Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Mzee Titus Mbawala alikuwa anafundisha mambo ya ndoa kwa wachumba waliokuwa wanajiandaa kufunda ndoa kwenye kigango kimoja cha Parokia ya Tabata.
Alifundisha mambo mengi na hasa yahusuyo mambo ya unyumba. Akitumia mifano mbalimbali ya Kibiblia kuweka msisitizo. Dada mmoja aitwaye Mercy alikuwa akimsikiliza kwa makini aliamua kuuliza swali kama ni muhimu au lazima mume na mke "wafike" pamoja wakati wanatekeleza ndoa yao.
Mzee huyo alijibu kuwa kwa kawaida ingepaswa wote wafike wakati huo huo lakini mara nyingi wanaume wamekuwa wakifika kwanza na kuwaacha wake zao hata safari hawajaanza.
Aliendelea na mafundisho ya ndoa kwa muda na kama saa nzima ikapita baada ya kuelezea asili ya ndoa katika simulizi la Adama na Eva. Alielezea kwanini kati ya Adamu na Eva Adamu alipewa adhabu kubwa sana lakini suala la "uadu" likatangazwa dhidi ya Eva.
Mzee huyo akawauliza wachumba wale wanafikiri ni kosa gani la Eva ambalo lilimfanya apewe adhabu kali namna hiyo?
Wachumba wale walifikiria sana lakini hakuna aliyeweza kuja na jibu. Mzee Mbawala akawauliza kama wamewahi kusikia jinsi wayahudi wanavyoelezea kosa la Eva. Hakuna aliyejibu.
Akiwa tayari kuwapa jibu lake ndipo Mercy alipoamka na kwa kujiamini alitoa jibu lake. "Kosa lake lilikuwa ni kula tunda kwanza" alisema na kuketi chini. Wenzake waliona mantiki yake na kutingisha vichwa vyao kwa kumkubalia.
Mzee Mbawala akamuuliza "unaelewa nini Biblia inaposema kuwa alikula tunda kwanza".
Mercy katika kujiamini kwake alijibu "kwamba alifika kwanza kabla ya mumewe!"
Alifundisha mambo mengi na hasa yahusuyo mambo ya unyumba. Akitumia mifano mbalimbali ya Kibiblia kuweka msisitizo. Dada mmoja aitwaye Mercy alikuwa akimsikiliza kwa makini aliamua kuuliza swali kama ni muhimu au lazima mume na mke "wafike" pamoja wakati wanatekeleza ndoa yao.
Mzee huyo alijibu kuwa kwa kawaida ingepaswa wote wafike wakati huo huo lakini mara nyingi wanaume wamekuwa wakifika kwanza na kuwaacha wake zao hata safari hawajaanza.
Aliendelea na mafundisho ya ndoa kwa muda na kama saa nzima ikapita baada ya kuelezea asili ya ndoa katika simulizi la Adama na Eva. Alielezea kwanini kati ya Adamu na Eva Adamu alipewa adhabu kubwa sana lakini suala la "uadu" likatangazwa dhidi ya Eva.
Mzee huyo akawauliza wachumba wale wanafikiri ni kosa gani la Eva ambalo lilimfanya apewe adhabu kali namna hiyo?
Wachumba wale walifikiria sana lakini hakuna aliyeweza kuja na jibu. Mzee Mbawala akawauliza kama wamewahi kusikia jinsi wayahudi wanavyoelezea kosa la Eva. Hakuna aliyejibu.
Akiwa tayari kuwapa jibu lake ndipo Mercy alipoamka na kwa kujiamini alitoa jibu lake. "Kosa lake lilikuwa ni kula tunda kwanza" alisema na kuketi chini. Wenzake waliona mantiki yake na kutingisha vichwa vyao kwa kumkubalia.
Mzee Mbawala akamuuliza "unaelewa nini Biblia inaposema kuwa alikula tunda kwanza".
Mercy katika kujiamini kwake alijibu "kwamba alifika kwanza kabla ya mumewe!"