Kiwanda cha kuassemble magari Tanzania...kitarudi kweli?

Ubungoubungo

JF-Expert Member
Jul 28, 2008
2,502
739
Jamaniee, Mungu atupe nini sisi watz? Kule Liganga kuna chuma ambayo tutaweza kuchimba kwa miaka hata mia, kule mchuchuma na mbinga kuna makaa ya mawe tunayoweza kuchimba kwa muda wa miaka hamsini. tunayo bahari kuingizia mashine na vito vinginge tusivyonavyo. makaa ya mawe kutengeneza umeme mwingi. gesi kutengeneza umeme na matumizi ya ndani. mafuta nayo kuna uwezekano mkubwa kuwepo.

zamani tulikuwa na kiwanda cha kuassemble magari kule kibaha(NYUMBU), si mnakumbuka magari ya nyumbu jamani? kiwanda kile kilikufa kifo cha mende(mende akifa kimgongo asipolalia kifua anaweza akaozea hapohapo). what makes us tzs kutokuhimiza kiwanda kipya cha magari hapa jamani? wakati chuma tunayo ya kumwaga. uranium kama ni kutengeneza umeme etc tunayo ya kumwaga hapa(in mbinga and around lake nyasa). wakenya wana assemble magari tayari, na sisi tunang'a macho tu. wakenya wangekuwa na resources hizi, wangekuwa mbali sana.

kama kuna kiongozi aliyeshika rungu humu(mimi sijashika rungu ndo maana sauti au impact yangu haiwezi kuwa kubwa kama ile ya watu tuliowapa dhamana), huko china,uturuki,japan etc mnakopeleka wanafunzi, basi pelekeni wanafunzi kwenye mambo ya technologia, ili wakirudi tuanzishe vitu vyetu.

Kuna kijana mmoja kule kanda ya ziwa alisoma Japan, akafanya field kule kwenye kampuni ya kutengeneza boat, kwasasa amerudi hapa bongo, anatengeneza boti nzuri na za kisasa kule ziwa victoria sana. yaani very good ship builder aisee. nina uchungu sana na nchi yangu kwakweli.
 
Last edited:
Haya mawazo makubwa ndugu,

Ingekuwa Rwanda Kagame angesema liwe na likawa..sasa Tz Uswahili mwingi!!!
 
Mkuu Ubungoubungo, unataka hayo yafanyike ili iweje?

Hili ni swali gani mkuu.hebu jipange uulize tena. ninataka ifanyike ili iweje? ina maana wewe hutaki kitu kama hicho kifanyike? kwa kifupi, inaniuma kuwa tulikuwa na nyumbu ikafa. tunazo maligafi zote tunazoweza kuzitumia kutengeneza vitu vyetu. hata trekta tu la kusukumwa na mikono tunaagiza nje. hakuna hata machine moja tunayotengeneza sisi wenyewe hapa tz au basi hata wawekezaji wafanye hayo hapa kwetu. kuna faida nyingi jambo kama hilo likitokea. shein alienda India wakamwahidi watakuja kuweka kiwanda cha kuassemble matrecta hapa. lakini kimyaaa. na hao wanaoenda japan na nchi zingine kutafuta wawekezaji, wanatafuta wawekezaji wa aina gani? wawekezaji wa kuja kuwekeza kwenye kilimo? ambacho hata sisi hapa tutawekeza? wawekezaji wa kuja kufuga ng'ombe wa kisasa ufugaji unaofundishwa secondary? au wa kuweka kiwanda cha maziwa kama kile cha kina uhuru kenyatta kule Arusha. tunataka uwekezaji ambao ni mkubwa, huu mdogo sisi wenyewe hapa ni wawekezaji. tunahitaji kununua au kuimport technologia iingie hapa ili tusiendelee kuwa watumwa wa bidhaa za nje.

leo hii tz inaogopa kujiunga na kenya, hakuna sababu nyingine, ila ni woga kwasababu kenya wanavyo viwanda vingi bora kuliko tz, wamewekeza kwenye elimu kuliko tz na ardhi yao ina value kubwa kuliko ardhi ya tz ndio maana yote imemilikiwa kama asset. sasa, watu kama wewe wanauliza swali kama hilo, vipi mzeee.
 
Mkuu Ubungoubungo, unataka hayo yafanyike ili iweje?


