Kizungumkuti Dowans

ukifuatilia kauli zake nyingi za karibuni utagundua kuwa yupo kwenye mashaka fulani na kuna kitu anategeategea kwa kujaribu kupata mass support

Mi nilimsoma ITV siku ya kufungua studio ya Flora Mbasha,ile confidence imeondoka amekuwa muoga kabisa na mnyenyekevu,nikajua hapa anahusika,hakujibu hata tuhuma moja while jana yake ndo zilikuwa zimesemwa kwenye kongamano la katiba,kwa mtu jeuri kama yule anahusika,otherwise angeshafikisha watu mahakamani.
 
Let him stay silent on dowans. Probably anajua recipes zote zilizotumika kupika Richmond na Dowans. Aseme ninizaidi ya kujua kwake? nothing...
 
Chadema wamtwisha JK deni la Dowans
Sunday, 23 January 2011 09:50


dk%20willbrodslaa1.jpg

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa


Claud Mshana
Mwananchi

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa, amesema wanaopaswa kulipa deni la Dowans ni Rais Jakaya Kikwete na Kamati kuu ya CCM.Dk Slaa imetoa kauli hiyo siku moja baada ya Kikao cha Kamati Kuu ya CCM kubariki Dowans ilipwe Sh 94 bilioni kufuatia kampuni hiyo kushinda kesi katika Mahakama ya Biashara ya Kimataifa (ICC), dhidi ya serikali ya Tanzania.

Akihutubia katika Kongamano lililoandaliwa na Baraza la Vijana wa Chadema na kuwashirikisha vijana wa chama hicho walioko vyuo vikuu jijini Dar es Salaam jana, Dk Slaa alisema amepata taarifa kuwa wajumbe wa Kamati Kuu wakiongozwa na Rais Kikwete walikubali Dowans ilipwe na Serikali.

"Ni uzembe umefanyika katika suala hilo, mimi nasema alipe Rais Kikwete na Kamati Kuu ya CCM,” alisema Dk Slaa huku akishangiliwa na mamia ya wanafunzi na wafuasi wa chama hicho waliofurika Viwanja vya Mabibo External.

Kuhusu hukumu hiyo, Dk Slaa alisema kuna mambo mengi ambayo yako kinyume na sheria lakini hakuna mtu anayejali kuyashughulikia.

Alitoa mfano wa taarifa zilizopo kuwa kesi hiyo haijawasilishwa mahakama kuu ya biashara kama inavyohitajika kisheria ili malipo yafanyike na kwamba kilichopelekwa ni viambatanisho vya kesi.

“Kuna utata mkubwa sana katika kesi hii, kwanza kesi yenyewe haijasajiliwa katika Mahakama Kuu kama inavyotakiwa, kilichowasilishwa huko ni Indices (Viambatanisho) za kesi, tunataka Mwanasheria Mkuu atupe maelezo,” alisema Dk Slaa.

Alifafanua kuwa Kampuni ya uwakili ya Rex Attorney iliyokuwa mshauri wa Serikali wakati wa kuvunja mkataba huo, inapaswa itoe maelezo wakati huu Dowans inatakiwa kulipwa.
“Rex Attorney ni nani, aliishauri nini Serikali kuhusu kuvunja mkataba na anaishauri nini kuhusu kuilipa Dowans?” alihoji.

Hali ya Siasa
Akizungumzia hali ya siasa nchini, Dk Slaa alisema hadi sasa, nchi imechanganyikiwa na kusisitiza kauli yake kuwa nchi hii haitawaliki.

Huku akikatizwa na kelele za mara kwa mara kutoka kwa wanafunzi waliofurika katika viwanja hivyo, Dk Slaa alisema anashangazwa na jinsi serikali inavyozuia watu kuzungumzia masuala ya siasa.

“Ukitaka watu wasiongee siasa unataka nini, hii ni kasumba ya viongozi wasiopenda kufikiri, wanaolichanganya taifa na kusababisha migogoro mikubwa,” alisema na kuongeza:
“Viongozi wa dini wanapokemea watu wanaotenda maovu katika siasa wanasemwa kuwa wanaingilia siasa, lakini Rais Kikwete alipowaita viongozi hao Kunduchi kuwaomba kura walikuwa hawaongei siasa?,” alihoji.

