Kitine: Nchi sasa yaongozwa kienyeji

Gentlemen (and Ladies) wa JF lets try not to get too personal on these discussions, we will lose the context.When it gets too personal wengine inakuwa vigumu kuchangia!

We hang the petty thieves and appoint the great ones to public office-Mwiba

- Mkuu wangu Lole, sisi wananchi wote wa Tanzania hatujalala kiasi hicho cha kutoelewa maana ya sheria zetu, kuhusu mapungufu ya kibinadam na wizi, mwizi anatakiwa kwenye sheria sio kwenye majukwaa ya siasa na waandishi wa habari,

- ndio maana taifa letu limedumaaa, kwamba kiongozi akiiba eti ni mapungufu tu kama ya viongozi wengine waasherati, lakini tumsikilize anachosema anyways bila kujali wizi wake, kweli hii ina make a sense kwako? I mean kwangu it does not kwa sababu ni watu kama Kitine, Mwalimu aliwatayarisha kwa makusudi ili baadaye akiwa hayupo waje simamia maadili ya uongozi wa taifa letu. Ninaijua siri yote ya Mwalimu kuwapeleka Kitine na wenzake wengine wengi ambao hawatajwi nje ya taifa letu wakati ana-retire, moja ya sababu zake ilikuwa kwamba one day mambo yakitaka kuharibika katika uongozi wetu warudi haraka sana tena by anymeans necessary kuliokoa taifa letu kama litapotea njia za maadili ya uongozi wa Mwalimu, halafu huyu anajua siri zote zilizolifanya taifa letu kwenda mrama sasa kama kweli anataka mabadiliko aseme yote, lakini sio hadithi za bulicheka!
 
Last edited by a moderator:
Inabidi viongozi wa miaka hiyo wapewe madaraka tena ili nchi irudi katika line iliyovyooka
 
Tunahitaji wazee kama akina Kitine wasimame kukekea wazi kabisa maovu yote ya CCM, na la zaidi ni kwamba wajitokeze mwaka 2010 ili wachaguliwe kuiongoza nchi iliyo kwenye 'auto-pilot'. Hatuna haja ya kusuburi 2015 tena.
 
Mambo ya kuchagua viongozi kwa kuangalia sura na siyo ufanisi inatutupa pabaya sasa. Haya handsome ndo huyoooooo!

Wengi wanaoijua Tanzania wanaionea huruma sasa hivi. Mpaka lini???
 
Anachosema Mzee Kitine kuhusu nchi kuongozwa kienyeji ni kweli kabisa. Viongozi wengi wamekuwa wababaishaji mno na sijui wamepata vipi huo uongozi. Wanapenda mno uongo kwa sisi wadanganyika!!! Hivi hatuna namna ya kujua watu kabla ya kupewa nyazifa za juu za uongozi? Ama ndio urafiki na undugu wa kugawana nafasi za umma.
Kweli tunahitaji mabadiliko na We need strong leaders when it comes to bold changes...we should never allow things to take us by chance!!! Sasa leo hii we spend more time dealing with petty issues and forget about development.
Nafikiri tufikirie kuwa na mfumo wenye nia ya makusudi ya kuawaandaa vijana wenye uwezo wa kuwa leaders right from the scratch kuwa viongozi wa baadae
Tusiwaachie mafisadi wakaendelea kutuchagulia wapendwa wao. Watayaendeleza matatizo tuliyo nayo leo mpaka yatumalize mana yanafanana fanana Cancer
 
Hawa CCM ni kama wanajichimbia kaburi lao wenyewe. Hili suala la kukumbatia mafisadi litakuja kuwaumiza sana 2010.

Kwenye siasa hisia pekee inatosha kuwafanya wananchi waamini kama ni ukweli. Ukiangalia toka mambo ya ufisaidi yajitokeze, nafikiri mtu akija na conclusion ya kwamba CCM inakumbatia mafisadi atakuwa hajakosea kabisa. Kuna ushahidi wa kutosha wa mazingira kuonyesha hivyo.

CCM watapoteza majimbo mengi sana 2010 shauri ya huu ufisadi.

Mimi maombi yangu ni CCM igawanyike ili mwaka 2010 kuwe na mapambano makubwa huko kwenye majimbo. Dalili za viongozi wa zamani kuanza kuongea wazi wazi ni kama ni ishara tosha kwamba huenda CCM ikagawanyika ifikapo 2010.
 
Nakubaliana na Kitine kwa asilimia 100. Haiji kichwani kabisa mtu kama Chenge bado ni mbunge na kiongozi wa CCM.
 
