Kona ya Soka la Zenji.... Ni hapa

Kibunango

Platinum Member
Aug 29, 2006
8,416
2,263
Leo tunaanza habari ya Chelsea(Miembeni) ya Zenj kutwaa kombe la Mapinduzi baada ya kuibanjua Polisi kwa bao 2-1, katika mechi ya dezo iliyofanyika hapo Zenj....
 
Huku kuna mpira nako au kuna foliti. Duh! Kombe la mapinduzi.. huu mpira au siasa!!!
 
Leo tunaanza habari ya Chelsea(Miembeni) ya Zenj kutwaa kombe la Mapinduzi baada ya kuibanjua Polisi kwa bao 2-1, katika mechi ya dezo iliyofanyika hapo Zenj....

Naskia Zenji kwa uchawi kwenye mpira mnatisha kwelikweli au mambo yamebadilika siku hizi?
 
Naskia Zenji kwa uchawi kwenye mpira mnatisha kwelikweli au mambo yamebadilika siku hizi?
Kamanda, suala la uchawi ni huko S'wanga, Zenj ni ball tu, au umesahau ule usemi wa "Ingawa tumefungwa chenga twawala..."
 
Ukata waikwamisha ZFA Ghana

CHAMA cha Soka Zanzibar (ZFA), kimeshindwa kuwasafirisha viongozi wake watatu kwenda kuhudhuria mkutano mkuu wa Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF), kutokana na ukata.
Kikao hicho kinachofanyika nchini Ghana, Januari 19, ikiwa ni siku moja kabla ya kuanza kwa kivumbi cha fainali za Kombe la Mataifa Afrika, kila nchi mwanachama inatakiwa kuwakilishwa na viongozi watatu.

Kutokana na ukata huo, ZFA imelazimika kusafirisha kiongozi mmoja pekee, Rais Ali Ferej Tamim ambaye aliondoka jana alfajiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Kenya.

Kwa mujibu wa Msemaji wa ZFA, Maulid Hamad Maulid, alithibitisha kubaki kwa viongozi wengine wawili kutokana na kukosekana fedha za kwenda na kurudi nchini Ghana.

Alisema, CAF hutoa nauli pamoja na kuhudumia gharama nyingine kwa kiongozi mmoja tu wa juu wa ZFA huku wengine wawili hugharamiwa na Chama cha nchi husika.

"Ni kweli tumeshindwa kuwapeleka Makamu wa Rais na Katibu Mkuu wa ZFA kutokana na ukosefu wa fedha unaotukabili kwa muda mrefu," alisema Maulid.

Aidha, alifafanua kuwa baada ya kuwasiliana na mashirika kadhaa yanayotoa huduma ya ndege visiwani Zanzibar, walielezwa kuwa nauli ya kiongozi mmoja kwenda na kurudi ni dola za Marekani 1050.

Hata hivyo alisema ZFA haikupeleka maombi yao katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kushindwa kuelezea sababu za msingi za kutoomba msaada wa serikali.

Mkutano Mkuu wa CAF, ambao huhudhuriwa na viongozi wa vyama vyote wanachama wa shirikisho hilo, unatarajiwa kuzungumzia masuala mbalimbali ya maendeleo ya soka katika Bara la Afrika.

Zanzibar ilipata nafasi ya kushiriki katika mkutano huo, baada ya kupatiwa uanachama wa muda wa CAF ambao uliiwezesha klabu zake kushiriki katika mashindano yanayoandaliwa na CAF.

Aidha, kushindwa kuhudhuria kwa viongozi hao, kunaonyesha wazi kuwa ZFA inahitaji msaada wa hali na mali kwa ajili ya kujiendesha yenyewe pamoja na kuweza kushiriki katika nyanja za kimataifa.

ZFA bado inalilia uanachama wa CAF kwa lengo la kupata uanachama wa FIFA ambao bado ni gumzo kubwa miongoni mwa wadau wa soka.

Kama ZFA itapatiwa uanachama wa kudumu CAF, Zanzibar itaweza kushiriki katika fainali za Mataifa ya Afrika kupitia timu yake ya taifa ‘Zanzibar Heroes' tofauti na ilivyo sasa ambayo ni sehemu ya timu ya Taifa Stars.

Wadau wa soka waliozungumza na Tanzania Daima walisema wakati umefika kwa viongozi wote wa ZFA kuweka tofauti zao kando dhidi ya viongozi wa SMZ kwa manufaa ya soka ya Zanzibar.

Walisema migogoro inayoendelea baina ya viongozi hao, inazidi kuirudisha nyuma Zanzibar katika mbio zake za kuelekea kunako soka la kulipwa katika nchi zilizoendelea.
 
Wazenj waanza Vibaya Afrika

Timu ya Chipukizi ya Pemba jana Jumamosi iliangushiwa mvua ya mabao na Green Buffaloes ya Zambia baada ya kufungwa 5-0 katika mchezo wa kwanza wa raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho la klabu za Afrika, kwenye Uwanja wa nyumbani wa Gombani.

Green Buffaloes walipata bao lao la kwanza katika dakika ya 12 lililofungwa na Leven Tembo, aliyeongeza la pili dakika 11 baadaye, huku Sebastian Mwansa akiongeza la tatu katika dakika ya 30. Emmanuel Mayuku na Morgan Anjeme walifunga la nne na la tano katika dakika za 60 na 80.

Kocha mkuu wa Chipukizi iliyokuwa ikishangiliwa na watazamaji wachache waliofika uwanjani Ahmed Mumba alikiri kuzidiwa kimbinu kutokana na kutokuwa na uzoefu wa mashindano ya kimataifa.

Alisema pia timu yake imesheheni wachezaji wazee hivyo sasa anahitaji chipukizi zaidi.

Nao mabingwa wa Zanzibar Miembeni juzi Ijumaa usiku walitota kwa kufungwa na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini kwa bao 1-0 katika mchezo kwanza wa raundi ya kwanza ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika.

Source: Reta Raha
 
ZFA Wanatia Aibu

Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) kimesema kimepokea kwa masikitiko barua ya kuondolewa kwa kiongozi wa chama hicho, ambaye alikuwa afuatane na Miembeni kwenda nchini Afrika Kusini kwa mechi dhidi ya Mamelodi Sundowns ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika.

Msemaji wa ZFA, Maulid Hamad Maulid alieleza kuwa uongozi wa Miembeni umeeleza hauna fedha za kumgharimia kiongozi huyo.

``Uamuzi huo unakwenda kinyume na taratibu za kimataifa, barua yao tumeipokea na tunaifanyia kazi, ndio maana tumeamua kuitisha kikao cha Kamati ya Utendaji kujadili maamuzi hayo,`` alieleza.

Alisema kwamba kikao cha Kamati hiyo ya Utendaji kitakutana leo ili kujadili uamuzi huo na kuangalia hatua zaidi za kuchukua.

Alisema kwamba kwa kuzingatia kanuni ya ZFA, Miembeni wanapaswa kugharamia mjumbe katika msafara wao.

Msafara wa Miembeni unatazamiwa kujumuisha watu 30, ambapo watakwenda kwa mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo baada ya kufungwa Ijumaa iliyopita 2-1.

Habari zaidi zimesema kwamba Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, ambaye alikuwa aambatane na timu hiyo ni Msemaji wa ZFA, Maulid Hamad Maulid na ndiye aliyekuwa ameteuliwa kufuatana na timu hiyo
 
Shamuhuna anapaswa kuwajibika kwa migogoro ya ZFA?

MCHEZO wa soka visiwani hapa, katika siku za hivi karibuni unazidi kukatisha tamaa kutokana na chuki, mifarakano, majungu na fitina ambazo zinaelekea kuupeleka mchezo huo kaburini na kubaki kuwa historia miongoni mwa wapenda soka wa Zanzibar.
Hizo ni kauli za wadau wa soka, wakiwemo viongozi wa juu wa chombo kinachosimamia mchezo huo visiwani hapa (ZFA), baada ya wawakilishi wawili wa Zanzibar katika mashindano ya kimataifa kujikuta wakiianza vibaya michuano hiyo, huku malumbano yakizidi kushamiri kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BTMZ) na chama chenye jukumu la kusimamia mchezo wa soka Zanzibar.