Udini
Dk Slaa pia alitumi nafasi hiyo kuwaonya viongozi wanaoeneza maneno kuwa kuna udini nchini.

Alisema dhana hiyo inachochewa na viongozi dhaifu wanaotafuta hoja itakayomeza hoja za msingi za maendeleo ya taifa.

Dk Slaa ambaye alishika nafasi ya pili katika matokeo kura z urais kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita alisema anashangazwa na kauli za Rais Kikwete kuwa kuna harufi ya udini wakati hachukui hatua yoyote na wakati udini ni kosa la jinai kwa vile ni sawa na ubaguzi.

“Kama rais analalamika kuwa kuna udini na hachukui hatua, nani achukue hatua, hatujaona mtu yeyote aliyekamatwa kwa kuhubiri udini, Watanzania bado tunaishi kama ndugu tena kwa amani,” alisema Dk Slaa.

Alitoa mifano ya mwaka 1987 kulipoibuka vuguvugu kubwa la udini, lakini aliyekuwa rais kipindi hicho, Mzee Ali Hassani Mwinyi, alichukua hatua za kuunda kamati kutoka madhehebu yote iliyoshughulikia kiina cha tatizo hilo na kulimaliza.

Alisema hakuwahi kusikia Rais mstaafu Mwinyi akikemea udini majukwaani na kushangaa kauli za Rais Kikwete juu ya kuwepo kwa udini ambao hakuna hata mmoja aliyechukuliwa hatua za kisheria.

Vyuo vikuu na Siasa
Akizungumzia vyuo vikuu kujihusisha na siasa, Dk Slaa alisema ni jambo la ajabu kwa wanafunzi kuzuiwa kushiriki siasa wakati vyuo vinawafundisha siasa.

“Mwalimu Julius Nyerere alianza harakati za ukombozi akiwa chuoni, kwenye vyuo ndiko kunakopikwa watu wanaofikiria, ndio kituo cha mawazo na hoja za maendeleo, tunataka viongozi makini na si viongozi wa propaganda,” alisema Dk Slaa na kuongeza:
“Nchi isiyotaka kuchukua changamoto kutoka kwa vijana itakuwa imepotea. Wakati umefika vyuo viwe ni msaada kwa nchi na wanafunzi wanatakiwa wawe huru”.

Kiongozi huyo wa Chadema aliituhumu Bodi ya Mikopo kuwa imejaa upendelea na kuongeza na kwamba alishawahi kutoa mapendekezo ivunjwe na kuundwa mpya.

Akizungumzia viongozi wa nchi kupewa shahada za heshima, Dk Slaa alisema inasikitisha kuona kuwa chuo ambacho hata hakina program ya Shahada Uzamili, kinakuwa na sifa ya kutoa shahada ya heshima.

“Degree (shahada ya kwanza) hazigawanywi kama karanga, haya ni matokeo ya kupendeleana, chuo chenyewe kina matatizo chungu nzima, wakuu wake wanatoa ‘degree’ hizo ili waendelee kunufaika,” alisema huku akishangiliwa na wanafunzi hao waliokuwa wakitamka “UDOM...UDOM....UDOM....” wakimaanisha chuo Kikuu cha Dodoma.

Mabere Marando
Kwa upande wake, Wakili wa Kujitegemea na mwanachama wa Chadema, Mabere Marando, alisema suala la katiba mpya kwa sasa halina mjadala tena.

“Katiba mpya, tupende tusipene, Kikwete apende asipende, CCM ipende isipende, lazima iandikwe upya hilo si suala la mjadala tena,” alisisitiza Marando a kuongeza:
“Hoja iliyopo ni je viongozi walio madarakani wanasoma alama za nyakati au wapo tu kama kisiki wanasubiri wafagiwe na upepo”.

Marando pia aliponda hali ya kupingana iliyojitokeza kwa mawaziri, baraza la vijana wa CCM kupingana na wazee kuwa ni ishara kuwa chama hicho kinaelekea kufa.

“Chama chochote cha siasa kinazaliwa, kinakua, kinazeeka na kinakufa, CCM sasa inakufa. Hebu kisaidieni kife bila ya sisi kupata madhara,” alisema Marando ambaye ni mmoja wa waasisi wa mageuzi nchini.

