KLH News Alert:: Zitto Azuiwa Kuhutubia Moshi

Kuzuiwa ni kitu cha lazima hasa kwa watu hawa wanaopanda mbegu ya chuki,Tanzania ninchi ya amani na utulivu,lakini nia na lengo la watu hawa ni kujenga fitina baina ya wananchi na uongozi,kitu ambacho mizizi yake ikishika na kuota basi mjue kuwa mwisho wake itachanua na Tz ya jana na leo itakuwa kumbukumbu tu,nikikatisha maneno itakuwa hapatawaliki,na hakuna serikali itakayokaa madarakani ikaongoza ,mambo yatakuwa haya haya au zaidi ya haya ya kupandikiziana chuki,amani tuliyonayo itapotea kabisa na kurudi kwake itakuwa kwa mbinde,nasema watu hawa kama wana ushahidi wa uhakika kwa nini wasifungue kesi mahakamani,sababu wanayo sheria zipo,leo kupita Tanzania nzima kueneza sumu ambayo hata wao wakiachiwa madaraka basi wasifikirie kuwa sumu wanayoipanda itakuwa imekuwa diluted kwa kuwepo kwao kwenye ngazi za uongozi,huko itakuwa kujidanganya na kutudanganya,haya mambo hayafai kuzungumzwa na kukaa kama makonda wanaopiga debe safari za mabasi wataishia kupigana wenyewe kwa wenyewe wakati abiria yuko ndani ya basi.
Huu ni uzushi ambao wapinzani hawa wanaojidai kuungana mbele ya macho ya Watanzania ,wakidhani watavuka salama na kujinyakulia wapiga kura wengi kwa chaguzi zijazo kwa kuwavunga au kwa kuvujisha siri za walioko madarakani,uzushi ambao bila ya wasiwasi wowote naamini kabisa katika mtandao wa walaji kuna waliozikwa na kuachwa kwenye mataa.
Nasema tena kwa kichwa kipana waswahili tuna methali isemayo dua ya kuku haimpati mwewe.
Hawa sasa watasema na kuitisha vikao mpaka waulizane mbona fedha inayotumika kwa vikao ni nyingi na huku Muungwana amekwisha mwaga vumbi akiwaambia hizo kelele ni za mlango hazimsitui mwenye nyumba.


Juzi mmepigwa shule ya bure kuwa "Amani sio sera bali ni matokeo ya kazi nzuri inayofanywa na siasa safi" Kama unataka tukurudishe shule sawa tu.
 
Huyu Jk anaonekana afadhali kwa sababu alikuwa hajapewa kibano sawasawa na wapinzani na ukweli kwamba anaamini bado yupo popular. Nakwambia kwa jinsi mambo yanavyokwenda huyu bwana atakuwa tyrany kuliko Mkapa. Tazama hayo matokeo ya udiwani, umewahi kuona wapi wapinzani wanashinda viti vya udiwani kwa kiwango tunachoona. Tulizoea katika viti 100, wapinzani wanapata kimoja,sasa katika viti 3, wapinzani wanapata kiti. it is becoming serious for JK and good for the country and I am afraid this could be the beginning of JK' tyranny. However, I like your optimisim and hate my pessimism!