Nakubaliana na Kitine kwa asilimia 100. Haiji kichwani kabisa mtu kama Chenge bado ni mbunge na kiongozi wa CCM.

Ila inaingia akili kwa Mkaoa kuendelea kupeta tu kama malaika?

Na vipi zile $64,000...Kitine na mke wake walizirudisha?
 
Ila inaingia akili kwa Mkaoa kuendelea kupeta tu kama malaika?

Na vipi zile $64,000...Kitine na mke wake walizirudisha?

Nyani,

Kitine alifanya makosa na kuadhibiwa. Anachosema sasa ni sahihi na ndio ukweli wenyewe.

Kwa mwendo wa sasa wa viongozi wasio na maadili tusitegemee kitu.
 
Jamani wacheni hawa CCM wajikaange na mafuta yao. Kwani 2010 iko mbali? Hata mtoto mdogo anajua kuwa CCM ni chama cha mafisadi. Mzee Kitine kasema ukweli na haupingiki. Uteuzi wa viongozi unategemea mtandao, uswahiba na siyo uwezo kama ilivyokuwa enzi za Mwalimu. TANU bwana kilikuwa chama cha watu. Ni vema wazee wengine wenye busara kama Kitine wakajitokeza na kuukemea ufisadi wa CCM!
 
Naanza kuhisi kwamba ongezeko la magonjwa kama 'Kisukari' 'presha' 'kansa' miungoni mwa watanzania kunauwezekano wa kuchangiwa na utawala mbovu wa serikali ya ccm. Ukisoma majibu ya MH.Chilligati hakika yanachefua kiasi cha kuharibu mpangilio wa hormone za mwili,sasa upuuzi kama huu ndizo taarifa za kawaida kwa jamii yetu. Nafikiri utafiti unaweza thibitisha haya.
Ni vema CCM wangekaa kimyaa.........
 
Nyani,

Kitine alifanya makosa na kuadhibiwa.

Anachosema sasa ni sahihi na ndio ukweli wenyewe.

Kwa mwendo wa sasa wa viongozi wasio na maadili tusitegemee kitu.

- Kitine hakuadhibiwa kama sheria inavyosema, baada ya kamati ya bunge kugundua kua yeye na mkewe wameliibia taifa, walitakiwa kwenda kwenye sheria kama kina Mramba na Yona, lakini ukafanywa ujanja ujanja ulioishia kumrudisha Kaburu CCM, na Kitine akaishia kulipa only nusu kama alilipa kweli, ya zile pesa, Kitine hakuadhibiwa mkuu ila kwa aibu alijuzulu na kuendelea kuwa mbunge, mpaka alipokimbizwa na wananchi wa Makete.

- kitu ambacho yeye sasa hakitaki anasema kiongozi akishajulikana kuwa ni fisadi atolewe nafasi zote, yeye ufisadi wake ulithibitishwa hata na sheria, lakini hakuachia ngazi zote wala kwenda kwenye sheria, lakini sasa anataka wengine waondolewe na kufikishwa kwenye sheria na kuachia ngazi zote, tunasema hivi hana huo ubavu, aweke mfano wa uongozi usio wa kienyeji kwa kutangulia yeye kwanza kwenye sheria!

- Anachosema sio sahihi, ila kuna yasiyo sahihi hajayasema na anayajua sana kwa sababu ya nafasi alizowahi kuzishika katika taifa, kwa mtizamo wangu serikali yetu iemkua ikiendeshwa kienyeji hata yeye akiwa kiongozi, maana kama isingekua yeye na Mbilinyi, walitakiwa kutoa hizi interview wakiwa jela kama wezi wengine wa kuku na mbuzi.

Maadili na sheria, ni vitu viwili tofauti Kitine na mkewe wamevunja sheria za jamhuri, sasa kwa taifa lisiloendeshwa kienyeji kama anavyotaka, alitakiwa kuwa jela sio kutupa empty lectures kwenye majukwaa ya siasa.
 
- Kitine hakuadhibiwa kama sheria inavyosema, baada ya kamati ya bunge kugundua kua yeye na mkewe wameliibia taifa, walitakiwa kwenda kwenye sheria kama kina Mramba na Yona, lakini ukafanywa ujanja ujanja ulioishia kumrudisha Kaburu CCM, na Kitine akaishia kulipa only nusu kama alilipa kweli, ya zile pesa, Kitine hakuadhibiwa mkuu ila kwa aibu alijuzulu na kuendelea kuwa mbunge, mpaka alipokimbizwa na wananchi wa Makete.