Kuhusu mabadiliko ya katiba, Marando alitoa mfano wa katiba mpya ya Kenya kuwa ina vipengele ambavyo ni lazima katiba yetu iwe navyo.

Alitoa mifano ya Ibara ya 71 ya Katiba ya Kenya kuwa masuala ya madini lazima yaidhinishwe na Bunge kabla ya serikali kutia saini mkataba wowote ule.

Alisema pia Ibara ya 152 ya katiba hiyo kuwa inamtaka Rais kuchagua baraza la mawaziri nje ya bunge na wabunge watakuwa na kazi ya kukubali au kukataa uteuzi wake.


John Mnyika
Naye Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika, alionya kuwa iwapo viongozi walioingia madarakani kwa hila hawatabadilika, nchi inaweza kugeuka na kuwa kama Tunisia.

Joseph Mbilinyi (Sugu)
Kwa upande wake Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu Sugu aliyekuwa kivutia kikubwa katika kongamano hilo, aliwataka wanafunzi wa vyuo vikuu kusoma kwa bidii na kuja kuikomboa nchi.

Sugu ambaye alilazimishwa na wanachuo hao kuongoza kuimba wimbo wa taifa wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo, alisema amekuwa mstari wa mbele katika kupigia kelele matatizo yanayowakabili wanafunzi vyuoni na kuwasisitiza kusoma ili watumie elimu yao katika siasa za kweli na si propaganda.


Kutoka Dodoma, Israel Mgussi na Masoud Masasi wanaripoti kuwa,
Chadema mkoani Dodoma kimefanya maandamano ya amani kuunga mkono maandamano yaliyofanywa na chama hicho mkoani Arusha Januari 5, mwaka huu kupinga mchakato wa uchaguzi na matokeo ya Meya wa Jiji la Arusha.


Katika maandamano ya jana ambayo mamia ya wafuasi wa chama hicho walijitokeza Chadema ilitoa tamko la kulaani Jeshi la Polisi kwa madia kuwa linaendelea kuwakumbatia waovu wanaoitafuna nchi kwa kuwatisha na kuwaua raia wasiokuwa na hatia.


Mkurugenzi wa Oganizesheni na Mafunzo wa chama hicho taifa, Benson Singo Kigaila ambaye ndiye alipokea maandamano hayo katika Viwanja vya Barafu mjini hapa alisema Tanzania na nchi tajiri lakini inashindwa kuendelea kutokana kushamiri kwa ufisadi.


Alisema hata askari polisi ambao wamekuwa wakitumiwa na baadhi ya watu wasioitakia mema nchi, wamekuwa wakifanya hivyo kutokana na kutotambua umhimu wa ustawi wa taifa lao.


“Ndugu zangu, nchi hii mali yetu, hatujaikodisha,hatuwezi kuvumilia maovu yanayoendelea,uchaguzi wa Arusha lazima urejewe upya,l azima wananchi tuwe tayari kupigania uhuru wetu, tunafahamu hata maauaji yaliyotokea kule Arusha haikuwa bahati mbaya,”alisema Singo.


Katika maandamano hayo ambayo yalianzia ofisi za chama hicho mkoa kupitia Soko Kuu la Majengo,Hospitali ya Mkoa, Barabara ya Morogoro na kuishia Viwanja vya Barafu yaliongozwa na askari polisi waliokuwa wakilinda usalama.
 
Nimekuwa nikisikia watu mbalimbali wakiwemo wabunge, wanasiasa wasio wabunge, wanaharakati na makundi mengine ya kijamii yakipinga hadharani juu ya malipo ya Dowans. Sasa ni wakati wa kuondoa tofauiti zenu kiitikadi, kisiasa na kidini na kuunda kundi moja. Kundi litakalosema kwa sauti moja na sauti kubwa zaidi dhidi ya ubadhirifu huu. Kundi ambalo kwa kauli moja na rahisi itakuwa rahisi kuamua hatua za kuibana serikali dhidi ya wizi huu.

Kumbukeni hata kule Kenya walikuwa wanafanikiwa sana katika mambo kama haya kwa kuunda makundi bila kujali chama au dini ya mtu. Mnakumbuka wakati wa Katiba kielelezo, ilivyoundwa kundi la orange na kundi la banana?

Nawaasa akina Kafulila na wabunge wenzake, akina Slaa, akina Sitta (hapo najua itakuwa ngumu), wahadhiri maarufu, wanaharakati na watetezi wa haki za binadamu (akina Ananilea Nkya), viongozi wastaafu na watu wote wenye mapenzi mema, wakutane waunge kundi moja kwa ajili ya kupambana na uozo huu.
 
Wana JF,

Nadani hii ni njia nzuri na ya kizalendo. Wapenda nchi wote tunapaswa kuunganiha nguvu bilamkujali itikadi za vyama vyetu au tofauti zetu zingine zote. Sisi sote kwanza ni watanzania na hatuna kiunganishi kingine isipokuwa mama yetun mpenzi Tanzania. ikiharibiwa na wachache tutaumia sisi katika unyonge wetu. Ili jitihada yeyote isionekane kuwa ni la kundi ninashauri au NGO zinazokubalika na jamii nzima au Taasisi kama udsm au chombo chochote kunachoweza kujitokeza kuandaa forum hiyo ijitokeze na kwa muda mfupi tuijadili kuona kama inakubalika, hata hivyo:

1) Muda wa maneno umekwisha sasa yanatakiwa maamuzi magumu na hatua za kiutekelezaji, vinginevyo nchi itaendelea kwisha
2) maamuzi ya pamoja ya wadau wote yataondoa hofu yeyote ambayo kwa sasa inajitokeza kati ya kundi na kundi lingine. maamuzi ya pamoja ya makundi ni njia ya mkato ya kupata mawazo ya jamii nzima katika mudas mfupi unaowezekana.
3. Ndugu zangu, hoja ya Dowans imeficha maovu mengi sana katika jamii yetu. Utata unaoonyeshwa na DOWANS ni tip of the ICEBERG katika aina mbalimbali ya ufisadi iliyoko, Yanayojionyesha kwa mfano:
a) wakati hukumu ya mahakama ya kimataifa ya biashara imeelezwa kusajiliwa kwenye mahakama ya biashara, uchunguzi wetu unaonyesha kuwa hukumu hiyo haihjasajiliwa katika Registry ya mahaklama ya Biashara ya Tanzania. Badala yake Annexes chacheche ndizo zilizosajiliwa katika "normal Registry" ya High Court. Hii tafsiri yake nini na nani ana ghilibiwa. Ni kwanini mahakama imepokea tu annexes badala ya hukumu yenyewe kama inavyotakiwa na sheria?
b) Role ya Rex Attorneys hasa nini katika saga hii nzima? uhusiano ulioko katika mchakato wa kuishauri serikali kuuza mitambo ya Dowans na sasa Dowans ilipwe na taarifa kuwa Rex walikuwa wakipanga katika jengo la RA kabla ya kumaliza na kuhamia jengo lao unatia mashaka makubwa sana.
c) Tamko la UVCCM na KAMATI KUU ya CCM ambayo kwa nje yanaonekana kupingana yamebeba utata na maswali makubwa zaidi kuliko ambavyo haijawahi kutokea kabisa katika historia ya nchi hii. Ukizingatia kundi la RA lilishinda kumwondoa Spika na kumweka Spika aanayedhaniwa kwa wa "maslahi" kwao, jitihada za RA kurudisha mara kadhaa hoja ya Richmond Bungeni wakati wa Bunge la 9 na msukumo wa kulirejesha hoja hiyo Bungeni hasa toka UVCCM ni lazma utazamwe kwa jicho la makengeza na wote walio serious katika vita dhidi ya ufisadi.
d) Kitendo cha Serikali kuwa na kauli tofauti kwa kila msemaji, waziri wa fedha kutamka wazi kuwa Hazina haina fedha za kulipa, Rais kupitia Kamati Kuu (kitendo ambacho dhahiri ni kujificha nyuma ya Kamati Kuu na kukwepa au kushinikiza cabiniet kwani uamuzi huu si wa kisera). Hii ni hali ya hatari sana kwa mustakabali wa nchi na rasilimali zake.

