Chatu ingawa sijamla mla nimewahi kumchuna ngozi ana nyama mzuri tu na hana sumu, pia taarifa nilizonazo nyama yake ni tamu so ni poa. Pia ikumbukwe binadamu hapa duniani ana kitu kimoja kikuu kinachofanana ambacho ni kula vyote vinavyomzunguka visivyo sumu kwake. Hakuna haya ya kushangaa! Mkunga, Kamongo ni nyoka wa majini; wanaliwa, kwa nini chatu siliwe? Huo ni mfano mmoja tu. Pia ifahamike kwamba njia moja nzuri ya kuangamiza viumbe wengine waharibifu na waletao madhara kwa jamii ni KUWALA. Jimbo moja nchini India waliwahi kuhamasisha wakazi wao kula PANYA (ambae walidai ana nutrition benefits nyingi ikiwamo kuongeza hamasa ya kujamiiana) kwa vile walileta uharibifu mkubwa.
Mkuu nini tena unataka kunitafunachatudume