Ngomo
JF-Expert Member
- Oct 15, 2009
- 200
- 95
maisha ya kizazi cha sasa yapo hatarini kupoteza lugha tunazo zitumia. Ukiangalia kwa makini vijana wa sasa hawafahamu kuongea kwa ufasaha kiswahili, kiingereza, na hata lugha zetu za asili hawazijui. Na mbaya zaidi hata wabunge bungeni wamekuwa wakifanya makosa yale yale ya kuchanganya kiswahili na kiiengereza. Ukienda vijijini hata lugha zetu za asili hazitiliwi mkazo tena. Napendekeza kuwepo na sheria inayo kataza matumizi ya lugha mbili kwa wakati mmoja.