Mwanzoni mwa mwezi huu, mashabiki wa soka walielekeza macho na masikio yao katika viwanja vya Amaan na Gombani kushuhudia vipigo kwa timu zao mbili za Miembeni na Chipukizi na kuondoa matumaini ya soka la zamani kurejea Zanzibar.

Wakati hayo yakitokea, viongozi wa Miembeni nao chupuchupu kutwangana makonde na wenzao wa ZFA Taifa, katika kikao kilichoitishwa kujadili gharama za mjumbe wa Chama cha Soka Taifa atakayeambatana na Miembeni nchini Afrika Kusini, kwa ajili ya pambano la marudiano dhidi ya Mamelodi Sundown.

Mzozo huo uliibuka kati ya Naibu Mkurugenzi wa Miembeni, Abubakar Bobea na Makamu wa Rais wa ZFA, Alhajj Haji Ameir baada ya Miembeni kuendelea kutetea msimamo wake wa kutomgharamia mjumbe wa chama hicho, katika safari hiyo ya bondeni.

"Kama mnataka tumlipie nauli mjumbe wenu, bora aende Mzee Zam Ali (Katibu Mkuu ZFA), ambaye ana matatizo ya presha na huko tutamsaidia kupata matibabu, badala ya Maulid Hamad Maulid (Msemaji wa ZFA)…. mnataka mambo, wakati hamna uwezo, kama hamna pesa bora mjiuzulu," alisema Bobea.

Uongozi wa Miembeni, uliitwa na ZFA Taifa makao makuu ya chama hicho yaliyopo katika Uwanja vya Amaan, kueleza sababu za kukataa kumgharamia mjumbe wake, kwenda Afrika Kusini, kitendo ambacho ZFA inadai kuwa ni kinyume na taratibu za mashirikisho ya soka ya kimataifa ya CAF na FIFA.

Uongozi wa Miembeni, hivi karibuni uliwashtua wapenda soka kwa madai ya kutokuwa na uwezo wa kumgharamia mjumbe huyo, licha ya kutangaza kuwa itaondoka na ujumbe wa watu 31 kwenda Afrika Kusini, akiwemo Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Wilaya ya Mjini, Nassor Salum ‘Aljazeera', ambaye ni hasimu mkubwa wa ZFA taifa.

Aljazeera katika siku za hivi karibuni, aliushangaza umma pamoja na Rais wa ZFA, Ali Ferej Tamim, kutokana na kujivika kofia isiyomwenea ya kuiwakilisha Miembeni katika kikao cha majadiliano kilichofanyika kabla ya mechi ya Miembeni na Mamelodi Sundown.

Mgawanyiko wa vyombo vyenye dhamana ya michezo, umesababisha viongozi wa ZFA taifa kutoaminiwa katika masuala ya fedha, kutokana na Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BTMZ), kwa kushirikiana na wizara husika, kutoa fedha moja kwa moja kwa klabu bila kupitia ZFA taifa, jambo linalolalamikiwa na viongozi wa chama hicho.

Hivi karibuni Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, kupitia BTMZ ilizipa Miembeni na Chipukizi, sh milioni 20 kwa ajili ya maandalizi ya michezo yao ya awali, kitendo ambacho kiliwashangaza viongozi wengi wa ZFA Taifa.

"Ni kweli Aljazeera alihudhuria kikao kile, mimi nilishangaa kumwona, lakini baadaye nilipouliza niliambiwa kuwa anaiwakilisha Miembeni na yeye ni mmoja kati ya watu wanaotoa mchango mkubwa ndani ya klabu hiyo," alisema Ali Ferej Tamim.

Kamati tendaji ya ZFA Taifa, ilimteua Msemaji wake, Maulid Hamad Maulid, kuongozana na timu hiyo nchini Afrika Kusini, ambako kiutaratibu hutakiwa kuandika ripoti ya mchezo, jambo ambalo litawagharimu Miembeni endapo wataondoka bila ya kiongozi yeyote kutoka chama cha kitaifa.

