BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Ufisadi mpya CCM
na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
MKURUGENZI wa Kikundi cha Sanaa cha Tanzania One Theatre (TOT), Kapteni John Komba, anakabiliwa na tuhuma za ubadhirifu wa mamilioni ya fedha katika kikundi hicho, kinachomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima imegundua.
Tuhuma hizo zimeibuliwa katika taarifa ya ukaguzi maalumu, uliofanywa na kitengo cha ukaguzi cha CCM, kwa maagizo ya Katibu Mkuu, Yusuf Makamba, kutokana na tuhuma zilizowasilishwa kwake dhidi ya Kapteni Komba.
Ukaguzi huo, ulifanyika kuanzia Machi 3 hadi 16, mwaka huu na baadaye Aprili mosi hadi hadi 6, na taarifa yake kuwasilishwa rasmi kwa Makamba Aprili 22.
Katika taarifa hiyo ya uchunguzi ambayo Tanzania Daima ina nakala yake, Komba anadaiwa kutafuna sh milioni 30 za mishahara ya wafanyakazi wa TOT ya miezi 14.
Uchunguzi huo ambao umepata baraka za chama, unadai kuwa CCM ilitoa sh 37,442,923 kwa ajili ya kulipa malimbikizo ya mishahara ya miezi 14 kuanzia Julai 2006 hadi Agosti 2007 kwa awamu, lakini ni sh milioni sita tu, ndizo zilizolipwa kwa wafanyakazi kwa mishahara ya miezi miwili.
Ukaguzi umebaini kuwa, CCM ilitoa sh milioni 37.4 kwa ajili ya kulipa malimbikizo ya mishahara ya miezi 14 kuanzia Julai 2006 hadi Agosti kwa awamu mbili.
Malipo ya awamu ya kwanza yalifanyika 21/ 11/ 2007 kwa hati ya malipo namba 056996 ya sh 18,532,458 na tarehe 21/12/2007 kwa hati ya malipo namba 1343 sh 18,910,465, jumla ni sh 37,442,923, ilisema taarifa hiyo ya uchunguzi ambayo Tanzania Daima imeiona nakala yake.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Kapteni Komba pamoja na afisa...(anatajwa jina afisa mwingine), bado wanadaiwa malimbikizo ya sh milioni 30,514,625.
Ukaguzi uliona orodha ya majina waliyosainishwa watumishi hao wa TOT kwa miezi miwili tu jumla ya sh 6,928,298, watumishi waliulizwa na ukaguzi, walithibitisha walilipwa malimbikizo ya miezi miwili tu, ilisema taarifa hiyo.
Pia viongozi hao wa TOT, wanahusishwa na udanganyifu wa kulipa warithi wa marehemu wasio waasisi wa chama jumla ya sh 27.3 milioni, lakini baadhi ya waliotajwa kwenye orodha ya malipo, wamekana kupewa fedha zozote.
Kwa mujibu wa dokezo lililosainiwa na kiongozi mmoja wa TOT, linaonyesha jina la marehemu, jina la mrithi na kiasi cha pesa alicholipwa.
Dokezo hilo linaonyesha kuwa marehemu Godfrey Lugendo, mrithi wake Mwantumu Haji, alisaini sh milioni 4,320,000, marehemu Leyla Khatibu, mrithi wake Monica Robert, alisaini sh 6,750,000, Fred Mshana, mrithi wake Benson Mshana, alisaini sh 4,880,000, Hamimu Hemera, mrithi wake, Mwanakombo Ahamed, alisaini sh 4,240,000 na Salum Poogwe, mrithi wake Nuru Salum, alisaini sh 7,200,000 na hivyo kufanya kiasi cha fedha zote zilizolipwa kwa ajili ya warithi hao kufikia sh 27,200,000, jambo ambalo uchunguzi umebaini kwamba si la kweli.
Madai mengine anayotuhumiwa nayo Komba ni kuwapunja wafanyakazi wa TOT kwa kuwalipa posho ya sh 20,000 kwa siku wanapokuwa nje ya Dar es Salaam badala ya sh 40,000 zinazotolewa na chama.
