Kiwango cha ajira kwetu

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,502
19,341
Kwa vile nimekuwa mtu wa mitini mara nyingi, inawezekana kuwa jambo hili limekisha ongelewa hapa kijiweni. Najua kuwa mwaka jana tuliwahi kuwa na thread ya kutathmini utendaji wa serikali ya Mwungwana Kikwete lakini sikumbuki tuliishia wapi, na nilipojaribu kuitafuta sikufanikiwa kuipata.

Kumbukukumbu yangu kuhusu muundo wa serikali zetu tangu tupate uhuru siyo nzuri sana na nitashukuru sana kama kuna mtu atakayeweza kunikumbusha. Ninataka kuongelea swala la kazi na ajira. Mwanzoni baada ya uhuru kulikuwa na Wizara ya Kazi na Ustawi wa Jamii; baadaye ikaja Wizara ya Mawasiliano, Kazi na Ujenzi; na nadhani mwishoni kulikuwa na Wizara ya Kazi na Utumishi ingawa sina uhakika kuwa Mkapa alikuwa na wizara ya namna ipi kuhusu kazi. Wizara ya kazi ilikuwa na jukumu la kuhakikisha kuwa waajiriwa wote wanatendewa haki na matajiri wao.


Rasi Kikwete alipoingia madarakanai aliunda Wizara iliyokuwa na neno ajira na hilo ndilo jambo ninalotaka tulichambue. Wakati ule nilisema kuwa Col. Kikwete alikuwa anawadanganya walala hoi wanaohangaika kutafuta ajira; nikasema kuwa uingizaji wa msamiati "ajira" katika jina la mojawapo ya wizara zake ilikuwa ni namna ya kujikosha kuwa serikali yake itawashughulikia vijana kupata ajira, lakini hakukuwa na lolote bali danganya toto tu.


Sasa jana jioni nikiwa hapa Crystal City Marriott nilipata nafasi ya kusikiliza wimbo wa Nakaaya unaosema Mr. Politician na kilichonikuna ni pale dada huyu alipoongelea ile ahadi ya "ajira nje nje." Nikasema nikurudi kijiweni nitawaomba rafiki zangu tuliongelee tena,

Swali langu ni, je ni nini majukumu ya Wizara hii, na je unemployment rate ya Tanzania ikoje leo hiiu ukilinganisha na mwishoni mwa mwaka 2005? Uanajua kuwa nemployment ndilo tatizo la kwanza linaleta mabadiliko ya kisiasa katuka nyingi hapa duniani. Nadhani kuwa wazee wenzangu mnalikumbuka sana tatizo la unemployment pale Uingereza baada ya vita ya Forkalnds ambalo ndilo lilipekea kuundwa kwa bendi ya reggae ya UB-40 (yaani unemployment benefit form number 40) pamoja na mambo mengine. Wakai huo uzalendo ulisaida kulinda utawala wa Mama Chacha.

Je Wizara hiyo ya kazi na ajira inatoa huduma gani kwa watanzania wasiokuwa na ajira? je, inawalipa social security allowance au unemployment benefit yoyote ile, je inasimamia kuhakikisha kuwa ajira hazitolewi kwa watu nje wakati kuna atanzania wanazihitaji? Nimwahi kuruka na ATCL kutoka Dar kwenda Mwana wakati mhudumu mle ndani alikuwa m-South Africa, na sikuelewa kabisa kama kweli dada zetu hawajui kuhudumia ndani ya ndege zinazofanya domestic flights.
 
Kichuguu,

..hii hoja yako ni nzito sana na inahitaji kuchangiwa. lakini sasa hivi wananchi wamejikita zaidi ktk ufisadi.

..Hakuna allowance ya namna yeyote ile kwa watu waliokosa ajira Tanzania. Hata mafao ya waliopunguzwa kazi ni kitendawili kwa wananchi.

..nimesahau the exact number ya vijana wanaoingia kwenye work-force kila mwaka. lakini nakumbuka somewhere kwenye mijadala hii, kuna waliodai kwamba kutokana na ahadi za uchaguzi za Kikwete kuhusu ajira, come 2010 Tanzania itakuwa na surplus ya nafasi za kazi!!

..umegusia kuhusu wahudumu wa ndege toka South-Africa. hili suala hata mimi linanikera sana. sina matatizo na kuajiri daktari bingwa, mhadhiri chuo kikuu, mwalimu wa hesabu/kemia/fizikia toka india, au mwalimu wa kiingereza toka kenya. lakini napinga kabisa ku-import madereva, wahudumu wa hoteli na ndege, makarani wa benki, na kada nyingine zisizohitaji mafunzo ya muda mrefu.

..nadhani ifike mahali Bunge na serikali watamke kwamba ajira fulani fulani ni kwa ajili ya WAZAWA. vilevile ukiajiri mtu wa nje basi iwe ni kwa mkataba wa kuwa attached na Mtanzania atakayechukua nafasi yake. nadhani Saudi Arabia walitumia utaratibu kama huo walipotaifisha visima vya mafuta.

..hili suala la ajira kwa wa-Tanzania litakuja kuwa mwiba pale tutakaposaini mkataba wa FREE MOVEMENT OF LABOR na wenzetu wa Afrika Mashariki. sijasikia viongozi wakilijadili kwa kina suala hili.
 
Nikitumia takwimu zilizotolewa Tabora mwaka 2004 mbele ya dokta Shein (VP) kiwango cha watafuta ajira kwa mwaka ni karibu watu 400,000 hawa ni wale wanaokuwa wametoka na kumaliza shule kuanzia elimu ya sekondari mpaka chuo.

Hakuna suala nyeti kama masda ya ajira, serikali nyingi katika nchi zenye umakini zimeangushwa kwa kutotoa na kuvumbua ajira kwa wananchi.

Wakati wa uchaguzi hapa kwetu umma huwa hauko makini na suala la ajira kwa ilani za vyama, na wagombea kwa kulijua hili hutanguliza ng'ombe na pilau ili wasio na ajira wale na wafurahi kipindi cha uchaguzi.

Ajira pamoja na kuongelewa na JK bado haijaonekana kupatikana kwa kile kilichoitwa ajira milioni 1 kila mwaka na kinachoonekana sasa ni ajira za majaji ambao kwa upande wangu hatuwahitaji kwa wingi kama tunavyowahitaji mahakimu wasomi na wapigania haki za binadamu.



Ukosefu wa ajira ni kama bomu la saa
 
Huwezi kutoa "unemployment benefit" katika workforce ambayo robo tatu yake ni unemployed or underemployed.You simply cannot economically afford to do that.

You need to have adequate production to be able to afford such generous liberality.

What we need is some serious production, even work programs by the government.I am surprised some smart economist hasn't turned up a "win-win" scheme (as JK would have it). Wanafanya kazi gani hawa watu?
 
Kichuguu

JK nchi imemshinda anachoangalia ni share zake tu zinafanyaje huko kwa Sinclair et al. Once you are a president ni lazima uchukue maamuzi mazito yeye alisema ajira nje nje wakati anataka kuneemesha tumbo, lake hivi sasa hana lolote la maana maamuzi yake mengi anangojea ushauri kutoka kwa TAKUKURU, Kamati za Bunge n.k. Wengine anawachekea anawaambia wajirekebishe. Ati mwizi ajirekebishe. Absolutely SI.

Kinachostaabisha akipewa hizo taarifa anafungia mafaili kwenye kabati lake pale Magogoni na case closed. Tumepata rais.
 
Kama hiyo idara ya ajira haishughuliki na kuhakikisha kuwa watanzania wanapata ajira, na wale wasiokuwa na ajira wanasaidiwa, then kulikuwa hakuna haja ya kuundwa kwake. Idara pekee tuliyokuwa tunahitaji kwa muda huu ni ile ya Kazi ambayo ina majukumu ya kulinda maslahi baina ya waajiri na waajiriwa. Idara ya utumishi imekuwa inadhughulika na ajira na maslahi ya watumishi wa serikali.

Kikwete alituahidi ajira nje nje lakini nionavyo mimi nadhani ajira nyingi zimekuwa kwa watu wa nje wakati raia wetu wengi wakipewa kazi za kijungujiko.
 
viongozi wa tanzania wanaamini AJIRA ni issue inayojisolve automaticaly bila mikakati madhubuti.
utasikia kiongozi anabwabwaja kuwa mkutano wa Sullivan umetoa ajira kwa watanzania!!yaani clueless kabisa!ajira kwa kitu cha wiki?yanihakuna permanent startegies at all kwenye wizara namaeneo yanayosimamia workforce.
viongozi wetu hawajui kuwaajira hutengenezwa.kwa policies na planning madhubuti.shurti ziwe za longterm.sio zimamoto.

sidhani kama tatizo la ajira litapatiwa muafaka hivi karibuni kwa mipango hewa ya politicians
ni wakatimuafaka wananchi kuanza kuomba stratergic detailed plans ya ahadi za hawa wanasiasa wetu.
 
viongozi wetu hawajui kuwaajira hutengenezwa.kwa policies na planning madhubuti.shurti ziwe za longterm.sio zimamoto.
Yep!


Obe signature yako hapa chini, :)
Ngula: Unemployment definitely a time-bomb
2007-09-01 08:50:40
By David Mambo

The Secretary General of Trade Union Congress of Tanzania (TUCTA) Nestory Ngulla has expressed his concern over the overwhelming unemployment level, saying it`s a time bomb in need of concerted efforts to deal with.

According to Ngulla the rates of unemployment and underemployment are quite high, particularly amongst the youth, who lack voice in decision making bodies, making them vulnerable to social exclusion and poverty.

`We in the association would like to stress the need to provide every support to ensure that the implementation of these two programmes succeed in creating adequate jobs, especially for youth. Stakeholders must play their role with diligence to ensure that these programmes succeed,` he added.


Nani amewahi kusikia hizo programmes Ngula is talking about? Please share with us!
(National Employment Creation Programme, Employment Report and Youth Employment Action Plan)


.
 
Back
Top Bottom