Kitine kamtupia dongo Kikwete na serikali yake yote. Kikwete ana uwezo kabisa wa kufufua uchunguzi dhidi ya kashfa au ufisadi wowote uliofanywa na Kitine alipokuwa madarakani. Mramba na Yona si wamefunguliwa mashtaka kwa waliyoyafanya wakati wa awamu ya tatu. Hivyo hivyo Kikwete anaweza kuamuru Kitine apandishwe Kizimbani.

- - kitu ambacho yeye sasa hakitaki anasema kiongozi akishajulikana kuwa ni fisadi atolewe nafasi zote, yeye ufisadi wake ulithibitishwa hata na sheria, lakini hakuachia ngazi zote wala kwenda kwenye sheria, lakini sasa anataka wengine waondolewe na kufikishwa kwenye sheria na kuachia ngazi zote, tunasema hivi hana huo ubavu, aweke mfano wa uongozi usio wa kienyeji kwa kutangulia yeye kwanza kwenye sheria!

Sawa, lakini pamoja na Kitine kutoondolewa madarakani alipohusika na kashfa au ufisadi haimanishi kwamba basi wengine wote waliofanya ufisadi au kashfa nzito basi waachiwe kupeta tu eti kwa kuwa Kitine hakuondolewa basi na wengine waachwe tu!!!. Pia kumbuka kwamba wakati Kitine alipofanya kasha na ufisadi wake hali ilikuwa tofauti sana na sasa, maana miaka ile Watanzania tulikuwa hatujadili matatizo yoyote ndani ya nchi yetu kama ilivyo hivi leo, thanks to JF where we dare to talk openly.

- - Anachosema sio sahihi, ila kuna yasiyo sahihi hajayasema na anayajua sana kwa sababu ya nafasi alizowahi kuzishika katika taifa, kwa mtizamo wangu serikali yetu iemkua ikiendeshwa kienyeji hata yeye akiwa kiongozi, maana kama isingekua yeye na Mbilinyi, walitakiwa kutoa hizi interview wakiwa jela kama wezi wengine wa kuku na mbuzi.

Maadili na sheria, ni vitu viwili tofauti Kitine na mkewe wamevunja sheria za jamhuri, sasa kwa taifa lisiloendeshwa kienyeji kama anavyotaka, alitakiwa kuwa jela sio kutupa empty lectures kwenye majukwaa ya siasa.

Anachosema Kitine kina ukweli mkubwa ndani yake kwamba nchi inaendeshwa kienyeji ahadi zote za Kikwete wakati wa kampeni yake maisha bora kwa kila Mtanzania, kuipitia upya mikataba ya dhahabu ili kuhakikisha Watanzania tunanufaika na rasimali zetu na ardhi mpya, nguvu mpya na kasi mpya mpaka sasa hivi hatujaona lolote. Huko ungeni tunaona jinsi Dikteata Sitta anavyominya uhuru wa Wabunge kujadili mambo mbali mbali ambayo yana maslahi makubwa ya nchi yetu. Anawaburuza tu wabunge anavyotaka yeye ili kulinda maslahi ya CCM bila kujali kufanya hivyo kunaathiri vipi maslahi y Watanzania.

Kikwete tangu aingie madarakani kamfukuza kazi juzi Mkuu wa wilaya kwa kuamuru Walimu wachapwe viboko lakini wale waliombeba ili aupate ULAIS (isomeke URAIS) akina Karamagi, Rostam Azizi, Lowassa, Msabaha na wengine wengi waliokuwa na kashfa ya aina moja au nyingine anawaogopa na aliwaomba wajiuzulu badala ya kuwafukuza kazi. Hatuhitaji kuwa na Rais asiye jasiri, mwoga ambaye hata siku moja haweki mbele maslahi ya nchi na Watanzania waliomchagua bali marafiki zake na chama chake Kunyamazia uozo unaoendelea ndani ya nchi yetu hakutasaidia lolote bali hali ndiyo itazidi kuwa mbaya maana Watanzania kama binadamu wengine popote pale duniani hatuna kiongozi mstaafu ambaye ni malaika hakuwahi kutenda kosa lolote lile alipokuwa madarakani. Hivyo wastaafu wote wataamua kujinyamazia na kuachia nchi ikitekwa na kutafunwa na mafisadi wachache maana viongozi walio madarakani maadili yote ya uongozi wameamua kuyaweka pembeni ili kulinda maslahi yao, ya marafiki zao mafisadi na ya chama chao ambacho sasa kinaonekana ni cha kifisadi na kupoteza imani miongoni mwa Watanzania walio wengi.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Dr. Kitine is right

1.Hivi kwa nini Kitine hakufikishwa mahakamani kwa makosa yake.

2.nani alitoa hukumu kuwa arudishe nusu ya pesa?....je aliyetoa hiyo hukumu ana authority hiyo?

3.Hivi Jambazi lililokamatwa likitoa lead ya majambazi mengine............tusilikilize kwa sababu lenyewe ni lijambazi........eehh

4. Hivi Dr. Kitine kwani hajui kuwa ana makosa aliyoyafanya huko nyuma.....kwa hiyo kujua kwake kuwa ana makosa.....kwa hiyo akaamua kuwa chizi kusema ukweli eeh

wengine hapa tuna makosa yetu........lakini haiondoi haki yangu yakusema ukweli....and it will be up to you judge kama nilichosema ni kweli au uongo au kina maana kulinagna na elimu zenu
 
Ina maana wazee wa hili baraza mnajifanya hamjui undani wa so called Kitine scandal? Ina maana wote hapa hamjui aina ya mahusiano ya huyo anayeitwa mke wa Kitine na Kitine wakati ule kiasi cha kufikia kumbebesha Mzee Kitine Msalaba wote wa huo wizi? Ina maana wote tumesahau mchakato mzima wa scandal ya Kitine wakati ule wa harakati za safisha njia mtandao upite?

Hivi kama kila kinachosemwa mtaani ama magazetini kitachukuliwa kama kipimo cha nani ana uhalali wa kusemea maslahi ya taifa na nani hana ni kweli tutakuwa na mtu wa kusema pale nchi inapoelekea kuzimu?

Naomba mmoja kati yetu hapa ambaye hajawahi kushutumiwa kwa kosa lolote lile?

Hivi humu ndani hatuna watu waliotumia fedha za serikali isivyo halali, ama katika kulipiwa masomo yao wakati wanakosa vigizo ama wakati mwengine hata kutokuwa wanafunzi, ama kutumia bank statements fake kupata visa na wakati mwengine kutumia statements za hao hao tunaowaita mafisadi, ama kuishi ughaibuni kinyume cha sheria kwa wakati fulani, ama kudanganya uhalisia wao ama hata uraia wao halisi ili kuweza kuishi ughaibuni, ama kukiuka kulipa kodi na madai mengine halali ama ughaibuni au nyumbani?

Hivi ni wangapi humu ndani ambao wanaishi ughaibuni na kuhodhi akaunti za benki na wamefanya wajibu wao wa kutoa taarifa Benki Kuu na kulipa kodi wanazopaswa kama raia wengine nchi kama ambavyp taratibu na sheria za nchi zinavyoelekeza?.

Je wote waliofanya haya na mengine hawapaswi kusema kuwa nyumba yetu Tanzania ina ufa unao ongezeka kwa kasi?

Naamini tunahitaji watu kama Kitine kuongea ingawa kuna hatari zake? Tutakuwa tunajidanganya kama tunadhani kuwa aliyesema pale ni Kitine pekee. Kuna wengi nyuma yake, watu binafsi na makundi nyeti. Kitine anawakilisha wengi na mengi. Hali ni mbaya ndugu zangu....

Na hili la nyang'au Lyumba ndio limekoroga mambo kabisa.......
 
bali hali ndiyo itazidi kuwa mbaya maana Watanzania kama binadamu wengine popote pale duniani hatuna kiongozi mstaafu ambaye ni malaika hakuwahi kutenda kosa lolote lile alipokuwa madarakani. Hivyo wastaafu wote wataamua kujinyamazia na kuachia nchi ikitekwa na kutafunwa na mafisadi

- Mkuu BAK, mengine yote yako sawa lakini tatizo langu ni hapa tu, umalaika wa viongozi wetu wa zamani hauna anything to do na kuvunja sheria kama alivyofanya Kitine, na sasa anataka kuirekebisha system iliyomponya yeye mwenyewe na kuvunja sheria, lakini anataka kuanza na wengine, ila sio yeye.

- Wastaafu wote waliowahi kuvunja sheria wakapona kutokana na ubovu wa system yetu kama huyu Kitine, hawawezi kutusaidia lolote, tunao viongozi wasafi na wanaweza kuongea na tukasiliza,

- Michael Milken alikuwa m-US mwenye akili nyingi sana za uchumi, lakini alipovunja sheria pamoja na kwamba alijitahidi sana kuwaonyesha serikali yake njia zote za wizi alizozifanya ili wamuache huru bado walimfunga jela kwanza ndio wakampa nafasi ya kuwaelimisha wananchi wa US kuhusu ubovu wa sysytem yao ya uchumi.

Huwezi kuwa mlevi halafu ukawaambia watoto wako wasiwe walevi, it just does not work!
 
Dr. Kitine is right

1.Hivi kwa nini Kitine hakufikishwa mahakamani kwa makosa yake.

2.nani alitoa hukumu kuwa arudishe nusu ya pesa?....je aliyetoa hiyo hukumu ana authority hiyo?

3.Hivi Jambazi lililokamatwa likitoa lead ya majambazi mengine............tusilikilize kwa sababu lenyewe ni lijambazi........eehh

4. Hivi Dr. Kitine kwani hajui kuwa ana makosa aliyoyafanya huko nyuma.....kwa hiyo kujua kwake kuwa ana makosa.....kwa hiyo akaamua kuwa chizi kusema ukweli eeh

wengine hapa tuna makosa yetu........lakini haiondoi haki yangu yakusema ukweli....and it will be up to you judge kama nilichosema ni kweli au uongo au kina maana kulinagna na elimu zenu

Yeah...ukweli ni ukweli hata usemwe na nani. Lakini alikuwa wapi siku zote hizi kuanza kuusema huo ukweli? Angesema kipindi bado yuko kwenye serikali ya Mkapa ingependeza zaidi. Na ingependeza mara mia zaidi kama angejisalimisha mwenyewe mikononi mwa vyombo vya sheria kwa ubadhirifu wake anaotuhumiwa kufanya kama anakubali alifanya makosa.
 
- Mkulu wangu with all due respect mimi ni msafi na clean na sina ufisadi wa anything na ninaamini tupo wabongo wengi sana kama mimi ambao tunaweza kulisaidia hili taifa kwa kuanza na one, na kufuta mafisadi wote!

Respect Mkuu!

Heshima mbele kwanza.

Usafi wako waachie wengine wausemee mkuu,. Hata hao tunaowashutumu kwao wao ni wasafi. Ila historia ya mtu ikianikwa, alipozaliwa,kukulia,kusomeshwa, ulivyopata kazi, unapofanyia n.k. yawezekana kabisa usafi wako ni wa mashaka.

Wapo waliosomeshwa kwa pesa za ufisadi wa baba zao, hao nao keshokutwa watatwambia ni wasafi.

Usafi wetu hu mashakani tunapolelewa kwenye miongo mitatu ya tawala zinazoshutumiwa kwa Rushwa kila kukicha.
 
Heshima mbele kwanza.

Usafi wako waachie wengine wausemee mkuu,. Hata hao tunaowashutumu kwao wao ni wasafi. Ila historia ya mtu ikianikwa, alipozaliwa,kukulia,kusomeshwa, ulivyopata kazi, unapofanyia n.k. yawezekana kabisa usafi wako ni wa mashaka.

Wapo waliosomeshwa kwa pesa za ufisadi wa baba zao, hao nao keshokutwa watatwambia ni wasafi.

Usafi wetu hu mashakani tunapolelewa kwenye miongo mitatu ya tawala zinazoshutumiwa kwa Rushwa kila kukicha.

- Ninasema hivi hapa tunajadili maadili na sheria zetu za taifa na jamhuri, hatuongelei kama niliwahi kuiba pipi nilipokuwa mdogo, unless kuna mengine unayotaka kusema lakini unashindwa kama ninakusoma between the lines, ila sijawahi kusomeshwa na hela za ufisadi, hapana nimesoma shule bure under Mwalimu, Europe nimesomeshwa na na kulipiwa na serikali bure kama ilivyokuwa kwa wananchi wengi zamani, na US nimejisomesha kwa hela zangu mwenyewe za jasho langu na risiti ninazo.

- La usafi wangu as far as uongozi wa taifa is concerned karibu sana mkuu, kama ni ishu kwa taifa, lakini ninasema taifa letu lina wasafi wengi sana na mimi nikiwa mmojawapo, na tunaweza kulisafisha bila kushusha standards za taifa morally kwa visingizio kwamba wote ni wachafu na hatuhitaji kuwasiliza viongozi wachafu kwa sababu sisi wote wananchi wa Tanzania sio wachafu na mimi nikiwa mmojawapo.

Thanxs!
 
Back
Top Bottom