Kosa alilofanya Kikwete 2005 na bado anafanya!

Asante WoS, hawa ndio Watanzania tulivyo na sasa za nchi yetu, ni maneno mengi na vitendo vichache. ili kuingia bungeni na kuonekana ni mbunge machachari, lazima ujue kupiga sana domo hata kama wanachi wako wanakula majani.
Prof. Shivji aliwahi kusema, kuna wanasiasa hawapendi siasa bali wanataka madaraka kuneemesha matumbo yao. lakini pia kuna wananchi wanauchungu na nchi hii lakini hawako tayari kuisogelea siasa kwa sababu ni mchezo mchafu. Mmmoja wenye uchungu na nchi hii ni Mzee Mwanakijiji na wengine wengi wamo hata huku JF pia wamo. Uwezo wa kusema sana upo, tatizo ni uwezo wa kutenda!.
Kwa wenzetu mlio mbali, endeleeni kusema tuu, sisi tuliyoko huku jikoni, wengine wetu tilishatenda na tukatendwa unakia mahali unalazimika kuchagua ama ujinyamazie utunze familia yako siku ipite, ama utende, utendwe, usahaulike na hutasota tena maana utakuwa umekwisha habari yako, tatizo ni familia. Ukitanguliza mapenzi yako kwa nchi yako, huu ndio uzalendo wa kweli, utasema lolote na kufanya lolote kwa ajili ya nchi yako, ukitanguliza mbele familia yako, familia yako, kabla ya kusema na kutenda, unajiuliza mara mbili mbilimbili 'so what?'. na wengine wetu huamua kukaa kimya bila kusema lolote, bila kutenda lolote na kuiacha siku ijipitie, ikawa asubuhi, ikawa jioni, siku ikapita.

Pasco,huo ndiyo ukweli kwa walio wengi.Kama ni uchambuzi na upembuzi wa matatizo ya nchi yetu na viongozi wake hakuna kilichobakia.Hali halisi inajulikana, matatizo, mapengo, viunzi/vikwazo vyote vinaeleweka.Mapendekezo yameshatolewa katika kila eneo.Kilichobaki ni utekelezaji tu.Inanikumbusha tafiti chungu nzima ambazo zimefanyika na mapendekezo lukuki kutolewa na maripoti kibao kujaza mashelfu na sasa technolojia imerahisha uhifadhi wa haya matokeo.
The country is heavily pregnant with ideas - what is needed now is the midwife to deliver the baby.And we all know that it is painful to deliver.....nani yuko tayari kuumwa uchungu wa kuzaa??? Ingewezekana kukwepa nadhani hakuna mwanamke angeukubali uchungu wa kuzaa.... ila nature has its own way to ensure whether u like it or not utazaa!Bahati mbaya sana mimba iliyopo kwa sasa haina cha kuisukuma izaliwe....kuzaa ni hiari..tutasubiri sana.
Ukisema eti wananchi waandamane kupinga mambo fulani kama walivyofanya nchi nyingine, tulion akilichowapata wazanzibari kipindi kile cha uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi.Nani anataka kufa? nikifa, nani atakumbuka kuwa nilifia nchi waje wanilelee wanangu? Sana sana watu wanaweza kunicheka na kusema yule naye! Haya kimbelembele kimeiponza familia yake... ona sasa wanae wanavyotaabika!
Binafsi sioni mabadiliko makubwa saaaana katika kizazi hiki ambacho kimeshaharibika kuanza fikra, mitizamo na vipaumbele vya maisha.
Haya ni mawazo yangu ya moyoni yasio na unafiki wa kufurahisha baraza.
 
........'if you can't beat them, join them' and fight from within.
Honestly, I'm among the people disapointed by the oppositions in Tanzania, ni njaa na ubinafsi tuu umewajaa. hebu tuangalie mfano mdogo tuu wa huu uchaguzi mdogo wa jimbo la Busanda (nitakuwepo huko). Jimbo lilikuwa linashikiliwa na CCM, tayari Cuf wameshateua mgombea, NCCR, wameteua na Chadema tayari. bado UDP lazima watateua, all this ya nini?. si wanampa mgombea wa CCM a walkover victory?. kwa nini hawana umoja?.

Are you out of your mind?????
Waungane??? I dont buy that Idea.
Dawa si kuitoa sisiem madarakani kwa umoja wa wapinzani (a.ka. Kenya) bali ni kubadili mfumo mfu wa sasa na kuweka mpya kwa kukichagua chama kipya na si umoja wa wapinzani.
 