Ngojeni niwape kichomo,kwa wanaofahamu upinzani,Mh.Kikwete alikuwa mpinzani ndani ya CCM,baadhi ya vyama vya upinzani vilichelewa kupeleka jina la mgombea wakisubiri ikiwa Muungwana ataamua kuacha au kutemwa ndani ya kinyang'anyiro,waliomsaidia na kumwonyesha njia za kupita ni CUF kwa kumpa mikoba ambayo aliweza kuifuata na kufanikiwa hayo ni katika kipindi hicho ambacho alikuwa akijitayarisha ,na kwa kweli alikuwa amekwisha kata tamaa hajui ni namna gani ataweza kupenya,akamegewa na kuambiwa lazima ufanye hiki na kile,ukamate huyu na yule wote uwadhibiti kimawazo na kiakili,kipi aliambiwa afanye hilo silisemi kwani halitakuwa na faida kwa wakati huu tulio nao.
Kama kuna mtu ana uchungu na Nchi yake basi katika maraisi wote waliopita Mh.Kikwete ni nambari moja ukimwondoa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambae kwangu mimi simuweki katika kundi la Uraisi bali namwona ni mpigania uhuru.Maraisi ni hawa waliosoma na kusomeshwa na yeye,yeye ni baba au Baba wa Taifa mara nyingi mababa wazamani wanakuwa hawana elimu.
Mh.Kikwete ni lazima ajijenge ndani ya uongozi wake ni lazima achuje pumba na mchele,hapo ndipo alipo yumo katika mchakato wa hali juu,kwa kweli wandugu hili sio jambo rahisi au jepesi ni kitu kigumu sana sana(Tough),ndio ukaona au kusikia kuwa ndani ya CCM kuna makundi,hili ni jambo la lazima wakati nia yako na ya mwenzako ni tofauti nia ya Mh.Kikwete na ya wenzake ni tofauti tena tofauti sana,Mh.kila anapopanga anajaribu kutafuta watu walio tulia na kuwapambanunua watu hawa ndani ya magogo ya msitu mzito wa CCM sio rahisi,ni jambo linalohitaji uangalizi na ukakamavu wa hali ya juu kabisa kwani ni mambo ya mitandao ndani ya CCM,msitegemee ndani ya uongozi wake wa mwaka na nusu atafanikiwa kama kuwasha taa ya umeme nasema ni tough na hatari sana,kuna watu wanasema na yeye alihusika katika mambo ya ufisadi,kwa kweli inawezekana kabisa kuwa na yeye alihusika ,waswahili wanasema ukitaka cha uvunguni sharti uiname na yeye nia yake ilikuwa kuukamata Uraisi hivyo ilibidi lazima aonekane ni mwenzetu ili avuke mitihani ya kukubalika kuna kipindi aliteleza na kutaka kujivuta kwa mgongo wa Tanganyika na G?,lakini Mwalimu akaizima ile hoja na kwa vile ni mtu wa karibu na mwalimu, na mwalimu ni baba akaona mwanawe alitaka kupotea akamtuliza na kumpa ujiko mwengine ,hapo alisoma na kujikita mpaka akawa ni mwenzetu hatuna wasi wasi nae lakini,haraka yake ikaonekana na wakongwe ambao walikwisha muweza mpaka aliposituliwa na CUF afanye cha kufanya.Nia na madhumuni yake ni kuikoa Tanzania na waTanzania na kama ilivyoonyweshwa hapa njia mbaya alizotumia au mambo 50 sijui yote hiyo ilikuwa ni njia lazima azipite ili kufanikisha lengo lake ,leo lengo limetimia sasa ni kuondoa trace za magogo ili aanze kazi ya kuijenga Tanzania ya leo ya kizazi kipya.Hivyo mnachotakiwa ni kumuunga mkono na haya ya ufisadi ni lazima yafuatiliwe,ila kama mnasema alitumia fedha za walala hoi ili ashinde basi sio kosa ,ni kuambiwa tu sasa la kufanya ni kuonyesha namna atakavyozirudisha fedha hizo ndani ya mikono ya Watanzania kwa vitendo,pia nawaomba mtahadhari na ahadi za uchaguzi,nyingi ya ahadi za uchaguzi zinakuwa za kujenga tamaa au kumjengea mwananchi tamaa,hazina ukweli,kitu muhimu ni nia ya yule mchaguliwa ambayo nia ya Mh.Kikwete kwa kweli ni nzuri sana sana haijapata kutokea kwa mgombea yeyote ,Mheshimiwa nakuhakikishieni atawajengea mazingira mazuri ya uchaguzi kila anaeshinda ashinde kwa ridhaa ya wananchi wa jimbo lake,vyombo vya dola viwe na heshima na viheshimike,raia athamini na athaminiwe yaani ni mambo mengi tu,unajua kuondoa utawala mbovu uliojikita katika dhuluma si jambo rahisi na la mara moja,utawala au tawala zilizopita zilikuwa zimeshaiharibu Tanzania kuanzia juu hadi kwenye mashina mabalozi wenye kata na wenye mitungi,huko kote kensa ya dhulma ilikuwa imeshatambaa kuing'owa kunahitaji mida na ushirikiano na sio chuki.Mh.Kikwete anaambilika.
 
Ngojeni niwape kichomo,kwa wanaofahamu upinzani,Mh.Kikwete alikuwa mpinzani ndani ya CCM,baadhi ya vyama vya upinzani vilichelewa kupeleka jina la mgombea wakisubiri ikiwa Muungwana ataamua kuacha au kutemwa ndani ya kinyang'anyiro,waliomsaidia na kumwonyesha njia za kupita ni CUF kwa kumpa mikoba ambayo aliweza kuifuata na kufanikiwa hayo ni katika kipindi hicho ambacho alikuwa akijitayarisha ,na kwa kweli alikuwa amekwisha kata tamaa hajui ni namna gani ataweza kupenya,akamegewa na kuambiwa lazima ufanye hiki na kile,ukamate huyu na yule wote uwadhibiti kimawazo na kiakili,kipi aliambiwa afanye hilo silisemi kwani halitakuwa na faida kwa wakati huu tulio nao.....