Habari kutoka ndani ya ZFA, zinasema chama hicho kimewasiliana na Chama cha Soka Afrika Kusini na kueleza kuwa hakijatuma mjumbe yeyote katika msafara wa timu hiyo, baada ya Miembeni kumkataa mjumbe aliyeteuliwa na kamati tendaji kuongozana na msafara huo.

Taarifa zilizopatikana zinaeleza kwamba, huduma wanazozitumia ZFA taifa hivi sasa zinajadiliwa kwa karibu, ikiwemo ofisi wanazotumia, samani na mishahara ya wafanyakazi wasiopungua 10, kutokana na viongozi wa ZFA kushindwa kumuomba radhi Naibu Waziri Kiongozi na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Ali Juma Shamuhuna kama walivyoahidi katika siku za hivi karibuni.

Chimbuko la mgawanyiko baina ya vyombo vyenye dhamana na michezo, imetokana na makovu ya uchaguzi mkuu wa chama hicho kutokana na kuanguka kwa baadhi ya wagombea waliokuwa wakiungwa mkono na serikali na hivyo kupoteza imani kwa baadhi ya viongozi waliopo madarakani.


Source: TZ Daima
 
Shamuhuna anapaswa kuwajibika kwa migogoro ya ZFA?

MCHEZO wa soka visiwani hapa, katika siku za hivi karibuni unazidi kukatisha tamaa kutokana na chuki, mifarakano, majungu na fitina ambazo zinaelekea kuupeleka mchezo huo kaburini na kubaki kuwa historia miongoni mwa wapenda soka wa Zanzibar.
Hizo ni kauli za wadau wa soka, wakiwemo viongozi wa juu wa chombo kinachosimamia mchezo huo visiwani hapa (ZFA), baada ya wawakilishi wawili wa Zanzibar katika mashindano ya kimataifa kujikuta wakiianza vibaya michuano hiyo, huku malumbano yakizidi kushamiri kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BTMZ) na chama chenye jukumu la kusimamia mchezo wa soka Zanzibar.

Mwanzoni mwa mwezi huu, mashabiki wa soka walielekeza macho na masikio yao katika viwanja vya Amaan na Gombani kushuhudia vipigo kwa timu zao mbili za Miembeni na Chipukizi na kuondoa matumaini ya soka la zamani kurejea Zanzibar.

Wakati hayo yakitokea, viongozi wa Miembeni nao chupuchupu kutwangana makonde na wenzao wa ZFA Taifa, katika kikao kilichoitishwa kujadili gharama za mjumbe wa Chama cha Soka Taifa atakayeambatana na Miembeni nchini Afrika Kusini, kwa ajili ya pambano la marudiano dhidi ya Mamelodi Sundown.

Mzozo huo uliibuka kati ya Naibu Mkurugenzi wa Miembeni, Abubakar Bobea na Makamu wa Rais wa ZFA, Alhajj Haji Ameir baada ya Miembeni kuendelea kutetea msimamo wake wa kutomgharamia mjumbe wa chama hicho, katika safari hiyo ya bondeni.

“Kama mnataka tumlipie nauli mjumbe wenu, bora aende Mzee Zam Ali (Katibu Mkuu ZFA), ambaye ana matatizo ya presha na huko tutamsaidia kupata matibabu, badala ya Maulid Hamad Maulid (Msemaji wa ZFA)…. mnataka mambo, wakati hamna uwezo, kama hamna pesa bora mjiuzulu,” alisema Bobea.

Uongozi wa Miembeni, uliitwa na ZFA Taifa makao makuu ya chama hicho yaliyopo katika Uwanja vya Amaan, kueleza sababu za kukataa kumgharamia mjumbe wake, kwenda Afrika Kusini, kitendo ambacho ZFA inadai kuwa ni kinyume na taratibu za mashirikisho ya soka ya kimataifa ya CAF na FIFA.

Uongozi wa Miembeni, hivi karibuni uliwashtua wapenda soka kwa madai ya kutokuwa na uwezo wa kumgharamia mjumbe huyo, licha ya kutangaza kuwa itaondoka na ujumbe wa watu 31 kwenda Afrika Kusini, akiwemo Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Wilaya ya Mjini, Nassor Salum ‘Aljazeera’, ambaye ni hasimu mkubwa wa ZFA taifa.

Aljazeera katika siku za hivi karibuni, aliushangaza umma pamoja na Rais wa ZFA, Ali Ferej Tamim, kutokana na kujivika kofia isiyomwenea ya kuiwakilisha Miembeni katika kikao cha majadiliano kilichofanyika kabla ya mechi ya Miembeni na Mamelodi Sundown.

Mgawanyiko wa vyombo vyenye dhamana ya michezo, umesababisha viongozi wa ZFA taifa kutoaminiwa katika masuala ya fedha, kutokana na Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BTMZ), kwa kushirikiana na wizara husika, kutoa fedha moja kwa moja kwa klabu bila kupitia ZFA taifa, jambo linalolalamikiwa na viongozi wa chama hicho.

Hivi karibuni Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, kupitia BTMZ ilizipa Miembeni na Chipukizi, sh milioni 20 kwa ajili ya maandalizi ya michezo yao ya awali, kitendo ambacho kiliwashangaza viongozi wengi wa ZFA Taifa.

“Ni kweli Aljazeera alihudhuria kikao kile, mimi nilishangaa kumwona, lakini baadaye nilipouliza niliambiwa kuwa anaiwakilisha Miembeni na yeye ni mmoja kati ya watu wanaotoa mchango mkubwa ndani ya klabu hiyo,” alisema Ali Ferej Tamim.

Kamati tendaji ya ZFA Taifa, ilimteua Msemaji wake, Maulid Hamad Maulid, kuongozana na timu hiyo nchini Afrika Kusini, ambako kiutaratibu hutakiwa kuandika ripoti ya mchezo, jambo ambalo litawagharimu Miembeni endapo wataondoka bila ya kiongozi yeyote kutoka chama cha kitaifa.

Habari kutoka ndani ya ZFA, zinasema chama hicho kimewasiliana na Chama cha Soka Afrika Kusini na kueleza kuwa hakijatuma mjumbe yeyote katika msafara wa timu hiyo, baada ya Miembeni kumkataa mjumbe aliyeteuliwa na kamati tendaji kuongozana na msafara huo.

Taarifa zilizopatikana zinaeleza kwamba, huduma wanazozitumia ZFA taifa hivi sasa zinajadiliwa kwa karibu, ikiwemo ofisi wanazotumia, samani na mishahara ya wafanyakazi wasiopungua 10, kutokana na viongozi wa ZFA kushindwa kumuomba radhi Naibu Waziri Kiongozi na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Ali Juma Shamuhuna kama walivyoahidi katika siku za hivi karibuni.

Chimbuko la mgawanyiko baina ya vyombo vyenye dhamana na michezo, imetokana na makovu ya uchaguzi mkuu wa chama hicho kutokana na kuanguka kwa baadhi ya wagombea waliokuwa wakiungwa mkono na serikali na hivyo kupoteza imani kwa baadhi ya viongozi waliopo madarakani.


Source: TZ Daima


duh shughuli si ndogo,chanzo cha yote haya ni nini?

hivi tuseme ni siasa au kuna zaidi ya hilo?

mkuu wa kikuona wahusika kuwa umepesti tu watakukaripia ww(jokes)
 
duh shughuli si ndogo,chanzo cha yote haya ni nini?

hivi tuseme ni siasa au kuna zaidi ya hilo?

mkuu wa kikuona wahusika kuwa umepesti tu watakukaripia ww(jokes)
Siasa kwa upande mkubwa ndio chanzo cha migogoro ZFA... kila waziri akiingia madarakani anataka ZFA yake na kushindwa kabisa kuheshimu matakwa ya vilabu vinavyochagua viongozi hao...

*nimekopi na kupaste kwa kisomi zaidi... kwani nimeweka na source ya huko nilikokopi....! kheee heeeee heeee!
 
Klabu zote zatolewa kombe la CAF...

Zanzibar teams have been eliminated in the CAF competitions at preliminary stage.

Miembeni and Chipukizi FC have bowed out after losing both legs - home and away.

South Africa`s Mamelodi Sundowns hit Miembeni 4-0 in the African Champions League second leg match in South Africa on Friday. Sundowns scored two goals in each half.

Sundowns also won 1-0 when Miembeni hosted them in the first leg at Amaan Stadium two weeks ago.


The South African club have advanced with a 5-0 aggregate.

Chipukizi which were competing in the Confederation Cup were also hammered 2-0 by Green Bufaloo of Zambia in the return leg match in Lusaka over the weekend.

Bufaloo also won 5-0 in the first leg match in Zanzibar



Chanzo: The Guardian
 
Zantel Kumwaga Mamilioni Zenj... ni baada ya kuamua kudhamini soka la Zenj ambalo kwa miaka mingi limekuwa likisuasua kutokana na tatizo la ukata kwa vilabu vingi visiwani humo. Kuna kipindi kampuni za Laga zilijaribu kutaka kudhamini soka huko visiwani pasipo mafanikio...

Zaidi Hapa..


Zantel, ZFA waanguka wino

Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel jana ilitiliana rasmi mkataba na Chama cha soka cha Zanzibar (ZFA) wa kudhamini Ligi Kuu ya soka ya Zanzibar.

Hafla ya utiaji saini ilifanyika kwenye ofisi za ZFA na kuhudhuriwa na wawakilishi wa timu 122 zinazoshiriki katika ligi hiyo.

Katika kudhamini kila timu inatazamiwa kupata kiasi cha Sh. milioni tano ili kufanikisha ushiriki wake kwenye ligi hiyo.
Katika shughuli hiyo kila timu ilipewa seti mbili za jezi zenye nembo ya Zantel.

Pia kampuni ya Zanzibar Bottlers nayo imeingia katika udhamini wa ligi hiyo, ambapo itatoa vinywaji wakati wa mechi za ligi hiyo. Mkurugenzi wa Kampuni, Taufiq Turkey alidai kuwa kampuni yake katika udhamini huo utakaogharimu kiasi cha Sh. milioni tano, itatoa sare za waamuzi na kutoa posho zao.

SOURCE: Nipashe
 
Zantel Kumwaga Mamilioni Zenj... ni baada ya kuamua kudhamini soka la Zenj ambalo kwa miaka mingi limekuwa likisuasua kutokana na tatizo la ukata kwa vilabu vingi visiwani humo. Kuna kipindi kampuni za Laga zilijaribu kutaka kudhamini soka huko visiwani pasipo mafanikio...

Zaidi Hapa..

Zantel, ZFA waanguka wino

Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel jana ilitiliana rasmi mkataba na Chama cha soka cha Zanzibar (ZFA) wa kudhamini Ligi Kuu ya soka ya Zanzibar.

Hafla ya utiaji saini ilifanyika kwenye ofisi za ZFA na kuhudhuriwa na wawakilishi wa timu 122 zinazoshiriki katika ligi hiyo.

Katika kudhamini kila timu inatazamiwa kupata kiasi cha Sh. milioni tano ili kufanikisha ushiriki wake kwenye ligi hiyo.
Katika shughuli hiyo kila timu ilipewa seti mbili za jezi zenye nembo ya Zantel.

Pia kampuni ya Zanzibar Bottlers nayo imeingia katika udhamini wa ligi hiyo, ambapo itatoa vinywaji wakati wa mechi za ligi hiyo. Mkurugenzi wa Kampuni, Taufiq Turkey alidai kuwa kampuni yake katika udhamini huo utakaogharimu kiasi cha Sh. milioni tano, itatoa sare za waamuzi na kutoa posho zao.

SOURCE: Nipashe

isije ikawa ndio kutia mafuta kwenye moto maana pesa hizo na kwa vile mawasiliano mema baina ya smz na zfa
 
isije ikawa ndio kutia mafuta kwenye moto maana pesa hizo na kwa vile mawasiliano mema baina ya smz na zfa
Naona hii itasaidia zaidi vilabu kuliko hao ZFA, SMZ kwa upande mwingine watoe ruhusa ya kuendelezwa kwa viwanjwa vingine vya fotibali, na waache malumbano yasio na faida yoyote katika soka na ZFA...
 
