WAKATI hatima ya kumpata mgombea urais wa Zanzibar kupitia CCM inaelekea ukingoni mwishoni mwa wiki hii, makundi ya ushabiki yanahaha kuwapigia debe wagombea watatu ambao ni Dk Ali Mohamed Shein, Dk Ghalib Bilal na Shamsi Vuai Nahodha.
Jana rais mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk Salmin Amour (Komando) aliwasili mjini Dodoma akiwa katika ndege moja na Waziri wa Kiongozi Vuai Nahodha ambaye ni mmoja wa wagombea.
Kwa muda mrefu sasa Dk Salmin haudhurii mikutana na vikao vya chama kutokana na kusumbuliwa na macho, hali inayoonyesha kuwa hatua ya sasa ya kumpata mgombea urais wa Zanzibar kupitia CCM ina unyeti wake.
Makundi hayo yameunda ushindani mkubwa miongoni mwa wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM itakayofanyika kesho, mjini Dodoma.
Kwa mujibu wa taarifa tulizozipata kutoka Dodoma wakati wajumbe na wagombea wanaendelea kuwasili, kuna mchuano mkali miongoni mwa makundi ya wapambe wao.
Fununu zaidi kutoka muongoni mwa wajumbe wa CCM zinasema kuna utofuati kati ya wajumbe wa Zanzibar na wa Bara kuhusu uungwaji mkono wa wagombea hao.
Uchunguzi umebaini kwamba, wafuasi wa vigogo hao wamekuwa wakitambiana na kuelekeza kampeni kwa wajumbe wa Halmashauri ya CCM (Nec), ambao ndio watakaopiga kura kumchagua mtu mmoja atakayeshindana na wapinzani katika kinyang'anyiro hicho.
Taarifa zinaeleza kuwa ingawa Dk Bilal anatajwa kuwa mshindani mkubwa katika kinyang'anyiro hicho, nafasi yake kuingia tatu bora ina utata kutoka na tuhuma za wafuasi wake kuendeleza kutoa lugha isiyonzuri.
Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba amedokeza kuwa katika uteuzi huo chama hakitafanya makosa kwa kumteua mtu ambaye watu watamguna na kugoma kumchagua.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jioni, Makamba alisema Kamati Kuu ya CCM itakutana kesho sambamba na Halmashauri Kuu ambayo itaanza kikao mara baada ya kumaliza kamati ili kuzuia kuvuja kwa maamuzi yaliyofikiwa.
Akizungumza katika mahojiano maalum na TBC1 juzi, Makamba alisema mgombea urais wa Zanzibar atapatikana kwa sifa zake na jinsi atakavyojieleza mwenyewe mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC).
Hapa hakuna cha mgombea kupita kwa kupigiwa debe wala nini, CCM haiwezi kufanya makosa katika hili kwa kuwa tukimpitisha asiyefaa, watu wataguna na wakiguna ina maana tutashindwa katika uchaguzi; hivyo mgombea atapatikana kupitia sifa tulizozianisha na atakavyojieleza,alisema Makamba.
Hata hivyo wakati Makamba akitoa kauli hiyo juzi asubuhi, wasomi na wachambuzi wa masuala ya siasa walisema kulingana na mfumo wa utawala uliopo nchini, rais hawezi kutoka nje ya Baraza la Mawaziri.
Wasomi hao waliwatabiria kwamba, Dk Shein, Vuai na Bilal kuwa ndio wenye nafasi kubwa ya kuteuliwa na Kamati Kuu.
Hata hivyo, walionya kuwa kulingana na siasa za visiwa vya Zanzibar, anahitajika kiongozi imara atakayeweza kuimarisha mshikamano baina ya Wazanzibari.
Mhadhiri Msaidizi wa Kitivo cha Siasa ya Sayansi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally alisema CCM inakabiliwa na changamoto kubwa na kwamba kati ya waliojitokeza kutaka kuteuliwa wapo ambao hawaaminiki kutokana na rekodi na misimamo yao katika uongozi.
Lakini katika kinyanganyiro hiki natoa nafasi kwa Dk Shein, Vuai na Dk Bilal, alisema Ally.
Profesa Mwesiga Baregu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augostine alisema Zanzibar wamezoea michuano mikali ya kisiasa na kwamba, si mara ya kwanza kujitokeza wagombea wengi katika nafasi hiyo.
Mtu ambaye hakuhusika katika mitafaruku hiyo ni Dk Shein na inaonekana ataweza kuwaunganisha Wazanzibari na hata maamuzi ya kumteua yanaweza yasiwagawe Wazanzibari, alisema Profesa Baregu na kuongeza:
Pia Dk Shein hayuko kwenye kambi ya akina Karume wala Dk Salmini, au CCM Asilia na CCM Mtandao, hivyo haya ni mambo yatakayomfanya achaguliwe, alisema Profesa Baregu.
Mhadhiri wa Sheria wa UDSM, Dk Sengondo Mvungi alisema idadi kubwa ya wanaowania urais wa Zanzibar imeonyesha kiwango cha juu cha uelewa wao wa katiba ya nchi na haki zao.
Mwenyekiti mwenza wa Mpango wa Utafiti wa Elimu ya Demokrasia (Redet), Dk Benson Bana alisema: Kwanza tuwapongeze tu wametambua haki yao na wameonyesha ukomavu wa demokrasia.
Wanachama 11 waliojitokeza kuwania urais kumrithi Amani Abeid Karume ambaye amemaliza muda wake ni Nahodha, Ali Juma Shamhuna, Dk Shein, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa Zanzibar, Haroun Ali Suleiman, Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mohamed Aboud na Dk Gharib Bilal.
Wengine ni balozi wa Tanzania nchini Italia, Ali Karume, Hamad Bakari Mshindo, Omar Sheha Mussa, Mohamed Yusuf Mshamba na Mohamed Raza Dharamsi.
Wachambuzi wengine wa siasa wanasema sio rahisi kwa Haroun na Shamsi kuingia wote katika tatu bora kwa vile wanatoka katika jimbo moja la Makunduchi.
Ali Karume ambaye ni mdogo wa Rais Amani Karume amekuwa akitamba kwamba, kutokana na elimu yake na uzoefu katika siasa, ana nafasi kubwa ya kuteuliwa na chama chake kama vigezo vilivyowekwa na vitafuatwa.
Mohammed Aboud ambaye katika kikao cha kamati maalumu kilichofanyika Zanzibar wiki iliyopita kilimjadili na baadhi ya wajumbe kutoa tuhuma za kughushi vyeti, amekuwa akijitetea kuwa madai hayo hayana msingi na kuwa yuko tayari kutoa ufafanuzi mbele ya vikao vya juu vya chama vyenye maamuzi ya mwisho.
Mohammed Raza amelalamikia kutoalikwa katika kikao cha CC kinachofanyika kesho na kudai kwamba kutoonekana kwake Dodoma hakumaanishi kujitoa katika kinyanganyiro hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti wa CCM nilikwenda katika ofisi zetu za chama kutaka ufafanuzi nikaelezwa niende katika ofisi ya masjala ili kupata utaratibu zaidi kuhusu kwenda katika kikao cha NEC Dodoma," anasema Raza katika barua yake kwa Rais Kikwete.
Dk Salmin akilitua mjini Dodoma saa 8:10 kwa ndege ya Shrika la Ndege la Precision akiwa ameongzana na mgombea wa Urais, Nahodha pamoja na Asha Abdalah Juma ambaye ni Waziri na Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala bora, Ramadhani Abdalah, baadhi ya wabunge na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.
Komandoo Salmin, alikuwa wa kwanza kushuka na kufuatiwa na Nahodha na viongozi mbali mbali wa serikali na CCM walifika kuwalaki.
Mgombea mwingine wa Urais wa Zanzibar, Dk Shein aliwasili jana majira ya saa tano asubuhi akifuatiwa na mgombea mwingine, Mohamed Aboud ambaye ni Naibu Waziri wa Afrika ya Mashariki.
Hata hivyo hadi jana mchana ilikuwa haijafahamika kama Bilal amefika Dodoma ingawa wapiga kampeni wake wameuteka mji wa Dodoma.
Wakati viongozi hao wakitua, makundi ya wapiga kampeni wa Urais wa Zanzibar kutoka maskani mbali mbali, wamewasili mjini hapa tangu juzi usiku na jana walikuwa wametanda ofisi za CCM na kwenye nyumba za kulala wageni.
Wengi wa makada hao wa CCM kutoka Zanzibar walikuwa ni Gharib Bilal toka maskani za mikoa mitano Zanzibar wakiongozwa na wajumbe wa maskani kubwa ya Kisonge, ambao walionya kuwa kamwe hawatakubali kusikia vikao vya juu ya CCM vimemwengua.
Kada maarufu wa CCM Zanzibar na mmoja wa waasisi ya jumuiya ya vijana wa Afro-Shiraz, Baraka Mohamed Shamte, alisema chaguo la Wazanzibar wote ni Bilal na kama CCM Bara ikilazimisha kumleta mwingine kitakachotokea watajuta.
Shamte alikuwa Katibu wa CCM katika wilaya mbali mbali, ikiwepo Wete Pemba, Unguja Mjini na Pangani mkoani Tanga, kabla ya kurejea Zanzibar.
Tangu mwaka 2000 chaguo la Wazanzibari ni Bilal na hadi sasa na kama wanataka CCM iendelee kuwepo Zanzibar waturejeshee Bilal kuwa mgombea wa Urais,alisema Shamte.
Wajumbe wengine, Ally Mzee na Mohamed Issa Ramadhani ambao walisema wanajua CCM bara wanamtaka Makamu wa Rais, Dk Shein, lakini wajuwe Zanzibar wanamtaka Bilal au Nahodha.
Kada Mwingine wa CCM toka Zanzibar, Jamal Ramadhani ambaye alikuwa anaongoza ujumbe wa watu 200 toka Zanzibar alisema, CCM isifanye mzaha katika suala la uteuzi wa mgombea wa Urais Zanzibar.
Katibu wa Uenezi na Itikadi wa CCM Zanzibar, Vual Alli Vuai alimweleza mwandishi wa habari hizi mara baada ya kufika jana kuwa kamati maalum iliyopitia majina ya wagombea Zanzibar imemaliza kazi yake sasa imebaki kazi ya CC na Halmashauri Kuu.
Habari hii imeandaliwa na Salma Said, Zanzibar, Mussa Juma, Dodoma,
Sadick Mtulya na Salim Said, Dar
Source: Mwananchi.
Kazi ipo kesho
Jana rais mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk Salmin Amour (Komando) aliwasili mjini Dodoma akiwa katika ndege moja na Waziri wa Kiongozi Vuai Nahodha ambaye ni mmoja wa wagombea.
Kwa muda mrefu sasa Dk Salmin haudhurii mikutana na vikao vya chama kutokana na kusumbuliwa na macho, hali inayoonyesha kuwa hatua ya sasa ya kumpata mgombea urais wa Zanzibar kupitia CCM ina unyeti wake.
Makundi hayo yameunda ushindani mkubwa miongoni mwa wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM itakayofanyika kesho, mjini Dodoma.
Kwa mujibu wa taarifa tulizozipata kutoka Dodoma wakati wajumbe na wagombea wanaendelea kuwasili, kuna mchuano mkali miongoni mwa makundi ya wapambe wao.
Fununu zaidi kutoka muongoni mwa wajumbe wa CCM zinasema kuna utofuati kati ya wajumbe wa Zanzibar na wa Bara kuhusu uungwaji mkono wa wagombea hao.
Uchunguzi umebaini kwamba, wafuasi wa vigogo hao wamekuwa wakitambiana na kuelekeza kampeni kwa wajumbe wa Halmashauri ya CCM (Nec), ambao ndio watakaopiga kura kumchagua mtu mmoja atakayeshindana na wapinzani katika kinyang'anyiro hicho.
Taarifa zinaeleza kuwa ingawa Dk Bilal anatajwa kuwa mshindani mkubwa katika kinyang'anyiro hicho, nafasi yake kuingia tatu bora ina utata kutoka na tuhuma za wafuasi wake kuendeleza kutoa lugha isiyonzuri.
Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba amedokeza kuwa katika uteuzi huo chama hakitafanya makosa kwa kumteua mtu ambaye watu watamguna na kugoma kumchagua.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jioni, Makamba alisema Kamati Kuu ya CCM itakutana kesho sambamba na Halmashauri Kuu ambayo itaanza kikao mara baada ya kumaliza kamati ili kuzuia kuvuja kwa maamuzi yaliyofikiwa.
Akizungumza katika mahojiano maalum na TBC1 juzi, Makamba alisema mgombea urais wa Zanzibar atapatikana kwa sifa zake na jinsi atakavyojieleza mwenyewe mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC).
Hapa hakuna cha mgombea kupita kwa kupigiwa debe wala nini, CCM haiwezi kufanya makosa katika hili kwa kuwa tukimpitisha asiyefaa, watu wataguna na wakiguna ina maana tutashindwa katika uchaguzi; hivyo mgombea atapatikana kupitia sifa tulizozianisha na atakavyojieleza,alisema Makamba.
Hata hivyo wakati Makamba akitoa kauli hiyo juzi asubuhi, wasomi na wachambuzi wa masuala ya siasa walisema kulingana na mfumo wa utawala uliopo nchini, rais hawezi kutoka nje ya Baraza la Mawaziri.
Wasomi hao waliwatabiria kwamba, Dk Shein, Vuai na Bilal kuwa ndio wenye nafasi kubwa ya kuteuliwa na Kamati Kuu.
Hata hivyo, walionya kuwa kulingana na siasa za visiwa vya Zanzibar, anahitajika kiongozi imara atakayeweza kuimarisha mshikamano baina ya Wazanzibari.
Mhadhiri Msaidizi wa Kitivo cha Siasa ya Sayansi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally alisema CCM inakabiliwa na changamoto kubwa na kwamba kati ya waliojitokeza kutaka kuteuliwa wapo ambao hawaaminiki kutokana na rekodi na misimamo yao katika uongozi.
Lakini katika kinyanganyiro hiki natoa nafasi kwa Dk Shein, Vuai na Dk Bilal, alisema Ally.
Profesa Mwesiga Baregu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augostine alisema Zanzibar wamezoea michuano mikali ya kisiasa na kwamba, si mara ya kwanza kujitokeza wagombea wengi katika nafasi hiyo.
Mtu ambaye hakuhusika katika mitafaruku hiyo ni Dk Shein na inaonekana ataweza kuwaunganisha Wazanzibari na hata maamuzi ya kumteua yanaweza yasiwagawe Wazanzibari, alisema Profesa Baregu na kuongeza:
Pia Dk Shein hayuko kwenye kambi ya akina Karume wala Dk Salmini, au CCM Asilia na CCM Mtandao, hivyo haya ni mambo yatakayomfanya achaguliwe, alisema Profesa Baregu.
Mhadhiri wa Sheria wa UDSM, Dk Sengondo Mvungi alisema idadi kubwa ya wanaowania urais wa Zanzibar imeonyesha kiwango cha juu cha uelewa wao wa katiba ya nchi na haki zao.
Mwenyekiti mwenza wa Mpango wa Utafiti wa Elimu ya Demokrasia (Redet), Dk Benson Bana alisema: Kwanza tuwapongeze tu wametambua haki yao na wameonyesha ukomavu wa demokrasia.
Wanachama 11 waliojitokeza kuwania urais kumrithi Amani Abeid Karume ambaye amemaliza muda wake ni Nahodha, Ali Juma Shamhuna, Dk Shein, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa Zanzibar, Haroun Ali Suleiman, Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mohamed Aboud na Dk Gharib Bilal.
Wengine ni balozi wa Tanzania nchini Italia, Ali Karume, Hamad Bakari Mshindo, Omar Sheha Mussa, Mohamed Yusuf Mshamba na Mohamed Raza Dharamsi.
Wachambuzi wengine wa siasa wanasema sio rahisi kwa Haroun na Shamsi kuingia wote katika tatu bora kwa vile wanatoka katika jimbo moja la Makunduchi.
Ali Karume ambaye ni mdogo wa Rais Amani Karume amekuwa akitamba kwamba, kutokana na elimu yake na uzoefu katika siasa, ana nafasi kubwa ya kuteuliwa na chama chake kama vigezo vilivyowekwa na vitafuatwa.
Mohammed Aboud ambaye katika kikao cha kamati maalumu kilichofanyika Zanzibar wiki iliyopita kilimjadili na baadhi ya wajumbe kutoa tuhuma za kughushi vyeti, amekuwa akijitetea kuwa madai hayo hayana msingi na kuwa yuko tayari kutoa ufafanuzi mbele ya vikao vya juu vya chama vyenye maamuzi ya mwisho.
Mohammed Raza amelalamikia kutoalikwa katika kikao cha CC kinachofanyika kesho na kudai kwamba kutoonekana kwake Dodoma hakumaanishi kujitoa katika kinyanganyiro hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti wa CCM nilikwenda katika ofisi zetu za chama kutaka ufafanuzi nikaelezwa niende katika ofisi ya masjala ili kupata utaratibu zaidi kuhusu kwenda katika kikao cha NEC Dodoma," anasema Raza katika barua yake kwa Rais Kikwete.
Dk Salmin akilitua mjini Dodoma saa 8:10 kwa ndege ya Shrika la Ndege la Precision akiwa ameongzana na mgombea wa Urais, Nahodha pamoja na Asha Abdalah Juma ambaye ni Waziri na Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utawala bora, Ramadhani Abdalah, baadhi ya wabunge na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.
Komandoo Salmin, alikuwa wa kwanza kushuka na kufuatiwa na Nahodha na viongozi mbali mbali wa serikali na CCM walifika kuwalaki.
Mgombea mwingine wa Urais wa Zanzibar, Dk Shein aliwasili jana majira ya saa tano asubuhi akifuatiwa na mgombea mwingine, Mohamed Aboud ambaye ni Naibu Waziri wa Afrika ya Mashariki.
Hata hivyo hadi jana mchana ilikuwa haijafahamika kama Bilal amefika Dodoma ingawa wapiga kampeni wake wameuteka mji wa Dodoma.
Wakati viongozi hao wakitua, makundi ya wapiga kampeni wa Urais wa Zanzibar kutoka maskani mbali mbali, wamewasili mjini hapa tangu juzi usiku na jana walikuwa wametanda ofisi za CCM na kwenye nyumba za kulala wageni.
Wengi wa makada hao wa CCM kutoka Zanzibar walikuwa ni Gharib Bilal toka maskani za mikoa mitano Zanzibar wakiongozwa na wajumbe wa maskani kubwa ya Kisonge, ambao walionya kuwa kamwe hawatakubali kusikia vikao vya juu ya CCM vimemwengua.
Kada maarufu wa CCM Zanzibar na mmoja wa waasisi ya jumuiya ya vijana wa Afro-Shiraz, Baraka Mohamed Shamte, alisema chaguo la Wazanzibar wote ni Bilal na kama CCM Bara ikilazimisha kumleta mwingine kitakachotokea watajuta.
Shamte alikuwa Katibu wa CCM katika wilaya mbali mbali, ikiwepo Wete Pemba, Unguja Mjini na Pangani mkoani Tanga, kabla ya kurejea Zanzibar.
Tangu mwaka 2000 chaguo la Wazanzibari ni Bilal na hadi sasa na kama wanataka CCM iendelee kuwepo Zanzibar waturejeshee Bilal kuwa mgombea wa Urais,alisema Shamte.
Wajumbe wengine, Ally Mzee na Mohamed Issa Ramadhani ambao walisema wanajua CCM bara wanamtaka Makamu wa Rais, Dk Shein, lakini wajuwe Zanzibar wanamtaka Bilal au Nahodha.
Kada Mwingine wa CCM toka Zanzibar, Jamal Ramadhani ambaye alikuwa anaongoza ujumbe wa watu 200 toka Zanzibar alisema, CCM isifanye mzaha katika suala la uteuzi wa mgombea wa Urais Zanzibar.
Katibu wa Uenezi na Itikadi wa CCM Zanzibar, Vual Alli Vuai alimweleza mwandishi wa habari hizi mara baada ya kufika jana kuwa kamati maalum iliyopitia majina ya wagombea Zanzibar imemaliza kazi yake sasa imebaki kazi ya CC na Halmashauri Kuu.
Habari hii imeandaliwa na Salma Said, Zanzibar, Mussa Juma, Dodoma,
Sadick Mtulya na Salim Said, Dar
Source: Mwananchi.
Kazi ipo kesho