Kituo cha Polisi cha Mugumu chavamiwa!

Taarifa zilizotufikia punde zinasema kuwa wananchi wenye hasira wakiwa na silaha za jadi, wamevamia kituo cha polisi mjini Mugumu wakishinikiza kuwahukumu watuhumiwa wa mauaji!kweli hawa makurya hawana imani na polisi. Mh Vuai ameligusia hili kupitia taarifa ya habari ya ITV. Je wananchi kujichukulia sheria mikononi ni matokeo ya wananchi kutokuwa na imani na CCM

attachment.php


attachment.php


attachment.php


attachment.php


Source: Mdau -Mugumu

Kwanza: hakuna kabila linaloitwa MAKURYA kama ulivyoandika hapo juu. Wilaya ya Serengeti kuna watu wa makabila mbalimbali wakiwemo wachaga, wajita, wajaluo, wangoreme, wahehe, wamakonde, wanata, wasukuma, wanyamwezi na makabila mengine mengi tu. Hivyo ni makosa kuwajumuisha watu wote wa Mugumu kuwa ni MAKURYA. Ni vyema ungetumia neno WANANCHI au WAKAZI wa MUGUMU. Kwa ufupi sikutarajia matumizi ya ukabila wa kiwango hiki kwa "Great Thinker" kama wewe.

Pili: suala la wananchi kutokuwa na imani na jeshi la polisi ni la kitaifa na halina uhusiano na watu wa kabila moja peke yake. Hata hapa Dar es salaam, penye watu wa makabila yote ya Tanzania, vibaka wanachomwa moto kwa sababu ya wananchi kutokuwa na imani na mfumo mzima wa kutoa haki wakiwemo jeshi la polisi, idara ya mahakama, ofisi ya mwendesha mashtaka wa serikali, ofisi ya mwanasheria wa serikali na jeshi la magereza magereza.

Tatu: suala wananchi kujichukulia sheria mkononi lina sura nyingi. Kubwa ni kutokuwa na imani na mfumo wa kisheria wa nchi. Ni kwa kiasi gani hawana imani na CCM siyo rahisi kujua kwa sasa hasa ukizingatia kuwa CCM ni chama tawala na kimeshinda uchaguzi mkuu muda siyo mrefu uliopita. Na kama sikosei wilaya ya Serengeti ni moja ya wilaya ambazo CCM ilishinda kwa kishindo.

Kwa mtazamo wangu wananchi wengi bado hawajaweza kuhusianisha ubovu wa mfumo wa sheria za nchi na uwepo wa CCM madarakani kama chama tawala.
 
Jamani kwa hili kweli wananchi walichokifanya si cha busara.Mimi nilikuwa safarini wilayani Serengeti nilifika eneo la tukio kituoni kulikuwa na askari wachache pia gari la polisi halikuwepo kituoni walikuwa kwenye msafara wa NW wa TAMISEMI Agrrey Mwanli.Ilibidi gari la polisi likatishe safari kwenye msafara wa NW lirudi kituoni kuja kuongeza nguvu kuwasambaratisha hao wananchi waliokuwa wamekivamia kituo. Hakika kwa jinsi wananchi walivyokuwa na jazba gari la polisi lingechelewa kwa dk kama kumi uharibifu mkubwa ungetokea

Unaona sasa hapa ndipo penye shida kubwa sana na nyie watu wa polisi.

Wananchi walikuwa wamekusanyika kituo cha polisi wakiendelea na mazungumzo na askari waliokuwepo kituoni na hakukuwa na fujo yoyote zaidi ya baadhi yao kupiga kelele za kuwataka wauaji. Hilo gari lilipofika tu kituoni hawakutaka kuuliza kinachoendelea, wao walianza moja kwa moja kushambulia wananchi kwa risasi za moto. Kama wananchi wangekuwa wamekusudia kufanya uhalifu, muda wote wako hapo kituoni karibia saa nzima si wangeshatekeleza huo uhalifu ama uharibifu?? halafu wewe unadanganya eti wangechelewa dakika kumi tu wangekuta hali ni mbaya, hebu kuwa mkweli katika hili.Tatizo la msingi hapa ni polisi kujigeuza mahakimu na majaji, kituo cha polisi mugumu kimegeuzwa kuwa mahakama, hili jambo halikubaliki kwa namna yoyote ile.
 
