Pantoni hiyo watu wanawahi kazinihii nini ndugu?
Na angawaachia mjazane hadi kivuko kuzidiwa na kuzama mngeleta lawama. ifike mahali watz wajali uhai wao sio watu wana behave kama wanyama,mnajua kabisa kivuko kidogo mnataka muende wote kwa wakati mmoja,mmezoea hivyo kwenye daladala na mabasi ya mikoani likipata ajali mnamlaumu dereva kwa kuwajaza kama mahindi kwenye gunia, hamjitambui??!!Kivuko ndio kilikua kinaondoka kigamboni, kivuko kikubwa kilikuwa kibovu hivyo kilibakia kile kidogo tu na muda huo wa asubuhi watu ni wengi sana.
kilichotokea kivuko kidogo kilivyofika watu wakaanza kuingia kwenye kivuko, dereva wa pantoni alivyoona kivuko kimejaa na watu wanaendelea kuingia, akaamua kuondoa kivuko bila ya kutoa taadhali yoyote aidha kupiga honi au kutoa matangazo. wakati ametoa ule mlango aliuinua juu, sasa lilivyosogea na watu wengi bado wapo mlangoni ulizidiwa mlango ukashuka watu ndio wakaingia majini, vilio vikatawala na taharuki kubwa ikatokea! Cha ajabu yeye aliendelea na safari watu ikabidi wasukumane kuelekea ndani kujinusuru na ndio ikawa salama kwao.
pamoja na vivuko vibovu lakini dereva wa leo alifanya kosa kubwa sana la kucheza na maisha ya watu. wahusika wamchulie hatua kali
Unaongea wewe....Wasiwasi wenu tu wakati maji ya hapo Kigamboni ni madogo sana na kina chake hakizidi tumboni. Owoga wenu tu!
Unaongea wewe....
Sio kuishi Kigamboni tu.Inabidi mtu ukiishi kigamboni ujifunze kuogelea
so,so,so ndio nini sasa hiki ,kwani ukitumia Kiswahili hutaelewekatatizo watu wanasogeaga mbele kikikaribia kufika so uzito na COE vinahama na engine hazina nguvu wakati mwingine iko moja so lazma kipoteze mwelekeo,,wakati mwingine mwendeshaji anawalowesha makusudi kuwasogeza nyuma
unapajua kigamboni lakini, nikusaidie tu, kwa d'salaam hiyo ni "one of the best place to reside evernakumbuka jamaa yangu aliniambia kujenga kigamboni ni sawa na kujenga kwenye hifadhi ya barabara,na sasa naona kigamboni ni eneo hatarishi kuliko hata jangwani
Licha ya kukanyagana kingeweza fyeka miguu yao kwa wale walio sloo kama kilikuwa kinajaribu kupaki.Watu wanaweza kuuana kwa kukanyagana tu sababu ya HOFU. Naona kilikuwa kimefika kabisa!
Mida mingine paniki ndip inaua watu, sasa hapo kulikuwa na haja gani ya kupaniki, mbona kipo ktk gati kabisa?
Ni kweli aisee!Licha ya kukanyagana kingeweza fyeka miguu yao kwa wale walio sloo kama kilikuwa kinajaribu kupaki.
Mpaka watu wazame kwenye maji na kufa huyo Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ndio atachukuwa hatuwa. yaani hiyo nchi yetu inaongozwa na Viongozi wasanii kweli ni hatari sana mtu kuishi Kigamboni unahatarisha usalama wako poleni sana Mliopatwa na mkasa wa kutaka kivuko kizame.Kivuko cha MV Magogoni kupata hitirafu, kumepoteza mwelekeo na kuacha njia yake hali ilozua taharuki kwa abiria.
Vilio na kelele zilisikika pale maji yalipoanza kupanda ndani ya kivuko.
Hali hiyo ilisababisha abiria waanze kujitosa ndani ya maji kwa wale wanaojua kuogelea. Hakika watu wa Kigamboni wanatembea roho mkononi.
Poleni kwa wote Mliofikwa na mkasa huu
View attachment 322468 View attachment 322469 View attachment 322470
Serikali Iwasaidie watu wa Kigamboni, hii si mara ya kwanza, mara nyingi huwa wanasaidiwa na Wanajeshi(Jeshi la majini la pale Kigamboni.
Serikali ilinunua Kivuko cha Kwenda Bagamoyo wakati hapa Dar tu tabu.
Natumia nafasi hii Kuwaomba wanajeshi wetu waende pale kigamboni kutoa msaada kwani leo abiria ni wengi na wengine hawajui watavuka saa ngapi.
View attachment 322475 View attachment 322476
==================
Updates;
Mbunge wa jimbo la Kigamboni Dr. Faustine Ndugulile, alishamwandikia barua, Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kuhusu hili titizo. Haya hapa chini ni Maelezo yake ambayo ameyaweka kwenye hii thread.
Bonyeza hapa
Wengine tumekulia kusikokuwa na mabwawa wala mito.Sio kuishi Kigamboni tu.
Mtu unatakiwa ujue kukoga, iwe ni sehemu ya maisha yako.
Sie wengine kukoga tokea wadogo maji tunayaweza