Kivuko cha MV Magogoni chapoteza mwelekeo, abiria wajitosa majini

nini kilitokea hasa? ina maana kivuko kilikuwa overloaded mpaka mlango ukataka kuzama au? ila mara nyingi nikiangalia tabia za abiria wa pantoni nashangaa sana.
Mimi sikuwepo.

Lakini sijawahi kuona ferry imeanza kuondoka na watu mlangoni hivyo . Tunakagaaga masaa kusubiri watu wasukumane sukumane wengine waamue kushuka.

Naona leo captain aliamua awaonyeshe
 
images

Mbona kama lishakamilika..
 
Poleni sana wote mliopata huo mkasa serikali imeshapewa taarifa hakuna hatua zilichukuliwa
 
Mimi sikuwepo.

Lakini sijawahi kuona ferry imeanza kuondoka na watu mlangoni hivyo . Tunakagaaga masaa kusubiri watu wasukumane sukumane wengine waamue kushuka.

Naona leo captain aliamua awaonyeshe
Ok.............
 
Kuna jamaa humu JF alidai daraja la kigamboni halina. maana!hii nchi ni mabingwa wa kukosoa juhudi za serikali za JPM!
Mkuu huyo alikuwa anamkashifu kikwetu kwa kujenga daraja lisilokuwa na maana yoyote na sio magufuli


Cc: Big boss
 
NAULI YA KIVUKO IONGEZWE.WANAVUKA WATU WENGI WASIO NA SAFARI MUHIMU.WATU 10 HUENDA HOSP KUONA MGONJWA MMOJA.MWINGINE HUVUKA AKANUNUE SIGARA UPANDE WA PILI
 
Mkuu katika hali ya uwiano kuhusu usalama wa abiria anayepanda chombo chochote kinachosafirisha watu baharini ,ziwani au kwenye mito ni vizuri abiria wavae maboya ya usalama kabla ya kupanda vyombo hivi ili ikitokea suala kama hili ni rahisi kwao kuokolewa ata kama hawajui kuogelea ,lile boya au life Jacket ni muhimu sana kwa abiria kuvaa muda wote wa safari za majini,lakini tofauti na vyombo vingi uwa abiria wanapopanda hivi vyombo hawapewi kuvaa kabla ya safari kuanza tunaomba vyombo husika kuzingatia hili naamini wale watu wenye taaluma ya mambo haya watasaidia kutoa elimu kwa wamiliki wa vyombo ili wazingatie usalama wa abiria kabla ya safari kuanza wapewe Life Jacket wavae kwanza sio kusubiri mpaka ajali kama hizi zitokee ndio tuchukue hatua.
 
Kivuko cha MV Magogoni kupata hitirafu, kumepoteza mwelekeo na kuacha njia yake hali ilozua taharuki kwa abiria.

Vilio na kelele zilisikika pale maji yalipoanza kupanda ndani ya kivuko.

Hali hiyo ilisababisha abiria waanze kujitosa ndani ya maji kwa wale wanaojua kuogelea. Hakika watu wa Kigamboni wanatembea roho mkononi.

Poleni kwa wote Mliofikwa na mkasa huu
View attachment 322468 View attachment 322469 View attachment 322470
Serikali Iwasaidie watu wa Kigamboni, hii si mara ya kwanza, mara nyingi huwa wanasaidiwa na Wanajeshi(Jeshi la majini la pale Kigamboni.

Serikali ilinunua Kivuko cha Kwenda Bagamoyo wakati hapa Dar tu tabu.

Natumia nafasi hii Kuwaomba wanajeshi wetu waende pale kigamboni kutoa msaada kwani leo abiria ni wengi na wengine hawajui watavuka saa ngapi.
View attachment 322475 View attachment 322476

==================

Updates;

Mbunge wa jimbo la Kigamboni Dr. Faustine Ndugulile, alishamwandikia barua, Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kuhusu hili titizo. Haya hapa chini ni Maelezo yake ambayo ameyaweka kwenye hii thread.

Bonyeza hapa
Nikiwa ni mmoja kati ya watu walio shuhudia tukio hili la leo alhamisi asubui tarehe 11/02/2016 tukio lililo tokea kwa uzembe wa utawala na uongozi wa vivuko vya kigamboni.
Nikiwa mmoja wa mwathiliwa nimeshuhudia dhaili kuwa dereva akiforce kuondoa kivuko pasipo utalatibu wala ishara na kuwafanya watu nusura wazame katika maji,
tunaomba selikari iboreshe huduma za vivuko na kuwafukuza watumishi wasio waadilifu na wasio jari maisha ya watanzania wenzao na kukosa uelewa wa kuona nini hatima yake kwa mazoea haya ya kutokujari abiria wanapo panda vivuko hivyo ikiwemo wakina mama,watoto wa shule,wazee vijana na wengine ni walemavu.
sio busara kabisa watu waje kufa katika maji alafu ndio tusikie mnafanya jitiada za kuboresha vivuko huo utakuwa ni unafiki.huduma ni mbovu acheni siasa katika sehemu hatalishi zilizo zungukwa na maji yenye kina kilefu hizi ni roho za watu.
View attachment 322512 View attachment 322511 View attachment 322510
Hiko kivuko kilisumbua tangu asubuhi. Fundi alizamia akidai kuondoa uchafu hata hivyo engine ilisua sua sana
 
Kivuko ndio kilikua kinaondoka kigamboni, kivuko kikubwa kilikuwa kibovu hivyo kilibakia kile kidogo tu na muda huo wa asubuhi watu ni wengi sana.
kilichotokea kivuko kidogo kilivyofika watu wakaanza kuingia kwenye kivuko, dereva wa pantoni alivyoona kivuko kimejaa na watu wanaendelea kuingia, akaamua kuondoa kivuko bila ya kutoa taadhali yoyote aidha kupiga honi au kutoa matangazo. wakati ametoa ule mlango aliuinua juu, sasa lilivyosogea na watu wengi bado wapo mlangoni ulizidiwa mlango ukashuka watu ndio wakaingia majini, vilio vikatawala na taharuki kubwa ikatokea! Cha ajabu yeye aliendelea na safari watu ikabidi wasukumane kuelekea ndani kujinusuru na ndio ikawa salama kwao.
pamoja na vivuko vibovu lakini dereva wa leo alifanya kosa kubwa sana la kucheza na maisha ya watu. wahusika wamchulie hatua kali
 
Back
Top Bottom