Kongamano la mswada wa kuanzisha mchakato wa katiba mpya lazua hisia nyingi

Mtu wa Mungu

JF-Expert Member
Nov 9, 2010
444
19
Kwa zaidi ya mwezi sasa media zimetulisha kiasi cha kutuvimbisha akili habari za Loliondo-sijui taifa limefaidika nini zaidi ya kuchochea maafa ya wanaokufa kwa sababu ya kujazwa matumaini matupu (empty hopes) kwa kudhani ni imani ya uponyaji wa mungu asiyejulikana!!!
Kwa ratiba ya vikao vya bunge la Aprili , wiki ijayo (Aprili 7,2011) serikali ya ccm inaweka mbele ya wabunge mswada wa kuweka mchakato wa kuwapa waTz katiba mpya kwa staili ya serikali ya ****** na chama chake ya kupata katiba mpya ya kuwaongoza waTz kwa kipindi kingine cha miaka 50 ijayo!!!!!!!!
Kwa wale waliofuatilia kwa karibu sana kongamano la wasomi wa Chuo Kikuu cha Dsm , UDSM, ikiongozwa na UDASA, Jumamosi tarehe 2/4/2011, lililohudhuriwa pia na baadhi ya vyama vya siasa vilivyoalikwa, wakiwemo cdm,nccr, udp, cuf, ccm bila vigogo (waliingia mitini), kumezaliwa hisia nyingi zenye mwelekeo tofauti-wengine wakiona hii ni janja tu ya ccm na serikali yake ya kuwahadaa waTz kama walivyozoea kufanya na kutoka bila majeraha!!!!!!
Swali la msingi ni hili kwamba nani atatoka mshindi safari hii???? Kwenye uchaguzi wa Oktoba 2010 ****** na chama chake cha sisiemu walitoka washindi kwa kuchakachua matokeo!!!!!; je safari hii nani atatoka mshinda ???????? Great Thinkers hebu tupeni mtazamo na changamoto zilizo mbele yetu katika suala nyeti na la msingi kwa msitakabali wa taifa hili lenye kuongozwa na imani za kishirikina??????????????????!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Wananchi lazima tushinde vingenevyo tuanze kujilaumu wenyewe kwa uzembe wa kushindwa kudai haki zetu. Prince Bagenda katika kongamano lile alituasa kuwa vitu vingine lazima tuvitudai.
 
Haiki siku zote haipewi mtu, haki huchukuliwa kwa ujasiri mkubwa to kwa wanyanyasaji toke maha ilikofichwa na Na mafisadi.

Hatua kamambe iko njiani hivi sasa endapo ukaidi wa CCM juu ya MUSWAD wao huo juu ya Katiba utapelekwa kama ulivyo kwa kupuuza matakwa ya umma.
 
Back
Top Bottom