Ni kwa misingi hii ninatoa mwito kwana JF na wana vikundi mbalimbali kama Wanabidii, NGO's na wote wanaokerwa kweli katika nafsi, mioyo na roho zao na ufisadi huu tuchukue hatua ya makusudi kuwa na mjadala wa jumla na kuwa na maamuzi ya hatua ya kiutendaji bila kuangalia au kujali chochite kile kinachotugawa au kutetenganisha au kututofautisha na wengine. Katika kutengana tutaPARANGANYIKA NA KUSHINDWA KATIKA KULINDFA TAIFA, RASILIMALI, NA TUNU ZA TAIFA LETU AMBAZO KILA KUKICHA ZINAENDELEA KUMOMONYOKA.

Nawashukuru sana.
 
Hili lifanyike Haraka kabla watanzania hawajasambaratishwa na ugumu wa maisha kwa ongezeko la bei ya mafuta na milipuko ya bei ya chakula na kutufanya kusahau dowans,katiba ,kwani njaa inaweza kukupotezea uwezo wa kufikiri na kupambanua hali ya taifa lako wakati familia inalia njaa
 
DR.tunaomba kuandamana maana tumechoka sana.plse tunaomba yawe maandamano ya INCHI NZIMA TANGANYIKA!PLSE TUPE MUONGOZO
 
Huku Sumaye akigusia kwa kifupi, kambi hiyo ndogo ya upinzani imetoa tamko katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam jana, ambalo Katibu wake David Kafulila, alisema kitendo cha Serikali kutaka kuilipa Dowans kabla suala hilo halijafikishwa bungeni ni sawa na kuchezea moto.

“Chimbuko la Dowans liliangusha Serikali madarakani, hivyo Serikali inatakiwa kutoa nafasi kwa sakata hili kwenda bungeni ili ieleze iweje kampuni ‘batili’ ilipwe kiasi hiki cha fedha,” alifafanua Kafulila, hatua ambayo itaiweka Serikali ya CCM katika ncha ya kisu.

Katibu huyo wa kambi hiyo ndogo, alifafanua kwamba ndani ya Serikali kila kiongozi ana mtazamo wake kuhusu malipo ya Dowans na kusisitiza, suala hilo linatakiwa kuchukuliwa kwa uzito mkubwa.

“Sakata la Dowans Tanzania ni sawa na ‘Goldenberg scandal’ iliyoangusha utawala wa chama cha Kanu nchini Kenya, kashfa hii ilianza mwaka 1993 na kumalizika 2002, Richmond na Dowans ilidumu tangu 2006 hadi sasa hakuna majibu,”alisema Kafulila Kafulila ambaye amewasilisha kusudio lake la kutaka kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhoji sababu zinazoifanya Serikali isiwajibike kwa kuliingizia taifa hasara ya mabilioni ya fedha kwenye sekta ya nishati, alisema Serikali ikipuuza suala la Dowans itapunguza uhalali wake wa kisiasa.

“Pamoja na kuwa kambi hii si rasmi, lakini hatuwezi kukaa kimya katika mambo ya msingi, Dowans ni suala ambalo haliwezi kuzimwa hivi hivi tu wakati ukweli haujajulikana, na kwambia CCM itang’oka madarakani sababu ya Dowans kama ikifanya mchezo, historia ya Kanu itawahukumu,” alisema Kafulila. Aliongeza kwamba, kama CCM hakitang'oka madarakani basi kuna uwezekano nchi ikakumbwa na machafuko.

“Dowans isilipwe mpaka sakata hili lifike bungeni na kupitishwa katika mkaa wa moto wa wabunge, wakilipuuza hili la malipo ya Sh94 bilioni basi wanaweza kupuuza hata malipo feki ya Sh100 bilioni,” alisema Kafulila.

Alifafanua, Dowans ikilipwa kabla ya kujadiliwa bungeni maana yake ni kwamba suala hilo litapanuka na kuongeza kuwa ikiwa hivyo, atawaomba wabunge wapige kura ya kutokuwa na imani na Serikali.

“Hivi hii nguvu na mbio kubwa za kuilipa Dowans zimetoka wapi, mbona malipo ya wastaafu wa EAC na walimu hayapewi kipaumbele, mimi hoja yangu imelenga zaidi hukumu ya ICC kuhusu kulipa Dowans kiasi hiki cha fedha,”alisisitiza Kafulila.

