina za sumu ya CCM (Nyoka wa magamba) fuatilia kauli za kuwapo udini, ukabila, ukanda nk. hapa nchini wakikusudia kuua nguvu za vyama vya upinzani. Hawa jamaa wakizidiwa wapo tayari hata kuwatumia viongozi wajinga wajinga wa dini ili kuanzisha vurugu ambazo zitasaidia kuwalinda wao na mali zao. Lakini bado naamini tunayo nafasi ya kutetea nchi yetu iliyopoteza mwelekeo. May the Almighty God save us from these people.
Time will tell, and God willing these people will pay for this one day. And they will pay so dearly that no one will ever try to imitate what they have done to our country. (end of update)
Tunaojua tabia ya unafiki wa CCM tuliposikia CCM inatarajia kuondokana na baadhi ya viongozi/wanachama wake wanaotajwa kuhusika na ufisadi mkubwa tulijua maigizo yanaanza hivyo tukakaa tayari. Watu wengi wameshabikia sana habari hiyo lakini wengine tunajua chama hiki kina unafiki mno kiasi kwamba hawa jamaa wasipotaka kuondoka wenyewe basi mambo yatafifia na kupotea.
Kama nakumbuka vizuri kelele zote kuhusu kuwapa watu hao siku 90, kuwaandikia barua nk. zimekuwa zikipigwa na viongozi wao wapya ndani ya Sekretarieti wengine hata bila kuulizwa sasa cha ajabu tayari wameshaanza kupingana wao kwa wao. Wengine wanasema siku 90 na kuwaandikia barua watuhumiwa wa ufisadi hayakuwa maazimio ya vikao vyao n.k n.k n.k
Habari ifuatayo kutoka Gazeti la Nipashe inaonesha hata anayepaswa kuandika hizo barua na lini zitaandikwa haijulikani. Hii inawezekana wapi kama si maigizoni tu? Mkiambiwa CCM wanajaribu kufanya kiini macho katika kushughulikia ufisadi mtasema mnadanganywa?
CHANZO: NIPASHE
mpendazoe kaua kabisa,kasambaratisha chama!
Yaani ingawa wengi walimlaum kwamba hayo sio mambo ya msingi
ya kuongelea saivi (na kweli sio),ila ni mazuri sana kwa magamba kujikuna day n night!
Hadi muwasho ukiisha,2015 hawajaleta hata mtumbwi ziwa victoria,kigoma itakua kama wapi sijui