Kwanza: hakuna kabila linaloitwa MAKURYA kama ulivyoandika hapo juu. Wilaya ya Serengeti kuna watu wa makabila mbalimbali wakiwemo wachaga, wajita, wajaluo, wangoreme, wahehe, wamakonde, wanata, wasukuma, wanyamwezi na makabila mengine mengi tu. Hivyo ni makosa kuwajumuisha watu wote wa Mugumu kuwa ni MAKURYA. Ni vyema ungetumia neno WANANCHI au WAKAZI wa MUGUMU. Kwa ufupi sikutarajia matumizi ya ukabila wa kiwango hiki kwa "Great Thinker" kama wewe.

Pili: suala la wananchi kutokuwa na imani na jeshi la polisi ni la kitaifa na halina uhusiano na watu wa kabila moja peke yake. Hata hapa Dar es salaam, penye watu wa makabila yote ya Tanzania, vibaka wanachomwa moto kwa sababu ya wananchi kutokuwa na imani na mfumo mzima wa kutoa haki wakiwemo jeshi la polisi, idara ya mahakama, ofisi ya mwendesha mashtaka wa serikali, ofisi ya mwanasheria wa serikali na jeshi la magereza magereza.

Tatu: suala wananchi kujichukulia sheria mkononi lina sura nyingi. Kubwa ni kutokuwa na imani na mfumo wa kisheria wa nchi. Ni kwa kiasi gani hawana imani na CCM siyo rahisi kujua kwa sasa hasa ukizingatia kuwa CCM ni chama tawala na kimeshinda uchaguzi mkuu muda siyo mrefu uliopita. Na kama sikosei wilaya ya Serengeti ni moja ya wilaya ambazo CCM ilishinda kwa kishindo.

Kwa mtazamo wangu wananchi wengi bado hawajaweza kuhusianisha ubovu wa mfumo wa sheria za nchi na uwepo wa CCM madarakani kama chama tawala.


Tata ogambere buya!!

Labda nikusaidie tu kidogo kwamba, CCM hawakushinda kwa kishindo serengeti bali walichakachua kwa kishindo!!

Siasa za serengeti kama wewe ni mkaazi ama mwenyeji wa huko utakuwa unazielewa sana, kuna rafu nyingi sana zilichezwa kuanzia kwa mkurugenzi wa halmashauri ambaye ndiye alikuwa msimamizi wa uchaguzi hadi jeshi la polisi na uongozi wa ccm taifa, mkoa na wilaya.
Unafahamu kwamba jk alipofika mugumu na kugundua hali mbaya ya mgombea wao alitoa maagizo kwamba viongozi wa wilaya hadi taifa wahakikishe kebwe anashinda, akishindwa wajue hawana kazi,sasa hapo unategemea mkurugenzi na vyombo vingine husika visingehakikisha ccm inachakachua kwa kishindo ili kulinda ujira wao??
 
wanasihasa ndo nini?attation ndo nini? hivi si muwe mnaandikia tu kiswahili?? shukle za kata hizi zimeleta mambo sana khaaaa..halafu manalaumu oooh mitihani ya NECTA migumu mtafaulu vipi kama hiki ndo kiingereza chenu...
sasa mbona unamkosoa mwenzako wakati na we unakosea,SHUKLE ndo nini?MANALAUMU ndo nini?
 
Kiukweli taarifa hii imenisikitisha,wakati watu wanapambana na jeshi la polic iwe inatenda haki kwa raia na pia nguvu zitumike kuwaelimisha wananchi wasichukue sheria mkono,kama picha inavyojieleza wapo karibia wananchi 30 na mikuki,mapanga na marungu,kituo kiujumla kinaweza kuwa na askari wapatao kumi na kuendelea,wanapokuja na virungu kuwadai watuhumiwa badala ya kushinikiza wapelekwe mahakani kwenye haki,unategemea kutatokea nn kama askar aliyefunzwa vizuri na mkononi ana smg yenye lisasi 30?kwa matukio kama haya kulaumu jeshi la police naona kama hatulitendei haki,wakirusha mikuki kuzuri jeshi lenye silaha ya moto wasijibu mapigo?na nn maana ya kujihami?tuwaelimishe wananchi kutochukua sheria mkono na upande wa pili tulielimishe jeshi letu litende haki,kwani haki ndio msingi wa kila kitu
 
Teh teh teh teh
Hizo mishale zinanikumbusha kipindi cha dulilo na kotoreja pia kutemya.

Kufuatilia wasambo usiku kucha. Ikipigwa dulilo, hata kama wametenga msosi homu ulitakiwa kuucha na kuelekea eneo la tukio. Vilevile kuna 'mwanho'. Hata kama ni saa nane usiku utatoka tu. Kweli Ujamaa ni mzuri.
 
Basi kuna wanasihasa fulani watanunua hiyo kesi wanapenda kweli kuseek attation kwa gharama yoyote kaaazi kweli kweli

Acha mambo ya Tanzania na Watanzania wenyewe wayamalize. Mbona sisi hatuingilii mambo yenu kule Gujarati mnapouana!
 
kikwete si ukabidhi tu nchi kwa dr wa ukweli slaa make naona mbeleni ni giza totoro
 
Kiukweli taarifa hii imenisikitisha,wakati watu wanapambana na jeshi la polic iwe inatenda haki kwa raia na pia nguvu zitumike kuwaelimisha wananchi wasichukue sheria mkono,kama picha inavyojieleza wapo karibia wananchi 30 na mikuki,mapanga na marungu,kituo kiujumla kinaweza kuwa na askari wapatao kumi na kuendelea,wanapokuja na virungu kuwadai watuhumiwa badala ya kushinikiza wapelekwe mahakani kwenye haki,unategemea kutatokea nn kama askar aliyefunzwa vizuri na mkononi ana smg yenye lisasi 30?kwa matukio kama haya kulaumu jeshi la police naona kama hatulitendei haki,wakirusha mikuki kuzuri jeshi lenye silaha ya moto wasijibu mapigo?na nn maana ya kujihami?tuwaelimishe wananchi kutochukua sheria mkono na upande wa pili tulielimishe jeshi letu litende haki,kwani haki ndio msingi wa kila kitu

Jeshi la polisi ni lakulaumiwa 100%. Hawa watu wangeonyesha mfano kwanza then response ya wananchi ingekua tofauti. Binadamu wakawaida anapokwenda kum-confront mwenzie anapima akilini kwake reaction ya mwenzie itakua vipi. Mara nyingi kama unayekwenda kukutana naye ni mtu anayetumia nguvu zaidi badala ya hoja na wewe vile vile unajiaandaa kinguvu nguvu; the opposite is always true. Nimeshaudhuria semina mbali mbali majaji na mawakili wanazotoa kwa polisi, jeshi (vyombo vya dola) kuhusu utumiaji wa nguvu kupita kiasi, haki za mshtakiwa etc. It is so sad maana NGO's zinapoteza hela kuwalipa hawa watu posho yakuja kwenye semina alafu hawajifunzi chochote. Hii yote ni kwasababu viongozi walionao (kutoka ngazi za juu) wamewafundisha ku-jichukulia sheria mikononi hivyo wanachojifunza ni zero. Wananchi wameshawasoma polisi na wao wana-respond hivyo hivyo. Shame shame shame!
 
Jamani kama great thinkers mbona sijaona mjadala unaofanana na sisi kwenye hoja hii?

Inabidi sisi tuone picha na tuzisome beyond maandishi huko ndiko tunakotakiwa tuibue mijadala.
Wakuu lets move the forum to that level and keep it there. (i dont mean we should be too seriuos but at times we should try to reflect the name )

for me i see- DESPAIRED PEOPLE WHO HAVE LITTLE TRUST TO THE RULE OF LAW!!

DO U ALSO SEE THAT? WHY IS THIS SO?

NAOMBA KUWASILISHA:pound:
 
Sintoshangaa nikisikia kuwa Mkoa wa Mara wameamua kujitenga na kuanzisha Serikali yao...
Manake huu Mserikali wa Kikwete hauna maana yeyote kwa wananchi wake...
 
Back
Top Bottom