Dawa si kuitoa sisiem madarakani kwa umoja wa wapinzani (a.ka. Kenya) bali ni kubadili mfumo mfu wa sasa na kuweka mpya kwa kukichagua chama kipya na si umoja wa wapinzani.

We all know the WHAT, WHERE, WHY.
Tell us the HOW,WHEN and WHO!
 
that is what I said. Tatizo watu wana haraka mno ya kuruka ikifika mahali pa action. But this time, nimejifunza kitu kimoja usitawategemee watu wa JF as a group to do something. They are good in talking (like typical Tanzanians) but they never act. That is why I believe if you can do something, go and do it. Let the others keep talking.

Ndivyo tulivyo kwa hio hata JK hana kosa.... Maweeeee :)
 
Pasco,huo ndiyo ukweli kwa walio wengi.Kama ni uchambuzi na upembuzi wa matatizo ya nchi yetu na viongozi wake hakuna kilichobakia.Hali halisi inajulikana, matatizo, mapengo, viunzi/vikwazo vyote vinaeleweka.Mapendekezo yameshatolewa katika kila eneo.Kilichobaki ni utekelezaji tu.Inanikumbusha tafiti chungu nzima ambazo zimefanyika na mapendekezo lukuki kutolewa na maripoti kibao kujaza mashelfu na sasa technolojia imerahisha uhifadhi wa haya matokeo.
The country is heavily pregnant with ideas - what is needed now is the midwife to deliver the baby.And we all know that it is painful to deliver.....nani yuko tayari kuumwa uchungu wa kuzaa??? Ingewezekana kukwepa nadhani hakuna mwanamke angeukubali uchungu wa kuzaa.... ila nature has its own way to ensure whether u like it or not utazaa!Bahati mbaya sana mimba iliyopo kwa sasa haina cha kuisukuma izaliwe....kuzaa ni hiari..tutasubiri sana.
Ukisema eti wananchi waandamane kupinga mambo fulani kama walivyofanya nchi nyingine, tulion akilichowapata wazanzibari kipindi kile cha uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi.Nani anataka kufa? nikifa, nani atakumbuka kuwa nilifia nchi waje wanilelee wanangu? Sana sana watu wanaweza kunicheka na kusema yule naye! Haya kimbelembele kimeiponza familia yake... ona sasa wanae wanavyotaabika!
Binafsi sioni mabadiliko makubwa saaaana katika kizazi hiki ambacho kimeshaharibika kuanza fikra, mitizamo na vipaumbele vya maisha.
Haya ni mawazo yangu ya moyoni yasio na unafiki wa kufurahisha baraza.

samahani sana ningependa kukuuliza swali binafsi kama haikusumbui, hivi unajishughulisha au ume/nasomea nini? nakuuliza hivyo kwa maana unaonekana kuwa ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa kufikiri na kuchanganua mambo hiyo posti imedhihirisha hivyon ni wachache sana wenye uwezo huo!
 
Mwkjj:mimi ni kati ya wale uliowataja ambao wanaamini ukimweka Mkapa na Kikwete side by side, Mkapa anashinda hands down katika leadership in general.
Wote wana HUGE misgivings zao but at least Mkapa hakuleta blahblah alikuwa mtendaji. Huyu msanii ni porojo nyingi lakini vitendo ni zero!
Kama kuiba wote wanaiba! Hakuna mwenye afadhali. But at least wakati wa Mkapa there was hope now.. it's just gloom and doom! Mi naomba tu-suggest to Zambians na Kenyans wamchukue JK kama rais wao si tuchague mwingine!

hapa nipo pamoja na wewe mkuu, pamoja na madudu yake, lakini uongozi wa Mkapa at least uliirudishia nchi heshima na kuipa mwelekeo. Leo hii sijui hata nchi inakoelekea ni wapi, yaanio tupotupo tu
 
Susuviri, This is what Tanzania need. Currently we just need a transitional leader other than JK from there we can stabilise not with JK!

And it depends on what kind of transional leader do we want... a politician or mwanajeshi?
 
Wangapi tumeisoma ILANI ya UCHAGUZI ya CCM ya mwaka 2005? Ukiisoma ile vizuri utaona JMK anafanya "zaidi" ya alivyotakiwa kufanya na ilani hiyo! Tatizo liko kwa CCM, sio JMK. Tukiweza kuiondoa CCM, mengine yoote tunayoyataka yawe, yatakuwa tena kwa ziada. La kujiuliza labda CHAMA mbadala wa CCM ni kipi?
 
