fikirikwanza
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 7,452
- 3,065
Ni kweli kosa letu la kwanza ni kuiamini CCM hata baadhi yetu kutumika vibaya kuilinda pale ambapo ilipaswa kuanguka kifo cha mende. CCM ilipaswa iondoke enzi za NCCR, Ikapaswa iondoke kwa mara nyingine enzi za CUF, sasa inapaswa iondoke ktk enzi za CHADEMA. Tunaweza kushindwa tena kufanya hivyo, CHADEMA pia inaweza kushindwa kufanya hivyo kutokana na kuaminiwa sana na Wananchi kama ilivyowahi kuaminiwa NCCR na CUF.
Kosa la pili ni kudhani ni lazima CHADEMA waiondoe CCM, hapana. Sio kazi ya CHADEMA kuiondoa CCM, ndo maana kila nikisia CCM inapigana na CHADEMA, najua sasa kweli CCM inaondoka, yaani mfa maji hutapata kwa silokuwepo.
Suala la CCM kuondoka liko mikononi mwa wananchi, suala la CHADEMA kupewa nchi liko mikononi mwa wananchi wale wale watakao inyima kiti CCM waipe CHADEMA Ukumbi.
Ikifikia wakati CHADEMA wakawa na jukumu la kuondoa CCM , hakika hawataweza maana jukumu hilo ni la wananchi; Tusifanye makosa hayo kwa mara ya pili. CHADEMA watatuongoza pale tu ambapo tuwawapa ridhaa hiyo tuliyowanyanganya CCM, na wajue kuwa tunaweza kuwanyanganya vilevile na kuwapa NCCR au TLP iwapo hawatafanya yale tuliyokusudia.
UKOMBOZI NI WATU na WATU NDO WATANZANIA WENYEWE SIO CHAMA NA WANACHAMA WAKE
Kama chama chochote cha upinzani kinataka ridhaa hiyo kutoka kwa wananchi, kijishughulishe na matatizo ya wananchi orodha ni ndefu sana na inajulikana. CHADEMA kwa sasa wako mbele sana na mbali sana, lakini sio hoja CCK wakawatimulia vumbi? sio hoja CUF waka-regroup na kufanya vema.
Kosa la pili ni kudhani ni lazima CHADEMA waiondoe CCM, hapana. Sio kazi ya CHADEMA kuiondoa CCM, ndo maana kila nikisia CCM inapigana na CHADEMA, najua sasa kweli CCM inaondoka, yaani mfa maji hutapata kwa silokuwepo.
Suala la CCM kuondoka liko mikononi mwa wananchi, suala la CHADEMA kupewa nchi liko mikononi mwa wananchi wale wale watakao inyima kiti CCM waipe CHADEMA Ukumbi.
Ikifikia wakati CHADEMA wakawa na jukumu la kuondoa CCM , hakika hawataweza maana jukumu hilo ni la wananchi; Tusifanye makosa hayo kwa mara ya pili. CHADEMA watatuongoza pale tu ambapo tuwawapa ridhaa hiyo tuliyowanyanganya CCM, na wajue kuwa tunaweza kuwanyanganya vilevile na kuwapa NCCR au TLP iwapo hawatafanya yale tuliyokusudia.
UKOMBOZI NI WATU na WATU NDO WATANZANIA WENYEWE SIO CHAMA NA WANACHAMA WAKE
Kama chama chochote cha upinzani kinataka ridhaa hiyo kutoka kwa wananchi, kijishughulishe na matatizo ya wananchi orodha ni ndefu sana na inajulikana. CHADEMA kwa sasa wako mbele sana na mbali sana, lakini sio hoja CCK wakawatimulia vumbi? sio hoja CUF waka-regroup na kufanya vema.