Hafidh Ally amenidhalilisha - Tenga

Rais wa Shirikisho la soka nchini (TFF) Leodgar Tenga amemjia juu mjumbe wa kamati ya utendaji wa Chama cha soka cha Zanzibar (ZFA) ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Dimani (CCM) Hafidh Ally kwa kumtolea kauli za kumdhalilisha bungeni hivi karibuni.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Tenga alisema kauli zilizotolewa na Ali ni za kushangaza kwa kuwa zilikuwa zikimlenga yeye binafsi (Tenga) na sio TFF.
Nimesikitishwa sana na kauli ya kejeli na dharau zilizotolewa juu yangu na ndugu yangu Hafidh Ali, kwa kweli sioni sababu ya yeye kutoa zile ukizingatia nimekuwa nikichukua hatua na uongozi wa soka nchini kama Rais wa TFF,î alisema Tenga.

Tenga alisema ameanza kumfahamu Hafidh tangu akiwa mwamuzi wa soka wa kimataifa na yeye (Tenga) akiwa Katibu Mkuu wa FAT na kuanzia kipindi hicho hawakuwahi kutupiana maneno ya kejeli na dharau kama alivyofanya Hafidh.
Alisema kauli ya Hafidh Ali ya kumshtumu kuwa yeye (Tenga) ana kiburi na jeuri na anachangia Chama cha soka cha Zanzibar (ZFA) kutopewa uanachama wa Shirikisho la soka la Kimataifa (FIFA) siyo ya kweli kwa kuwa mchakato mzima uliokuwa ukifanywa na ZFA wa kupata uanachama huo ulikuwa ukipigiwa debe na TFF chini ya Rais wake, ambaye ni yeye.

Sababu za ZFA kutopewa uanachama yeye (Hafidh) anazifahamu na anazijua juhudi tulizokuwa tukizifanya pamoja kati yetu sisi (TFF) pamoja na ZFA kuhakikisha Zanzibar wanapata uanachama huo iweje leo anakuja na maneno ya kunidhalilisha,î alihoji Tenga.

Alisema kwa sasa Hafidh ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya ZFA na pia ni mkufunzi na mjumbe wa kamati ya waamuzi ya CECAFA wakati yeye (Tenga) ni Mwenyekiti wa CECAFA hivyo kitendo cha kutoa maneno hayo amemkejeli kiongozi wake jambo ambalo ni kinyume na maadili ya mchezo wa soka.

Tenga alisema sasa umefika wakati kwa viongozi wa michezo nchini kutoa kauli za ukweli na zenye uhakika ili kuepusha migongano na maswali kwa wananchi.

Hivi karibuni mbunge huyo akichangia hotuba ya bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu, alimshutumu Tenga kwa kuwa na kiburi na kejeli na ndiye anayechangia ZFA, wasipate uanachama wa FIFA na hivyo kuleta mgogoro kati ya ZFA na TFF.
 
Miembeni FC lose sponsor

Ibrahim Makungu who used to support Miembeni as a team director has parted ways with the former Zanzibar champions.

Makungu has handed over the team to the club elders, a decision reached barely few weeks after the Isles top flight side failed to retain their premier soccer title.

Makungu said his decision was accelerated by the team’s elders who demanded to be handed back the authority to manage their team.

“It was a decision based on meeting the demands of the team elders and no one else”, said Makungu.

However, Makungu said courtesy of his strong devotion to the club, he would maintain the payroll of the players that amounts to two million shillings on monthly basis.

He urged the elders of the club to maintain peace and stability for the benefit of their fans who enjoy big majority in Zanzibar and across the country.
Makungu owns Zanzibar Ocean View soccer team that won promotion into the top flight division this season.

The departure of Makungu has been dominating street talks throughout Zanzibar as fans ponder the future of the team in terms of financial support.
Most of the Zanzibar teams that used to enjoy single handed sponsorship have kissed a hand of good bye from the premiership berth in the past. These include Mohamed Raza’s Shangani and Mlandege that was ditched by Abdulsatar Daud.

Malindi that also were enjoying strong financial backing from businessman Naushad Mohamed are also struggling to keep premiersh.

Source: IPPMEDIA
 
mimi naona sisi UNGUJA tuachane na soccer,naona kama tuna untapped talents na potential kubwa ya kucheza NETBALL
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom