Kongamano la Azimio la Arusha

Bernadi James mwanafunzi wa UDSM,anasema kabla ya kurudisha azimio la Arusha ni lazima kwanza tuvunje azimio la Zanzibar.....anakumbusha ubinafsishaji wa nyumba za serikali ambao ni matokeo ya azimio za Zanzbr
 
Prosessor shivji anachangia sasa hoja zilizotolewa:
anasema amefarijika kuwa azmio bado linakubalika miongoni mwa jamii hasa vijana
 
Shifji anaanza kuchambua tofauti ya viongozi na watawala....anasema Azimio halikuzungumzia kuhusu utawala bora, dhana hii ilitolewa na World bnk, anasema azimio linazungumzia uongozi bora na liloiweka muongozo ili viongozi wasijegeuka watawala
 
Shivji: Azimiohalikuzumzia maadili, lilikuwa na masharti/miiko...hii ni kwa sbb maadili hayapimiki
 
Shivji: katiba ya mwaka 77 bado inataja ujamaa na kujitegemea na uliweka miiko ya uongozi, baada ya kukubali uliberali neno ujamaa na kujitemgemea halikuondolewa ila neno ujamaa na kujitegemea lilikuwa defined
 
Shivji: katiba ya CCM ya 77 ilisema njia kuu za uzalishaji zilikuwa mikononi mwa dola, katika katiba hii hili liliondolewa
 
Defn ya sasa mbona haijinyambulishi, na huwezi elewa maana halisi?
Nimeshaisoma, haieleweki, huwezi kuona mjamaa na mbepari. Almost wote ni Wajamaa....
 
Shivji;
Mwalimu alisema alikuwa anaomba Mungu kusiwe na vyama vingi kwa idadi bali viwe viwili kama Marekani, na vyote viwe na msingi wa ujamaa, ila viwe vinatofautiana kwa namna ya kuitekeleza
 
Shivji:
Vyama vyote vya siasa lengo lao ni kuingia madarakani, na kwa njia hii wanaweza kutumia njia yoyote ili kuingia madarakani. Kwa hiyo tusitegemee kama vinaweza kubadilisha mfumo wa jamii iliyo kubwa.
 
Shivji;
Ngombaremwilu ndiye aliyetoa hoja kuwa wafanyabiashara wanaweza kuwa wanachama wa CCM, hii ilikuwa ni enzi ya kipindi cha mzee Ruksa.

Kabla ya hapo CCM ilikuwa ikifahamika kwa ajii ya wakulima na wafanyakazi.
 
Dah,nilipata Taarifa nikiwa nje ya Dar....nasikitika sana kukosa kuhudhuria kongamano hili
 
Ibrahim Kaduma;
Lengo la miiko lilikuwa ni kujenga maadili ya kijamaa, kwa hiyo maadili yanafundishika.
Anachallenge point ya Shivji kuwa maadili hayafundishiki.
 
Kaduma;
Kulipokuwa na tatizo kama la Shinyanga wafungwa kufa mawaziri waliwajibika, wafungwa walipotoroka Ukonga mawaziri na makamishna wa magereza walijiuzuru.

MY take: Mbona Mbagala na Gongo la Mboto hakuna aliyewajibika?
 
Kaduma:
Maadili yanaanzia mahali, unatekeleza kitu fulani then ndo inakuwa tabia ya taifa. Anakumbusha jinsi Mwinyi alipojiuzulu wakati ule wafungwa walivyokufa na pia yule waziri aliyejiuzulu wakati wafungwa walipotoroka gereza la ukonga.
 
Kaduma:
Azimio la Zanzibar lilikuwa na lengo la kuahalisha wizi wa viongozi ambao hawakuwa na maadili ya uongozi.
 
Shivji: Ngombaremwilu ndiye ayetoa hoja kuwa wafanyabiashara wanaweza kuwa wanachama wa CCM hii ilikuwa ni enzi ya kipindi cha mzee ruksa, kabla ya hapo CCM ilikuwa ikifahamika kwa ajii ya wakulima na wafanyakazi

AA halikuuliwa pale Zanziba na Azimio la Zanzibar, bali na hotuba ya Kingunge Ngombale Mwiru pale Chimwaga pale Dodoma. Na huo ukawa ndio mwanzo wa mafisadi kuingia katika chama na ndio mwanzo wa Kingunge mwenyewe kubadilika kuwa fisadi naye na kusahau misingi ya AA.
 
Back
Top Bottom