Kikwete aliwekwa ikulu na wezi walioanzisha makampuni feki na wakaiba mabilioni benki (account, check, na kampuni numbers zimewekwa hapa JF).

Msaada mwingine ulikuwa ni wa pesa za Rostam Aziz alizopata toka kwa wafanyabiashara haramu wa kiirani (evidence zitawekwa hapa baada ya uchunguzi wa US congress dhidi ya Rostam Aziz kuwa tayari).

Hizi propaganda zako ni yesterday newz
 
Ngojeni niwape kichomo,kwa wanaofahamu upinzani,Mh.Kikwete alikuwa mpinzani ndani ya CCM,baadhi ya vyama vya upinzani vilichelewa kupeleka jina la mgombea wakisubiri ikiwa Muungwana ataamua kuacha au kutemwa ndani ya kinyang'anyiro,waliomsaidia na kumwonyesha njia za kupita ni CUF kwa kumpa mikoba ambayo aliweza kuifuata na kufanikiwa hayo ni katika kipindi hicho ambacho alikuwa akijitayarisha ,na kwa kweli alikuwa amekwisha kata tamaa hajui ni namna gani ataweza kupenya,akamegewa na kuambiwa lazima ufanye hiki na kile,ukamate huyu na yule wote uwadhibiti kimawazo na kiakili,kipi aliambiwa afanye hilo silisemi kwani halitakuwa na faida kwa wakati huu tulio nao.
Kama kuna mtu ana uchungu na Nchi yake basi katika maraisi wote waliopita Mh.Kikwete ni nambari moja ukimwondoa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambae kwangu mimi simuweki katika kundi la Uraisi bali namwona ni mpigania uhuru.Maraisi ni hawa waliosoma na kusomeshwa na yeye,yeye ni baba au Baba wa Taifa mara nyingi mababa wazamani wanakuwa hawana elimu.
Mh.Kikwete ni lazima ajijenge ndani ya uongozi wake ni lazima achuje pumba na mchele,hapo ndipo alipo yumo katika mchakato wa hali juu,kwa kweli wandugu hili sio jambo rahisi au jepesi ni kitu kigumu sana sana(Tough),ndio ukaona au kusikia kuwa ndani ya CCM kuna makundi,hili ni jambo la lazima wakati nia yako na ya mwenzako ni tofauti nia ya Mh.Kikwete na ya wenzake ni tofauti tena tofauti sana,Mh.kila anapopanga anajaribu kutafuta watu walio tulia na kuwapambanunua watu hawa ndani ya magogo ya msitu mzito wa CCM sio rahisi,ni jambo linalohitaji uangalizi na ukakamavu wa hali ya juu kabisa kwani ni mambo ya mitandao ndani ya CCM,msitegemee ndani ya uongozi wake wa mwaka na nusu atafanikiwa kama kuwasha taa ya umeme nasema ni tough na hatari sana,kuna watu wanasema na yeye alihusika katika mambo ya ufisadi,kwa kweli inawezekana kabisa kuwa na yeye alihusika ,waswahili wanasema ukitaka cha uvunguni sharti uiname na yeye nia yake ilikuwa kuukamata Uraisi hivyo ilibidi lazima aonekane ni mwenzetu ili avuke mitihani ya kukubalika kuna kipindi aliteleza na kutaka kujivuta kwa mgongo wa Tanganyika na G?,lakini Mwalimu akaizima ile hoja na kwa vile ni mtu wa karibu na mwalimu, na mwalimu ni baba akaona mwanawe alitaka kupotea akamtuliza na kumpa ujiko mwengine ,hapo alisoma na kujikita mpaka akawa ni mwenzetu hatuna wasi wasi nae lakini,haraka yake ikaonekana na wakongwe ambao walikwisha muweza mpaka aliposituliwa na CUF afanye cha kufanya.Nia na madhumuni yake ni kuikoa Tanzania na waTanzania na kama ilivyoonyweshwa hapa njia mbaya alizotumia au mambo 50 sijui yote hiyo ilikuwa ni njia lazima azipite ili kufanikisha lengo lake ,leo lengo limetimia sasa ni kuondoa trace za magogo ili aanze kazi ya kuijenga Tanzania ya leo ya kizazi kipya.Hivyo mnachotakiwa ni kumuunga mkono na haya ya ufisadi ni lazima yafuatiliwe,ila kama mnasema alitumia fedha za walala hoi ili ashinde basi sio kosa ,ni kuambiwa tu sasa la kufanya ni kuonyesha namna atakavyozirudisha fedha hizo ndani ya mikono ya Watanzania kwa vitendo,pia nawaomba mtahadhari na ahadi za uchaguzi,nyingi ya ahadi za uchaguzi zinakuwa za kujenga tamaa au kumjengea mwananchi tamaa,hazina ukweli,kitu muhimu ni nia ya yule mchaguliwa ambayo nia ya Mh.Kikwete kwa kweli ni nzuri sana sana haijapata kutokea kwa mgombea yeyote ,Mheshimiwa nakuhakikishieni atawajengea mazingira mazuri ya uchaguzi kila anaeshinda ashinde kwa ridhaa ya wananchi wa jimbo lake,vyombo vya dola viwe na heshima na viheshimike,raia athamini na athaminiwe yaani ni mambo mengi tu,unajua kuondoa utawala mbovu uliojikita katika dhuluma si jambo rahisi na la mara moja,utawala au tawala zilizopita zilikuwa zimeshaiharibu Tanzania kuanzia juu hadi kwenye mashina mabalozi wenye kata na wenye mitungi,huko kote kensa ya dhulma ilikuwa imeshatambaa kuing'owa kunahitaji mida na ushirikiano na sio chuki.Mh.Kikwete anaambilika.

mbona unaji changanya kule nyuma ume walaumu wapinzani kwa kile unacho kiita kupanda chuki, sasa anaye panda hiyo mbegu ni mwizi au yule anayesema fulani ni mwizi.
pili, watu walimpa hayo matumaini muungwana lakini ktk kipindi hichi cha miezi 18 ameshindwa kuonyesha cheche zake na tatu kuna maamuzi ambayo yamefanyika katika uongozi wake ambayo si sawa kama hiyo ya richmond, buzwagi, kesi ya chitalilo etc.
sasa kiongozi kama yeye anaposhindwa hata suala la chitalilo of all the people , ni kiongozi kweli mwenye nia nzuri? au la viongozi wa Vyama vya Ushirika, maana Nkapa anaweza kuwa ni mfupa mgumu kidogo kuutafuna , lakini hayo mengine.
Mbona hao akina Molel inawa ni vingunge huko Arusha wamewatuhumu?
Atakuwa Chitalilo.
Haya kuna Shule kule Shinyanga ilikuwa ipigwe mnada bei inakuwa inflated, mpaka Mkuu wa Mkoa analazimishia madiwani kununua Shule kwa Bei hiyo na President na machinery yake wapo tu hawakemei kitu kama hiko. Kulikoni?
 
Mwiba nilisha kupa onyo ukadhani nakutania. Hapa ni JF huwa wanakuja wajuvi upuuzi kama wewe wanayeyuka jioni .Kaa macho maana unaanza kula matapishi yako.

Haya unayo yaleta hapa hayana connection na mada yenyewe .Kindly fungua mada ya kumpa sifa JK na tutakuja ama kukuunga mkono ama kumkoma Nyani giladi. Tumia muda kidogo kujifunza Mwimba maana hapa kuna miiba zaidi yako. Unajichanganya na unaharibu mada ya Zitto kuzuiwa kuhutubia wananchi .

JK is a raising and soon shinnig tyrany kwa kuona toka mbali anatumia maneno kama makelele ya wapinzani hayamnyimi usingizi huku pesa zetu na mali zetu zinatumiwa na wazungu vibaya na wenye Nchi adhirika .

Alisema hivyo kwa chitalilo na kweli kesi hakuna wavuja jasho wanahangaishwa . Je hii ndiyo demo unayo ongelea kwamba italetwa na JK ?Kwanza anategemea kuileta lini ? Na ataanzia wapi ? Tunamtaka aanze na kumwacha Zitto aungurume kwa uhuru maana ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na Mtanzania na katiba inampa uhuru wa kukutana na watu na kutoa mawazo .
 
Anhaa,aliwekwa Ikulu ,sawa sikatai ,hata katika michezo ya macowboy wanaiba pamoja na mwisho hugeukiana tena kama haitoshi hata kuuwana,hapo hakuna jipya,naweza kusema nia na madhumuni yake yametimia,kuwa Raisi mwenye lengo zuri tu,alichokitaka amekipata,hizo ni zile njia ambazo nimesema kwa mtu yeyote yule kama si mwenzetu asingeweza kuukwaa uraisi wa Tanzania,unajua huwezi huwezi kuwakamata wezi au wavuta unga kama wewe humo kwenye kundi na njia za kuwakamata watu hawa ni lazima baadhi ya makachero wawemo ndani ya action vyenginevyo,hakamatwi mtu,kama unasikia maspy hawa huwemo ndani ya utawala wa nchi,huwemo ndani ya vyombo vya usalama jeshi na kila sehemu muhimu,na zaidi Mh.Kikwete aliwahi kusikika akisema anawajua watu wote wanaohusika na ufisadi hivyo huwezi kuwajua kama wewe hukuwa mmoja wao kwa njia moja au nyingine,nasema tumepata Raisi mzuri ambae kama angekuwa mbaya angekwisha kuwakamata na kuwakata shingo wote hao na kusema walikuwa walikuwa wezi wa mali ya umma.
Umesema msaada,hapo naona haina haja ya kuongeza neno wakati ni kitu amepewa kujisadia na ilivyokuwa ni muhimu kwa kutimiza lengo lake basi sioni kama kuna ubaya wa kuupokea,lengo ni kuukwaa Uraisi ili kuleta mabadiliko kwa Mtanzania,kuna zaidi ya hilo.
Nikichoma hapo kwa Rostam huyo ni muislamu wa madhehebu ya shia na aliwadanganya mashia wenzake wa kiirani wakanunua sehemu Geita ya kuchota mali ya asili baada ya kuanza kuvuta na kuona mambo yote sawa akawachomea utambi wenziwe na kuwahusiha na alkaida jamaa wakatiwa mbioni wakarudi kwao Rostam akarisi mali na kuendelea kutesa,vile vile kama nilivyosema kuna mitandao na hii haitaki mchezo kama mnavyofikiria,inatakiwa kutrace kama unavyopima radioactive zilizomwagika kwenye ardhi ili watu wapate kuishi na kupanda kuvuna na kunywa hali kadhalika kuepusha taathira kwa vinavyozaliwa.Ndio ukamsikia Muungwana akisema mambo yanachunguzwa.
 
Anhaa,aliwekwa Ikulu ,sawa sikatai ,hata katika michezo ya macowboy wanaiba pamoja na mwisho hugeukiana tena kama haitoshi hata kuuwana,hapo hakuna jipya,naweza kusema nia na madhumuni yake yametimia,kuwa Raisi mwenye lengo zuri tu,alichokitaka amekipata,hizo ni zile njia ambazo nimesema kwa mtu yeyote yule kama si mwenzetu asingeweza kuukwaa uraisi wa Tanzania,unajua huwezi huwezi kuwakamata wezi au wavuta unga kama wewe humo kwenye kundi na njia za kuwakamata watu hawa ni lazima baadhi ya makachero wawemo ndani ya action vyenginevyo,hakamatwi mtu,kama unasikia maspy hawa huwemo ndani ya utawala wa nchi,huwemo ndani ya vyombo vya usalama jeshi na kila sehemu muhimu,na zaidi Mh.Kikwete aliwahi kusikika akisema anawajua watu wote wanaohusika na ufisadi hivyo huwezi kuwajua kama wewe hukuwa mmoja wao kwa njia moja au nyingine,nasema tumepata Raisi mzuri ambae kama angekuwa mbaya angekwisha kuwakamata na kuwakata shingo wote hao na kusema walikuwa walikuwa wezi wa mali ya umma.
Umesema msaada,hapo naona haina haja ya kuongeza neno wakati ni kitu amepewa kujisadia na ilivyokuwa ni muhimu kwa kutimiza lengo lake basi sioni kama kuna ubaya wa kuupokea,lengo ni kuukwaa Uraisi ili kuleta mabadiliko kwa Mtanzania,kuna zaidi ya hilo.
Nikichoma hapo kwa Rostam huyo ni muislamu wa madhehebu ya shia na aliwadanganya mashia wenzake wa kiirani wakanunua sehemu Geita ya kuchota mali ya asili baada ya kuanza kuvuta na kuona mambo yote sawa akawachomea utambi wenziwe na kuwahusiha na alkaida jamaa wakatiwa mbioni wakarudi kwao Rostam akarisi mali na kuendelea kutesa,vile vile kama nilivyosema kuna mitandao na hii haitaki mchezo kama mnavyofikiria,inatakiwa kutrace kama unavyopima radioactive zilizomwagika kwenye ardhi ili watu wapate kuishi na kupanda kuvuna na kunywa hali kadhalika kuepusha taathira kwa vinavyozaliwa.Ndio ukamsikia Muungwana akisema mambo yanachunguzwa.