Taarifa hiyo inasema wasanii wa TOT wanaposafiri kwa shughuli za chama, viongozi wanne hulipwa sh 40,000 kwa siku na waliobaki hulipwa sh 30,000.
Wanaokwenda CCM kuchukua fedha hizo ni ama Kapteni Komba au Gasper Tumaini (ofisa mwingine wa TOT). Fedha hizi huwa haziingii katika vitabu vya TOT, wala wasanii hawasaini hati za malipo, bali husainishwa katika karatasi na mhasibu hausiki kulipa fedha hizo, ilisema taarifa hiyo.
Mbali ya tuhuma za ubadhirifu wa fedha, Komba ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na Mbunge wa Mbinga Magharibi, anatuhumiwa kusajili gari la CCM kwa jina la asasi yake isiyo ya kiserikali inayojulikana kwa jina la Educare Girls.
Inadaiwa kuwa alisajili gari jipya la chama hicho, aina ya NISSAN Civilian, Mini Bus lililosajiliwa kwa namba TZT 8978, kwa jina lake na baadaye akaliuza gari hilo kwa sh 2,300,000, wakati limenunuliwa kwa sh 16,200,000.
Pia anakabiliwa na tuhuma za kuuza gari la chama, aina ya Mitsubishi Canter, lenye namba za usajili, TZR 6056, kinyume cha utaratibu na wakaguzi wanasema hajasema alipata kiasi gani na fedha hizo zilitumikaje.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, gari hilo lilinunuliwa kwa ajili ya kubeba wasanii na vyombo vya muziki.
Imeelezwa kuwa kabla ya uchaguzi mkuu wa 2005, CCM ilitoa magari matatu kwa Komba kwa ajili ya TOT.
Magari hayo ni Scania lenye namba za usajili T596 ABJ kwa ajili ya kuvuta tela; Isuzu Forward namba T 488 AHD na basi dogo aina ya Coaster, namba T 203 ABC.
Kutokana na tuhuma hizo, uchunguzi huo umependekeza kuwa kuanzia sasa mali zote za TOT, zisajiliwe kwa jina la CCM na Kapteni Komba na Tumaini, warejeshe fedha zote walizopata kwa kuuza magari kinyume cha taratibu na chama kiwachukulie hatua za nidhamu.
Kwa mujibu wa mapendekezo hayo, lori aina ya Scania, ambalo Kapteni Komba anadai kuwa ni lake, kitengo cha maadili na usalama, kimeagizwa kichunguze zaidi kwa kuwahoji wahusika.
Kuhusu magari ambayo kadi zake hazijulikani ziko wapi, CCM ichukue hatua za kufuatilia yalikonunuliwa na Kapteni Komba atakiwe kutoa maelezo na pia mali zote zilizoandikwa kwa jina la mmiliki Colleta Investment, zibadilishwe umiliki wake na kuwa chini ya CCM, ilisema taarifa hiyo.
Akizungumza na Tanzania Daima, Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi wa CCM, Amos Makala, alikiri kupata ripoti hiyo, lakini akasema alikuwa bado hajaipitia, kwani wakati inatoka alikuwa masomoni nje.
Alisema hata hivyo ukaguzi uliofanywa ni utaratibu wa kila mwaka unaofanywa kwenye taasisi zinazopata ruzuku ya CCM, ikiwamo TOT.
Kwa upande wake Kapteni John Komba, alisema taarifa hiyo imejaa chuki na majungu na katika kuthibitisha hilo, Komba alisema binafsi hajaipata, lakini tayari vyombo vya habari vimesambaziwa ripoti hiyo.
Hata hivyo alisema kilichopo ndani ya ripoti hiyo, bado kinahitaji majibu kutoka kwake, ambayo atayawasilisha kwenye chama mara atakapopata ripoti hiyo.
Mimi ni msafi, hakuna ufisadi hapa, hii ni chuki tu maana kama kungekuwa na ukweli, kwanini vyombo vya habari havijapewa taarifa za taasisi nyingine ambazo pia zinapata ruzuku ya chama? alihoji.
na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
MKURUGENZI wa Kikundi cha Sanaa cha Tanzania One Theatre (TOT), Kapteni John Komba, anakabiliwa na tuhuma za ubadhirifu wa mamilioni ya fedha katika kikundi hicho, kinachomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima imegundua.
Tuhuma hizo zimeibuliwa katika taarifa ya ukaguzi maalumu, uliofanywa na kitengo cha ukaguzi cha CCM, kwa maagizo ya Katibu Mkuu, Yusuf Makamba, kutokana na tuhuma zilizowasilishwa kwake dhidi ya Kapteni Komba.
Ukaguzi huo, ulifanyika kuanzia Machi 3 hadi 16, mwaka huu na baadaye Aprili mosi hadi hadi 6, na taarifa yake kuwasilishwa rasmi kwa Makamba Aprili 22.
Katika taarifa hiyo ya uchunguzi ambayo Tanzania Daima ina nakala yake, Komba anadaiwa kutafuna sh milioni 30 za mishahara ya wafanyakazi wa TOT ya miezi 14.
Uchunguzi huo ambao umepata baraka za chama, unadai kuwa CCM ilitoa sh 37,442,923 kwa ajili ya kulipa malimbikizo ya mishahara ya miezi 14 kuanzia Julai 2006 hadi Agosti 2007 kwa awamu, lakini ni sh milioni sita tu, ndizo zilizolipwa kwa wafanyakazi kwa mishahara ya miezi miwili.
Ukaguzi umebaini kuwa, CCM ilitoa sh milioni 37.4 kwa ajili ya kulipa malimbikizo ya mishahara ya miezi 14 kuanzia Julai 2006 hadi Agosti kwa awamu mbili.
Malipo ya awamu ya kwanza yalifanyika 21/ 11/ 2007 kwa hati ya malipo namba 056996 ya sh 18,532,458 na tarehe 21/12/2007 kwa hati ya malipo namba 1343 sh 18,910,465, jumla ni sh 37,442,923, ilisema taarifa hiyo ya uchunguzi ambayo Tanzania Daima imeiona nakala yake.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Kapteni Komba pamoja na afisa...(anatajwa jina afisa mwingine), bado wanadaiwa malimbikizo ya sh milioni 30,514,625.
Ukaguzi uliona orodha ya majina waliyosainishwa watumishi hao wa TOT kwa miezi miwili tu jumla ya sh 6,928,298, watumishi waliulizwa na ukaguzi, walithibitisha walilipwa malimbikizo ya miezi miwili tu, ilisema taarifa hiyo.
Pia viongozi hao wa TOT, wanahusishwa na udanganyifu wa kulipa warithi wa marehemu wasio waasisi wa chama jumla ya sh 27.3 milioni, lakini baadhi ya waliotajwa kwenye orodha ya malipo, wamekana kupewa fedha zozote.
Kwa mujibu wa dokezo lililosainiwa na kiongozi mmoja wa TOT, linaonyesha jina la marehemu, jina la mrithi na kiasi cha pesa alicholipwa.
Dokezo hilo linaonyesha kuwa marehemu Godfrey Lugendo, mrithi wake Mwantumu Haji, alisaini sh milioni 4,320,000, marehemu Leyla Khatibu, mrithi wake Monica Robert, alisaini sh 6,750,000, Fred Mshana, mrithi wake Benson Mshana, alisaini sh 4,880,000, Hamimu Hemera, mrithi wake, Mwanakombo Ahamed, alisaini sh 4,240,000 na Salum Poogwe, mrithi wake Nuru Salum, alisaini sh 7,200,000 na hivyo kufanya kiasi cha fedha zote zilizolipwa kwa ajili ya warithi hao kufikia sh 27,200,000, jambo ambalo uchunguzi umebaini kwamba si la kweli.
Madai mengine anayotuhumiwa nayo Komba ni kuwapunja wafanyakazi wa TOT kwa kuwalipa posho ya sh 20,000 kwa siku wanapokuwa nje ya Dar es Salaam badala ya sh 40,000 zinazotolewa na chama.
Taarifa hiyo inasema wasanii wa TOT wanaposafiri kwa shughuli za chama, viongozi wanne hulipwa sh 40,000 kwa siku na waliobaki hulipwa sh 30,000.
Wanaokwenda CCM kuchukua fedha hizo ni ama Kapteni Komba au Gasper Tumaini (ofisa mwingine wa TOT). Fedha hizi huwa haziingii katika vitabu vya TOT, wala wasanii hawasaini hati za malipo, bali husainishwa katika karatasi na mhasibu hausiki kulipa fedha hizo, ilisema taarifa hiyo.
Mbali ya tuhuma za ubadhirifu wa fedha, Komba ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na Mbunge wa Mbinga Magharibi, anatuhumiwa kusajili gari la CCM kwa jina la asasi yake isiyo ya kiserikali inayojulikana kwa jina la Educare Girls.
Inadaiwa kuwa alisajili gari jipya la chama hicho, aina ya NISSAN Civilian, Mini Bus lililosajiliwa kwa namba TZT 8978, kwa jina lake na baadaye akaliuza gari hilo kwa sh 2,300,000, wakati limenunuliwa kwa sh 16,200,000.
Pia anakabiliwa na tuhuma za kuuza gari la chama, aina ya Mitsubishi Canter, lenye namba za usajili, TZR 6056, kinyume cha utaratibu na wakaguzi wanasema hajasema alipata kiasi gani na fedha hizo zilitumikaje.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, gari hilo lilinunuliwa kwa ajili ya kubeba wasanii na vyombo vya muziki.
Imeelezwa kuwa kabla ya uchaguzi mkuu wa 2005, CCM ilitoa magari matatu kwa Komba kwa ajili ya TOT.
Magari hayo ni Scania lenye namba za usajili T596 ABJ kwa ajili ya kuvuta tela; Isuzu Forward namba T 488 AHD na basi dogo aina ya Coaster, namba T 203 ABC.
Kutokana na tuhuma hizo, uchunguzi huo umependekeza kuwa kuanzia sasa mali zote za TOT, zisajiliwe kwa jina la CCM na Kapteni Komba na Tumaini, warejeshe fedha zote walizopata kwa kuuza magari kinyume cha taratibu na chama kiwachukulie hatua za nidhamu.
Kwa mujibu wa mapendekezo hayo, lori aina ya Scania, ambalo Kapteni Komba anadai kuwa ni lake, kitengo cha maadili na usalama, kimeagizwa kichunguze zaidi kwa kuwahoji wahusika.
Kuhusu magari ambayo kadi zake hazijulikani ziko wapi, CCM ichukue hatua za kufuatilia yalikonunuliwa na Kapteni Komba atakiwe kutoa maelezo na pia mali zote zilizoandikwa kwa jina la mmiliki Colleta Investment, zibadilishwe umiliki wake na kuwa chini ya CCM, ilisema taarifa hiyo.
Akizungumza na Tanzania Daima, Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi wa CCM, Amos Makala, alikiri kupata ripoti hiyo, lakini akasema alikuwa bado hajaipitia, kwani wakati inatoka alikuwa masomoni nje.
Alisema hata hivyo ukaguzi uliofanywa ni utaratibu wa kila mwaka unaofanywa kwenye taasisi zinazopata ruzuku ya CCM, ikiwamo TOT.
Kwa upande wake Kapteni John Komba, alisema taarifa hiyo imejaa chuki na majungu na katika kuthibitisha hilo, Komba alisema binafsi hajaipata, lakini tayari vyombo vya habari vimesambaziwa ripoti hiyo.
Hata hivyo alisema kilichopo ndani ya ripoti hiyo, bado kinahitaji majibu kutoka kwake, ambayo atayawasilisha kwenye chama mara atakapopata ripoti hiyo.
Mimi ni msafi, hakuna ufisadi hapa, hii ni chuki tu maana kama kungekuwa na ukweli, kwanini vyombo vya habari havijapewa taarifa za taasisi nyingine ambazo pia zinapata ruzuku ya chama? alihoji.