Wewe hauko tofauti na wabunge wa TZ. Manake wao ndio huwa wanapiga makofi au kubisha jambo wasilolijua kisa, limetoka kwa mtu ambaye ni/si mwana mtandao. Kama baadhi ya watu aggressive wasingeforce tuanze kuwa na internet facilities bongo, sidhani hata kama wewe ungekuwa unaisikia jamii forums. And as I remember, miaka ya 70 - 80 ukisikia internet ilikuwa ni mshangao. Achilia mbali, internet, hata TV stations, nafikiri utanielewa. Sasa swala la magari nalo ni jambo linalowezekana kama ilivyokuwa kwa TV Stations, Simu za Mikononi n.k. Si kubwa kama unavyofikiria, manake wabongo tuna kasumba ya kuogopa ukubwa wa jambo. Yaani hata ukimpelekea biashara ya maana, ataanza kushtuka, "hivi mimi nitaweza kweli"..!! Huu ni udhaifu walionao viongozi wetu, kiasi cha kupelekea kuiuza nchi kwa wageni, the same qn walianza nalo "hv sisi tutaweza kweli kuchimba madini" n.k.

Nakumbuka kuna mdau mmoja aliwahi kusema kuwa, "watanzania wengi hasa viongozi wanafikiri kwamba, kwa kuwa wao hawawezi, basi kila mtanzania hawezi". Something which is wrong.

Sasa hv cost za kuagiza gari plus clearing charges and plus wizi wa bandarini ni usumbufu na mateso tosha. Sasa ndugu unavyosema lifanyike ili iweje, unanishangaza kidogo. Unless utuambie kuwa huna dreams za kununua gari.
 
Wewe hauko tofauti na wabunge wa TZ. Manake wao ndio huwa wanapiga makofi au kubisha jambo wasilolijua kisa, limetoka kwa mtu ambaye ni/si mwana mtandao. Kama baadhi ya watu aggressive wasingeforce tuanze kuwa na internet facilities bongo, sidhani hata kama wewe ungekuwa unaisikia jamii forums. And as I remember, miaka ya 70 - 80 ukisikia internet ilikuwa ni mshangao. Achilia mbali, internet, hata TV stations, nafikiri utanielewa. Sasa swala la magari nalo ni jambo linalowezekana kama ilivyokuwa kwa TV Stations, Simu za Mikononi n.k. Si kubwa kama unavyofikiria, manake wabongo tuna kasumba ya kuogopa ukubwa wa jambo. Yaani hata ukimpelekea biashara ya maana, ataanza kushtuka, "hivi mimi nitaweza kweli"..!! Huu ni udhaifu walionao viongozi wetu, kiasi cha kupelekea kuiuza nchi kwa wageni, the same qn walianza nalo "hv sisi tutaweza kweli kuchimba madini" n.k.

Nakumbuka kuna mdau mmoja aliwahi kusema kuwa, "watanzania wengi hasa viongozi wanafikiri kwamba, kwa kuwa wao hawawezi, basi kila mtanzania hawezi". Something which is wrong.

Sasa hv cost za kuagiza gari plus clearing charges and plus wizi wa bandarini ni usumbufu na mateso tosha. Sasa ndugu unavyosema lifanyike ili iweje, unanishangaza kidogo. Unless utuambie kuwa huna dreams za kununua gari.

Asante mkuu kuelewesha huyu jamaa. nafikiri imefika kipindi watz tujaribu kusapoti vitu kama hivi. tunacho chuo cha inginia pake chuo kikuu cha dsm. vitu vingi vinavyotengenezwa pale ni vinu vya kusagia mahindi kijijini au mashine za kukata mbao kwa maselemala, majiko ya vigae na vitu kama hivyo. inawezekana watu wanayo knowledge lakini selikali haijajikita huko.

leo hivi wanafunzi wanaoongoza kwa wingi tz ni wanafunzi wa arts subjects, sio sayansi ya pyisikia wala biologia. tunao madaktari wachache, mainjinia wachache hata wale wa kusaidiana na wachina tu wachache. wanafunzi ndo wanazidi kukimbia masomo ya sayansi, kwasababu siasa imekuwa ni biashara. nchi zingine ukiambiwa mtu injinia, ni tajiri sana. lakini tz ukiambiwa mtu mwanasiasa, yaani ujue lazima amejilimbikizia. Mungu atusaidie tuamuke, tuweke kipaumbele kwenye sayansi zaidi kuliko siasa. tufanye mabadiliko yetu sisi wenyewe. tunaweza.
 