Bado nasubiri uanze kusema ni mwanaccm gani apigiwe kura mwaka 2015! so far naona unaimba vibwagizo tu, anza wimbo mwaya!

Kama kawaida ya JF, utakuwa unasubiriwa hapa ili uonyeshwe namna ya kumkoma giladi nyani the JF way!
 
Post yako hapo #22 inahusika:

Wengi tuliamini, na pengine bado kuna nafasi ndogo iliyobaki kuamini kuwa Kikwete huyu wa sasa ni yule tuliyemtumainia wakati wa uchaguzi.

Kwa bahati mbaya, dalili zinazidi kujionyesha kuwa sivyo na muda unazidi kumwishia kutoonyesha kwamba kweli ndiye.

Mwiba, kama upo karibu nae, 'time is running out.' Watu tutaanza kuamini hana uwezo wa kuongoza. Nia njema tu bila kuonyesha matendo havitupeleki mbali. Kama mtu unayo nia njema na nchi yako, halafu unaweka vichaa kwenye sehemu mhimu za uongozi, nk kweli tuendelee kukuamini tu kwamba unayo nia njema na nchi yetu?
 
Mwiba nilisha kupa onyo ukadhani nakutania. Hapa ni JF huwa wanakuja wajuvi upuuzi kama wewe wanayeyuka jioni .Kaa macho maana unaanza kula matapishi yako.

Haya unayo yaleta hapa hayana connection na mada yenyewe .Kindly fungua mada ya kumpa sifa JK na tutakuja ama kukuunga mkono ama kumkoma Nyani giladi. Tumia muda kidogo kujifunza Mwimba maana hapa kuna miiba zaidi yako. Unajichanganya na unaharibu mada ya Zitto kuzuiwa kuhutubia wananchi .

JK is a raising and soon shinnig tyrany kwa kuona toka mbali anatumia maneno kama makelele ya wapinzani hayamnyimi usingizi huku pesa zetu na mali zetu zinatumiwa na wazungu vibaya na wenye Nchi adhirika .

Alisema hivyo kwa chitalilo na kweli kesi hakuna wavuja jasho wanahangaishwa . Je hii ndiyo demo unayo ongelea kwamba italetwa na JK ?Kwanza anategemea kuileta lini ? Na ataanzia wapi ? Tunamtaka aanze na kumwacha Zitto aungurume kwa uhuru maana ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema na Mtanzania na katiba inampa uhuru wa kukutana na watu na kutoa mawazo .
Mimi naona nipo kwenye mstari ila katika kila habari kwa tulivyozoea waTanzania kuna mazungumzo baada ya habari,mnavyotaka nyinyi awe Raisi dictator ,mtu wa amri tu,Zitto anatembeza chuki ambayo ikishika kasi hata yeye mwenyewe itamdhuru,hivi hamlioni hili,nawaombeni msitazame mambo kwa karibu jaribuni kuwa na foresight au kuona mbali,tazameni kwa makini matokeo ya baadae msitazame hapa kwa jazba ya kinachoelezwa ni kweli,kwani hata muungwana hajakataa kuwa si kweli,lakini mtazamo unaojengwa sio mzuri kwa taifa la kesho.
 
Updates jamani mulioko bongo,

bado zitto amezuiwa kuhutubia au jamaa wamelegeza kamba baada ya JF kupata hii news? Hii sababu ya kuzuia huu mkutano bado sioni uzito wake au ndio mambo ya kumpiga mrema mabomu yanataka kuanza?
 
Naomba kuuliza.

Je unataka JK tumuunge mkono kwa lipi? Na kwa nini?

Baada ya hapo nakupa ushauri mwingine tena kwamba fungua thread mpya ya JK na sifa zako na utuachie hii ya Zitto iendelee kuchangiwa.
 
Naomba kuuliza.

Je unataka JK tumuunge mkono kwa lipi? Na kwa nini?

Baada ya hapo nakupa ushauri mwingine tena kwamba fungua thread mpya ya JK na sifa zako na utuachie hii ya Zitto iendelee kuchangiwa.

Lunyungu,

mwiba kafanya makusudi kabisa ili kuvuruga report uliyokuwa unaendelea kutupatia kuhusu hii issue ya zitto.

Mwiba is here for that purpose na kama huamini just wait for the tone......
 
