Usisogelee wala kushika bulb ya namna hiyo, piga simu tanesco
Hilo linawezekana endapo switch ikiwa inatatizo
kuna leakage current , earthing sio nzuri.
maji ya mvua yalikuwa yanachirizika ndani ya switch na kuisababisha kuunga(on) mkondo na taa kuwaka,mchiriziko ukikata switch inakata mkondo(off) na taa inazima,kitendo kinaendana na kasi ya mchiriziko wa maji ya mvua.
maji ya mvua yalikuwa yanachirizika ndani ya switch na kuisababisha kuunga(on) mkondo na taa kuwaka,mchiriziko ukikata switch inakata mkondo(off) na taa inazima,kitendo kinaendana na kasi ya mchiriziko wa maji ya mvua.
May be!!
Kwetu kuna mabanda ya uwani sasa mvua ikipiga ukutani circuit breaker inakata umeme nyumba nzima je hili nalo husababishwa na nini?
baadhi ya umeme unaopaswa kurudia njia ya circuit breaker unakatisha njia ya ukutani kukamilisha mkondo aridhini(earth leakage)kwa njia ya maji ya mvua yaliyopenya katika sehemu uchi(bare) ya mfumo wa umeme vibandani.breaker hiyo ni nzuri kwa matumizi.
Pia radi huwa inasababisha kitu kama hicho, kuna wakati nilikuwa nafanya kazi mikoa ya Kagera wakati wa mvua kuna radi sana, tena zile za nguvu,kuna wakati hata mvua hainyeshi inapiga radi kubwa na generator kubwa iliyokuwa ofisini kwetu inajiwasha yenyewe na wakati mwingine hata jenerator isipojiwasha taa zinawaka na kuzima na hapo ni wakati wa ule mwanga mkali kabla ya ule mngurumo mkubwa wa radi.
Sijui umeme wa radi huwa unajiungaje hapo na kuswitch on generator.