Wangapi tumeisoma ILANI ya UCHAGUZI ya CCM ya mwaka 2005? Ukiisoma ile vizuri utaona JMK anafanya "zaidi" ya alivyotakiwa kufanya na ilani hiyo! Tatizo liko kwa CCM, sio JMK. Tukiweza kuiondoa CCM, mengine yoote tunayoyataka yawe, yatakuwa tena kwa ziada. La kujiuliza labda CHAMA mbadala wa CCM ni kipi?

Kuna tofauti gani kati ya JK ya CCM? kama 'tukiiondoa' CCM si itakuwa ni sawa na kumuondoa Kikwete? Kutokana na kauli yako, iwapo Kikwete akiamua kuondoka CCM na kuingia chama cha upinzani (ambacho kitaonekana serious) basi watanzania hawatakuwa wamefanya kosa wakimchagua tena?
 
samahani sana ningependa kukuuliza swali binafsi kama haikusumbui, hivi unajishughulisha au ume/nasomea nini? nakuuliza hivyo kwa maana unaonekana kuwa ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana wa kufikiri na kuchanganua mambo hiyo posti imedhihirisha hivyon ni wachache sana wenye uwezo huo!

Asante Mkuu!
Kama ulivyosema mwenyewe hili ni suali la binafsi, na jibu lake pia litakuwa binafsi.Kuliweka hapa jamvini itakuwa siyo binafsi tena Mkuu.
 
Sio tu Kikwete atakayekuwa ameondoka bali kundi lote hili la WATAWALA waliotufikisha hapa tulipo sasa. Kumwona Kikwete kwamba ndiye kashindwa, ni mtizamo sahihi lakini FINYU kidogo. Hofu yangu ni kuwa nje ya CCM sijaona CHAMA au KIONGOZI mbadala.
 
Alishaonyesha hili tangu siku ya kwanza-siku alipoapishwa. Nilikwenda pale uwanja wa Uhuru kwa nia ya kusikia live jinsi nchi inavypewa mwelekeo mpya. lakini nilichoambulia ni kusikia falsafa ya kupokezana vijiti, nikajua tangu wakati ule kuwa tumeliwa

Mpita Njia,
Falsafa mbofumbofu kwa JK zimeendelea kuwa nyingi na kweli zinaudhi na kukera. Ukizisikia tu unaongeza maumivu ya kupoteza matumaini. Baya zaidi siku hizi kaanza kuibukia hata nadharia zisikuwa na mashiko kujibu maswali magumu. Matatizo ya kitaalamu hasa kiuchumi anayajibu kisiasa zaidi!

My take:
Bora kumsikiliza Mjoba Mrisho Mpoto hasa ile verse inayosema:
Kiitikio cha globalization kimeimbwa vizuri sana
Wageni wamefurahishwa na ule ubeti uliiouongeza "Mbio zetu toka uhuru mpaka hapa tulipo"
 
Kwakweli waTZ tulikosea sana kumpa madaraka ya urais huyu mkwere! Hakuwahi kuwa serious in anything kabla ya urais na bado kaendelea kuwa vile alivyokuwa! Cha ajabu bado kuna watu wanamuona eti aendelee kuwa rais kwa kipindi kingine kwa utaratibu wa utamaduni wa CCM... hizi ni fikra mgando!

Lipumba alipongeza maamuzi ya wananchi ya kumchagua kwa kishindo Bwana kikwete kuwa Rais wa Tanzania, lakini aliwatahadharisha kwamba yeye anamfahamu Kikwete kuwa ni mtu wa MIZAHA sana. sikumuelewa wakati ule bwana lipumba nikhisi kwamba labda ni kajiwivu fulani. sasa hivi baada ya kufanya trend analysis nimeanza kumuelewa alikua anamaanisha nini.
 
Lipumba alipongeza maamuzi ya wananchi ya kumchagua kwa kishindo Bwana kikwete kuwa Rais wa Tanzania, lakini aliwatahadharisha kwamba yeye anamfahamu Kikwete kuwa ni mtu wa MIZAHA sana. sikumuelewa wakati ule bwana lipumba nikhisi kwamba labda ni kajiwivu fulani. sasa hivi baada ya kufanya trend analysis nimeanza kumuelewa alikua anamaanisha nini.

Nami nayakumbuka maneno haya sana, laiti wote tungeona kama Prof. Lipumba! but still hatujaona maana anapigiwa upatu kushinda kwa kishindo 2010 .
 
Sio tu Kikwete atakayekuwa ameondoka bali kundi lote hili la WATAWALA waliotufikisha hapa tulipo sasa. Kumwona Kikwete kwamba ndiye kashindwa, ni mtizamo sahihi lakini FINYU kidogo. Hofu yangu ni kuwa nje ya CCM sijaona CHAMA au KIONGOZI mbadala.


Naomba fafanua huo ufinyu. Mimi naamini Kikwete ndiye kashindwa hence kuifelisha nchi kwa sababu yeye ndiye ameshika usukani. Yeye ndiye anayetarajiwa kutoa dira na mikakati ya wapi tuelekee. Ana uwezo wa kusema chochote atakacho nchi hii na kikatendeka. Anao uwezo wa kuibadilisha CCM completely, kama angekuwa na nia hiyo. Una maanisha nini kusema ni mtizamo finyu? Kikwete akiondoka akiingia madarakani mtu safi mwenye mwelekeo na nguvu za kuongoza (from any party including CCM) atasafisha uozo wote uliopo na kuweka watawala safi na wenye uwezo wa kuiongoza nchi. Viongozi mbadala wapo tele nje ya CCM, unahitaji miwani kuwaona labda! Unataka uwaoneje? au waweje? Wanahitaji kupewa nafasi ili waonekane wanachofanya; hivi sasa wamebanwa from all angles... ubabe tu kila mahali.
 
Wangapi tumeisoma ILANI ya UCHAGUZI ya CCM ya mwaka 2005? Ukiisoma ile vizuri utaona JMK anafanya "zaidi" ya alivyotakiwa kufanya na ilani hiyo! Tatizo liko kwa CCM, sio JMK. Tukiweza kuiondoa CCM, mengine yoote tunayoyataka yawe, yatakuwa tena kwa ziada. La kujiuliza labda CHAMA mbadala wa CCM ni kipi?


Hapo Mkuu unadanganya wanajamii. Mimi sijaisoma lakini wote tumesikia propaganda zao kuwa wanaleta maisha bora kwa kila mwananchi kwa ari, kasi na nguvu mpya. Leo hii, wananchi wanashindwa ku-afford mlo mmoja kwa siku, dozi ya malaria shida, ada ya mtoto shule ngumu, mashule meeengi ndio hayo; walimu vitabu, hakuna. Tunasubiriana kwenye foleni masaa matatu kutoka hapo Mwenge kufika kazini mjini hali kadhalika kurudi. Maji na umeme tunauziana kwa bei ya bidhaa za anasa licha ya upatikanaji usiotabirika.

Haya yote ni mambo CCM inayo kwenye ilan yao ya maisha bora kwa kila mtanzania; au mwenzangu wewe unaielewaje hiyo? Kazi ya huyo kiongozi wao ni kuhakikisha anadeliva hayo yote! Ni lipi katika hayo yanakufanya uamini na uaminishe umma kwamba amefanya na ziada?
 
Pasco,huo ndiyo ukweli kwa walio wengi.Kama ni uchambuzi na upembuzi wa matatizo ya nchi yetu na viongozi wake hakuna kilichobakia.Hali halisi inajulikana, matatizo, mapengo, viunzi/vikwazo vyote vinaeleweka.Mapendekezo yameshatolewa katika kila eneo.Kilichobaki ni utekelezaji tu.Inanikumbusha tafiti chungu nzima ambazo zimefanyika na mapendekezo lukuki kutolewa na maripoti kibao kujaza mashelfu na sasa technolojia imerahisha uhifadhi wa haya matokeo.
The country is heavily pregnant with ideas - what is needed now is the midwife to deliver the baby.And we all know that it is painful to deliver.....nani yuko tayari kuumwa uchungu wa kuzaa??? Ingewezekana kukwepa nadhani hakuna mwanamke angeukubali uchungu wa kuzaa.... ila nature has its own way to ensure whether u like it or not utazaa!Bahati mbaya sana mimba iliyopo kwa sasa haina cha kuisukuma izaliwe....kuzaa ni hiari..tutasubiri sana.
Ukisema eti wananchi waandamane kupinga mambo fulani kama walivyofanya nchi nyingine, tulion akilichowapata wazanzibari kipindi kile cha uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi.Nani anataka kufa? nikifa, nani atakumbuka kuwa nilifia nchi waje wanilelee wanangu? Sana sana watu wanaweza kunicheka na kusema yule naye! Haya kimbelembele kimeiponza familia yake... ona sasa wanae wanavyotaabika!
Binafsi sioni mabadiliko makubwa saaaana katika kizazi hiki ambacho kimeshaharibika kuanza fikra, mitizamo na vipaumbele vya maisha.
Haya ni mawazo yangu ya moyoni yasio na unafiki wa kufurahisha baraza.

Tusipende kuwasemea watu wengine. Kama wewe mambo yako ni mazuri na unaona bora familia yako ukae nayo kimya mle wenyewe huku wengine wanahangaika na maisha magumu na kwamba hiyo haikusumbui, we endelea. Itakapofika mahali sisi tunaonyonywa (kwa sababu ya matabaka na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea) tukaona hakuna faida tena ya kuishi maana tumepuuzwa na kunyimwa haki muda mrefu, tutajitokeza mitaani tukiandamana na this time itakuwa fujo ya kuua mtu. Hutakuwa tena na option ya kukaa kimya na familia yako ku-enjoy peke yenu.

Kinachotakiwa ni kuepuka kuifikisha jamii kwenye hatua hiyo kwa kushirikiana wote sasa hivi kuhakikisha tuna uongozi wa haki unaotujali maisha yetu sote. Ili hiyo itokee ni wajibu wetu sisi tulioelimika (sio waliosoma tu) na wenye nacho, kupiga kelele kwa nguvu iwezekanavyo kwa ajili ya wanyonge ili nao wajisikie wanacha kujivunia maisha kwenye nchi yao. Nakushauri wacha woga, kizazi hiki ndio chenye kuleta mabadiliko ya nchi hii. Kama ukiogopa, usieneze woga kwa wengine maana hautosaidia nchi yako. Jiamini.
 
Kama ukiogopa, usieneze woga kwa wengine maana hautosaidia nchi yako. Jiamini.

I like ur admonition and theoretical patriotism! I doubt it if you had read my post in its entirety coz ungeona mwisho kabisa nime sema "haya ni mawazo yangu binfsi........" which means hulazimishwi kukubaliana nayo kama ambavyo hata mimi silazimiki kukubaliana na mawazo yako.

Maadam unataka kufanya ujasiri, Can you show the way then? And by the way... I thought I was addressing PASCO seconding his idea..mhhhh it kindav scared you stiff?? Im really sorry for that.
 
Last edited:
Are you out of your mind?????
Waungane??? I dont buy that Idea.
Dawa si kuitoa sisiem madarakani kwa umoja wa wapinzani (a.ka. Kenya) bali ni kubadili mfumo mfu wa sasa na kuweka mpya kwa kukichagua chama kipya na si umoja wa wapinzani.
Ndugu yangu Msanii, Naomba respect. Nimetoa mawazo yangu kuwa 'bila wapinzani kuungana, hakuna kitu', ni mawazo yangu naomba uyaheshimu, na wewe 'you dont buy that idea', ni mawazo yako nayaheshimu, hii 'Are you out of your mind ya nini?.
respect.
 
I like ur admonition and theoretical patriotism! I doubt it if you had read my post in its entirety coz ungeona mwisho kabisa nime sema "haya ni mawazo yangu binfsi........" which means hulazimishwi kukubaliana nayo kama ambavyo hata mimi silazimiki kukubaliana na mawazo yako.

Maadam unataka kufanya ujasiri, Can you show the way then? And by the way... I thought I was addressing PASCO seconding his idea..mhhhh it kindav scared you stiff?? Im really sorry for that.
Thanks WoS for being yourself. I honestly admire you for who you are from point of your writings, which is something good.

Kuna baadhi ya discussions watu wanakuwa too emotional mpaka they loose focus na kuchangia kwa jazba mawazo yanayokuja kuonekana kama utopia, na ukiwa realist, honest na true to your self, unaweza onekana 'an enemy of the people'. Mimi nashukuru nilishayazoea hayo, sioni shida kubishana na mtu kwa jambo ambalo naamini ndio ukweli wangu hata kama tutaishia kugombana, ukweli utakapotimia, tutapatana tuu, 2010 ni Kikwete tena, tuendelee kujadili, kubishana na kunyoosheana vidole, baada ya October, 2010, tutapatana tena na kusubiri 2015 tuje kubishana tena.
To be true to yourself is to prioritize your priorities, wengine maslahi ya taifa mbele, wengine maslahi binafsi mbele, wengine kazi mbele, wengine pesa mbele, wengine pombe mbele, wengine 'chini' mbele, wengine watu mbele, wengine marafiki mbele, wengine makundi mbele, wengine JF mbele na wengine God na familiy kwanza and everything else comes next, 'I am a family man father of five!'.
 
Back
Top Bottom