Alipoulizwa kwamba haoni kurudisha sakata la Dowans bungeni linaweza kuibua mengine kuhusu sakata la Richmond ambalo lilisababisha mawaziri kujiuzulu, Kafulila alisema; ...ninachokwenda kuhoji bungeni ni suala la hukumu ya ICC kuilipa Dowans, nataka maelezo katika hilo, najua kuna ambayo hayakusemwa katika ripoti ya Richmond iliyotolewa bungeni na ile kamati ya akina Mwakyembe, inawezekana yakaamka tena, hilo sijui, lakini likiwa hivyo atakayevuliwa nguo chafu na kuvalishwa safi ataonekana.
Source: Mwananchi

Watch out......
 
Dr. Slaa,

Asante sana kwa mchango wako muhimu na uliojaa mbolea. Umetumia hoja kuonesha njia tunayotakiwa kwenda. Sasa kuhusu hili la kuunganisha makundi mbalimbali, ni hoja yenye nguvu sana kwa sababu ni rahisi kuinyooshea mkono CHADEMA, kwa mfano, inapojitokeza sana, na pia kui-target. Lakini ni ngumu zaidi kupambana na muungano wa kada mbalimbali.

Pia hapo utaifa utakuwa wazi zaidi, maana tunapigania jambo la kitaifa. tunaanzia wapi?

Vyama kama CHADEMA vitafakari na kufanyia kazi hili. Vyama vingine pia viache kuangalia maslahi yao binafsi, viangalie mambo ya kitaifa zaidi. tatizo moja naliona sasa ni vyama kujaribu kudhoofishana, wanasahau kwamba kwa kufanya hivyo wanaipa nguvu CCM.

CHADEMA pia msifunge mlango kabisa kwa kushirikiana na vyama vingine.Onyesheni na kufanya "confidence building measures".

K wa upande wa wanaharakati, hawa wanaweza kuanza kwa kuitisha makongamano yanayoshirikisha vyama vyote, kama ilivyofanyika pale Nkrumah. lakini mada iwe mustakabali wa taifa letu. Vyama kama UDASA pia bado vina majukumu ya kufanya katika hili, bila kusahau Kigoda cha Mwalimu Nyerere, na wengine
 
a) wakati hukumu ya mahakama ya kimataifa ya biashara imeelezwa kusajiliwa kwenye mahakama ya biashara, uchunguzi wetu unaonyesha kuwa hukumu hiyo haihjasajiliwa katika Registry ya mahaklama ya Biashara ya Tanzania. Badala yake Annexes chacheche ndizo zilizosajiliwa katika "normal Registry" ya High Court. Hii tafsiri yake nini na nani ana ghilibiwa. Ni kwanini mahakama imepokea tu annexes badala ya hukumu yenyewe kama inavyotakiwa na sheria?

Kama hili ni kweli, suala hili linaelekea pabaya. Nikirudi kwenye hoja ya Tuko, ni Watanzania wachache sana, kama wapo, wanaomini kuwa Dowans inastaili hayo malipo. Almost every Tanzanian is against the payment. Fuatilia mazungumzo ya watu mitaani, vijiweni, maofisini, kwenye mitandao, sijaona mtu mtu anayesupport kuilipa Dowans except serikali. Hata serikali yenyewe imegawanyika juu ya hili suala.

Jitu ambacho kina-lack ni concrete action to stop the government making the payment. Kwa kweli we need to immediate action to stop the payment going through. Mahakama ikishaamua Dowan ilipwe, that is it.

Dr W. Slaa, kwa uzoefu wako bungeni, badala ya kusubiri mpka kikao kijacho, hivi hakuna kipengele chochote kwenye Katiba au sheria za Bunge, kinachoruhusu kunyanyika kwa emergency session bungeni juu ya suala la Dowan? Dowan is a national tragedy waiting to happen.
 
Mkuu sisi tuko tayari kwa maandamano ya nchi nzima, tunaomba maelekezo... mwezi uliopita nilikuwa Mbeya na Iringa kweli watu wako tayari.. hivi pia niko Dar pia same tunaomba for the first time nchi izizime kwa kudai haki zetu. Hatuna mwingine isipokuwa wewe kwani tunakuamini sana mkuu
 
Back
Top Bottom