Kodi za gari barabarani lisipoingiliwa vizuri linaweza kuwa janga kwa watu wengi

Mkata Mtaa

Senior Member
Jun 10, 2016
136
141
Hii sheria ya TRA kwamba kama uliuza gari lakini aliyenunua akubadilisha umiliki kodi utadaiwa wewe kwa nini gari yenyewe isijisimamie yenyewe, kama hailipiwi kodi ikamatwe gari husika maana kila gari inajitegemea kwa usajiri wake.

gari kama iko geraji kutokana na mtu kukosa pesa ya kutengeneza au kutokuwepo vipuri vyake, kwa nini wasisubiri siku ikiingia barabarani ikamatwe.

Mwisho kuna gari zimepata ajali ambazo gari hazitengenezeki kabisa, watu wakauza kama chuma chakavu na ripoti za polisi wakatupa maana walijua mwisho wa gari umefika, mfano kuna mabasi na malori, malori mengine yamepata ajali nje ya nchi kama Congo au Zambia wakakata kama chuma chakavu watalipaje hizo faini kubwa hivyo, maana wengine wameshapoteza malori na mabasi mengi aliyopata ajali.

TRA yenyewe ilikuwa haitoi elimu vizuri kuhusu kodi za gari,
Ili kunusuru watu kwenye hili janga ni bora kuwaambia watu wote wenye gari gereji ambazo hazitengeneki na waliyokata kama chuma chakavu waripoti TRA ili zifutwe baada ya hapo ndio sheria ianza kutumika ipasavyo, la sivyo wananchi wengi wataingia kwenye matatizo makubwa maana wengine hiyo pesa hawana tena na hawakufanya kwa maksudi.

Nawasilisha.
 
Hii kitu hatari mimi leo imenitokea hapa kichwa kina moto kinoma tena jamaa wanakuja mpaka kitaa hapo ukilipa za TRA bado za yono nchi imekuwa mgumu kuishi kwakweli
 
Nchi hii haina wataalamu wa kutoa ushauri,kila jambo ni kukurupuka tu.
Kila siku kupanga foleni mara kuhakiki VAT,mara VITAMBULISHO,mara BVR,mara VYETI,mara LESENI za udereva,
Hivi watanzania watafanya kazi saa ngapi au siku gani,hivi inashindikana kuweka utaratibu mzuri usiolazimisha foleni au wote kwa pamoja?
Hili jambo la malipo ya Roadlicence,kwanini hawatoi elimu angalau kufikia Desemba,ili waanze januari kwa magari yaliyo barabarani sasa hivi.
Unadai gari ambayo mmiliki alikufa na mimi nilinunua moja kati magari yake unanipa mimi adhabu ya kujua kwanini yeye hakulipa na siyo kwa gari ninayotumia mimi,dah kodi za hivi si za kuwasaidia masikini bali kuwakandamiza.
 
Vitu kama hivi ndo tulitegemea wabunge wetu watuwakilishe huko bungeni,lakini badala yake baadhi yao wanaona muhimu ni kuonekanana "live" kwenye luninga.kwa hili TRA wanatuburuza.
 
Mimi nakuunga mkono kwa kauli yako, ikiwa kama Raia watafanyiwa kitu hicho na basi wafanya kazi wote wa TRA nao wafukuzwe na washtakiwe kwasababu wao ndio chanzo cha serikali kukosa mapato Kutokana na raia kutolipa motor vehicle, ukisajili gari lazima uache taarifa zako zote kamili ikiwamo namba ya simu na anuani yako, kwanini mwisho wa mwaka wasikuletee bili mpaka ipite miaka na miaka, huo ni uzembe wao, tunatakiwa tuanzie hapa sio huko walipo vurunda wao, wataka kumwambia Rais wanafanya kazi nzuri ya kukusanya kodi kumbe ni waongo, hilo watanzania tunatakiwa tusilikubali, eti nasikia kuna watu sasa hivi ndio wanatumiwa msg wanadaiwa mapato na serikali kwa kutolipia magari yao miaka ya nyuma wakati magari yenyewe yalisha kufa muda mrefu. Wanataka kutuibia kinguvu.
 
Hii sheria ya TRA kwamba kama uliuza gari lakini aliyenunua akubadilisha umiliki kodi utadaiwa wewe kwa nini gari yenyewe isijisimamie yenyewe, kama hailipiwi kodi ikamatwe gari husika maana kila gari inajitegemea kwa usajiri wake.

gari kama iko geraji kutokana na mtu kukosa pesa ya kutengeneza au kutokuwepo vipuri vyake, kwa nini wasisubiri siku ikiingia barabarani ikamatwe.

Mwisho kuna gari zimepata ajali ambazo gari hazitengenezeki kabisa, watu wakauza kama chuma chakavu na ripoti za polisi wakatupa maana walijua mwisho wa gari umefika, mfano kuna mabasi na malori, malori mengine yamepata ajali nje ya nchi kama Congo au Zambia wakakata kama chuma chakavu watalipaje hizo faini kubwa hivyo, maana wengine wameshapoteza malori na mabasi mengi aliyopata ajali.

TRA yenyewe ilikuwa haitoi elimu vizuri kuhusu kodi za gari,
Ili kunusuru watu kwenye hili janga ni bora kuwaambia watu wote wenye gari gereji ambazo hazitengeneki na waliyokata kama chuma chakavu waripoti TRA ili zifutwe baada ya hapo ndio sheria ianza kutumika ipasavyo, la sivyo wananchi wengi wataingia kwenye matatizo makubwa maana wengine hiyo pesa hawana tena na hawakufanya kwa maksudi.

Nawasilisha.
Hizi ni dalili za Nchi kufirisika kwa hiyo inatafuta hela kwa nguvu,unallipiaje barabara ambayo huitumii.
 
Tatizo ninalioliona ni kuwa TRA hawatoi elimu kwa wahusika. Yan mambo yamekuwa ni kuviziana. Kwani wanashindwa nini kutoa elimu elekezi kuhusu hilo. Watuambie ni sehemu gani imeandikwa gari ukiuza au ikiharibika tukatoe taarifa kwao.mbona hayakusemwa kipindi chote hicho mpaka leo umeingia uongozi mpya ndio tuishi kwa kuchimbua hizo wanazosema sheria ingawa sijui zipo kwenye kitabu gani.
 
Kwa logic ndogo tu maana yake watu itabd waanze kununua used cars from Japan /German /UK etc hizi za kibongo za mkononi hatari Sana, Outcomes yake itakua ni nini?Watu wakiagize magari Nje Bandari itaanza kupiga kazi vzr lkn only and only if kama watu watakua na uwezo wa kununua magari toka nje. La sivyo gari inaenda kua mzigo na soon haice & public transport zitapata mafuriko
 
Issue ya road licences ni pasua kichwa sana,njia pekee nayo washauri watu jambo la kwanza I) kabla hujanunua gari kwa mtu hakikisha plate number yake umeiverify kwenye simu yake..kuna ile code ya maxi malipo 15341 unaiicheck tu kwa simu yako kwa kuingiza namba za gari husika kujiridhisha kama inadaiwa au la usiishie kuamini sticker ambazo zinabandikwa kwenye vioo maana wabongo tumekuwa wasanii utabandikiwa sticker fake bure kumbe gari haijalipiwa motor vehicles wala insurance.

2)inatokea umemuuzia mtu gari tumia njia ambayo me niliwahii ifanya,Kuna mtu nilimuuzia gari akawa alikuwa hana TIN namba nilichokifanya nilimpa black and blue kuwa nakupa mwezi mmoja ubadirishe jina la mmiliki na unijulishe baada ya kupata tin namba yako vinginevyo baada ya mwezi me nitareport gari yangu imeibiwa na ukikamatwa nayo itakula kwako kwakuwa gari bado itakuwa inasoma jina la mmiliki WA kwanza.Jamaa fasta akapata Tin na akabadili jina na nakala akanipa.

3) naishauri TRA code ya magari wangeingiza hata kama ni shilingi hamsini katika kila lita moja ya mafuta unayonunua hii ikiwa na maana kuwa utalipa motor vehicle kutokana na utumiaji WA gari lako,ukiwa busy kama daladala au mabasi ya mikoani motor vehicle yako itakuwa kubwa kuliko mtu anaetumia gari kwenda nalo kazini na kurudi.

Faida ya jambo hili ni kuwa serikali itapata mapato mengi kuliko hivi sasa pia hautakuwa mzigo hata kwa raia maana atakuwa anakatwa kodi bila kupata Yale maumivu ya kudunduliza pesa mwisho WA mwaka,faida nyingine foleni zitapungua mijini maana watu hatutatumia magari pasipokuwa na sababu maalumu.
 
Jambo la muhimu ni serikali kubadili mfumo huu uchwara wa kukimbizana na Road License kwa kuwalipisha watu ambao magari yao yamepaki nyumbani au gereji.
Mtu hatumii barabara halafu analipa ushuru wa barabara.

Kuna wazo zuri sana la kuiweka Road license kwenye mafuta.
Ili mtu alipie kwa kadiri anavyotumia barabara.

Lakini pia kila mtu anapouza gari anakua na formu ya mauziano.
Huwezi kuuza au kununua gari kama karanga bila mkataba wa mauziano.
Hivyo serikali haina nia ya kumuumiza mtu yeyote kwa hili la Road License. Hapa kila mtu aliyenunua gari kihalali atalipa R. L kwa kipindi alichotumia gari.
Tatizo linakuwa kwa wale waliopark magari yao bila kutoa taarifa.Hapa serikali itoe ufafanuzi kamili.
 
1. Elimu kwa mlipa kodi ilitakiwa kutolewa kwanza kabla ya kuanza kwa hili zoezi.

2. TRA wanalazimisha kufikia malengo ya makusanyo ilhali hali ya uchumi wa nchi ni mbaya ndio maana wanakuja na hivi vituko.
 
Umenikumbusha machungu! Ilikamatwa gari yangu na nikaambiwa nadaiwa, nilipokwenda Tra na kuwaambia sidaiwi kwa kuonyesha nakala zangu ila wakasema unadaiwa gari ya zamani na hujailipia tangu elfu mbili na kumi.
Hiyo ni gari niliyomuuzia mtu tangu mwaka huo na hata alipo sijui, ilibidi tu nilipe hizo milioni tatu ili niikomboe gari hii.
 
Back
Top Bottom