Mjomba wa taifa
JF-Expert Member
- Apr 20, 2012
- 231
- 161
Uvumilivu huu haupo duniani kote isipokuwa unapatikana katika nchi ya maziwa na asali Tanzania. Wananchi wamekuwa wakilipa kodi kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali kwa ustawi wa taifa. Inashangaza kuona kuwa Television ya Taifa imekuwa ikijiendesha kwa pesa za watanzania wote pasipo kujali itikadi lakini imekuwa inashangaza kwa kuonesha mambo mbalimbali ya CCM tu na si vyama vingine vya siasa hasa jembe letu CHADEMA.
mfano mzuri ni TBC ilipoamua kusitisha kurusha live kampeni za CHADEMA mwaka 2010 pale Jangwani ilipotokea TBC kukatiza matangazo ya kampeni pasipo sababu ya msingi.
Kesho Jumamosi CHADEMA wanamkutano na wananchi pale Jangwani, hadi sasa ITV wametangaza kuwa watarusha matangazo ya mkutano huo live, vipi kuhusu TBC ambayo wananchi wanalipa kodi ili wapate huduma ya habari? Au tuamini kuwa TBC ni mali ya CCM na ipo kwa ajili ya kuonyesha mikutano ya CCM pekee??
mfano mzuri ni TBC ilipoamua kusitisha kurusha live kampeni za CHADEMA mwaka 2010 pale Jangwani ilipotokea TBC kukatiza matangazo ya kampeni pasipo sababu ya msingi.
Kesho Jumamosi CHADEMA wanamkutano na wananchi pale Jangwani, hadi sasa ITV wametangaza kuwa watarusha matangazo ya mkutano huo live, vipi kuhusu TBC ambayo wananchi wanalipa kodi ili wapate huduma ya habari? Au tuamini kuwa TBC ni mali ya CCM na ipo kwa ajili ya kuonyesha mikutano ya CCM pekee??