Kizazi cha cha wanasiasa kama Nyerere, Karume na wenzao wengi waliweza kuhamashisha umma wa watanzania hasa vijana wa shule kuanzia waliokuwa ktk ngazi ya shule za msingi/ sekondari na vyuo vya elimu ya juu umuhimu wa uhuru wa kisiasa na kupambana na ukoloni mamboleo na ubeberu wa mataifa makubwa. Tujiulize ni vipi kipindi hiki sasa, wanasiasa wanaona wale wanaoeneza ukoloni mamboleo na ubeberu kuwa watatukomboa kiuchumi, kijamii na kisiasa? kwa kufungua milango ya 'uwekezaji' toka nje bila mipaka ya kizalendo!
Nyerere na wenzie walihakikisha nyimbo nyingi za kimapinduzi kama wimbo wa 'Bara La Afrika' wenye maneno ':
''Bara la Afrika lahitaji ukombozi,
Ukoloni ni mbaya na Ubaguzi wa rangi
Mataifa haya ya Ulaya ndiyo Afrika kuivamia
Wahenga wetu wa zamani walikataa ubeberu,
Walikataa ukoloni........
Hebu tusikilize wimbo huu wa vijana wa kutoka Bagamoyo walivyoguswa na nyimbo hizo za kimapinduzi za enzi hizo kuwa bara la Afrika lahitaji ukombozi na kuamua kuzipakua ktk youtube kama historia ya kuwa ubeberu upo hai ktk wimbo maarufu 'Bara la Afrika ( African Nation) :
Nyerere na wenzie walihakikisha nyimbo nyingi za kimapinduzi kama wimbo wa 'Bara La Afrika' wenye maneno ':
''Bara la Afrika lahitaji ukombozi,
Ukoloni ni mbaya na Ubaguzi wa rangi
Mataifa haya ya Ulaya ndiyo Afrika kuivamia
Wahenga wetu wa zamani walikataa ubeberu,
Walikataa ukoloni........
Hebu tusikilize wimbo huu wa vijana wa kutoka Bagamoyo walivyoguswa na nyimbo hizo za kimapinduzi za enzi hizo kuwa bara la Afrika lahitaji ukombozi na kuamua kuzipakua ktk youtube kama historia ya kuwa ubeberu upo hai ktk wimbo maarufu 'Bara la Afrika ( African Nation) :
Last edited by a moderator: