Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,316
- 10,782
Salaam wanaJF!
Tukiwa tunaelekea kutimiza miaka 50 ya uhuru wa bendera wa Tanganyika kumezuka na mwenendo wa serikali ya CCM kutumia nguvu nyingi kutangaza yale yayoitwa mafanikio ya miaka 50 ya uhuru! Tumeona kuanzia bungeni pale wabunge wengi wa serikali (hapa namaanisha wabunge wa CCM) walipokua wakijitaidi kuaminisha wadanganyika kwamba nchi "imethubutu, imeweza na imesonga mbele" kwa kutolea mifano mbalimbali kama wingi wa taasisi za elimu, wingi wa majengo ya zahanati na vituo vya afya, wingi wa wanafunzi wanajiunga na shule (huku kukiwa na wingi wa ongezeko la wasiojua kusoma na kuandika); urefu wa barabara za lami n.k. Msisitizo wa wabunge hao ni kwamba nchi imeendelea sana kuliko ilivyokua mwaka 1961.
Sambamba na hayo tumeona pia wizara, idara na taasisi mbalimbali za dola na serikali zikitumia maonyesho kuonesha mafanikio ya miaka 50 ya uhuru; katika wiki kama mbili hivi tumeona wizara ya ujenzi na idara zake na pia wizara ya elimu na idara zake.
Sasa nimejiuliza hivi si kuna msemo wa kiswahili kwamba KIZURI CHAJIUZA NA KIBAYA CHAJITEMBEZA; hivi kwa mtindo huo wa serikali ya CCM, huu msemo si unaihusu?!
Mambo mazuri iwe maendeleo ya nchi au mtu mmoja mmoja hayapaswi kutangazwa kwa nguvu na gharama kubwa kama inavyojitokeza sasa, haya mambo yanaonekana yenyewe tu...mimi naona wanapoteza muda na pesa bure..hizo pesa si ni bora wangeongezea katika miradi ya umeme kama kule Rufiji, miradi ya barabara vijijini; miradi ya maji n.k.?! Na hii ni trailer, sipati picha hicho kilele hapo 9/12..sijui bajeti yake ni kiasi gani?
Ninafanya mchakato wa kuanzisha petition ya kupinga sherehe hizo zisifanyike, kwani hakuna cha kusherekea katika miaka hii 50 ya giza, njaa na kiu.
Nawasilisha.
Asante.
Tukiwa tunaelekea kutimiza miaka 50 ya uhuru wa bendera wa Tanganyika kumezuka na mwenendo wa serikali ya CCM kutumia nguvu nyingi kutangaza yale yayoitwa mafanikio ya miaka 50 ya uhuru! Tumeona kuanzia bungeni pale wabunge wengi wa serikali (hapa namaanisha wabunge wa CCM) walipokua wakijitaidi kuaminisha wadanganyika kwamba nchi "imethubutu, imeweza na imesonga mbele" kwa kutolea mifano mbalimbali kama wingi wa taasisi za elimu, wingi wa majengo ya zahanati na vituo vya afya, wingi wa wanafunzi wanajiunga na shule (huku kukiwa na wingi wa ongezeko la wasiojua kusoma na kuandika); urefu wa barabara za lami n.k. Msisitizo wa wabunge hao ni kwamba nchi imeendelea sana kuliko ilivyokua mwaka 1961.
Sambamba na hayo tumeona pia wizara, idara na taasisi mbalimbali za dola na serikali zikitumia maonyesho kuonesha mafanikio ya miaka 50 ya uhuru; katika wiki kama mbili hivi tumeona wizara ya ujenzi na idara zake na pia wizara ya elimu na idara zake.
Sasa nimejiuliza hivi si kuna msemo wa kiswahili kwamba KIZURI CHAJIUZA NA KIBAYA CHAJITEMBEZA; hivi kwa mtindo huo wa serikali ya CCM, huu msemo si unaihusu?!
Mambo mazuri iwe maendeleo ya nchi au mtu mmoja mmoja hayapaswi kutangazwa kwa nguvu na gharama kubwa kama inavyojitokeza sasa, haya mambo yanaonekana yenyewe tu...mimi naona wanapoteza muda na pesa bure..hizo pesa si ni bora wangeongezea katika miradi ya umeme kama kule Rufiji, miradi ya barabara vijijini; miradi ya maji n.k.?! Na hii ni trailer, sipati picha hicho kilele hapo 9/12..sijui bajeti yake ni kiasi gani?
Ninafanya mchakato wa kuanzisha petition ya kupinga sherehe hizo zisifanyike, kwani hakuna cha kusherekea katika miaka hii 50 ya giza, njaa na kiu.
Nawasilisha.
Asante.