.
zamani tulikuwa na kiwanda cha kuassemble magari kule kibaha(NYUMBU), si mnakumbuka magari ya nyumbu jamani? kiwanda kile kilikufa kifo cha mende(mende akifa kimgongo asipolalia kifua anaweza akaozea hapohapo). what makes us tzs kutokuhimiza kiwanda kipya cha magari hapa jamani? wakati chuma tunayo ya kumwaga. uranium kama ni kutengeneza umeme etc tunayo ya kumwaga hapa(in mbinga and around lake nyasa). wakenya wana assemble magari tayari, na sisi tunang'a macho tu. wakenya wangekuwa na resources hizi, wangekuwa mbali sana.
.
Mkuu,

1. kiwanda cha ku-assemble magari(Scania)kiliitwa TAMCO.
2.Kwa (T.A.T.C)Kushindwa kwenda na kasi ya mabadiliko ya kitekinolojia, Ule mradi wa kutengeneza magari (nyumbu)kwa ajili ya matumizi ya Jeshi letu umesimama kwa sasa,ila kiwanda bado kinajishughulisha na uzalishaji wa vipuri na zana tofautiX2.
3.Wa-kenya walitengeneza gari dogo (sedan)wakaliita 'Uhuru' lakini halikuweza kumudu ushindani dhidi ya modeli kama subaru,toyota,n.k.

**Making Cars is more than just the raw materials,you will be suprised how much time&money companies like BMW and MERCEDEZ spend/invest on RESERCH only.
 
Twende moja baada ya jingine.... Nyumbu ilikufa au iliuawa?

iwe ilikufa au iliuawa, iwe na iliharibiwa na mtu wa hapa tz au wa nje hiyo haituhusu. ndio maana hata uongozi kila wakati unabadilika. leo hii kuna uongozi mpya, unaotakiwa kuwa na mawazo mapya. kama ilikufa hatuwezi kukata tamaa kuianzisha tena. kama iliuawa hatuwezi kutakishwa tamaa na walioiua, tutatafuta njia ya sisi wapya kuifufua. hivyo the issue is not kushindana kuona jinsi ilivyokufa au uawa hapa. the issue is, tunayo material yote ambayo tunaweza fanya kitu lakini hakuna muelekeo wa kuelekea huko. direction iliyopi sio hiyo kwa viongozi wetu. usiwe kama makabila mengine wanaofikiri hadi leo hii rais bado nyerere. mawazo ya mwaka 47 sio mawazo ya mwaka 2009 mkuu. toa supportive points sio kudiscourage. siajabu humu ndani kuna kina kikwete na wengine wengi, inaweza ikawa challenge kwao na wakaliweka kwenye kipaumbele ili uache kununua magari ya japan kwa bei kubwa, ili ununue matrekta ya hapahapa, ili hata baiskeli tu zitengenezwe hapahapa.
 
Mkuu,

1. kiwanda cha ku-assemble magari(Scania)kiliitwa TAMCO.
2.Kwa (T.A.T.C)Kushindwa kwenda na kasi ya mabadiliko ya kitekinolojia, Ule mradi wa kutengeneza magari (nyumbu)kwa ajili ya matumizi ya Jeshi letu umesimama kwa sasa,ila kiwanda bado kinajishughulisha na uzalishaji wa vipuri na zana tofautiX2.
3.Wa-kenya walitengeneza gari dogo (sedan)wakaliita 'Uhuru' lakini halikuweza kumudu ushindani dhidi ya modeli kama subaru,toyota,n.k.

**Making Cars is more than just the raw materials,you will be suprised how much time&money companies like BMW and MERCEDEZ spend/invest on RESERCH only.

Asante mkuu. ni kweli data hizo mimi sikuwa nazo, ila nilikuwa na data kwamba tz tulishawahi kuwa na vehicle assembling kama hiyo. asante kwa kuleta uelewa zaidi ili mjadala uwe bora hapa. sasa, kama wanatengeneza vipuri, kinachowashinda kutengeneza magari hata la kutembea 40km/hr tu nini? ndo tutadumu hivyohivyo na vipuri hadi mwisho wa dunia? mawaziri wanaohusika na mambo kama hayo wameplay role gani katika hili.

kwanza mi nashangaa, hivi tunachosubiri kuchimba chuma liganga ninini?na makaa ya mawe ninini? makaa ya mawe na chuma kingekuwa cha faida kwetu kuliko gold na almasi ambayo tunafaidika kwa macho tu hii. kwani kikwete anapospend milioni miatano kwa safari za nje, anaenda kufanya nini?kutangaza kuwa duniani kuna nchi inaitwa tz? au anaenda kutafuta watu watakaowekeza kwenye vitu kama vivyo? huko india kwa kina mital na wengine si nako angeenda, kwani nchi ni marekani tu?

huko china je?kwanini tusitumie maliasili tulizonazo effectively?...
 
tehetehete, mshikaji hii mada umeing'ang'ania sana, inaonekana una uchungu mkubwa sana na nchi yetu. nafikiri sisi sote inabidi tuwe kama wewe. Kuna siku tu Mungu atatujalia sisi wabongo kufanya mabadiliko. ile inahitajika bidii ya ziada, ili katika nchi yetu kuwe na uwajibikaji/accountability kwa viongozi wetu ya kiwango cha juu sana, na kiongozi yeyote kuanzia nyumba kumi hadi rais atakayepewa dhamana kutuongoza, awe na ari ya kufanya kitu cha ziada kitakachomfanya tumchague tena awamu ingine. GOD BLESS TANZANIA.
 
sasa, kama wanatengeneza vipuri, kinachowashinda kutengeneza magari hata la kutembea 40km/hr tu nini? ndo tutadumu hivyohivyo na vipuri hadi mwisho wa dunia? mawaziri wanaohusika na mambo kama hayo wameplay role gani katika hili.....huko china je?kwanini tusitumie maliasili tulizonazo effectively?...

...Mkuu, gari lipo! tena mwendo wake ni wa kasi tu zaidi ya hata hiyo 40km/hr.(Tembelea banda lao kipindi cha maonyesho ya SabaX2).
Kumbuka dhamira/ndoto ya Mwl.(R.I.P) juu ya Tanzania Automotive Technology Centre ilikuwa si kutengeneza magari haya ya 'nyumbu' tu bali zana tofautiX2 kukidhi haja/matumizi ya JWTZ,tatizo tulishindwa kwenda sambaX2 na mabadiliko ya kitekinolojia.
Mkuu,i suppose u'll side with me on the fact that; for any change in technology,reserch is absolute imminent.....sasa uwaambiye hao waswahili(mawaziri)eti wawekeze kwanza ktk utafiti ni kama kuwadhihaki vile...na hili si tu ktk magari bali kwenye nyanja za kilimo,afya,elimu...hatuna utamaduni wa kuwekeza ktk utafiti!
 
...Mkuu, gari lipo! tena mwendo wake ni wa kasi tu zaidi ya hata hiyo 40km/hr.(Tembelea banda lao kipindi cha maonyesho ya SabaX2).
Kumbuka dhamira/ndoto ya Mwl.(R.I.P) juu ya Tanzania Automotive Technology Centre ilikuwa si kutengeneza magari haya ya 'nyumbu' tu bali zana tofautiX2 kukidhi haja/matumizi ya JWTZ,tatizo tulishindwa kwenda sambaX2 na mabadiliko ya kitekinolojia.
Mkuu,i suppose u'll side with me on the fact that; for any change in technology,reserch is absolute imminent.....sasa uwaambiye hao waswahili(mawaziri)eti wawekeze kwanza ktk utafiti ni kama kuwadhihaki vile...na hili si tu ktk magari bali kwenye nyanja za kilimo,afya,elimu...hatuna utamaduni wa kuwekeza ktk utafiti!

hapo umeongea vyema. sasa ni wewe pia unao wajibu kuwaambia hao wahusika, sisi sote tunao wajibu kwani nchi ni yetu sote. twende mbele.
 
hao wachina watakubali wajenge kiwanda hapa badala ya sisi kununua magari toka kwenye viwanda vyao? inawezekana lakini, ila sina uhakika.
 
nyerere alishakufa. mimi namsapoti huyu jamaa aliyeleta mada. nyerere alishakufa, sisi bado tunaishi. kama nyerere alishindwa, sisi tunaweza. miaka ile sio miaka hii.
 
....manake wabongo tuna kasumba ya kuogopa ukubwa wa jambo. Yaani hata ukimpelekea biashara ya maana, ataanza kushtuka, "hivi mimi nitaweza kweli"

Lakini kumbuka kuwa huo mradi unaozungumziwa ni mkubwa na haukuogopwa maana ulitekelezwa lakini ulitushinda pamoja na kutooga kuutekeleza. Tatizo lako unasoma yanayoandikwa juu juu. Think bwana mkubwa, haya mambo si rahisi kama unavyodhani
 
Back
Top Bottom