Mdanganywa
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 620
- 342
Tuliwa tumebaki na siku 13 tu kuingia kituoni ni wazi kwamba pressure ya kulinda kura inaongezeka kila kukicha.
Maoni yangu ni kwamba kila chama kina wakala wake kusimamia uchaguzi. Baada ya kuhesabu kura na kila mmoja akajulikana amepata ngapi naamini nakala hupelekwa NEC na mawakala wanatoka kituoni na nakala/kopi ya matokeo ya ushindi zikiwa na sahihi zao.
Kama ni hivyo basi safari hii tusidanganyike. Tutumie mbinu ileile ya mitandao ambayo imefanikiwa kufumua siri nyingi za ufisadi ambazo nyaraka zake zenye sahihi zimetembea humuhumu mitandaoni.
Kinachotakiwa ni nini? Wakala anatakiwa aipeleke kopi yake kwenye chama chake. Lakini chama pia kitoe ushirikiano kutuma kopi zile kwenye mitandao kwa njia ya kuzi-scan kama zilivyo-scan-iwa zile nyaraka.
Nasema hivi kwa sababu itakuwa ni nafasi nzuri kuyasoma matokeo bila kubabaishana na bila kusubiri kupigiwa hesabu za kujumlisha na Tume ya uchaguzi.
Tume ikishaona kopi za matokeo zinatembea mitandaoni na tunahesabu wenyewe haitakuwa na wataanzia wapi kutangaza vinginevyo?
Huwa tunapenda kukwamisha hoja kwa kusema jambo fulani vijijini haliwezekani kama hili. Siku hizi si lazima ufanye scan kama miaka ile. Hata kupiga picha yaani snapshot inaweza kusidia kama font ya maandishi si kubwa kiasi hicho na kisha picha ikatumwa kwa mtu atakayeweza kuifikisha mitandaoni.
Awezaye kuboresha wazo hili ruksa maana ni wazo limekuja ghafla kichwani kama ambavyo nafikiri wengi wetu sasa hivi wazo la kuibiwa kura au kuchakachuliwa matokeo ni kubwa kuliko chochote.
Maoni yangu ni kwamba kila chama kina wakala wake kusimamia uchaguzi. Baada ya kuhesabu kura na kila mmoja akajulikana amepata ngapi naamini nakala hupelekwa NEC na mawakala wanatoka kituoni na nakala/kopi ya matokeo ya ushindi zikiwa na sahihi zao.
Kama ni hivyo basi safari hii tusidanganyike. Tutumie mbinu ileile ya mitandao ambayo imefanikiwa kufumua siri nyingi za ufisadi ambazo nyaraka zake zenye sahihi zimetembea humuhumu mitandaoni.
Kinachotakiwa ni nini? Wakala anatakiwa aipeleke kopi yake kwenye chama chake. Lakini chama pia kitoe ushirikiano kutuma kopi zile kwenye mitandao kwa njia ya kuzi-scan kama zilivyo-scan-iwa zile nyaraka.
Nasema hivi kwa sababu itakuwa ni nafasi nzuri kuyasoma matokeo bila kubabaishana na bila kusubiri kupigiwa hesabu za kujumlisha na Tume ya uchaguzi.
Tume ikishaona kopi za matokeo zinatembea mitandaoni na tunahesabu wenyewe haitakuwa na wataanzia wapi kutangaza vinginevyo?
Huwa tunapenda kukwamisha hoja kwa kusema jambo fulani vijijini haliwezekani kama hili. Siku hizi si lazima ufanye scan kama miaka ile. Hata kupiga picha yaani snapshot inaweza kusidia kama font ya maandishi si kubwa kiasi hicho na kisha picha ikatumwa kwa mtu atakayeweza kuifikisha mitandaoni.
Awezaye kuboresha wazo hili ruksa maana ni wazo limekuja ghafla kichwani kama ambavyo nafikiri wengi wetu sasa hivi wazo la kuibiwa kura au kuchakachuliwa matokeo ni kubwa kuliko chochote.