Kuzuiwa ni kitu cha lazima hasa kwa watu hawa wanaopanda mbegu ya chuki,Tanzania ninchi ya amani na utulivu,lakini nia na lengo la watu hawa ni kujenga fitina baina ya wananchi na uongozi,kitu ambacho mizizi yake ikishika na kuota basi mjue kuwa mwisho wake itachanua na Tz ya jana na leo itakuwa kumbukumbu tu,nikikatisha maneno itakuwa hapatawaliki,na hakuna serikali itakayokaa madarakani ikaongoza ,mambo yatakuwa haya haya au zaidi ya haya ya kupandikiziana chuki,amani tuliyonayo itapotea kabisa na kurudi kwake itakuwa kwa mbinde,nasema watu hawa kama wana ushahidi wa uhakika kwa nini wasifungue kesi mahakamani,sababu wanayo sheria zipo,leo kupita Tanzania nzima kueneza sumu ambayo hata wao wakiachiwa madaraka basi wasifikirie kuwa sumu wanayoipanda itakuwa imekuwa diluted kwa kuwepo kwao kwenye ngazi za uongozi,huko itakuwa kujidanganya na kutudanganya,haya mambo hayafai kuzungumzwa na kukaa kama makonda wanaopiga debe safari za mabasi wataishia kupigana wenyewe kwa wenyewe wakati abiria yuko ndani ya basi.
Huu ni uzushi ambao wapinzani hawa wanaojidai kuungana mbele ya macho ya Watanzania ,wakidhani watavuka salama na kujinyakulia wapiga kura wengi kwa chaguzi zijazo kwa kuwavunga au kwa kuvujisha siri za walioko madarakani,uzushi ambao bila ya wasiwasi wowote naamini kabisa katika mtandao wa walaji kuna waliozikwa na kuachwa kwenye mataa.
Nasema tena kwa kichwa kipana waswahili tuna methali isemayo dua ya kuku haimpati mwewe.
Hawa sasa watasema na kuitisha vikao mpaka waulizane mbona fedha inayotumika kwa vikao ni nyingi na huku Muungwana amekwisha mwaga vumbi akiwaambia hizo kelele ni za mlango hazimsitui mwenye nyumba.

Watu wengine wajinga hata kuwaeleza unashindwa. Kuna amani? Amani ipi? Upofu na ukondoo huu ndio unaimaliza nchi yetu...Ipo siku na wewe utatambua hizi ngonjera unazoimba hapa hazina maana (kama utakuwa umeangaziwa). Amani????!!!!!
 
Polisi wamzuia Zitto kuhutubia TPC Moshi
* Wasema angefanya mkutano kungetokea fujo
* TPC washangaa mbona hawajazungumza na polisi

* Chadema wadai kuna mkono wa serikali


Na Daniel Mjema, Moshi


JESHI la Polisi mkoa wa Kilimanjaro jana lilizuia kufanyika kwa mkutano wa hadhara ambao ungehutubiwa na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Zitto Kabwe, katika uwanja wa Limpopo ulioko ndani ya eneo la Kiwanda cha Sukari cha TPC, kwa madai ya kuepusha vurugu ambazo zingetokea kwenye mkutano huo.


Kwa mujibu wa barua ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Moshi, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi(SSP), Kibwana Majid, endapo mkutano huo ungefanyika kungeweza kutokea vurugu kati ya menejimenti ya TPC na Chadema.


SSP Majid alisema katika barua hiyo ya jana, Jeshi la Polisi limepata taarifa ya kuwepo kwa matangazo kwa kutumia vipaza sauti juu ya kuwepo kwa mkutano huo ambao ungehutubiwa na Kabwe.


"Baada ya kufuatilia taarifa hizo viongozi wa TPC walinijulisha kwamba uwanja huo uko ndani ya utawala wa TPC na kwamba haukuwa na taarifa ya kufanyika kwa mkutano huo," ilisema barua hiyo.


"Kutokana na sababu hizo na nyinginezo za kiusalama, kwamba kunaweza kutokea vurugu kwa kutoelewana kati ya TPC na Chadema, hivyo ofisi hii inapendekeza kusitishwa kwa mkutano huo katika eneo hilo," ilisema sehemu ya taarifa hiyo.


Hata hivyo, Afisa Mtendaji wa TPC anayeshughulikia Utawala, Jaffar Ally alipohojiwa na mwandishi wa Mwananchi kwa simu jana, alishangazwa na kauli hiyo ya polisi na kusema TPC hawana mamlaka ya kuzuia mkutano wowote.


"Hapa mbele yangu nina barua ya Chadema ya mkutano ambayo imeandikwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi na sisi tumepewa nakala tu na hatukuwajibu kwa sababu tulijua kibali cha mkutano kinatolewa na Polisi," alisema.


Ally alisema hata Askofu Zakaria Kakobe na viongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Mashambani (TPAWU), waliutumia uwanja huo kufanya mikutano akashangaa TPC kuwekewa maneno kuwa wamewakatalia Chadema


"Hebu nipe namba ya hao watu wa Chadema niwasiliane nao ili nijue nini kilitokea kwa sababu hatujafanya kikao chochote na polisi wala Chadema, sasa tungesemaje kutatokea vurugu?" alihoji Afisa huyo.


Kabwe aliliambia Mwananchi kuwa yeye ni mgeni wa Chadema mkoa Kilimanjaro na mkutano huo ulikuwa ni wa kukiimarisha chama na angetumia mkutano huo kuzungumzia mambo muhimu ya maslahi ya nchi.


"Barua hii ya polisi bado hainiingii akilini kwamba Chadema tungegombana na TPC, sisi tunashangaa, kwani TPC ni chama cha siasa? Hapa naona kuna jambo," alisema.


Kwa upande wake, Katibu wa Chadema Mkoa wa Kilimanjaro, Akwiline Chuwa alisema sababu zilizotolewa na polisi ni za kisiasa zaidi na kuna kila sababu ya wao kuamini kuwa ni agizo la Serikali.


"Sisi hatujawahi kuwa na ugomvi na TPC na kimsingi walipokuwa na mgogoro na wafanyakazi tulikuwa tunaomba umalizike maana kuna wanachama wetu hapo, sasa leo tunashangaa tunapoambiwa tutapigana na TPC," alisema Chuwa.


Katibu huyo alisema tangu kuwapo kwa kampeni za kujaza nafasi za viti vya udiwani, serikali imekuwa ikitumia nguvu ya ziada kukabiliana na wapinzani, ikiwamo kuitumia vibaya ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Moshi.
 
Kufauru mtihani ndani ya SISIEMU ni kwa kuiba? Kweli chama chenu ni cha Maharamia.

Makundi ni dalili ya udhaifu ndani ya SISIEMU.

Mababa wa zamani wanakuwa hawana elimu!
Nyerere alikuwa ni msomi aliyebobea katika fani yake. Kikwete ni kilaza mkubwa katika fani yake, mchumi asiyejua kwa nini nchi yake ni masikini. Usomi wake unatoka wapi?

Mwiba, unaleta Porojo za vijiwe vya Kahawa hapa JF maelezo yako ni kama unasimulia mbinu za ushindi wa Yanga kwa kuzingua mazindiko na wanga wa bagamoyo na kuruka ukuta uwanja wa Taifa.
Sasa wamejengewa jiwanja, ili SISIEMU kuruka ukuta sharti wanunue Crane kubwa.

Kwako Mwiba nchi inaendeshwa kama familia ya mzee mwenye ng'ombe wengi na wake wengi, SISIEMU akiwa mke mkubwa mwenye mdomo na makalio makubwa .

Watu waliopo madarakani sasa hivi ni Maharamia kwa kila hali. maharamia hawa wanajaribu kujiosha nyuso zao kwa mate wakati maji yapo tele. Sijui uchambuzi wako una base kwenye nini!

Fedha na utajiri haujawahi kuwa kigezo cha maendeleo na furaha umasikini vilevile si jambo la kujivunia na halileti furaha,lakini kitendo cha kuruhusu wizi wa karne zote zijazo ni cha kimumiani.

Pengine kwa kufaidika kwako na makombo yaangukayo kutoka kwenye meza za mafisadi au kitu kifafanacho na hicho unamwaga sifa bila kuzingatia uhalifu wa kimataifa wa Wahuni wa SISIEMU wakiongozwa na Kikwete mwenyewe.
 
..sheria hizo hizo CCM wanazotumia kuwaadhibu upinzani ndio hizo hizo zitatumika kuwacharaza wakipigwa nje...si mnakumbuka Gallow aliyojenga saddam kuwaua wenzake ndio hiyo hiyo iliyokuja kumuua yeye na wenzake
 
..sheria hizo hizo CCM wanazotumia kuwaadhibu upinzani ndio hizo hizo zitatumika kuwacharaza wakipigwa nje...si mnakumbuka Gallow aliyojenga saddam kuwaua wenzake ndio hiyo hiyo iliyokuja kumuua yeye na wenzake

..hii imetulia koba!

..jambiya hukata pande zote!

..ni suala la awamu tu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom